M-wekeza kutoka Vodacom Riba 13%

M-wekeza kutoka Vodacom Riba 13%

sifahamu kama nisawa mkuu. Ila m-wekeza wao wanatoa 13% kwa mwaka hii inamaana kwa siku unaweza kupokea 1%-1. Something . Na hiyo faida haihesabiwi kwenye mtaji nimpaka mwezi uishe
Kwahiyo mwezi ukibisha ndio unapokea gawio lao Kwa pesa uliyowekeza
 
M -wekeza faida inajikusanya kila siku na itawekwa kwenye mtaji wako tarehe 2-5 ya mwezi.
 
Mkuu pesa niliweka Jana saa tano asubuhi ila mpaka Sasa hawajaweka riba yeyote kama ulivyoeleza wewe hapo maana kupo 00
Leo weekiend mkuu, iache hiyo pesa hadi siku za kazi uangalie salio. Its better kuangalia mtiririko unavyooenda baada ya kupokea riba ya mwezi then ugawanye kwa siku hela yako ilovyokaa huko M wekeza .
 
Leo weekiend mkuu, iache hiyo pesa hadi siku za kazi uangalie salio. Its better kuangalia mtiririko unavyooenda baada ya kupokea riba ya mwezi then ugawanye kwa siku hela yako ilovyokaa huko M wekeza .
Mkuu weekend huwa hawaweki riba
 
Mzee hawa jamaa inaonekana matapeli tu ngoja nikatoe pesa zangu aisee umesema faida inakua inawekwa Kila siku ila mpaka Leo sikua ya nne account inasoma faida 0
Ndio mkuu ni matapeli toa pesa yako na usiweke tena . Hili ndilo jibu ninaloweza kukupa 🤣
 
Kumbe ulikua unawapigia upatu matapeli Ili tutapeliwe aisee kumbe Kuna watu wanaroho mbaya sana humu au unalipwa mzee kutangaza wezi dah mungu kaniokoa nimesanuka mapema nishatoa pesa zangu zipo salama
Unahitaji elimu ya kutosha sana kuhusu uwekezaji. Wewe ni mgumu sana kuelewa mkuu
 
Kampuni ya vodacom &Sanlam imeanzisha mfuko wa uwekezaji ambapo mwekezaji atapata faida 13% kwa mwaka .

M-wekeza ni huduma inayomuwezesha mteja wa M-Pesa kuwekeza kima cha chini kabisa kuanzia TZS 1000 na zaidi kutoka M-Pesa na kupata faida nzuri bila gharama ya ziada.

Wateja wote wa M-Pesa wanaweza kujiunga na kusajili Akaunti za M-wekeza na kuanza kuwekeza Unachotakiwa kufanya ni kupiga *150*00#>Huduma za Kifedha>M-wekeza.

M-wekeza ni huduma ya kidigitali inayorahisha uwekezaji kiganjani mwako bila gharama za ziada.

Pia kupitia M-Wekeza mteja anaweza kuwekeza Kiwango chochote na kupata faida mpaka 13% endapo atawekeza fedha zake kwa mwaka mzima na unaweza pata taarifa ya kifedha ya uwekezaji wako muda wowote kiganjani mwako.

MAELEZO YA KINA

M-WEKEZA ni huduma inayomuwezesha Mteja wa M-Pesa kuwekeza kima cha chini kabisa kuanzia TZS 1000 na zaidi kutoka M-Pesa na kupata faida nzuri bila gharama ya ziada. M-WEKEZA inaweza kutumika na wateja wote wa M-Pesa wenye lengo la kuwekeza na kupata faida baada ya muda fulani. Kujiunga mteja utapiga *150*00# >Huduma za Kifedha>M-WEKEZA, faida za huduma hii M-WEKEZA ni huduma ya kidigitali inayorahisha uwekezaji kiganjani mwako bila gharama za ziada.
Pia kupitia M-Wekeza mteja anaweza kuwekeza Kiwango chochote na kupata faida mpaka 13% endapo atawekeza fedha zake kwa mwaka mzima na unaweza pata taarifa ya kifedha ya uwekezaji wako muda wowote kiganjani mwako.
Wateja wote wanaweza kufungua akaunti ya kuwekeza kwa ajili yako au kwa niaba ya rafiki mwenye namba ya Vodacom na mtumiaji wa M-Pesa. Hakuna makato yoyote ya mwezi au siku kwenye akaunti yako ya uwekezaji. Unaweza kuhamisha kiasi cha fedha au vipande kwenda kwenye akaunti nyingine ya rafiki bila makato ya ziada kupitia menyu ya M-WEKEZA. Fahamu kuwa wateja wote wana uwezo wa kupata taarifa ya kifedha muda wowote zinazoonesha , jumla ya pesa uliyowekeza, kiasi kilichopo ( Faida na Uwekezaji), taarifa za akaunti na kiasi kilichotoka na kuingia kwenye akaunti yako ya M-WEKEZA. Ahsante^JM

Hiyo 13% inakatwa kodi ya mapato?
 
Back
Top Bottom