Lumumba kwafukuta; Ya Dodoma yaanza kutoa cheche

Lumumba kwafukuta; Ya Dodoma yaanza kutoa cheche

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Tangu makada warudi toka Dodoma (mimi nilitangulia kurudi Dar es Salaam), hali si shwari ndani ya Ofisi Ndogo za CCM hapa Lumumba. Makada wanapingana kimakundi yaliyopata na kukosa ushindi kule Dodoma. Wapo makada wenye tabasamu la hamu na wale wenye sura zilzosheheni hasira. Hali si ile. Imebadilika.

Kazi zinakwenda polepole na hata hakuna wa kumuuliza mwingine kwa staha na raha. Maneno na matendo ya makada yamebadilika. Utaniutani uliokuwa ukituunganisha,umepungua na kuonekana unasumbua. Sasa ni urafiki wa kinafiki tu. Kwa werevu,tunayaona makovu ya Dodoma. Yanafanya kazi sasa. Kununiananuniana ofisini kumekwamisha hata Redio Uhuru kutenda kazi zake ipasavyo. TCRA wanaivizia kuifunga kwa kutolipa kodi. Kodi imekwamishwa.

Viongozi mpo? Hali si shwari chamani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
he! hakuna demokrasia ya kazi hapo lumumba? mzee kingunge kama alikua kaongeaa kitu.....
 
VUTA-NKUVUTE


Bintiyo nilikuwa nakusubiri kwa HAMU kubwa utupe ukoko uliobaki kule Dodomya.Niliona UNAFIKI toka Dodomya watu wakipiga makofi mengiiiiiiiiiiiiii lakini nikajiemea kamwe usiusemee moyo wa mtu.

Hakika Mwenyekigoda hakutumia BUSARA wala HEKIMA.Ningekuwa mimi kwenye viatu vyake ningefanya haya:

1.Kwenye Kamati ya maadili ningewaomba wagombea wote waliojipigia debe mapema wenyewe wajiondoe ili CHAMA kisipate mushkeli kwenye UCHAGUZI mkuu kwa kuambiwa kwamba CCM ilianza kampeni mapema.

2.Ningejiondoa kwenye uenyekiti nikamwachia Mangula kiti kwa kisingizio kwamba ....SITAKUWA huru kwenye kuamua wathungu wangesema 'INTEREST OF CONFLICTS'

3.Ningeacha waliobaki wajieleze kwenye kamati ya maadili na kila mmoja ajibu kulingana na INTERVIEW atakayokuwa amepewa na jopo la KAMATI ya maadili

4.Ningesubiri kwenye mkutano mkuu yale majina yakiwa yameshachambuliwa.

Kutoka hapo ningekuwa nimenawa mikono kama alivyofanya PONSIO PILATO,makundi yangekuwepo,lakini yangeweza kuelewa kwa uwazi kabisa bila kuleta CHUKI wala mvurugano kwenye chama, nina uhakiak ningetoka kifua mbele kwa uamuzi huu.

Simfagilii LOHASSA ila kilichofanyika ndiyo siyo sahihi.............

Naomaba ya tafakari haya kisha unijibu kama ningekuwa MSHINDI au?Na ndiyo maana nasema 'Tupewe nafasi Tu, Tusiwezeshwe kwani Tunaweza bila Kuwezeshwa'.
 
Last edited by a moderator:
Piganeni kabis, kama vipi Kingunge afanye yake siye huku tunashuhudia kwa mbaali.
 
Story za chini ya mwembe kazi ya Dodoma imeisha na Tingatinga liko mzigoni mtoa uzi inaonekana na wewe ni miongoni mwao kama vipi tupia picha zao kama hilo haliwezekani waambie watoke CCM maana hawalazimishwi kubakia huko!
 
Mzee wetu Kingunge anakinukisha,Mgombea wa mfukoni nayeye kuongea hawezi ni balaa tupu.Kingunge kinukishe sisi tunakuunga mkono
 
CCM mbona mnadharau wananchi?
Kwanini mlete mgombea wa ''kitengo'' na sio wa chama?
 
Tangu makada warudi toka Dodoma (mimi nilitangulia kurudi Dar es Salaam), hali si shwari ndani ya Ofisi Ndogo za CCM hapa Lumumba. Makada wanapingana kimakundi yaliyopata na kukosa ushindi kule Dodoma. Wapo makada wenye tabasamu la hamu na wale wenye sura zilzosheheni hasira. Hali si ile. Imebadilika.

Kazi zinakwenda polepole na hata hakuna wa kumuuliza mwingine kwa staha na raha. Maneno na matendo ya makada yamebadilika. Utaniutani uliokuwa ukituunganisha,umepungua na kuonekana unasumbua. Sasa ni urafiki wa kinafiki tu. Kwa werevu,tunayaona makovu ya Dodoma. Yanafanya kazi sasa. Kununiananuniana ofisini kumekwamisha hata Redio Uhuru kutenda kazi zake ipasavyo. TCRA wanaivizia kuifunga kwa kutolipa kodi. Kodi imekwamishwa.

Viongozi mpo? Hali si shwari chamani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Mzee wa busara mzee mwana kijiji katika vitu ambavo ccm hawataki kuvisikia ndio huu ukweli poleni hii ndio dhambi ya ubaguzi itawatafuna mpaka kiama na Kingunge kawaambia ukweli mchungu na hawataki kuusikia letu jicho.
 
Tetty, ninakuunga mkono kwa hayo mawazo yako..YANGEPUNGUZA SINTOFAHAMU KWA KIASI FULANI.
 
Hawa jamaa hucheza Na akili za watu saizi yapo kimya yakija him inakuwa taab
 
Hizi wishful thinking zenu mpaka lini?? Kama Mh.Magufuli aliweza kupata zaidi ya asilimia 80% ya kura zote,which means CCM sasa ni kitu kimoja i.e wana mshikamano thabiti,kama kuna watu waliokua wanasubiria igawanyike ili weweze kuishinda kirahisi hiyo wasahau.

Wacheni kuleta jamvini stori za kubuni ,mimi nawashaurini japangeni upya who knows labda mwaka 2055 mnaweza kufanikiwa mkiacha ubinafsi wa kugawa vyeo na Ubunge kwa marafiki zenu,ndugu zenu,wake zenu na washikaji zenu-je mkienda Ikulu si Taifa letu litafanana la URUSI enzi za Yelstin.

Hatusemi mambo ya kubuni hapa mifano/vihashilia vipo vya kuthibitisha hamjajipanga sawa sawa - kama UKAWA mnashindwa kuelewana nani abebe bendera ya upinzani nani anaweza kuwakabidhi Nchi Viongozi ambao masaa yote wapo kwenye chaotic Motions kama atoms za gesi ya Mnazi Bay/Songosongo!! Siwasem vibaya ila tukubaliane kwamba linapo kuja suala la kukabidhiwa Nchi - nyinyi bado saana ndio maana CUF wanawakacha.
 
Back
Top Bottom