onemediaonline
Member
- Feb 4, 2026
- 11
- 9
Akizungumza katika mahafali hayo, Mhe. Lusetula amewataka wahitimu wote kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kutumia elimu waliyoipata kama chachu ya kuleta maendeleo ya taifa.
“Nendeni mkaitumie vyema elimu na maarifa mliyoyapata ili kuchochea maendeleo ya taifa, zingatieni misingi ya amani na muwe wazalendo,” alisema Mhe. Lusetula.
Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Profesa Eliamani Sedoyeka, alimshukuru Mkuu wa Jeshi la Magereza kwa ushirikiano wa dhati uliopo kati ya chuo hicho na Jeshi la Magereza kupitia programu mbalimbali zinazowawezesha maafisa na askari kupata elimu itakayowasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao, hususan katika shughuli za urekebishaji wa wafungwa na mahabusu.
Aidha, Mrakibu wa Jeshi la Magereza (SP) Amos Atanas Maheri, ambaye ni miongoni mwa wahitimu wa shahada ya uzamili katika Chuo cha Uhasibu Arusha, ametunukiwa zawadi maalum baada ya kufanya vizuri zaidi katika masomo ya uongozi na utawala.