Maalum kwa wanaume waliolelewa na mama tu

Maalum kwa wanaume waliolelewa na mama tu

Live case ni Naseeb Abdul a.k.a Diamond Platnumz. Maisha yake si mnayaona?
 
Mama ndo kila kitu,nampenda sana!namuombea aishi miaka mingi nikikumbuka hasa alipokuwa akifanya vibarua kwenye mashamba ya watu ili tu nipate riziki na shule.umenikumbusha mbali sana!
 
Sidhani,anyway ni tabia ya mtu binafsi. Mimi nimelelewa na mama(mzee alirip nikiwa kwa tumbo),alafu ni last born ila hakukua na kudeka wala nini,maza alitulea kwa mkono wa chuma maana tulikua madume tu vinginevyo tungemshinda.

Niko strong sio lege lege,sinuni nuni ila nina hasira nyingi sana. Hao mashemeji zako ni tabia yao tu. Kuhusu kujali na kuthamini mke sijui maana sijaoa.

Hapo kwenye hasira.. Ni nini kimekufanya uwe na hasira??
 
labda niko nje kidogo mimi nimelelewa na bibi naweza kudhibisha hayo sipokuwa hilo la kununu kudeka na kulegea hayo hapana ,ila huruma utu wema na kama ulivyose kujali hayo yanahusu sana,, sijui lakini kwani mi ni bibi,lakini bibi na ni mama.
 
Hebu niambie kuna tatizo gani kwenye hili au mfano ulio utoa? Kwanini Mama aliye nilea asiwe wa kwanza halafu wa kwanza awe MTU niliye kutana nae ukubwani?
Si kila mama ana dekeza mtoto

Hata Mimi nimelelewa na Mama na yeye ndiye huwa anakuwa wa kwanza wengine wanafata na katika hili huwa sina mjadala kabisa!

Dedication
Nani kama Mama-Christian Bella

Nimekupenda buureee...nani kama mama koz mijitu mingine sijui ikoje kusema sema ovyo eti kumpa mom first priority ni kujidekezaweweeeee
Hata mwanaume anipendeje kama hampendi sana mom yake sintauelewa upendo wake
Kwangu.nukta nimemaliza
 
Hapo kwenye hasira.. Ni nini kimekufanya uwe na hasira??

Hiyo haimaanishi nakasirika muda wote,hapana,niko kawaida ila kama mtu ananiboa huwa kucalm down ni issue. Hasira zimekuja tu ila huwa najitahdi sana kuziresist,nimeshajua nilivyo kwa hiyo kwa kiwango kikubwa naweza kumanage hasira zangu. Temper management niko vizuri. Tumeumbika tofauti eti.
 
Mama ndo kila kitu,nampenda sana!namuombea aishi miaka mingi nikikumbuka hasa alipokuwa akifanya vibarua kwenye mashamba ya watu ili tu nipate riziki na shule.umenikumbusha mbali sana!

Acha kabisa,singo momz wana changamoto sana...thats why nakua makini sana nisije mpa binti mimba alafu kid wangu akalelewa na mama ake tu
 
Uongo mtupuuu.mimi mfano lakin hakuna ukweli...
 
Habari wandugu wa jukwaa hili!
Wajameni nimeambiwa na kusikia tabia walizonazo wanaume wengi waliolelewa na mzazi mmoja hasa Mama!
kuwa ni wanaume wanaojali na kuthamini Wake zao japo sijathibitisha hili!

Wengi Wao nimegundua ni watu wakudeka sana, wapo legelege sio wakamavu Pia wanasumbuliwa na tabia ya kununa kuna! Hili nimelithibitisha hata kwa mashemeji zangu! Naomba nilete hili mezani tuchangie kwa pamoja nifahamu nisiyoyajua mengine!

Asanteni


nililelewa na mama kininja...she plainly used to tell me I have to be strong ipo siku I will be a husband, father of the family na everything will turn around, I will have to look after her.

Hao malegelege wengi huwa wamelelewa na bibi (manyanya) zao.
 
huwa hawasumbuliwi na wanawake wanajua waishi vp na mwanamke kama kumpenda,kumtunza,kumjali na mengineyo anajua mke anahitaji nini na wakati gani kwani wanakuwa washajifunza halafu wanajua bajeti.Wana tofauti kiasi fulani na waliolelewa na wazazi wote au baba,lakini pia inategemea na mazingira ya makazi
 
Na wanaume waliolelewa na mama wa kambo je? Tufanyie na ufafili na hili basi ... nahs watakua waume wazuri sana!
 
Sio wote ila wengi wako hivyo. Na wanaume waliozaliwa peke yao kwenye familia huku wakizungukwa na wadada wengi wakoje?.

wengi wao kwa sababu ya kucheza mdako na Dada zao hujikuta wameangukia kwenye UBWABWA....
 
Kulelewa na dingi Noma sana....yaani mchaka mchaka kama mpo depo vile...unakuta dingi ana sura ngumu na watoto hamkumbuki dingi mara ya mwisho alicheka lini..akirudi home mpaka kuku wanatulia...si wanajua kamanda jemedari amirijeshi mkuu karudi...yaani kila mtu anasikilizia..leo kuna msala gani....
yaani akikuita ndani unajua lazima nitakuwa nimeshalizua tu na mwendo wake hukumu....tu..
unaweza ukakaa hata mwezi dingi hujamtia machoni...ingawa mnakaa nae nyumba moja...bora mama tu..akirudi kazini tunapata angalau hata vipipi..watoto tunagombania....I LOVE YOU MAMA.....
 
Nashauri usome Edwin Mtei's From Goatherd to Governor (Mchunga Mbuzi hadi Gavana wa Benki Kuu) . Mwasisi wa CHADEMA, chama kinachotarajia kuchukua DOLA, naye alilelewa na mama tu. Nimempigia simu kumwaririfu na kumsomea thread hii, akanijibu HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE ifikapo Oktoba 2015.

Wewe utakuwa umelelewa kama mtoto wa mitaani n baadaye ukavuta bangi!! Hii akili n hiyo chadema sio bure.
 
Pamoja na ukweli kwamba wapo strong women wanao lea watoto vizuri bila kudekeza ila bado huwa upungufu unakuja kuonekana tu. Malezi ya baba yana nafasi yake pia hata mama akiwa smart vipi. Mimi nilishaona tatizo la kutokuwa na msimamo as a man. Mara nyingi hawa watu huyumbishwa na saa nyingine huwa hawawezi kutoa final decision yeye kama yeye bila kushauriana na watu wengine. Na sometimes hawa watu hukosa sauti kama watawala katika familia zao. Ila hii si applicable kwa wote ila wengi wao ambao nimeshawahi ishi nao na kuwashuhudia wana hivyo vi chembe chembe

Kwa maelezo yako haya, unafikiri Mwenye nchi kalelewa na wazazi wangapi? Maana anatabia zote ulizotaja hapo.
 
baby's mama siku zote wanajua kupenda girls zao..... nimeona kwa kaka zangu na kwangu pia... au movie reference angalia think like a man.... and.... think like a man too utaona baby's mama wanavojua kupenda na kujali watu wao
 
Naona mleta mada umetuamulia sie wa ''TEAM MAMA THIS,MAMMA THAT,MAMA NATAKA THAT NOT THIS,MOOOOOM!!!??'',Afu hapo plus uwe Kitindamimba as i am yani raha sana.
Ila sio pkeyangu,Nassibu Domo naye inamuhusu e.t.c.
Ila naheshimu wanawake na kuwapenda koz if not for my mum,i would have never gotten where i am,even though not that far.
 
Back
Top Bottom