Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

huyo lazima aondoke, amecheza na Maalim Seif. Yeye alitarajia apige kelele za CUF kutumia fedha nyingi kujijenga Zanzibar pekee badala ya bara halafu wamuache. Ndio maana pamoja na wajumbe wa bara kumpa kura nyingi na kumfanya aongoze kati ya waliopigiwa kura kwenye baraza la uongozi na kumzidi hata Haji Duni bado ametoswa!. Maalim Seif alimwambia wazi Lipumba asipendekeze jina lake. Huyu hakugombea akashindwa bali jina lake halijapendekezwa kabisa na mwenyekiti wao kwa kushauriana na katibu mkuu. Kimbelembele chake cha kupinga upemba ndani ya CUF ndio kimemponza. Kila siku ilikuwa kulilia tu chama hicho kijijenge bara kumbe wenzake wana ajenda nyingine kabisa

...........ndiyohiyo

Naweza kukubaliana na wewe katika hili Mkuu Habarindiyohiyo.
Ajenda za CUF ni Zanzibar tu ukija na mkakati mwingine tofauti na maalim Seif & co wa kutaka kujitanua huku bara lazima watakukimbiza.Bwana Lwakatare kajimaliza mwenyewe kukimbilia chama cha wapemba angemwuliza James Mapalala yaliyomkuta.
 
Aliyewahi kuwa mbunge wa bukoba mjini kwa tiketi ya cufna naibu katibu mkuu, bwana lwekatare inasekana yuko kwenye hatua za mwisho kujiunga na chadema.

Hali hiyo imekuja baada ya mkutano mkuu wa cuf uliofanyika mwishoni wa february kuchagua viongozi mbali mbali na baada ya hapo kuna nafasi za kuteuliwa, bwana lwekatare alikosa nafasi yake ya naibu katibu mkuu.

Lwekatare amekosa uvumilivu wa mzee kawawa wa kupanda na kushuka kimadaraka?

Hivi Lwakatare anataka kuhamia Chadema kwa sababu ipi mojawapo?

1. Kuunganisha nguvu kwa ajili ya 2010
2. Kakosa madaraka CUF au
3. Itikadi yake imebadilika na kushabihiana na ya Chadema?
 
Hivi Lwakatare anataka kuhamia Chadema kwa sababu ipi mojawapo?

1. Kuunganisha nguvu kwa ajili ya 2010
2. Kakosa madaraka CUF au
3. Itikadi yake imebadilika na kushabihiana na ya Chadema?

Majibu 1, 2 na 3 yote ni sawa. :)
 
Ukisoma vizuri alama za nyakati, CUF imepoteza mvuto wa kitaifa na kimkoa. Mgombea mtarajiwa yeyote mwenye kupiga hesabu vizuri hata kama anao mtaji wa wapiga kura, kugombea kupitia CHADEMA ndiyo turufu yenye uwezekano mkubwa wa kushinda ubunge.
Hata Urais mgombea wa Chadema atashinda kiulaini,tunasubiri tu Chadema watuletee mgombe mzuri na waachane na Zitto type.
 
CUF hawana bao huku bara kwahiyo kwa Lwakatare kuhamia CHADEMA ni pigo kubwa kwao!! Hawa jamaa wa CUF wanawatumia tu hawa wakina Lipumba kuwa wanapresence huku bara lakini moyo wao na akili zao ziko Pemba na ndio maana wanamaono ya siku moja kuwa na Jamhuri ya Pemba!! Hata huyo Lipumba [MZIGO mzito mpe mnyamwezi siku si nyingi watamtema] Angalia jinsi walivyomdhalilisha Prof. Safari kwenye uchaguzi wao; mtu aliyejitolea kutetea kesi zao mpaka akapoteza ajira yake; that is CUF for you, only good kwa wapemba!!
 
Rwakatare alipokuwa CUF alikifanya chama hicho kisionekane cha kidni (cha kiislam), sasa kama akijitoa ndio kitakuwa chama cha kidini haswa. CUF inaelekea kuzimuni

Kama CUF Chama Cha kidini CCM itakuwa Cha Mitume ? Yaani mnakokotwa na mawazo finyu ,hebu ipangeni safu ya CCM kamati kuu tuone ,ipange Chadema kuanzia juu mpaka mkiani ila kama mnaiimbia CUF nyimbo hiyo basi endeleeni mpaka itakaposhika kasi hapo ndipo patakuwa patamu.
 
Hii move si nzuri kwa Bwana Lwakatare kwasababu kujitoa kwake CUF na kujiunga na CHADEMA itakuwa ni kutafuta cheo na si kutetea maslahi ya wananchi.Kwanini Lwakatare ajitoe CUF baada ya kuenguliwa katika safu za uongozi wa juu.
CUF ni chama chenye nguvu zaidi Zanzibar kuliko huku bara,maamuzi mengi makubwa yanafanywa na viongozi wajuu kutoka Zanzibar pengine Lwakatare kaonekana hana manufaa tena kwa chama.
bwana we usipotoshe watu, CUF wanafanya maamuzi yao kupitia taasisi za chama ambazo zinawakilishwa na wajumbe waliochaguliwa katika utaratibu wa kichama mfano baraza kuu la taifa, suala la kufanyika maamuzi na watu fulani halipo kabisa katika CUF na ndo maana wale wasiopenda utaratibu huu wa kufikia maamuzi wa uwazi usiokuwa na mizengwe wanashindwa kuyavumilia haya
 
wewe ndo kabisa unaelekea kushoto, angalia posti vizuri sababu ya Lwakatari ya kutaka kuhama CUF si Maalim Seif wala nini, tatizo ni madaraka, CUF ni chama cha mageuzi, kinakwenda na wakati na hakiogopi kufanya mageuzi kama yanafaida na mustakabali wa chama na maendeleo ya demokrasia ya nchi, we tazama wapenda madaraka wanavyoharibu harakati za upinzani nchini, ambao kwa kweli licha ya uchache wake bungeni kazi wanayofanya ni kubwa na watanzania tunaona kwa macho,ni muda gani wanaleta chokochoko katika vyama vya upinzani utakuta sana wakati ule mikutano mikuu ya kitaifa ya vyama hivi inapokuja na mageuzi yanayowagusa, ndo katika mwendo huu watu kama akina Tambwe wakafukuzia CCM kunako uzwa na kununuliwa madaraka na vyeo kwa fedha, na agulia tu walipofika huko wameanza na mkakati upi kama si kujikweza, kwa kweli wanasiasa hawa hawahitajiki katika zama hizi za ujenzi wa demokarasia tz
 
cuf hawana bao huku bara kwahiyo kwa lwakatare kuhamia chadema ni pigo kubwa kwao!! Hawa jamaa wa cuf wanawatumia tu hawa wakina lipumba kuwa wanapresence huku bara lakini moyo wao na akili zao ziko pemba na ndio maana wanamaono ya siku moja kuwa na jamhuri ya pemba!! Hata huyo lipumba [mzigo mzito mpe mnyamwezi siku si nyingi watamtema] angalia jinsi walivyomdhalilisha prof. Safari kwenye uchaguzi wao; mtu aliyejitolea kutetea kesi zao mpaka akapoteza ajira yake; that is cuf for you, only good kwa wapemba!!
ccm je?
 
Quote: Kibunango
Zagazaga hilo halina nafasi CCM

Unaongelea hii CCM iliyompokea na kumpa madaraka HIZA TAMBWE ama nyingine?



Ni CCM Asili na siyo ile Mtandao...

Mbona CCm asilia alizikwa nayo Mwl Nyerere ama kafufuka?
 
Rwakatare alipokuwa CUF alikifanya chama hicho kisionekane cha kidni (cha kiislam), sasa kama akijitoa ndio kitakuwa chama cha kidini haswa. CUF inaelekea kuzimuni

Kama kuna chama cha kidini au chenye sura ya kidini ni SISI M. hawa piga ua ni dini tupu. Hasa ile dini moja inayotawala huko visiwani. Imemkamata sultani hana pa kujigeuzia.
 
Wanachama na madiwani wake wa Cuf Bukoba atahama nao? kama akikosa cheo Chadema itakuwaje?Chacha WANGWE alikwenda Chadema akijua atafanya mabadiliko hali ikawa tofauti jee Lwekatare ametafakari hayo yote?
bora apiganie ubunge tena 2010 kwani akihamia Chadema kuna wanachama hawatamfuata atapoteza kura zake.kama ana uhakika wa ubunge basi ni bora kuliku unaibu katibu wa Cuf
 
CUF upemba umezidi na wanaitikadi za KISULTAN kabisa, kipindi Lwakatare alijaribu kubadilisha mfumo wa kisultani lakini kutokana na nguvu ya wengi ameshindwa kukiweka kiwe chama halali siasa. Ukiangalia wafuasi wengi wa CUF ni wale waisilam wajaidina na wapemba wengi hata upande wa visiwani CUF inanguvu zaidi Pemba kuliko UNGUJA hayo yote yanaonyesha CUF ni chama dini na ukabila.

Kwahiyo Lwakatare akiondoka CUF nisawa kabisa kwani juhudi zake za kukifanya chama kiwe cha kisiasa badala ya udini na ukabila zimeonekana.
 
Lwakatare hama tuu CUF haina msimamo,angalia Lipumba anaunga mkono ununuzi wa mitambo mitumba.
 
Lwakatare hama tuu CUF haina msimamo,angalia Lipumba anaunga mkono ununuzi wa mitambo mitumba.
Lipumba ni hovyoooooo kabisa u pofesa wake sijui kaupatia wapi?

........wanasiasawa tz hawafai kweri......muoneni Zitto leo kapewa bahasha kaota makucha.....na huyu lwakatare hata akiamua kuamia Republican is up to him.....
 
Lipumba ni hovyoooooo kabisa u pofesa wake sijui kaupatia wapi?

........wanasiasawa tz hawafai kweri......muoneni Zitto leo kapewa bahasha kaota makucha.....na huyu lwakatare hata akiamua kuamia Republican is up to him.....
Ni kweli kabisa sijui Elimu ina faida gani kama Wasomi ndio wanaoihujumu nchi,hawana mchango wowote wa manufaa kwa nchi.Nafikiri ndio maana Madagascar wamempa nchi DJ Rajolina baada ya kuona wasomi hawana jipya ila wanatumia elimu kuiibia nchi.Watanzania tuamke tuilinde nchi yetu.
 
Back
Top Bottom