Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,808
- 11,973
Maalim Seif akabidhiwa fomu za kuomba ridhaa ya Chama cha ACT Wazalendo kuwa Mgombea Urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Kakabidhiwa fomu hizo na Katibu Mkuu wa Chama, Ndugu Ado Shaibu katika Ofisi Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo iliopo Vuga, Zanzibar.
Maalim Seif amewashukuru sana wanachama wa ACT Wazalendo waliojitokeza kwa wingi kwenye Ofisi Kuu ya Chama, Vuga, Zanzibar kushuhudia tukio la kuchukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar leo asubuhi. "Ahsanteni sana kwa imani na mapenzi yenu kwangu". Kasema Maalim Seif.