passion_amo1
JF-Expert Member
- Dec 3, 2023
- 1,578
- 3,148
Wakuu habari za uzima?
Ndugu zangu wana JF kwa wale watu ambao wanaendaga club kupooza stress za wiki nzima nadhani watakuwa wameshakutana na hizi vurugu za watu wakibondwa na walinzi wa club kwa kusababisha vurugu.
Ndugu zangu mimi si mtu wa viwanja ila nina mashine zangu za kutengeneza popcorn(bisi) kwenye club mbili.
Kwa kweli wikiendi hiyo iliyoisha nilienda kuangalia maana nimemuweka kijana. Nilipofika mida ya saa nne usiku nilikuwa nyuma kabisa nikiangalia kijana akiwa anaendelea kupiga kazi yake.
Ikabidi nimuite muhudumu nimwambie aniitie jamaa anayetengeneza chipsi akaenda kumuita, jamaa kuja nikamuagiza chipsi huku nikiendelea kununua muda pale. Nikamuomba yule muhudumu aniitie kijana yule wa popcorn kule nyuma. Kwa kweli kijana hakujua kama nipo mule ndani akaja.
Kufika pale nikaongea nae nikamwambia vipi biashara akasema safi, basi ikabidi aulize kwa kushangaa. Nimeshangaa sana kukuona hapa kaka mkubwa leo, nikamwambia nimekuja tu kukuona.
Basi akawa anaitwa nikamuacha akaenda, kama dakika 15 baadae nikaona watu watatu wamemnyanyua jamaa juu akivuja damu, walipopita nae karibu na nje kutokea walimshusha na kuanza kumshushia kipondo. Aiseeeeh!!!
Yule jamaa alipigwa sana huku walinzi wakisema “wewe ukilewa unajifanya msenge huna akili kupanda juu ya meza na kuanza kugombana na watu”
Kwa kweli ilibidi nimuite aliyenihudumia chakula changu kulipa bili na kuondoka.
Nyinyi wamiliki wa ma club na ma bar makubwa embu muwafundishe hawa walinzi wasipige watu kwa namna ile.
Mlinzi kazi yake ni kutuliza ghasia na kama mtu anakuwa kirusi kwa kuondoa amani ya watu ndani humo inabidi atolewe nje na mara moja apelekwe polisi.
Kwa kile kipigo ni hatari sana, wamiliki wa ma club muwe makini na kujua hawa walinzi wanafanya nini wasije wakawaingiza kwenye matatizo.
Ndugu zangu wana JF kwa wale watu ambao wanaendaga club kupooza stress za wiki nzima nadhani watakuwa wameshakutana na hizi vurugu za watu wakibondwa na walinzi wa club kwa kusababisha vurugu.
Ndugu zangu mimi si mtu wa viwanja ila nina mashine zangu za kutengeneza popcorn(bisi) kwenye club mbili.
Kwa kweli wikiendi hiyo iliyoisha nilienda kuangalia maana nimemuweka kijana. Nilipofika mida ya saa nne usiku nilikuwa nyuma kabisa nikiangalia kijana akiwa anaendelea kupiga kazi yake.
Ikabidi nimuite muhudumu nimwambie aniitie jamaa anayetengeneza chipsi akaenda kumuita, jamaa kuja nikamuagiza chipsi huku nikiendelea kununua muda pale. Nikamuomba yule muhudumu aniitie kijana yule wa popcorn kule nyuma. Kwa kweli kijana hakujua kama nipo mule ndani akaja.
Kufika pale nikaongea nae nikamwambia vipi biashara akasema safi, basi ikabidi aulize kwa kushangaa. Nimeshangaa sana kukuona hapa kaka mkubwa leo, nikamwambia nimekuja tu kukuona.
Basi akawa anaitwa nikamuacha akaenda, kama dakika 15 baadae nikaona watu watatu wamemnyanyua jamaa juu akivuja damu, walipopita nae karibu na nje kutokea walimshusha na kuanza kumshushia kipondo. Aiseeeeh!!!
Yule jamaa alipigwa sana huku walinzi wakisema “wewe ukilewa unajifanya msenge huna akili kupanda juu ya meza na kuanza kugombana na watu”
Kwa kweli ilibidi nimuite aliyenihudumia chakula changu kulipa bili na kuondoka.
Nyinyi wamiliki wa ma club na ma bar makubwa embu muwafundishe hawa walinzi wasipige watu kwa namna ile.
Mlinzi kazi yake ni kutuliza ghasia na kama mtu anakuwa kirusi kwa kuondoa amani ya watu ndani humo inabidi atolewe nje na mara moja apelekwe polisi.
Kwa kile kipigo ni hatari sana, wamiliki wa ma club muwe makini na kujua hawa walinzi wanafanya nini wasije wakawaingiza kwenye matatizo.