Duu kuwa na huruma ndugu yangu, hii tu ndogo hali iko hivi ikijaa elnino si itauwa watu wa kutosha na kuharibu miundo mbinu kibao? haiji kwa Jina la YESU.
Tulitangaziwa El nino, na mvua hii ya leo si dalili njema!
Kwa wale wanaowacheka waliojenga mabondeni nadhani hawako sahihi! Kujenga kunaangalia factors nyingi, kuna watu Dar ndio kwao hawana kwengine tena, na kama watanzania wengi wanaomiliki maeneo ya kawaida, inawezekana shamba lao ndio limekuwa option pekee ya kiwanja maana hivi vya halmashauri ni lazima uwe na jina zito la ukoo au ushikwe mkono au uwe na pesa ya ziada! Kama familia yenu amebakisha ardhi hata kama ni katikati ya MTO hapo itaingia tamaa tu ya kupunguza adha ya kodi!
Kuna mabondeni mengine yalikuwa low risk areas lkn ujenzi holela wa baadhi ya matajiri hadi wameziba, au kupunguza au kuelekeza kwengine mifereji mikubwa na mito midogo ya asili hivyo kuleta maafa ktk maeneo ambayo hayakuwa flood prone!
Pole kwa wote, cha msingi Hawa ni watanzania waliokosa fursa na hivyo kutake risk!
Poleni wote mliokumbwa na maafa, kwa bahati mbaya au kama dharura ktk ilr risky business mliyoamua kuitake!
Mnapaswa kujifunza wote kuwa usalama wako unavuka gharama nyingine zote! Tunajua kuwa hizi si mvua za kwanza kwenu, somo litaendelea kila misimu ya mvua itakapokuwa inawadia, wachache mtakaoelewa please mfanye uamuzi sahihi! Kuwa displaced kunaweza kuuma sana, lkn with time utazoea, fikiria kuhama sasa kama una uwezo!
Wapuuzieni wanaowakebehi, maana hata waliopata malaria walipaswa wafukuzwe hospitali kwanini hawakutumia net, wenye ukimwi watafaa kuitwa wazembe, kipindupindu wachafu, na kwa maana nyingine tufunge hospitali maana sehemu kubwa ya maradhi kuna sehemu makosa yalifanyika ndio mtu akapata ugonjwa!
Poleni once again!