Lumumba kwafukuta; Ya Dodoma yaanza kutoa cheche

Lumumba kwafukuta; Ya Dodoma yaanza kutoa cheche

Majungu ndio jadi yetu,tokea huko nyuma wala si ajabu wapambe kununiana ndio maisha ya Lumumba
 
tangu makada warudi toka dodoma (mimi nilitangulia kurudi dar es salaam), hali si shwari ndani ya ofisi ndogo za ccm hapa lumumba. Makada wanapingana kimakundi yaliyopata na kukosa ushindi kule dodoma. Wapo makada wenye tabasamu la hamu na wale wenye sura zilzosheheni hasira. Hali si ile. Imebadilika.

Kazi zinakwenda polepole na hata hakuna wa kumuuliza mwingine kwa staha na raha. Maneno na matendo ya makada yamebadilika. Utaniutani uliokuwa ukituunganisha,umepungua na kuonekana unasumbua. Sasa ni urafiki wa kinafiki tu. Kwa werevu,tunayaona makovu ya dodoma. Yanafanya kazi sasa. Kununiananuniana ofisini kumekwamisha hata redio uhuru kutenda kazi zake ipasavyo. Tcra wanaivizia kuifunga kwa kutolipa kodi. Kodi imekwamishwa.

Viongozi mpo? Hali si shwari chamani!

Mzee tupatupa wa lumumba, dar es salaam

wakati haya yakiendelea huko lumumba ikulu kununiana ndio usiseme....makamu wa rais na waziri mkuu wanamsubiri kikwete arudi wamuulize ni nini kuwakosea adabu vile ...kuwanyima hata tano bora mmoja wao ..ina maana hana imani hata kidogo na wasaidizi wake ...kuna wanaowasukuma wajiuzulu especially wana maskani znz ...

Na mnafiki aliyewasha huu moto huyooo kaenda kueka mambo yake sawa uswiss ...tuna bahati tuna amani nchi nyingine ccm wangemuambia abaki huko huko kama nkuruzinza
 
Magufuli msukuma wetu kama hamtaki Piga Mbizi kwenye rami
 
CCM we acha tu. Wamempigisha makofi mwenyekiti--------tuna imani na Lowassa oya oya oyaaaa! Kazi kweli kweli.
 
Hizi wishful thinking zenu mpaka lini?? Kama Mh.Magufuli aliweza kupata zaidi ya asilimia 80% ya kura zote,which means CCM sasa ni kitu kimoja i.e wana mshikamano thabiti,kama kuna watu waliokua wanasubiria igawanyike ili weweze kuishinda kirahisi hiyo wasahau.Japangeni upya who knows labda mwaka 2055 mnaweza kufanikiwa,UKAWA mnashindwa kuelewana nani abebe bendera ya upinzani nani anaweza kuwakabidhi Nchi Viongozi ambao masaa yote wapo kwenya chaotic Motion kama atoms za gesi ya Mnazi Bay/Songosongo!!

acha ushamba wewe asilimia 80 za mazuzu unapiga kura bila kuhoji swali wanachama wote wale hata swali la uongo hakuna ndio maana bungeni mnapeleka mazuzu. tukisema mnabisha.
 
Khaa!!! Nyie mnachekesha sana. Mzee K mwenyewe kasema yeye anaongea tu lakini anajua kabisa hakuna kitakachofanyika. Kwa kifupi AMEKATWA full top. Hebu acheni ulevi bana.
 
Wengi walifurahi ila ipo siku watanuna
 
Kingunge chochea moto.Magufuli atatawara kwa remote kutoka msoga.Mzee kinukishe Lowasa arudishwe
 
Narudia, paruaneni huko, sisi tuanendela kuwacheki, maana mnagombania mwali aliyechukuliwa tayari.
 
Lowassa kama Yesu, wamemkata, dhambi yake CCM ni kifo, sbb naona UKAWA wanamchukua, sasa CCM ni kifo tu...!!!
 
Kingunge chochea moto.Magufuli atatawara kwa remote kutoka msoga.Mzee kinukishe Lowasa arudishwe


Sahihi kabisaaa... Magufuli atakuwa anapewa directives toka Msoga...

Lowassa ndie Rais... mwaka huu CCM wamejizika wenyewe
 
Story za chini ya mwembe kazi ya Dodoma imeisha na Tingatinga liko mzigoni mtoa uzi inaonekana na wewe ni miongoni mwao kama vipi tupia picha zao kama hilo haliwezekani waambie watoke CCM maana hawalazimishwi kubakia huko!

Tingatinga la kujaza mimba wanafunzi na kuhonga vimada nyumba za serikali au?
 
Kitendo cha kikwete kutuletea mgombea wa kwenye Briefcase hakikubaliki.
 
VUTA-NKUVUTE


Bintiyo nilikuwa nakusubiri kwa HAMU kubwa utupe ukoko uliobaki kule Dodomya.Niliona UNAFIKI toka Dodomya watu wakipiga makofi mengiiiiiiiiiiiiii lakini nikajiemea kamwe usiusemee moyo wa mtu.

Hakika Mwenyekigoda hakutumia BUSARA wala HEKIMA.Ningekuwa mimi kwenye viatu vyake ningefanya haya:

1.Kwenye Kamati ya maadili ningewaomba wagombea wote waliojipigia debe mapema wenyewe wajiondoe ili CHAMA kisipate mushkeli kwenye UCHAGUZI mkuu kwa kuambiwa kwamba CCM ilianza kampeni mapema.

2.Ningejiondoa kwenye uenyekiti nikamwachia Mangula kiti kwa kisingizio kwamba ....SITAKUWA huru kwenye kuamua wathungu wangesema 'INTEREST OF CONFLICTS'

3.Ningeacha waliobaki wajieleze kwenye kamati ya maadili na kila mmoja ajibu kulingana na INTERVIEW atakayokuwa amepewa na jopo la KAMATI ya maadili

4.Ningesubiri kwenye mkutano mkuu yale majina yakiwa yameshachambuliwa.

Kutoka hapo ningekuwa nimenawa mikono kama alivyofanya PONSIO PILATO,makundi yangekuwepo,lakini yangeweza kuelewa kwa uwazi kabisa bila kuleta CHUKI wala mvurugano kwenye chama, nina uhakiak ningetoka kifua mbele kwa uamuzi huu.

Simfagilii LOHASSA ila kilichofanyika ndiyo siyo sahihi.............

Naomaba ya tafakari haya kisha unijibu kama ningekuwa MSHINDI au?Na ndiyo maana nasema 'Tupewe nafasi Tu, Tusiwezeshwe kwani Tunaweza bila Kuwezeshwa'.

We binti wa Tupatupa una akili sana wewe, hebu pokea like yako hapo, sim yangu haina kitufe cha like
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom