Wimbo huu umepigwa DDC Mlimani Park ila sikumbuki mwimbaji.
Na huyu nani? Bendi gani?
Baba Anna eee
Ni lini utarudia nyumbani
Uje uwaone watoto wako
Uje uwaone baba na mama kwenu.......
(repeat)
[Lead]
Najua kazi nyingi zimekuzonga...
Huko uliko nako ni mbali sana baba Anna eeeee
Hata hivyo ufanye kila njia.....kwani kuna matatizo matatizo matatizo kwenu eeee
(Chorus)
[Wote]
Watoto wako wanakukumbuka...kila siku haweshi kukuuliza
Na mama naye ananung'unika....kwani miaka mingi imepita
Baba amekuwa mtu mzima...hawezi kuhangaika huku na kule
Kwa hiyo bwana ufanye haraka...matatizo yametuzidi mno yooooo
Fanya uje eeee
[Lead]
Leo nasema aaa......mimi naomba.....niko peke yangu.....
Maisha ya tabu.....kila kitu ni pesa.....chakula ni pesa....
Mavazi ni pesa.....ufanye haraka...bwana naomba eee
[Wote]Fanya uje eeee
hivi wapi nitapata lyrics za nyimbo za kiswahili kama Siwema,Kifo by Dr Remmy Ongala,Jojina na zile nyimbo za sikinde pleaseeeee!.
xoxo
Kelly01
Hapo najua kuna sehemu sehemu nitakuwa nimechapia, si unajua nyimbo hazina CD yenye booklet ya lyrics wala website ya fanbase, kwa hiyo unakumbuka ulivyosikia tu.
Halafu miaka kibao imepita.
hivi wapi nitapata lyrics za nyimbo za kiswahili kama Siwema,Kifo by Dr Remmy Ongala,Jojina na zile nyimbo za sikinde pleaseeeee!.
xoxo
Kelly01
- Kaulimtu mkuu acha hizi za kuchapia chapia katika zero tolerance nation, bwa! ha! ha! ha!
Es!
Kelly na wengine wote mliochangia nawashukuru kwa kutupeleka miaka ile ambapo muziki ulikuwa muziki.
Nitashukuru sana kama kuna atakayeweza kuniwekea maneno ya wimbo uliowahi kuimbwa na Fresh Jumbe enzi hizo ( nadhani late 80s) akiwa na Mlimani Park unaitwa " "Conjesta" - wimbo huu unaimbwa siku hizi na In Afrika Band ( kina Roy, Bob Rudala, Biz man na wengineo ) na wanaupiga vizuri mno kama kopi.
ninakumbuka baadhi ya maneno kama ifuatavyo:
Nimetembea, pande za dunia, mashariki na magharibi,
Sijapata kumpata mwingine mwenye mapenzi ya kweli....
Na sasa kwako mpenzi, nimefikia ukingoni ....
nitashukuru sana kama mwenye maneno yote atuwekee hapa.
Sitegemei kupenda mwingine tena zaidi yako wee Konjestaaaa...
Mtoto mwenye imani, ooh jesta nimeamua kukupenda wee pekee duniani
mtoto mwenye imani, ooh jesta nimeamua kukupenda wee pekee duniani.
Mapenzi mazito, sioni mwingine,wala sisikii la yeyote yule
Haya kazi kwako