Maajabu: Huu ndiyo Ukumbi wa Halmashauri ya Busokelo

Mleta uzi hakika amekurupuka nina mashaka na uwezo wake wa kufikiri, kwanza unapoishutumu Halmashauri kwamba kuna fedha zimeibwa au kutumiwa vibaya lazima uwe umefanya uchunguzi na kujiridhisha kwamba mradi huo umetengewa bajeti kiasi gani na zimetumika kiasi gani na je thamani ya fedha inaendana na kazi iliyofanyika? Na je umejengwa Kwa shughuli za ukumbi au matumizi mengine lakini Kwa sasa unatumika kama ukumbi Kwa muda?

Huwezi kuanza kuwashutumu viongozi kabla ya kufanya uchunguzi wa kina na unao Uhuru wa kuwauliza endapo Una mashaka na jambo lolote unaless otherwise utwambie kwamba uliwahoji viongozi na hawakukupatia ushirikiano, najua hukufanya hivyo ukaamua kukurupuka kuja kuweka upupu wako hapa.

Kwanza unaweza kukuta wewe unawashutumu viongozi wa Halmashauri lakini wanaoujua ukweli wanawapongeza viongozi Kwa kujenga hata hilo jengo uliloliona si kitu kuliko baadhi ya taasisi ambazo hadi sasa zinakodi kumbi za mikutano Kwa gharama kubwa Kwa siku(zaidi ya laki 5 Kwa siku)

Kwa faida yako kama ulivyoambiwa na mmoja wa wachangiaji hapo juu Linajengwa jengo la Utawala la Halmashauri lenye hadhi ya nyota 5 na ndani yake lina ukumbi wa kisasa.

Ninakushauri kabla ya kupost chochote JF fanya Kwanza uchunguzi sio kupost upuuzi wako na kuwapotosha watu.Kwa faida yako ukumbi wa jengo la Utawala la Halmashauri na ukumbi wa Halmashauri angalia picha, na ujenzi unaendelea tatizo lako umeona kwamba habari inayokufurahisha ni huo uliouita ukumbi lakini sio ujenzi wa jengo. View attachment 835929
Serikali kuu haijatenda fair iweje halmashauri mpya ya Tunduma ilitaka kuanza ujenzi wa majengo ya utawala kwa pesa za vyanzo vya halmashauri zaidi ya billion moja ikazihamishia kujenga hospital wakati hawajaleta pesa za kujengea admn.block ila huko kwingine wametuma?
Pesa zinazolipwa kama pango ya jengo la kukodi ni karibu robo tatu ya hizo huoni hii ni hasara?
 
Serikali kuu haijatenda fair iweje halmashauri mpya ya Tunduma ilitaka kuanza ujenzi wa majengo ya utawala kwa pesa za vyanzo vya halmashauri zaidi ya billion moja ikazihamishia kujenga hospital wakati hawajaleta pesa za kujengea admn.block ila huko kwingine wametuma?
Pesa zinazolipwa kama pango ya jengo la kukodi ni karibu robo tatu ya hizo huoni hii ni hasara?
walisaidiwa kuainisha kipaumbele. Tatizo kubwa itakuwa ni Hospitali kuliko admin block.
 
Tupo katika awamu ya tano yenye ndoto ya Tanzania ya Viwanda lakini kuna viongozi hawapo serious.

Huu ndiyo Ukumbi wa kimataifa wa halmashauri ya Busokelo unaoendelea kujengwa na watu walio serious wenye falsafa ya maendeleo.

Mwenyekiti yupo, Mkurugenzi yupo, Afisa manunuzi yupo, Mhandisi yupo.

Yaani nimeuangalia halafu nikasema hiiii

View attachment 835463
View attachment 835464
Huu ni mwonekano wa ndani. Unaweza fikiri ni kanisa ila sio kanisa ni project ya watu wanao mchezea rais wetu.
Mkuu nimependa hapo kwenye "UKUMBI WA KIMATAIFA" wakimataifa indeed
 
Hiyo ni zaidi ya kujitahidi na kubana matumizi kupita kiasi! Kwa faida yake mtoa mada afuatilie Halmashauri hii mara zote tangu kuanzishwa kwake inapata Hati safi katika kaguzi za CAG, unadhani ukumbi huo hajawahi kuuona? Halmashauri zenye kumbi nzuri ndio zinapata hati chafu.
Mnapata hati safi lakini mnajua michezo mnayocheza, hata huo ukumbi siyo kweli kwamba mlitumia fedha za mapato ya ndani fedha za uchaguzi na Idara ya ujenzi ndizo mlizotumia kujengea huo ukumbi, still hela mliyotumia na hatua ambayo jengo limefikia haziendani. hata sakafu mlishindwa kuweka hadi meneja wa TARURA kaja kuwasaidia
 
Tupo katika awamu ya tano yenye ndoto ya Tanzania ya Viwanda lakini kuna viongozi hawapo serious.

Huu ndiyo Ukumbi wa kimataifa wa halmashauri ya Busokelo unaoendelea kujengwa na watu walio serious wenye falsafa ya maendeleo.

Mwenyekiti yupo, Mkurugenzi yupo, Afisa manunuzi yupo, Mhandisi yupo.

Yaani nimeuangalia halafu nikasema hiiii

View attachment 835463
View attachment 835464
Huu ni mwonekano wa ndani. Unaweza fikiri ni kanisa ila sio kanisa ni project ya watu wanao mchezea rais wetu.
Busekelo ndiyo wapi?
Kwa majina yasiyokuwa maarufu, lazima uandike wilaya na mkoa wake.

Lakini aina hii ya uandishi, umeandika kama unamvizia mtu kwa kumwangalia usoni, ama unakimbzwa!
 
Mkuu sijakurupuka ni jengo la mikutano na leo mkutano huo ulikuwa unaendelea humo mjengoni
Umeumbuka unatafutia kick ya uteuzi Busokelo. Kwanza nawasifu sana Busokelo kwa kujenga ukumbi wa muda ili waondokane na gharama za kukodi ukumbi Mara kwa Mara. Busokelo Hongereni sana kwa kujiongeza na ndio maana Katika Halmashauri zinazofanya vizuri Tanzania ni pamoja na nyie Busokelo. Huyu Kanjanja mpuuzi tu hana ethos za uandishi wa Habari.
 
Mleta uzi hakika amekurupuka nina mashaka na uwezo wake wa kufikiri, kwanza unapoishutumu Halmashauri kwamba kuna fedha zimeibwa au kutumiwa vibaya lazima uwe umefanya uchunguzi na kujiridhisha kwamba mradi huo umetengewa bajeti kiasi gani na zimetumika kiasi gani na je thamani ya fedha inaendana na kazi iliyofanyika? Na je umejengwa Kwa shughuli za ukumbi au matumizi mengine lakini Kwa sasa unatumika kama ukumbi Kwa muda?

Huwezi kuanza kuwashutumu viongozi kabla ya kufanya uchunguzi wa kina na unao Uhuru wa kuwauliza endapo Una mashaka na jambo lolote unaless otherwise utwambie kwamba uliwahoji viongozi na hawakukupatia ushirikiano, najua hukufanya hivyo ukaamua kukurupuka kuja kuweka upupu wako hapa.

Kwanza unaweza kukuta wewe unawashutumu viongozi wa Halmashauri lakini wanaoujua ukweli wanawapongeza viongozi Kwa kujenga hata hilo jengo uliloliona si kitu kuliko baadhi ya taasisi ambazo hadi sasa zinakodi kumbi za mikutano Kwa gharama kubwa Kwa siku(zaidi ya laki 5 Kwa siku)

Kwa faida yako kama ulivyoambiwa na mmoja wa wachangiaji hapo juu Linajengwa jengo la Utawala la Halmashauri lenye hadhi ya nyota 5 na ndani yake lina ukumbi wa kisasa.

Ninakushauri kabla ya kupost chochote JF fanya Kwanza uchunguzi sio kupost upuuzi wako na kuwapotosha watu.Kwa faida yako ukumbi wa jengo la Utawala la Halmashauri na ukumbi wa Halmashauri angalia picha, na ujenzi unaendelea tatizo lako umeona kwamba habari inayokufurahisha ni huo uliouita ukumbi lakini sio ujenzi wa jengo. View attachment 835929
Mleta hoja umeona Ramani ya jengo la utawala la Busokelo? Jengo limeshaanza kujengwa. Ulishindwa hata kumuuliza Emmanuel Lengwa akupe uzoefu ni wapi linajengwa jengo la Utawala lenye Ukumbi wa Kisasa la Halmashauri?
 
Sasa kama mapato ya halmashsuri kwa mwaka ni mil.600 kwa nini isipate hati safi? Halmashauri zenye mapato kwa mkoa wa mbeya na songwe zinazokusanya zaidi ya bilioni 3 kwa mwaka kama jiji chunya na Tunduma haziwezi kupata hati safi coz zina miradi mingi sana inayotekelezwa kutumia pesa za ndani
Kwa hiyo mkikusanya pesa nyingi ndio mnakiuka sheria na kanuni za usimamizi wa miradi ya Serikali? Temeke, Kinondoni, Mufindi watasemaje? Acha kutuhadaa!
 
Mleta hoja umeona Ramani ya jengo la utawala la Busokelo? Jengo limeshaanza kujengwa. Ulishindwa hata kumuuliza Emmanuel Lengwa akupe uzoefu ni wapi linajengwa jengo la Utawala lenye Ukumbi wa Kisasa la Halmashauri?
Wapuuzi kama hawa wanaoleta hoja na mada zisizo na uchunguzi wala ukweli wowote bora kuwapiga ' Ban', wanaharibu sifa ya JF Kwa kuropoka ropoka tu.
 
Back
Top Bottom