Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

Lwekatare wa CUF kuhamia CHADEMA

....Hata hivyo huyo aliyevaa viatu vya Lwakatare sio mtu wa kuwa na mashaka nae. Ni mtu mwenye msimamao thabiti haswaaa.Nilimuona na kumsikiliza wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2005 akigombea jimbo la Mikumi na kushindwa na Clement wa ccm, lakini ukweli jamaa anajua kuzungumza, anajua kujenga hoja na kiukweli naamini jamaa anaweza....
Wanasahau kuwa CUF ni kama daladala, akishuka abiria mmoja wengine kumi wana'nga'ngania mlango.Libeneke kama kawa.
 
Napenda sana unvyosema na kupangilia hoja zako Kaka yangu Kitila. Hivyo ndio ukweli kuwa CUF wanajimaliza mwenyewe, maana nakumbuka kipindi fulani Prof Lipumba alisema CUF hakuna udini na kutaja majina ya Lwakatare, labda waseme kuwa wana ajenda nyingine

Kitila kazungumza hoja nzito na post yake ilikuwa inaonyesha kiwango chake kikubwa cha elimu.
Angalia sasa post za wale waliolewa maji ya kijani uone, utaona tofauti hata ya vyama hivi viwili, na utajua kwa nini nchi yetu iko hivi ilivyo......
 
Utaonaje ana hoja wakati umeisha mhukumu kuwa ni mbishi tu? Usiangalie mtu bali angalia anachosema na matendo yake. Kutofautiana kisiasa hakina maana ya uadui kiasi kila afanyacho mwenzio unaona kinyaa! Leo Obama anawasifia marais Lincoln na Reagan ambao walikuwa republicans. Wewe unaona tatizo gani kuziangalia kwa undani zaidi hoja za Zitto Kabwe? Au unaogopa kugeuka mlingoti wa chumvi?

Amandla.......
Ndugu yangu Fundi Mchundo, kumbuka mtu anapokuwa kiongozi anatakiwa kwanza awe mvumilivu, lakini pia anatkiwa awe makini na kauli zake anazozitoa maana kiongozi mwenye hadhi ya kuitwa Mhe Mbunge ana nadhamana kubwa kwa wananchi anaowawakilisha na watanzania wote kwa ujumla wake.

Sasa anaposimama na kusema Waziri majibu yake ni ya hovyo hovyo inatutia shaka,alipotamka mara ya kwanza ilichukuliwa kuwa ameteleza.

Lakini hata pale alipotakiwa afute kauli hiyo bado alisisitiza kauli yake hiyo ina maana kuwa alikuwa amekusudia.

Mwisho naomba nikushauri kuwa nduguyo anapokosea msaidie faini na siyo kesi.
 
Hapa mtasema mengi amabayo hayakuwahi kutoka midomoni mwenu, lakini Lwaks huyooooooooooooooo chadema. Mnayodhani kuwa yatakuwa maafa kumbe itakuwa baraka.
Ndege(Lwaks) katua CCM No.2 sasa, on his way to CCM No.1 tusiandikie mate.
 
Yeyote anahaki na uhuru wa kuhamia chama chochote anachopendezewa nacho. Hata wewe huenda ukahamia chama kingine anytime. Let say upo CCM sasa (ni kwasababu unaridhika na yale inayoyafanya au sababu nyingine). So, sababu hizo zikitoweka utahamia chama kingine.

Mtu anayesema atabakia chama hichohicho hata mambo yaweje huyo anamatatizo ktk mfumo wake wa kutafakari na kutoa maamuzi.

Aisee Nziku hiyo bottoline yako imenichekesha saaaaaana...
 
Wakuu FM na Mwanawasu Masatu wala msitoane macho.
Pamoja na uwezo, nguvu,umaarufu, uhodari, au sifa yoyote utakayoweza kumpa Lwakatare lakini bado ukweli unasimama kwamba CUF itaendelea kuwepo, kwa suala la kuwa imara kama zamani sina uhakika. Na kwa kuzungumzia bukoba watakuwa wamepoteza wanachama na wafuasi wengi sana, watakaomfuata lwakatare kama ataamua kuhama chama.
Hata hivyo huyo aliyevaa viatu vya Lwakatare sio mtu wa kuwa na mashaka nae. Ni mtu mwenye msimamao thabiti haswaaa.Nilimuona na kumsikiliza wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2005 akigombea jimbo la Mikumi na kushindwa na Clement wa ccm, lakini ukweli jamaa anajua kuzungumza, anajua kujenga hoja na kiukweli naamini jamaa anaweza. Joram Bashange aliwahi kuwa katibu wa TPAWU(tawi la kilombero sugar-sasahivi ILLOVO) wakati kiwanda hicho kinabinafsishwa kwa makaburu(ingawa kuna maneno ya chini chini kwamba makaburu walipewa K1 na mzee chenkapa & ze sumaye wakajigawia K2(samahani mzindakaya najua hupendi kuona huyu mzee akitajwa).Huyu bwana Bashange ameacha historia ya kukumbukwa kilombero sugar hadi kesho ukienda utasimuliwa, jinsi alivyokuwa imara kutetea haki za wafanyakazi wa kiwanda kile wakati wa ubinafsishwaji wake. Alipambana na uongozi wa wilaya, mkoa, na polisi kwa hoja kwenye vikao mbalimbali vilivyoitishwa kwa ajili ya kuweka mambo sawa na akawashinda.Inatajwa kuwa sababu mojawapo iliyopelekea Lukuvi kula shavu la uwaziri enzi za chenkapa ni baada ya kumtonya mzee mkapa madudu yaliyokuwa yamefanywa na watendaji kadhaa katika kushughulikia kadhia hiyo akiwemo waziri wa kilimo kipindi hicho mzee kimiti. Matokeo yake kimiti akapotezezewa baada ya uchaguzi mkuu wa 2000.Kumbuka tu kwamba vuguvugu la kubinafsisha kampuni ya kilombero sugar ilikuwa kati ya 1998 hadi 2000.
Nimalizie kwa kusema tu kwamba tumpe muda bw.Bashange tuone ataifanyia nini CUF, BTW bw.Bashange nae ni mtani wangu, dugu moja na Lwakatare (wote ni BK boys).Sasa sijui hapa Lipumba aliendeleza ukabila???!!!!anyway natania tu , turudi kwenye mada.

Marwa post yako ina ukweli mkubwa sana na si biased kama nyingi hapa zilivyo.
Ila tu napenda niweke wazi kuwa kafu itaendelea kuwapo Zanzibar tena zaidi Pemba lakini bara itaungana na vile vyama vingine si unajua? nncr,tlp,udp,dp na ww ongeza orodha hapo. Vipo kama havipo vile.
 
Ukimnyooshea mwenzio kidole kimoja, vinne vinakugeukia wewe, Si afadhai hata huyo Zitto kathubutu? wewe je? nyuma ya keyboard?

Bravo Zitto, songa mbele wala usirudi nyuma!

kathubutu kufanya nin?kutetea ununuzi wa mitambo ya dowans KWA NGUVU ZAKE ZOTE,KWA UWEZO WAKE WOTE,NA KWA AKILI YAKE YOTE?
..........nah!hainiingii akilini kabisa!lazima alitangaza njaa hapa

mwanasiasa wa kiwango chake akishaprove failures to that level,AACHIE NGAZI!uongozi,au siasa watu hawazaliwi navyo bwana

.........huyu chuo-mate wangu nae ALIONYESHA UDHAIFU MKUU,aliamua kuondoka ccm baada ya jina lake kutopita katika kuwania ubunge kule tarime,UROHO WA MADARAKA?AU NJAA?HUYU SI MWANASIASA!na bahati mbaya i knw him IN-OUT
 
Ndugu yangu Fundi Mchundo, kumbuka mtu anapokuwa kiongozi anatakiwa kwanza awe mvumilivu, lakini pia anatkiwa awe makini na kauli zake anazozitoa maana kiongozi mwenye hadhi ya kuitwa Mhe Mbunge ana nadhamana kubwa kwa wananchi anaowawakilisha na watanzania wote kwa ujumla wake.

Sasa anaposimama na kusema Waziri majibu yake ni ya hovyo hovyo inatutia shaka,alipotamka mara ya kwanza ilichukuliwa kuwa ameteleza.

Lakini hata pale alipotakiwa afute kauli hiyo bado alisisitiza kauli yake hiyo ina maana kuwa alikuwa amekusudia.

Mwisho naomba nikushauri kuwa nduguyo anapokosea msaidie faini na siyo kesi.[/QUOTE]

Na kama aliyeamua amekosea amefanya hivyo kwa tamaa ya rupia? Kwa nini nisimsaidie akate rufaa?

Kwa mtazamo kama wako, hata Mwalimu asingeweza kukaa katika bunge letu! Mbona hata yeye alikuwa na lugha kali zaidi ya hiyo aliyotumia Zitto. Mbunge anatakiwa kuweka maslahi ya waliomtuma mbele kuliko hizo trapping za uheshimiwa! Na vile vile mawaziri wanatakiwa wawaheshimu wabunge kwa kutoa majibu waliyoyafanyia kazi na yanayokubalika. Kwa kuwajibu wanavyofanya nako ni kuonyesha dharau kwao na kwa watu walio watuma. Ndio maana wana haki ya kukasirika. Badala ya kulalama basi mngeonyesha ni jinsi gani majibu ya huyo mheshimiwa hayakuwa ya 'ovyo ovyo'. Bunge hapatakiwi kuwa sehemu ya lele mama. Si mahali pa kuogopana. Tuaaangalie waingereza bunge lao. Hiyo ndio demokrasia. Na ndio itakayosaidia chama tawala kujiweka sawa. Badala ya kumbeza Zitto, wafanyie kazi hoja zake ili mwakani akose la kusema!

Amandla......
 
Kuhama toka CUF kwenda CHADEMA ni sawa na kubadilisha kiti kwenye basi la kusafiria.
 
Last edited:
Wakuu kwa habari kamili niliyo nayo Lwakatare bado anamiliki uanachama wa kafu hadi ijumaa ya wiki hii.
Stay tuned kujua nini kitatokea ijumaa huko Bukoba.
Nasubiri kupata info zaidi na nitawahabarisha.
Junius nawe utakuwepo huko Bukoba na Lipumba? Nasikia kuna bonge la party ya wana kafu Bukoba siku hiyo ya ijumaa😀 Sijui ameamua kuvunja kimya?
 
Ijumaa kuna jambo litatokea huko Bukoba kuhusu sakata hili.
Stay tuned.............
 
Wakuu kwa habari kamili niliyo nayo Lwakatare bado anamiliki uanachama wa kafu hadi ijumaa ya wiki hii.
Stay tuned kujua nini kitatokea ijumaa huko Bukoba.
Nasubiri kupata info zaidi na nitawahabarisha.
Junius nawe utakuwepo huko Bukoba na Lipumba? Nasikia kuna bonge la party ya wana kafu Bukoba siku hiyo ya ijumaa😀 Sijui ameamua kuvunja kimya?
Kama Chadema wakitoa mwaliko hapana shaka.
 
kathubutu kufanya nin?kutetea ununuzi wa mitambo ya dowans KWA NGUVU ZAKE ZOTE,KWA UWEZO WAKE WOTE,NA KWA AKILI YAKE YOTE?
..........nah!hainiingii akilini kabisa!lazima alitangaza njaa hapa

mwanasiasa wa kiwango chake akishaprove failures to that level,AACHIE NGAZI!uongozi,au siasa watu hawazaliwi navyo bwana

.........huyu chuo-mate wangu nae ALIONYESHA UDHAIFU MKUU,aliamua kuondoka ccm baada ya jina lake kutopita katika kuwania ubunge kule tarime,UROHO WA MADARAKA?AU NJAA?HUYU SI MWANASIASA!na bahati mbaya i knw him IN-OUT

Inaonekana pasipo shaka kabisa kwamba unachuki binafsi na Bw. Mwikwabe.Kama sivyo wewe utakuwa mshirika/mwanachama wa chama cha mafisadi, manake mlikereka sana kwa bw.Mwikwabe kuwatosa na kujiunga Chadema. Hapa tunazungumza habari ya Lwakatare kuihama CUF na kujiunga Chadema lakini wewe uko busy kumshambulia bw.Mwikwabe.
Kwani wangapi wamesoma na bw.Mwikwabe na walikuwa karibu zaidi nayew kuliko wewe lakini mbona hawasemi.Watu kama wewe sitashangaa kukuta kuwa hata UDSM hamkupenda awe rais na mlikuwa upande wa mpinzani wake kwahiyo mna wivu wa kijinga, tena hadi leo hii takribani miaka minne baada ya kutoka UDSM una mawazo ya kijima namna hiyo.
Kama una hoja juu ya Mwikwabe anzisha thread tukupe mambo sio kuanza kulia lia hapa eti unamjua in and out, upuuzi mtupu!!!Chuki zenu zimezidi baada ya kushindwa kulirudisha jimbo la tarime kwa chama cha mafisadi. Fungua akili yako kwa upana zaidi ndg yangu usiifungie akili yako ndani ya
box mwisho wake ni kuanza kushambulia watu kwa vioja badala ya kuleta hoja.
 
Fundi,
Huo mvuto wa Lwakatare hakuja nao CUF bali aliupata CUF.

Kuna utofauti kati ya Mwanafunzi aliyeko Lab na yule aliyeko class. Aliye class ataweza kujifunza na kusoma nadharia ilihali aliyeko Lab anaweza kuona matokeo ya nadharia kwa vitendo.

Unalolisema Bw. Masatu ni sawa na aliyeko sebuleni kubishana na mpishi juu ya chakula kuiva. Mpishi anasema chakula bado, aliye sebuleni anasema kimeiva, pakua.

Tuliokuwepo wakati mageuzi na vyama vinaingia hapa BK tunatambua kuwa CUF ni Lwakatare but vice versa is true not! Selestine Mutakyawa ni NCCR-Mageuzi lakini NCCR-Mageuzi siyo Selestine Mutakyawa.

Ni jambo la kawaida kabisa kwa Watwale mtu kuwa icon ya industry. Katika medani za kisiasa BK, Lwakatare ni selling Brand yeye kama Lwakatare na si kama Chama.

Thibitisha haya niliyoyaandika kwa kuangalia njugu za kadi za CUF zitakazorejeshwa kesho.

Masatu, Kuna ka-PM nakutumia
 
Acha ulimbukeni, upumbavu na ushenzi wako. Kama Lipumba anaweza kuwa prof wa Pumba wewe utakuwa profesa wa kinyesi! Unadhani u profesa unapatikana kwa kuandika JF.

Lipumba ni Profesa wa Pumba kweli si uongo. kama kashindwa kukipeleka chama kisomi, sasa tumsemeje?
Arudi darasani kufundisha pumba zake.
 
In reality CUF wanapita katika moja ya vipindi vigumu mno tokea kuanzishwa kwao kwenye miaka ya 90 mwanzoni.....

Nakumbuka zama zakuondolowa Mapalala mmoja kati ya waanzilishi wa mwanzo mwanzo kabisa wa CUF.... nakumbuka nusura pachimbike maana influence ya jamaa na uasisi wake kiasi vilileta mtikisiko kenye kambi ya CUF. Lakini what happened kila mtu anajuwa waliweza ku recover sana na hatimaye kujijenga.

Namkumbuka sana Maiko Nyaruba..jamaa alikuwa muongeaji hana mfano na naamini ali wa influence watu wengi mno kujiunga na CUF lakini yakamkuta yaliyomkuta.

Then ustadhi wangu Salim Msabbah yule aliyekuwa mbunge wa jimbo la mtendeni...very influential..na bright mno....nae aliondoka......Naila Jidawi, Akwilombe, e.t.c

The list is endless... ila waliweza kurecover huko nyuma.... Wilfred Lwakatare mmoja kati ya vijana tena wasomi mno ambao uwepo kwake CUF ulikuwa ni muhimu mno..angeweza kuvutia vijana wenzake na wasomi wenzake kujiunga na CUF.

CUF inavyoenekana haina mvuto na vijana wasomi unlike CHADEMA.. sababu hazijulikani whether hawaoewi nafasi za uongozi au vipi.... Nimeipenda mno approach ya CHADEMA ya kuwapa vijana nafasi za uongozi na mamuzi katka chama. Mwenyekiti wao ni kijana, then kina Kabwe and his co.

Naamini CUF bado ina hazina ya wanachama wengi mno Tanzania...na I will eat my words wanaweza wasipate mmbunge bara..lakini overall mgombea wa uraisi akawa next to wa CCM. Sababu nadhani wengi wa wanachama wao have something in common between them.

Kingwele.

Nafikiri sumu waliyoipandikiza chama cha kijani kwamba CUF ni chama cha kidini, hivyo inakuwa ngumu kidogo watu hao kujiunga na CUF waona may be hawato shine hasa hasa huku bara.Na kwa kundoka huyo jamaa(Lwakatare) ambae kidogo alikuwa anaondoa dhana hiyo kama alivyosema member mmoja ndio utakuwa msumari wa mwisho wa CCM na sumu yao kwa CUF.CUF watanyooshewa kidole mpaka.Yangu macho ngoja nivue na miwani yangu.
 
Aliingia chama ambacho hakikuwa size yake.....aende chadema akapige jembe la maendeleo ya demokrasia....aachane na unafiki na fitna hataziweza......
 
Back
Top Bottom