Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Ni kweli kabisa sijui Elimu ina faida gani kama Wasomi ndio wanaoihujumu nchi,hawana mchango wowote wa manufaa kwa nchi.Nafikiri ndio maana Madagascar wamempa nchi DJ Rajolina baada ya kuona wasomi hawana jipya ila wanatumia elimu kuiibia nchi.Watanzania tuamke tuilinde nchi yetu.


Na wewe unataka watz tumpe Nchi DJ Mbowe?...
 
Na wewe unataka watz tumpe Nchi DJ Mbowe?...

Achana naye huyo. Haoni kabisa jinsi Kikwete( ambaye mnamuita msanii na mcheza dansi) anavyoweka mambo sawa. Nyie pigeni kelele tu kuhusu Dowans, 2010 Kikwete yeye ni kueleza tu sekondari kata, zahanati na jinsi wanawake walivyopewa nafasi. Halafu mtaanza kulalamika tena akishinda kwa kishindo.

..........ndiyohiyo
 
Cuf ni chama cha kipemba hakina dira wala mwelekeo kila siku wanalilia maalim Seif awe rais zanzibar kitu ambacho hakiwezekani.Lwakatare inafaa aondoke CUF mapema lakini kitu ninachohofia ni uko unakotaka kwenda.
 
Na wewe unataka watz tumpe Nchi DJ Mbowe?...
Madagascar wamempa DJ juzi.labda ni habari njema kwa Mbowe kwani atakuwa DJ wa pili duniani kuwa Rais wa nchi.
 
Wakuu nimepokea picha hizi toka Bukoba na kuambiwa kwamba Lwakatare amefika Bukoba na kulakiwa na umati mkubwa wa wafuasi wake na kuhutubia mkutano mkubwa sana tangu 2005. Nasikia hii walikuwa wana beep SISI M waliokuwa wanadhani huyu bwana kaisha kisiasa kwa sababu mshindani wake kwanza ni waziri mtoto au niseme mtoto wa waziri na isitoshe alishawapotosha wana SISI M kwamba alimshinda mahakamani na anamdai pesa nyingi. Zaidi huyu waziri mtoto ni mfadhili mzuri wa shughuli za kijamii lakini ni ajabu bado Lwakatale kaonekana ana wafuasi kibao. Wengi ni walala hoi na inasemekana huyu mpinzani wake mkuu wafuasi wake wengi ni wafanyabiashara au kwa jina lingine matajiri.
Haya nawashushia mambo.
Ukweli ni kwamba SISI M bado wana shughuli 2010. Wasidhani jimbo la Bukoba mjini ni rahisi tena. Lazima waje na mbinu kali ambazo alitumia Hon Obama.


IMG_5499.jpg

IMG_5501.jpg

IMG_5502.jpg

IMG_5503.jpg

IMG_5507.jpg

IMG_5509.jpg

IMG_5510.jpg

IMG_5510.jpg

IMG_5511.jpg

IMG_5514.jpg

IMGP7740.jpg

IMGP7741.jpg
 
njaa za viongozi wetu wala hatutashangaa sana
 
Du kazi kweli kweli......! Ingefurahisha zaidi tungepata pia maelezo (independent) kutoka upande wa pili i.e Mwenyekiti, Naibu katibu mkuu, Katibu mkuu etc...ili na sisi mchango wetu usije ukawa biased unnecessarily!

Assuming kwamba maelezo ya upande wa pili yanaoana na haya, sijapenda Udictator uliotumika katika kumuengua huyu jamaa katika post yake ya Unaibu katibu mkuu! Pia sijapenda na ahadi hewa za kumlipa mafao yake kama ilivyoelezwa!

Vyama vya aina hii vinaweza kuwa na kazi kubwa sana kuhakikisha kuwa sera zake zinakubalika na wananchi walio wengi!
 
Mmmhhhh!!!! hizi siasa za Tanzania zinasikitisha sana. Ujumbe wa mheshimiwa Lwakatare ni somo tosha.

Kwanza inaelekea hivi vyama pamoja na viongozi wake wote akiwemo Lwakatare mwenyewe wameondoka na mambo ya CCM na bado wana mawazo kama CCM.

Huwezi kumwondoa mtu nafasi kubwa kama hiyo bila kumwambia kwanza mpaka anapata surprise kwenye kikao chenyewe. Huo usomi wa akina prof. Lipumba unaongozana na busara gani?

Kwa vijana mnaotaka kujiunga na siasa hilo ni somo kubwa kweli kweli. Hivyo vyama karibu vyote vina wenye navyo. Ni bora kuutumia muda wako vizuri kusaidia wananchi huko wilayani kuliko kushikana na hii mizee ambayo utafikiri bado iko kwenye era za TANU.

Badala ya kuongoza mabadiliko kwa kutenda haki, wanashindwa hata kuwatendea haki watu wanaoshinda nao kila siku.

Pili hili suala la kutegemea sana malipo kutoka kwenye vyama linatumaliza kabisa. Ndio maana kuna migogoro mingi, kila mtu anataka afaidi kidogo sehemu ya hiyo ruzuku. Lwakatare kama naibu katibu mkuu kweli kuna haja ya kutegemea gari la chama? Mfano aliotumia wa Nyerere na UDA ni muendelezo huo huo wa mawazo ya wanasiasa wa Tanzania. Kwani kuondoka kwa kupanda UDA kuna matatizo gani? Prof. Mmari alipopanda UDA mbona hakulalamika? Uki screw kazini unataka usindikizwe na Benz? Sehemu zote hata kwenye private companies za maana, unanyang'anywa kila kitu hapo hapo na kuonyeshwa mlango.

Ndio maana hizi nchi zetu haziwezi kuendelea shauri viongozi wetu na wasomi wetu wengi wana mawazo duni sana. Wanaweza kuwa ni wasomi waliobobea lakini fikra zao juu ya mambo mbalimbali ni mbovu!
 
CUF inapaswa kufanya mabaduiliko makubwa sana katika mfumo wake wa uongozi, la sivyo, inaelekea kuzimu
 
Hawa nadhani kama hali ni hii, basi ni kushney

lakini napata picha ye hegemony ya watu wa zanzibar ndani ya hiki chama kiasi watu wa bara wanaonekana wapo wapo tu.

Hivi viongozi wakuu wa CUF wasipokuwa wao, hakuna wengine...nina mashaka kama ndo hawa hakuna jipya

Na hili CCM watalipenda kweli, 2010 mteremko tu. 2015 wanatuwekea mwingine mambo msuano....upinzani usahau, am sorry
 
Naona kuna tatizo la kiswahili katika matumizi ya "L" na "R". Ninavyoelewa kuna kujiuzulu na si kujiuzuru, kuna kukithiri na si kukithili - of course inafuatana mhusika anatoka sehemu ama mkoa gani. Je, jina hasa ni Lwakatare, Rwakatare, Lwakatale au Rwakatale ?
Mimi ni mtani wako.
 
Naona kuna tatizo la kiswahili katika matumizi ya "L" na "R". Ninavyoelewa kuna kujiuzulu na si kujiuzuru, kuna kukithiri na si kukithili - of course inafuatana mhusika anatoka sehemu ama mkoa gani. Je, jina hasa ni Lwakatare, Rwakatare, Lwakatale au Rwakatale ?
Mimi ni mtani wako.


Duh, Mag3 usingesema kuwa ni mtani wake nilikuwa najiuliza imekuwaje leo manake sio kawaida yako mkuu!

Ni kweli haijahaririwa il yatumike maneno ya kiswahili sanifu yameathiriwa na lugha ya mama naona

By the way hivi yupo hapa hapa jamvini eeh?
 
Sounds to be a mature leader. But we need to hear the other side as well.
 
I always admire u for ur wisdom, haukurupuki lakini unatumia njia ambayo ni ya haki na hata mwenye nia ya kupakaza anakosa fursa ya kufanya hivyo.

Haki sawa unayoipigania ndani ya CUF si kwa faida yako tu bali italeta heshima na kuthamini michango ya wapiganaji ndani ya CUF na viongozi wa juu wasione Chama ni mali yao bali ni ya Watz wote kwani vinaendeshwa kwa ruzuku inayotokana na kodi zetu.

Naamini wakazi wa Bukoba Mjini wataendelea kuwa na wewe kwani ni mtetezi usiyeshusha silaha chini, uliyestaarabika na mkomavu wa siasa.

MUNGU AKUBARIKI, AKUPE NGUVU NA AKUONGEZEE HEKIMA NA MAARIFA ZAIDI!
 
Aende huko Chadema haya mambo ya ku beep yanampotezea muda
 
Vyama vyote vya upinzani ndivyo walivyo ,tuliona kwa marehemu Chacha kwa CHADEMA leo hii kwa Lwakatare CUF.Mambo yao ya ubadhirifu na kutofuata sheria pia kanuni yapo ktk degree ya juu sana kulinganisha na CCM.Ila hayaonekani kwa sababu resources zakufanya ubadhirifu ni ndogo sana.

Lakini ukichukuwa ratio ya ubdhirifu wao kwa resources zao with resepect na resources za CCM na material yao ,ukweli utaukubali kuwa vyama vya upinzani ni WORST.

Hapa sikitetei chama fulani ama kukiponda chama fulani LAKINI ni msimamo wangu tu na mtazamo wangu ya kwamba ktk nchi yetu TATIZO si chama bali kunatatizo somewhere around ambalo halifungamani na chama chochote ama itikadi yoyote.

Tunatakiwa tuli sort out hili tatizo hapo maendeleo yatakuja .MIMI pia naamini kwa 99.999999% UFISADI sio tatizo kwa kudumaa kwa nchi yetu japo kiuhalisia hatuhitaji.

most likely tatizo letu ni IQ na intellectual
 
Na hili suala la Mbunge Kagasheki -- huenda kuna kitu kinafichwa. Alitangaza kutogombea mwaka 2010 kumpisha Lwakatare kwa matarajio/makubaliano ajiunge CCM? Baadaye akaghairi? Was just thinking!!!
 
Wilfred na bado kwa maelezo yote haya wategemea kukaa na watu hawa kafu?

Je, unadhani watakusikiliza na kukubali mchango wako wakati ukiwa nje ya kafu? mbona tayari tulishakiona chama kwamba kinaelekea kuwa sisi m B?

Tafakari tena. Waachie kafu yao kama alivyowaachia Mapalala, nenda Chadema hata kama hukupata uongozi lakini nadhani mchango wako katika harakati ya kuinusuru nchi kutoka katika makucha ya majambazi hawa utaleta kitu.


Wengi tuko nje ya uongozi wa vyama lakini mioyo yetu iko katikamapambano kama wanachama ili kuinusuru nchi hii.

Mimi binafsi nakufahamu najua umahiri wako katika kupigania haki. Bado unaweza kuleta mabadiliko bila kuwa katika uoza wa kafu ya wazanzibari. Najua wewe ni kafu ya zanzibara
 
Back
Top Bottom