Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Aende huko Chadema haya mambo ya ku beep yanampotezea muda


Anaweza pia kuachana na siasa hakuzaliwa awe kwenye vyama, kama ni msomi afanye kazi za professional yake mchango kwa taifa utaonekana!
 
Anaweza pia kuachana na siasa hakuzaliwa awe kwenye vyama, kama ni msomi afanye kazi za professional yake mchango kwa taifa utaonekana!
Masa,
Nilmegundua siasa ni lazima mtu kuwa involved.

Hii ya kukaa hapa JF tu na kuweka post zetu bila kushiriki sisi wenyewe, hakuna mabadiliko tunayotaka yatakayotokea.

Ndio sababu JMK alikuwa anajidanganya kwa kusema kuwa kelele za mlango hazimzuii kulala. Alimaanisha kuwa hata tupige kelele lakini kama we are not involved katika siasa zenyewe, haisaidii kitu.

Ni lazima Wilfred aendelee kushiriki siasa.

FYI nyota yake kule Bukoba bado inang'ara. Akiacha kuji involve katika siasa atakuwa amewa let down wapenzi wake kule Bukoba.

Matokeo turn out ya wapiga kura katika jimbo la Bukoba mjini watapungua sana maana naamini, narudia naamini wengi watajikata kutopiga kura.

Na hii itakuwa ni kwa faida ya sisi M......
 
Ni lazima Wilfred aendelee kushiriki siasa.

FYI nyota yake kule Bukoba bado inang'ara. Akiacha kuji involve katika siasa atakuwa amewa let down wapenzi wake kule Bukoba.

Matokeo turn out ya wapiga kura katika jimbo la Bukoba mjini watapungua sana maana naamini, narudia naamini wengi watajikata kutopiga kura.

Na hii itakuwa ni kwa faida ya sisi M......

Mchukia Fisadi,
Kuna usemi unathibitisha maneno yako. Usemi huu unapatikana sana kwenye references za political Science kuwa "A Human Being is a Politician by Nature"

Sorry, check your PM please!
 
Kweli hata mi nimemiss sana michango yake hapa,, sijui amekumbwa na nini?

Tumsubilie aje atwambie Simba wa Yuda maalimu Seif alivo shiriki kumkata bogi mpambanaji Lwakatare kwa sababu za nyuma ya pazia!
 
Sitaki niwe bias katika hili suala la Bw Wilfred na wenzake wa CUF. Ninadhani tukipata maelezo ya upande wa pili tutakuwa tumepata mwanga mzuri zaidi wa sakata lake la uongozi.

But to chip in while waiting to hear much from the other side, ninaona kuwa Mh Wilfred alisahau kuwa uongozi ni dhamana tu na wala si kitu cha kulalamika hasa pale unapoukosa kwa mujibu wa taratibu halali. Nikisoma mawazo yake alitegemea kuwa ataendelea kuwa kiongozi bila ya kujali ukomo na kupisha wengine kuleta fresh idea. Yeye mwenyewe anakiri kuwa hali ya kisiasa kwa CUF upande wa bara si nzuri na amekuwa katika Uongozi wa juu kwa kipindi cha kutosha. Nafikiri ni vema akaondoa kinyongo na badala yake aendelee kuwaomba wakuu wake wampatie kile ambacho ni halali yake.
Lakini hata hivyo ametoswa wakati mbaya sana kwani ana kesi ambayo akishindwa hatakuwa nafasi ya 'kulazimisha' CUF ilipe gharama za kesi, nadhani hili CUF ndiyo labda limewaogopesha.

Vilevile, katika maelezo ya Mh Wilfred sijaona mahali popote akiutaka uongozi wa CUF uanzishe uchunguzi rasmi wa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za chama dhidi yake. Kitendo cha kulifumbia macho suala hilo inaonesha weakness kubwa katika uwajibikaji wake aidha na yeye 'anafunika kombe mwanaharamu apite' na kuhakikisha kuwa anakaa chini ya miguu ya wakuu wake ili yaishe.
 
mhhh....kweli inasikitisha huyu bwana nakumbuka enzi za mageuzi yanaanza alivyojitoa mhanga huku wanachi wa bukoba wasielewa wakimzomea na kuonekana chizi.............nfikiri ni muda muafaka wa kuja chadema
 
Sitaki niwe bias katika hili suala la Bw Wilfred na wenzake wa CUF. Ninadhani tukipata maelezo ya upande wa pili tutakuwa tumepata mwanga mzuri zaidi wa sakata lake la uongozi.

But to chip in while waiting to hear much from the other side, ninaona kuwa Mh Wilfred alisahau kuwa uongozi ni dhamana tu na wala si kitu cha kulalamika hasa pale unapoukosa kwa mujibu wa taratibu halali. Nikisoma mawazo yake alitegemea kuwa ataendelea kuwa kiongozi bila ya kujali ukomo na kupisha wengine kuleta fresh idea. Yeye mwenyewe anakiri kuwa hali ya kisiasa kwa CUF upande wa bara si nzuri na amekuwa katika Uongozi wa juu kwa kipindi cha kutosha. Nafikiri ni vema akaondoa kinyongo na badala yake aendelee kuwaomba wakuu wake wampatie kile ambacho ni halali yake.
Lakini hata hivyo ametoswa wakati mbaya sana kwani ana kesi ambayo akishindwa hatakuwa nafasi ya 'kulazimisha' CUF ilipe gharama za kesi, nadhani hili CUF ndiyo labda limewaogopesha.

Vilevile, katika maelezo ya Mh Wilfred sijaona mahali popote akiutaka uongozi wa CUF uanzishe uchunguzi rasmi wa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za chama dhidi yake. Kitendo cha kulifumbia macho suala hilo inaonesha weakness kubwa katika uwajibikaji wake aidha na yeye 'anafunika kombe mwanaharamu apite' na kuhakikisha kuwa anakaa chini ya miguu ya wakuu wake ili yaishe.

Kwa hapo juu naona nimeelewa tofauti. Hakukataa wala hapingi kupigwa chini ila utaratibu uliotumika. Naamini alistahiri kupewa walau taarifa mapema ili kuacha hilo swali la kwa nini wanamfanyia surprise. Hilo nadhani ni tatizo kubwa sana. Kwa sababu kama angekuwa ameelezwa toka mwanzo basi kusingekuwa na sababu ya yeye kushangaa! Kwa ngazi aliyokuwa nayo si vizuri kuacha kumweleza hata kama kitu hicho ni kibaya kwake. Na hili ndilo tatizo la viongozi wetu. Yaani hawana ubavu wa kumwambia mwenzao anapokosea. Na ndiyo maana huweza kuacha kufikiria kuwa hapo kulikuwa na mizengwe fulani (conspiracy).
 
Chukulia hawa CUF ndo wangekuwa wameshika dola, ikiwa wanaweza kumtendea hivi Naibu Katibu mkuu. Kwa mwananchi wa kawaida
 
Ndio maana itachukua muda kwa vyama vya upinzani kuaminika kuongoza nchi.Vingi bado havieleweki eleweki. Ni kama NGO za watu fulani hivi
 
Ni bahati mbaya sana kwamba TLP hawana ruzuku ya kutosha kum-bailout, lakini kama angejiunga huko angetengeneza timu nzuri sana na Lyatonga!
Kwa upande mwingine, ni haki ruzuku ya chama (Pesa ya walipakodi) kutumika kulipia kesi binafsi za wanachama? Kulipa pensheni za wanachama wastaafu kama Mloo alivyokuwa akilipwa 500,000/= kwa mwezi? Just curious!
 
Kwa hapo juu naona nimeelewa tofauti. Hakukataa wala hapingi kupigwa chini ila utaratibu uliotumika. Naamini alistahiri kupewa walau taarifa mapema ili kuacha hilo swali la kwa nini wanamfanyia surprise. Hilo nadhani ni tatizo kubwa sana. Kwa sababu kama angekuwa ameelezwa toka mwanzo basi kusingekuwa na sababu ya yeye kushangaa! Kwa ngazi aliyokuwa nayo si vizuri kuacha kumweleza hata kama kitu hicho ni kibaya kwake. Na hili ndilo tatizo la viongozi wetu. Yaani hawana ubavu wa kumwambia mwenzao anapokosea. Na ndiyo maana huweza kuacha kufikiria kuwa hapo kulikuwa na mizengwe fulani (conspiracy).

DarkCity,
Je haiwezekani kuwa Mh Wilfred amepewa lesser punishment kutokana makosa aliyoyafanya kwa vile ana mchango mkubwa katika CUF?

Maelezo ya Mh haoneshi tuhuma za ubadhirifu kama ndiyo tatizo kubwa la sakata nzima? Je huoni kwamba ingekuwa busara kwa Mh akajikita zaidi katika kusafisha jina lake dhidi ya tuhuma za ubadhirifu.

Ninawapa benefit of doubt uongozi wa CUF kuwa wana hoja ya msingi katika hili. Pili, uamuzi wa kuarifiwa au kutoarifiwa inategemea na hali tete iliyopo au nguvu na ushawishi wa Mh, kwa hiyo njia yeyote inaweza kutumika ili kudhibiti utulivu na amani ndani ya chama.
 
Mhe Lwakatare, pole sana ndugu yangu kwa masaibu hayo, ndiyo dunia hiyo. Mwenzio Mrema kule TLP amekiri wazi jana kuwa anakubaliana kabisa na CCM kuwa ''wapinzani ni mapaka tu!'', hawataweza kamwe kushika dola.

Kama ndivyo mnavyoongozana kwenye chama chenu, nani atathubutu kuwapa dola muitapanye kihivyo? Kumbe basi mwalimu Nyerere (Mwenyezi Mungu amlaze pema) alikuwa sahihi sana pale alipotamka hadharani kuwa hayuko tayari kuacha nchi yake inachukuliwa na ''mijibwa'' ya upinzani!

Kwa mwendo huu, wapinzani wataendelea kuwa wabwatukaji tu, lakini dola hawatoishika katu, hatutothubutu kuwapa!
 
Hivi huyu Mheshimiwa si tulitangaziwa (na Omutwale) kua atajiunga na jamvi letu hili jana mchana imekuaje? yumo humu?
 
Ni bahati mbaya sana kwamba TLP hawana ruzuku ya kutosha kum-bailout, lakini kama angejiunga huko angetengeneza timu nzuri sana na Lyatonga!
Kwa upande mwingine, ni haki ruzuku ya chama (Pesa ya walipakodi) kutumika kulipia kesi binafsi za wanachama? Kulipa pensheni za wanachama wastaafu kama Mloo alivyokuwa akilipwa 500,000/= kwa mwezi? Just curious!

ndio ni haki
 
Ni bahati mbaya sana kwamba TLP hawana ruzuku ya kutosha kum-bailout, lakini kama angejiunga huko angetengeneza timu nzuri sana na Lyatonga!
Kwa upande mwingine, ni haki ruzuku ya chama (Pesa ya walipakodi) kutumika kulipia kesi binafsi za wanachama? Kulipa pensheni za wanachama wastaafu kama Mloo alivyokuwa akilipwa 500,000/= kwa mwezi? Just curious!
Thubutu, Lyatonga yupi?Huyu mzee wa Kiraracha? Hapo umempoteza Lwakatare kwa ushauri huo.
 
Vyama vyote vya upinzani vimeshindwa kuonyesha demokrasia ya kweli ndani ya vyama hakuna chama cha upinzani kinachoweza kujidai hakina mizengwe katika uendeshaji wake. najiuliza hivi itakuwaje siku wakipewa dola.CUF ni chama kilichokosa demokrasia ya kweli hata katika chaguzi za viongozi wake.Professor Safari anaanda kitabu najua atatueleza mengi yaliyojificha jinsi alivyofanyiwa zengwe na Professor Lipumba na maalim Seif.

CHADEMA nako kulikuwa na zengwe la Chacha Wangwe na jinsi ruzuku inavyotumiwa vibaya.Pamoja na wabunge wa viti maalumu kutoka sehemu moja [Kilimanjaro]
 
Wakuu nimejaribu kumsoma huyu bwana na maandiko yake mengi lakini sijaona chochote cha kusema kinanistua... sio kwamba nakuwa mean lakini nimeona amelalamika zaidi ya kusema kile ambacho anafikiri kitarekebisha hali iliyomtokea.Halafu sehemu kubwa ya andiko lake imenifanya kuona kuwa huyu bwana he is selfish sana yaani ni kujiongelea yeye tu na matatizo yake.Nani amemwambia kuwa kuendesha VX ndio kuonekana nadhifu?Hii thinking yake kuwa yeye ana matatizo na kuamua kurudia rudia kua aliacha kazi kwa notisi ya masaa 24 na kuachia mishahara yake (As if hiyo mishahara ilikua ni mamilioni!!) imenifanya nimshangae sana huyu bwana.

Ni mawazo yangu tu
 
Back
Top Bottom