Maajabu Tanzania

Maajabu Tanzania

mwenzangu!? nilikuwa sijaona! ....lakini hii picha pia sina hakika kama ni ubungo. deki za ubungo kumbe zilipigwa asubuhi na mapema. kuna mtu alikuwa anashuhudia pale kwenye baa usiku; yeye aliwahi kupanda treni pale ubungo maziwa ndo akawa anasimulia pale kwenye baa nini aliona. ni sie wachelewaji kuamka ndo hatukuona hizo deki. Barabara zinapigwa deki? sijapata kuona mie. Bush na Klintoni hawakumpigia deki barabara.... huyu Obama kapendelewa mno jamani! kha.... au ndo yaleyale mtoto wa kwanza karudi kutoka safari ya mbali baba na mama wanahangaika kumfurahisha? mmh. Nakosa hata la kusema mie....

Nimpongeze Kikwete japo kwa hili. Safari hii kafanya jambo kubwa la kihistoria. Hii picha itatumika miaka mingi sana nina hakika. Kotekote Tanzania na Marekani. Pengine hata Kenya.

Mkuu, wakati Bush alipokuja hapa nchini mara ya kwanza, barabara za Arusha zilipigwa deki. Wakati huo alitembelea mahakama ya ICTR
 
Mkuu, wakati Bush alipokuja hapa nchini mara ya kwanza, barabara za Arusha zilipigwa deki. Wakati huo alitembelea mahakama ya ICTR


He! unisnambie. Nako Arusha? Bac huku kujikomba sasa.... Alipokuja Zing ping...sijui zing ping sijui nani yule wa china Walipinga deki? Au ni zile hela za Millenium challenge zinawasumbua? Lakini mbona naye china kajenga reli, wiwanda vya nguo, kafundisha watu kurusha mig fighter plane, na mengi tu mengine. Mbona marekani inapendelewa hivi? Au?
 
Back
Top Bottom