Lwakatare aizika rasmi M4C

Lwakatare aizika rasmi M4C

Status
Not open for further replies.
Wakuu, sio siri tangu alipokamatwa Mkurugenzi wa usalama wa cdm maanadamano ya cdm kupitia kauli mbiu ya M4C ni kama yamefutika rasmi. Ninawashauri hawa jamaa watafute kauli mbiou nyingine ya kuweza kuwahadaa watanzania.

Umetumwa????
 
Wakuu, sio siri tangu alipokamatwa Mkurugenzi wa usalama wa cdm maanadamano ya cdm kupitia kauli mbiu ya M4C ni kama yamefutika rasmi. Ninawashauri hawa jamaa watafute kauli mbiou nyingine ya kuweza kuwahadaa watanzania.

Naona Pasco ame LIKE hii post ya kihuni! M4C inaendelea kama kawaida, endeleeni kujidanganya, Muulizeni Kinana na Nape watawapa jibu huko walikofanya ziara hali ya CCM ikoje!
 
Last edited by a moderator:
M4c kwishney ilikuwa nguvu ya soda hata magari yao yako juu ya mawe
 
Kwani alieyemshtaki Lwakatare na rafiki yake Ludovick ni nani? na je, mshitaki huyo amehusisha vipi mashitaka hayo na chama? Njoo na evidence zinazonyesha kuwa aliyemshitaki Lwakatare amehusisha kesi hiyo na chama.

Kwa maswali yako haya, kama tayari una majibu yake basi inawezekana nitajifunza mengi zaidi kutoka kwako zaidi ya utakayojifunza kutoka kwangu endapo utajibu swali langu la awali yaani "ni kwa nini unafikiri inabidi iwe kesi yake na si ya chama?" na kama huna majibu ya maswali yako, basi itabidi tendeleze mjadala.
 
:rockon::rockon:
kaa ukielewa CCM inaelekea kufa,na kinachochea uongo dhidi ya CDM ili kuhadaa umma wa kitanzania bila mafanikio.
 
M4c ni kiama chenu mmekalia propaganda chadema wanasonga mbele
 
kwa matusi c.c.m ni waasisi, mchemba, lusinde, komba, nkamia, kigwangala, na yule wa cuf aliyesema kwamba mboe amejamba bungeni kakimbia,
 
Mkuu,
Hii ni kesi ya chama. We angalia mtiririko tu wa events ujue. Lakini wasichojua CCM ni kwamba walipolalia wao Chadema ilishaamkia hapo siku nyingi.



Kumekuwepo na shinikizo kubwa mitaani na zaidi kwenye mitandao ya kijamiii hasa facebook,Twitter,Blogs na hata huku JamiiForums kama mlivyoshuhudia la wafuasi wa Chadema na wapenda mageuzi wasio na vyama la kutaka Naibu katibu mkuu wa Chadema bara Zitto Zuberi Kabwe kujiuzulu nafasi yake.
Naungana na wote wanaomtaka ajiuzulu nafasi yake kama alivyopendekeza kwa lwakatare.Kitendo cha juzi kuja kulalamika humu kuhusiana na namba yake aliyokiri kwamba aliaacha kuitumia tangu mwaka jana mwezi july lakini bado ipo kwenye business card yake na kutaka pia kuaminisha umma kuwa taarifa ya Mabere Marando ina lengo la kumgeuza Dennis Msacky aliyemuita victim kuwa mtuhumiwa ni makosa makubwa yanayoweza kuvumilika
Inachosha kuona kiongozi kama huyu anashirikiana na wabaya wa chadema na kuwakingia kifua kwa gharama yoyote hata kuja huku kuwatetea na kurusha tuhuma kwa viongozi wa chama chake.
Kitendo alichofanya juzi kinathibitisha kuhusika kwake katika njama hizi na pia barua yake iliyodaiwa kuvuja aliyotuma kwa Katibu Mkuu wa Chama hicho na kurusha tuhuma ya moja kwa moja kwa ofisi ya katibu mkuu bila kufuata utaratibu wa vikao ni kuokosa umakini maana ni lazima watu wajiulize je Dr.Slaa angeibuka huku na kumjibu kama alivyofanya Ben Saanane alipojibizana nae kuhusu sakata la masalia ingekuaje?
Mwanzoni niliwashangaa sana vijana wa chadema walipokua wakimsema live kwewnye mitandao kuwa wamekosa imani naye na ni vyema angechukua uamuzi wa kujiuzulu na chama kifanye uchunguzi juu ya uhusika wake kwenye sakata hili.
Kwa kufanya hivyo atakua ame-Walk the talk kama ilivyotakiwa na mwanzisha mada mmoja huku siku chache zilizopita na pia zitto atakua amejipambambanua kwa kile alichokua akitaka kifanyike kwa Lwakatare kama kulikua hakuna ajenda ya siri na unafiki uliomsukuma kuandika barua kama ile

Inasikitisha kuona Chadema kilisimama nae kama timu alipotuhumiwa kuhongwa bungeni hata kamati yake ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwenye mashirika ya umma ilipovunjwa CHADEMA kiliungana na kusimama nae bega kwa bega lakini anataka chama kimtose mkurugenzi wake aliyebambikiziwa kesi na maadui wa Chadema huku akijaribu kuwatetea baadhi ya wahusika wanaotumika na usalama wa taifa kukiangamiza chadema.

Mawasliano yake na dennis msaki kama yalivyoripotiwa na mwanahalisi yanatosha kuibua haja ya kufanyika uchunguzi wa kina juu ya uhusika wa zitto katika sakata hili pamoja na uvujishahji wa barua iliyowekwa huku nay eye kudai alifanya uchunguzi na kugundua aliyeweka humu ni yule aliyeweka video ya Lwakatare na pia kuna kirusi Chadema.
Zitto kama ni muumini wa kweli wa alichosema kama hakuna ajenda ya siri nyuma yake aaachie ngazi ili uchunguzi ufanyiuke juu yake na mienendo inayokatisha tama vijana na kujaribu kuleta mgawanyiko ndani ya chama na mtizamo wa jamii dhidi ya chama chake.Ajipime aone kama bado wanachadema wanayo imani kwake.Yeye mwenyewe ni shuhuda wa mijadala inayomtaka ajiuzulu iliyotawala sasa kwenye mitandao
 
Mpaka sasa bado sijaelewa kwanini chadema wanaigeuza kesi binafsi ya Lwakatare na rafiki yake Ludovick kuwa kesi ya chama!!!

Rwakatare anabeba nembo ya Chama pamoja na nembo ya utaifa, hivyo kumuacha peke yake ni unafiki kwani asingekuwa mwanasiasa haya yasingemkuta. Mambo ya kila mtu kubeba mzigo wake ni ya CCM si ya CDM. Umenisoma???
 
Kwani alieyemshtaki Lwakatare na rafiki yake Ludovick ni nani? na je, mshitaki huyo amehusisha vipi mashitaka hayo na chama? Njoo na evidence zinazonyesha kuwa aliyemshitaki Lwakatare amehusisha kesi hiyo na chama.
Kesi ya Lwakatare.
Mkanda karekodia nyumbani kwake.
Ofisi za CDM zinapekuliwa kwa lengo lipi?, au ndio nyumbani kwa Lwakatare?.
 
Kwa maswali yako haya, kama tayari una majibu yake basi inawezekana nitajifunza mengi zaidi kutoka kwako zaidi ya utakayojifunza kutoka kwangu endapo utajibu swali langu la awali yaani "ni kwa nini unafikiri inabidi iwe kesi yake na si ya chama?" na kama huna majibu ya maswali yako, basi itabidi tendeleze mjadala.

Swala la kesi kuwa ya Lwakatare sio la kufikirika ni swala linaloonekana mahakamani kesi inaposomwa. Kwenye kesi kuna mshitaki na mshitakiwa.

Mshitaki ni DPP na washiakiwa ni Lwakatare na Ludovick. Hakuna doccument yoyote inayoitaja chadema kwenye kesi ya Lwakatare.

Tukio la kupanga ugaidi alilifanya Lwakatare mbele ya Ludovick wakiwa nyumbani kwa Lwakatare ni si kwenye ofisi ya chadema. Katika video Lwakatare haitaji chadema kuwa imemtuma.

Kimsingi chadema inalazimisha umaarufu wa kisiasa kupitia kesi binafsi ya Lwakatare. Ni sawa leo hii Dr. Slaa akigombania kiwanja na jirani yake halafu chadema waseme hiyo ni kesi ya chama!!!

Nadhani umeona wanaharakati wa vikundi mbalimbali vya dini ya kiislam ambao wamekuwa wakiifanya kesi ya kiwanja inayomkabidi Ponda kuwa ni swala la kidini. Hii haina tofauti na chadema wanavyoifanya kesi binafsi ya Lwakatare kuwa ni swala la chadema kwa lengo la kuwalaghai wananchi kuwa chadema inaonewa na imeshitakiwa na serikali ya CCM. Lakini the truth ni kwamba hakuna mtu aliyeishitaki chadema!
 
Kesi ya Lwakatare.
Mkanda karekodia nyumbani kwake.
Ofisi za CDM zinapekuliwa kwa lengo lipi?, au ndio nyumbani kwa Lwakatare?.

Kupekuliwa ofisi sio ajabu na kuna sababu mbili:
1. Mtu yeyote anapofayna kosa la jinai/kigaidi basi kunaweza kuwa na traces za mipango ya makosa hayo katika sehemu anayofanyia kazi. hata kama angekuwa anafanya kazi NMB nako kungepekuliwa.
Hili halijafanyika kwa Lwakatare tu, linafanywa sana na hata nyumba wakati mwingine hupekuliwa kwa kesi za ofisini, wakati mwingine hata nyumba ya rafiki inaweza kupekuliwa.
Lakini cha muhimu zaidi kumbuka kuwa chadema walianza kuikumbutia kesi kabla hata polisi hawajaingia kwenye ofisi za chadema kufanya upekuzi. Upekuzi ulifanyika baada ya Lwakatare kuhojiwa kutokana na majibu aliyotoa kwenye mahojiano.

2. Kitendo cha chadema kutumia nguvu sana kumtetea mtuhumiwa katika kesi yake binafsi bila kujua kama ametenda kosa au lah, inatia shaka kuwa pengine chadema inajua mengi zaidi na pengine ndani ya ofisi za chadema kunaweza kuwa na taarifa zaidi. Hata wewe ukiibiwa gari halafu akatokea mtu anamtetea kwa nguvu zote mtu aliyesemekana ameonekana na gari lako, utatambua kuwa pengine kwa kumchunguza mtetezi huyo wa mtuhumiwa unaweza kupata taarifa zaidi juu ya wizi wa gari hilo.

Kimsingi ilitegemewa chadema nao washtushwe na taarifa kuwa Lwakatare amepanga ugaidi, lakini cha ajabu hawajashtushwa na hata ushauri wa kulichunguza swala zima wameukataa na moja kwa moja wameconclude kuwa Lwakatare hana hatia. Hii inafanya watu wenye fikra huru waone pengine chadema inafahamu mipango ya Lwakatare.
 
Mtoa mada anatumia(MASABURI)kufikiria.Linapost ----- utadhani lenyewe linashirikishwa na katibu mkuu wa Magamba kusafirisha pembe za ndovu Vietnam.Watch your steps dude.
 
Rwakatare anabeba nembo ya Chama pamoja na nembo ya utaifa, hivyo kumuacha peke yake ni unafiki kwani asingekuwa mwanasiasa haya yasingemkuta. Mambo ya kila mtu kubeba mzigo wake ni ya CCM si ya CDM. Umenisoma???

Usichanganye mambo mawili: Kumpa msaada wa kisheria na kuihusisha kesi na chama. Lwakatare angeweza kupata msaada full wa kisheria toka kwa chadema au kwa watu wengine watakaoona haja ya kufanya hivyo bila kuhusisha kesi na chama.

Polisi hawajahusisha kesi na chama, DPP hajahusisha kesi na chama, Mahakama haijahusisha kesi na chama. Chadema peke yao ndio wako kwenye hekaheka za kuidanganya jamii kuwa chadema imeshitakiwa. Hakuna mtu aliyeishitaki chadema.

Unasema mambo ya kila mtu kubeba mzigo wake sio ya Chadema, lakini umesahau kuwa mwanaharakati mwingine wa chadema Ludovick ametelekezwa na chama chake kwa sababu yeye ni mtu wa chini sio kigogo kama Lwakatare. Unakumbuka pia yule mwanaharakati mwingine wa Chadema aliyeiba nguo za jeshi na kupiga picha na Godbless Lema sasa hivi anasota jela kwa sababu hakupata msaada hata kiduchu wa kisheria toka chadema kwa sababu sio kigogo. Unakumbuka kijana aliyeuawa kwenye maandamano ya chadema Morogoro, alizikwa kwao Tanga bila kiongozi yoyote wa chadema kufika kw sababu hakukuwa na waandishi wa habari na tukio hilo la mazishi halikuwa na maslahi kisiasa.

Ukitaka mifano zaidi nitakupa...
 
Swala la kesi kuwa ya Lwakatare sio la kufikirika ni swala linaloonekana mahakamani kesi inaposomwa. Kwenye kesi kuna mshitaki na mshitakiwa.

Mshitaki ni DPP na washiakiwa ni Lwakatare na Ludovick. Hakuna doccument yoyote inayoitaja chadema kwenye kesi ya Lwakatare.

Tukio la kupanga ugaidi alilifanya Lwakatare mbele ya Ludovick wakiwa nyumbani kwa Lwakatare ni si kwenye ofisi ya chadema. Katika video Lwakatare haitaji chadema kuwa imemtuma.

Kimsingi chadema inalazimisha umaarufu wa kisiasa kupitia kesi binafsi ya Lwakatare. Ni sawa leo hii Dr. Slaa akigombania kiwanja na jirani yake halafu chadema waseme hiyo ni kesi ya chama!!!

Nadhani umeona wanaharakati wa vikundi mbalimbali vya dini ya kiislam ambao wamekuwa wakiifanya kesi ya kiwanja inayomkabidi Ponda kuwa ni swala la kidini. Hii haina tofauti na chadema wanavyoifanya kesi binafsi ya Lwakatare kuwa ni swala la chadema kwa lengo la kuwalaghai wananchi kuwa chadema inaonewa na imeshitakiwa na serikali ya CCM. Lakini the truth ni kwamba hakuna mtu aliyeishitaki chadema!

Labda unaweza kutujibu ni kwa nini polisi walikwenda kupekua ofisi za Chadema. Upekuzi nyumbani kwa Lwakatare ungetosha kabisa.
 
Labda unaweza kutujibu ni kwa nini polisi walikwenda kupekua ofisi za Chadema. Upekuzi nyumbani kwa Lwakatare ungetosha kabisa.

Nimeshaweka post ya kujibu swali hili kwenye mjadala huu...
 
Unapoona Mwenyekiti wa chama na Katibu mkuu wa chama wanaongoza kikosi cha wapenzi, wananchama na mashabiki wa chama (CHADEMA) kwenda mahakamani kuhusiana na kesi hii, hii ni dalili tosha inayokuonyesha ni jinsi gani sakata la Lwakatare lilivyo juu ya mambo mengine ya chama.

Kuna watu watasema, CHADEMA ni taasisi lakini wakumbuke taasisi hii inaongozwa na watu. Maamuzi au matamshi ya Mwenyekiti au Katibu mkuu wa chama kuhusiana na chama ni sauti ya chama.

Dr. Slaa aliposema video ni 'feki', hiyo ilikuwa ni kauli ya chama. Mwenyekiti wa taifa aliposema hawamuacha pekee Lwakatare katika sakata hili, hii ilikuwa ni sauti ya CHADEMA.

Kinachofanyika sasa hivi ni kuhakikisha kauli za CHADEMA kupitia midomo ya viongozi wake zinakuwa niza kweli katika macho ya sheria hata kama katika macho ya fikra na busara za watu yanaona vingine.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom