Maajabu Tanzania

Maajabu Tanzania

huo ni ulimbukeni hivi na jk anavoendaga huko huwa wanadeki barabara.
 
Nimepita ubungo lami inapigwa Demi. Usicheze na Sirikali

Mwongo huyu. Mi nipo ubungo hapa. mbona amna mtu anapiga deki barabara. labda wafagizi ndo nilikuta wapo bize kile kinjia cha Ubungo maziwa wanafagia. Deki? aaaah....jamani punguzeni uongo. Barabara yenyewe ya kupiga deki iko wapi...Strabarg wametindua kila mahali.
 
Hapa hapa Dar Es Salaam kuna wakazi kibao hawana maji ila Obama anakuja maji yanapatikana hata ya kumwangalia barabara. Kweli Tanzania tunastahili kuchekewa na majirani.
Chezea Obama weye,shetani wetu na wa yote haya NI CCM TU.
 
Nıpo ubungo mataa: Morogoro road na Samnujoma road zınapıgwa dekı: Kwelı Obama Nomaaaaa.....! Tutashuhudıa mengı

Hilo si tatizo sana hata kama hizo barabara au sehemu yoyote atakayotembelea Obama ingekarabatiwa na kusafishwa kwa kurambwa kwa ulimi na kunakishiwa kwa mate! Tatizo ni matumizi hovyo na ya kijinga ya kodi za wananchi kwa manufaa ya wachache!
 
KUPIGWA DEKI imekuwa kana neno la utani na mizaha, eleza wanachofanya ninini ili wasomaji wajue!
Sometimes tunaexagerate mno taarifa zetu.
Wameweka gari linamwaga maji barabarani. Kule kwenye lami.
 
Mwongo huyu. Mi nipo ubungo hapa. mbona amna mtu anapiga deki barabara. labda wafagizi ndo nilikuta wapo bize kile kinjia cha Ubungo maziwa wanafagia. Deki? aaaah....jamani punguzeni uongo. Barabara yenyewe ya kupiga deki iko wapi...Strabarg wametindua kila mahali.
Si mwongo. Mimi nilipita saa kumi na moja asubuhi nimekuta wanamwaga maji na gari. pale ubungo maji.
 
Wanachezea maji wakati nina wiki mbili hili bombo halijatoa maji.
 
Si mwongo. Mimi nilipita saa kumi na moja asubuhi nimekuta wanamwaga maji na gari. pale ubungo maji.

Kuna Mpishano. Wewe upo ubungomaji alfajiri saa 11. Mleta uzi yupo Ubungo fulani saa 2.00 kasoro-ishiri. Mi nipo Ubungo stand saa 3 kasorobo. Kuna mmoja wetu anaongopa hapa. Kuimwagia maji barabara ndo deki? Strabag wanamwaga maji barabaran karibu kila siku kuanzia mjini hadi ubungo mataa. zote hizo deki?
 
nakumbuka barabara ya kilimanjaro mpaka arusha ilivyo pigwa deki kipind clinton ameenda uko
 
Inawezekana leo ukionekana unatupa kopo la maji au plastic bag ukaingia segerea bila kupitia mahakamani
 
Hilo si tatizo sana hata kama hizo barabara au sehemu yoyote atakayotembelea Obama ingekarabatiwa na kusafishwa kwa kurambwa kwa ulimi na kunakishiwa kwa mate! Tatizo ni matumizi hovyo na ya kijinga ya kodi za wananchi kwa manufaa ya wachache!

wewe ndo umeongea point mkuu, wengine wanapiga kelele tu, wagonjwa wana lala chini mahospitalini eti leo kaja mpumbafu mmoja nchi mpaka raisi mwenyewe ananyenyekea kama MUNGU kashuka kuja kutukomboa, niko natazama BBC NEWS, wao ndo wameongea sababu ya Obama kuja Tanzania ni competitions ya G8 kuweza ku exploit resources zilizopatikana especially Gesi ya mtwara, Naumia sana aiseeh ...
 
Ningefurahi awe anakuja kila mwisho wa mwezi ili jiji letu ling'ae.
 
Username ya mleta mada inaonyesha huenda nae ni mmoja ya wasafishaji au anauzoefu,
Hebu tuambie hili lilikuwepo? Kama ndivyo basi hiyo ni deki. Tofauti na hapo ni operation za kawaida za kumwaga maji.
2uje9e7e.jpg
 
Kila mara huwa nagombana na viongozi wangu kwa tabia yao ya kuwapa mashuka mapya wagonjwa waliolazwa wodini pale tunapotarajia ugeni, wakati mwingine mambo haya hufanyika hata pale ambapo dawa na vifaa tiba hamna. Yaani huwa najiona mpumbafu pale mgonjwa anaponiuliza eti 'hata panado hamna?'

Leo nimejifunza kitu, kumbe upumbafu huu unaanzia huko juu! Nadhani Ikulu!
 
nikawaida kwani hata wewe ukifikwa na ugeni mkubwa nyumbani kwako itabidi kila ki2 ukiweke sawa bhana
 
Back
Top Bottom