smarte_r
JF-Expert Member
- Nov 8, 2013
- 4,575
- 12,186
Kwa sasa kila mkazi wa dar awe mwana ccm, mwanachadema, awe wa no reform no election, awe wa october tuta-tick ana kipata cha mtema kuni kuhusu foleni ya barabarani inayosababishwa na utitiri wa malori, mengi yakiwa made in china.
Kila barabara mpaka zile za mitaani ambazo alizijenga Magufuli kwa kuziwekea lami, zimetapakaa malori.
Imefika wakati hata wale wenye magari madogo ya kutembelea, wanaona bora wapaki wachukue bodaboda wawahi kwenye appointment zao.
Katika barabara ambayo inavunja rekodi ya kuwa na malori mengi ni Mandela Road. siku za nyuma ilikuwa kidogo afadhali, ila siku za hivi karibuni foleni ni mda wote.
Nakumbuka marehemu Magufuli alikuja na mpango wa kutenga eneo kubwa nje ya dar, nadhani ni chalinze ili kujenga bandari kavu sambamba na kutenga eneo lingine wafanyabiashara ya usafirishaji wajenge yard za kulaza magari yao. plan ilikuwa makontena kutoka bandarini yabebwe na treni ya mizigo mpaka eneo hilo, baada ya hapo malori yabebe mkontena hayo kuyasifirisha mikoani na nchi jirani.
Naiuliza serikali ya samia, hii project imeishia wapi?, au baada ya kufariki Jpm na project ikafa?.
Kwasasa hali ya barabara za dar ni mbaya sana, yard za malori zimetapakaa kila pahali. mbaya zaidi zipo jirani na makazi ya watu ambao hutumia barabara za mitaani kama shortcut kufika kwenye main road then wafike maeneo mbalimbali ya jiji kujitafutia mkate wao wa kila siku.
Na nyinyi Waarabu na Wasomali ambao wengi wenu mmewekeza kwenye biashara ya usafirishaji, hamuwezi kujenga yard nje mji?. kuna raha gani kununua nyumba kumi mtaa mmoja wa uswahilini, unazivunja halafu unajenga yard ya kulaza malori?, kwanini msijenge hizo yard nje mji ambako mazingira ni rafiki na salama kwa aina hiyo ya uwekezaji?.
Sitaki kuzungumzia upotevu wa muda na hasara ambayo wakazi wa Dar wanaipata kwa kuchelewa kufika kwenye shughuli zao za kiuchumi. kiufipi tu ni kwamba, mtu ambaye yupo safarini kutoka Morogoro kwenda Kibaha, anawahi kufika kuliko yule anayetoka Mwenge kwenda Magomeni. hali ni mbaya sana.
Habari ifike kwa wahusika. Nawasilisha.
No Reform No Election.
Kila barabara mpaka zile za mitaani ambazo alizijenga Magufuli kwa kuziwekea lami, zimetapakaa malori.
Imefika wakati hata wale wenye magari madogo ya kutembelea, wanaona bora wapaki wachukue bodaboda wawahi kwenye appointment zao.
Katika barabara ambayo inavunja rekodi ya kuwa na malori mengi ni Mandela Road. siku za nyuma ilikuwa kidogo afadhali, ila siku za hivi karibuni foleni ni mda wote.
Nakumbuka marehemu Magufuli alikuja na mpango wa kutenga eneo kubwa nje ya dar, nadhani ni chalinze ili kujenga bandari kavu sambamba na kutenga eneo lingine wafanyabiashara ya usafirishaji wajenge yard za kulaza magari yao. plan ilikuwa makontena kutoka bandarini yabebwe na treni ya mizigo mpaka eneo hilo, baada ya hapo malori yabebe mkontena hayo kuyasifirisha mikoani na nchi jirani.
Naiuliza serikali ya samia, hii project imeishia wapi?, au baada ya kufariki Jpm na project ikafa?.
Kwasasa hali ya barabara za dar ni mbaya sana, yard za malori zimetapakaa kila pahali. mbaya zaidi zipo jirani na makazi ya watu ambao hutumia barabara za mitaani kama shortcut kufika kwenye main road then wafike maeneo mbalimbali ya jiji kujitafutia mkate wao wa kila siku.
Na nyinyi Waarabu na Wasomali ambao wengi wenu mmewekeza kwenye biashara ya usafirishaji, hamuwezi kujenga yard nje mji?. kuna raha gani kununua nyumba kumi mtaa mmoja wa uswahilini, unazivunja halafu unajenga yard ya kulaza malori?, kwanini msijenge hizo yard nje mji ambako mazingira ni rafiki na salama kwa aina hiyo ya uwekezaji?.
Sitaki kuzungumzia upotevu wa muda na hasara ambayo wakazi wa Dar wanaipata kwa kuchelewa kufika kwenye shughuli zao za kiuchumi. kiufipi tu ni kwamba, mtu ambaye yupo safarini kutoka Morogoro kwenda Kibaha, anawahi kufika kuliko yule anayetoka Mwenge kwenda Magomeni. hali ni mbaya sana.
Habari ifike kwa wahusika. Nawasilisha.
No Reform No Election.