kwani ww ni wa kaskazi au ni wale walio wengi mjengoni?Mbona ueleweki?Siku nimekuja na breaking news za wananchi wa Bukoba kumtaka ahame kafu, wewe ndiye ulinisakama kuwa mi ni mwongo😀
Leo kwa sababu hii habari kaisema mwenyekiti wako Lipumba, unakuja kutuletea old stories!
Mwaka huu kafu mtaumia sana maana yuko na kiongozi mwengine yuko njiani kuwakimbia pia. Huyo simtaji. Time will tell😀
Sasa kama si maumivu kwenu wewe na Lipumba mbona mnaonyesha ku panic?
Mmeshapigwa bao bwana😀tena la kisigino😀
Kwangu mi sintajali anakwenda chama kipi cha upinzani. Ila ni hamu yangu kuona kafu inakufa mikononi mwa Lipumba na Seif😀
Hata hivyo kwa kuwa wadau wengi wanatamani kuona nchi inakuwa na chama kimoja chenye nguvu cha upinzani, naona ndoto zao zinaelekea kutimia maana kitabaki Chadema. Kafu tlp nccr kwishney😀
Alafu mwambie Lipumba kuwa Bukoba kafu kwishney. Kama ilivyo Pemba kafu bila Seif si kafu ndivyo ilivyo Bukoba kafu bila Lwakat.... si kafu😀
unamaanisha chama cha kaskazini na kile cha majambazi?
Give me a break! hayo mambo ya ku bandwagon kampeni za CCM. Kwa hiyo Chadema nayo ni ya wachaga? Mbona hiyo nafasi ya Lwakatare kaingia somebody Joram i hope sio muislam!
Huyo Kitila "kachanganyikiwa" na masuala ya Housegirl wake sasa anamwaga utumbo tu
Kwa maneno yako Masatu! baada ya wanasiasa wetu kuzunguka koooote huko at lastlazima warudi CCM siyo? kwa maana hiyo hakuna haja ya kuzunguka saana ni bora kubaki tu CCm au?
Masatu, unaelewa lakini maana ya neno dhana? Au unataka kutuambia kuwa hakuna wenye imani hizo za CUF kuwa chama cha waislamu na Chadema cha wachaga? Au unadhani kukataa kuziona ndiyo zitapotea? Sasa mbona una-hope Joram sio muislamu?
Amandla..........
Fundi,
Kama ungenisoma vizuri utagundua nami nilikuwa najadili hoja hiyo hiyo ya Kitila. Na katika majibu yangu ndio likaja hilo suala la madai ya CCM na udini.
Huo mvuto wa Lwakatare hakuja nao CUF bali aliupata CUF. Simjui huyo Joram na uwezo wake lakini mpaka kufikia kupewa wadhifa hao hao waliompa wameona unwezo wake ikiwa pamoja na "mvuto"
Masatu Mkuu. Hizo hisia za udini zipo bila hata CCM kuhusika. Alichokifanya Kitila ni ku-caution kuwa CUF wawe waangalifu katika maamuzi yao.
Walichokifanya CUF kwa Lwakatare ni kumpa platform ambayo aliitumia vizuri. Si wote wenye uwezo huo. Ingelikuwa hivyo basi huko CUF tungewasikia wengi kuliko Lipumba na Maalim. Mimi binafsi namtakia kila la kheri huyo Joram maana tunahitaji watu wenye msimamo na mvuto katika vyama vya upinzani. Ana kazi nzito mbele yake.
Amandla....
Ni kawaida wapinzani kuhangaika wala hakuna cha ajabu kwani hana jipya atakalolifanyaKWA MUJIBU WA GAZETI LA NIPASHE LA TAR 24/JUNE/2009
Zile tetesi zilizokuwa zikijadiliwa sana hapa jamvini juu ya naibu katibu wa CUF bwana Lwakatare kuhamia CHADEMA zimekuwa si tetesi tena,baada ya mwanasiasa huyo kutua rasmi CHADEMA,na hadi muda huu ni kwamba 'mwanazuoni' huyu yupo biharamulo akikipa nguvu chama chake kipya katika kampeni