Mwenyekiti wa kamati ndogo ya ulinzi wa uhuru wa dini wa Bunge la Marekani, bwana Chris Smith, wakati akifungua kikao cha mwaka, ameeleza kuwa Tanzania imerudi nyuma kwenye ulinzi wa uhuru wa dini.
Ameeleza kuwa mapadre kadhaa wa Kanisa Katoliki, akiwemo katibu wa TEC Fr Kitima, ama walitekwa au kushambuliwa na kujeruhiwa baada ya kukosoa vitendo vya ukiukaji haki vinavyofanywa na Rais Samia.
Mwenyekiti Smith amesema kuwa kiongozi wa Upinzani Tundu Lisu bado yupo gerezani kwa uonevu, balozi Humphrey Polepole bado hajapatikani tangu atekwe, huku watanzania wengine, kama siyo kwa mamia, basi ni maelfu wamepotezwa.
Mwenyekiti huyo ameendelea kueleza kuwa zaidi ya matawi 2,000 ya makanisa yenye uhusiano na Askofu Gwajima wa kanisa la uzima na ufufuo yalifungwa baada ya Adkofu Gwajima kukosoa utekaji wa watu, na kwamba waumini wake walipigwa kila Jumapili walipokusanyika kuabudu.
Mwenyekiti Chris Smith ameilaumu jamii ya kimataifa, akisema kwamba kama jamii ya kimataifa ingekuwa imesimama pamoja na viongozi wa dini waliokuwa wakikemea ukiukaji wa haki za binadamu nchini Tanzania, huenda mauji ya Oktoba 2025 yasingetokea. Akaeleza kuwa mauaji ya Oktoba 29, yalihusisha mauji ya watoto yatima ombaomba wa barabarani, akina mama wajawazito; na pia wahudumu wa hospitali za dini walilazimishwa kuingiza majeruhi kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti.
NB: Vitendo vya kiharamia vya utekaji watu, uporaji uchaguzi, na mauji ya watu baada ya uchaguzi bandia, vimemfanya Samia kunuka Ulimwengu mzima.
Kwa upande mwingine, watanganyika hawajawa pekee yao, jamii ya kimataifa, kwa nyakati tofauti na kwa namna tofauti, imekuwa ikionesha kuwa ipo na watanganyika wanaoendelea kuomboleza na kupaza sauti dhidi ya uongozi haramu na batili unaodhulumu haki za wananchi, ikiwemo haki ya kuishi.
Tusikate tamaa, tuendelee kupaza sauti, wakati unakuja ambapo nao maharamia wanaojiona hakuna anayeweza kuwafanya lolote hata wakitenda uovu mbaya kiasi gani, nao watalipia sawasawa na uovu wao.
Habari kamili kwa Kiingereza hii hapa:
Ameeleza kuwa mapadre kadhaa wa Kanisa Katoliki, akiwemo katibu wa TEC Fr Kitima, ama walitekwa au kushambuliwa na kujeruhiwa baada ya kukosoa vitendo vya ukiukaji haki vinavyofanywa na Rais Samia.
Mwenyekiti Smith amesema kuwa kiongozi wa Upinzani Tundu Lisu bado yupo gerezani kwa uonevu, balozi Humphrey Polepole bado hajapatikani tangu atekwe, huku watanzania wengine, kama siyo kwa mamia, basi ni maelfu wamepotezwa.
Mwenyekiti huyo ameendelea kueleza kuwa zaidi ya matawi 2,000 ya makanisa yenye uhusiano na Askofu Gwajima wa kanisa la uzima na ufufuo yalifungwa baada ya Adkofu Gwajima kukosoa utekaji wa watu, na kwamba waumini wake walipigwa kila Jumapili walipokusanyika kuabudu.
Mwenyekiti Chris Smith ameilaumu jamii ya kimataifa, akisema kwamba kama jamii ya kimataifa ingekuwa imesimama pamoja na viongozi wa dini waliokuwa wakikemea ukiukaji wa haki za binadamu nchini Tanzania, huenda mauji ya Oktoba 2025 yasingetokea. Akaeleza kuwa mauaji ya Oktoba 29, yalihusisha mauji ya watoto yatima ombaomba wa barabarani, akina mama wajawazito; na pia wahudumu wa hospitali za dini walilazimishwa kuingiza majeruhi kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti.
NB: Vitendo vya kiharamia vya utekaji watu, uporaji uchaguzi, na mauji ya watu baada ya uchaguzi bandia, vimemfanya Samia kunuka Ulimwengu mzima.
Kwa upande mwingine, watanganyika hawajawa pekee yao, jamii ya kimataifa, kwa nyakati tofauti na kwa namna tofauti, imekuwa ikionesha kuwa ipo na watanganyika wanaoendelea kuomboleza na kupaza sauti dhidi ya uongozi haramu na batili unaodhulumu haki za wananchi, ikiwemo haki ya kuishi.
Tusikate tamaa, tuendelee kupaza sauti, wakati unakuja ambapo nao maharamia wanaojiona hakuna anayeweza kuwafanya lolote hata wakitenda uovu mbaya kiasi gani, nao watalipia sawasawa na uovu wao.
Habari kamili kwa Kiingereza hii hapa: