Bluray
JF-Expert Member
- Mar 25, 2008
- 3,449
- 137
Pamoja na kwamba sioni sababu ya ku-question nia yake ambayo ameitimiza kwa kuhamia chama kingine, naona haikuwa vyema kwake kusema alikuwa akilipwa kiasi gani na CUF. Masuala ya mshahara ni makubaliano yake na chama alichokuwepo. Na ni masualaya kibinafsi sana. Kinachotakiwa ni sababu za kuhama, na kuhamia CHADEMA, nia ya kuendeleza upinzani wa kidemokrasia na mikakati aliyonayo ya kisiasa baada ya kuondoka CUF.
Kuweza kupata wanachama wa CUF wenye nia ya kuhama nae ni hatua muhimu sana pia. Kwani anaingiza mtaji mpya kwenye chama chake kipya. Ila anatakiwa kuahidi kushirikiana na chama chake kipya na kujifunza imani zao, malengo yao na kupania kukiimarisha zaidi kwa kushirikiana na wenzake aliowakuta huko.
Siasa za upinzani Tanzania ni ngumu sana. Inabidi tumuelewe tu ndugu yetu huyo kwamba amebidi kuhama na zaidi ametumia haki yake kufanya hivyo. Tuheshimu maamuzi hayo, kwani kufanya hivyo ni kumtendea haki. Hakuna haja ya mtu kubaki sehemu moja ambayo una uhakika kuwa hutaweza kutoa mchango wowote kwa haki, na uhuru. Hasa baada ya kutokea yaliyotokea.
Kila binadamu hupenda challenges. Bila challenges maisha yanakuwa boring. Hivyo kuhama kwa Lwakatare inaweza kuwa ni challenge kwake, ni kwa manufaa yake kabla hayajawa manufaa kwa mwingine yeyote.
Jamaa mshamba haelewi hata issue nzima ya confidentiality na amicable parting, kashazoea kuachana na zogo zogo kama mke/mme mwenye wivu.
Yaani unaweza kumu asses mtu kwa mitihani midogo tu akakupa picha ya personality yake nzima, kama Pinda alivyoenda kutoa acceptance speech ya u PM bungeni huku kavaa suti na ki wife beater, unaona kazi tunayo kama Waziri Mkuu ndiye huyu, watu ooh mpe muda, wengine tukaona plae pale haya maboya, tena ya uchina.
Na huyu Lwakatare egotistic narcissist anayetafuta chati na ulaji wa chap chap si mwanasiasa anayeelewa siasa za Tanzania. Mwanasiasa aliyekomaa anayeelewa siasa za Tanzania ni aibu kujinadi kwa wazi hivyo, essentially kashajitangaza kwamba yeye ni wa chee sana na ana matatizo katika somo zima la PR.
Afadhali mara mia hata Zitto anajua principle ya pricelessness ya ideas na leadership mpaka kusema "I have no price tag" hata kama anayo price it is reassuring kumsikia mtu at least anajua kwamba anatakiwa asiwe na price.Huyu mshamba kashatutajia hela yake ndogo kuliko some belvedere shoes.