VUTA-NKUVUTE
Bintiyo nilikuwa nakusubiri kwa HAMU kubwa utupe ukoko uliobaki kule Dodomya.Niliona UNAFIKI toka Dodomya watu wakipiga makofi mengiiiiiiiiiiiiii lakini nikajiemea kamwe usiusemee moyo wa mtu.
Hakika Mwenyekigoda hakutumia BUSARA wala HEKIMA.Ningekuwa mimi kwenye viatu vyake ningefanya haya:
1.Kwenye Kamati ya maadili ningewaomba wagombea wote waliojipigia debe mapema wenyewe wajiondoe ili CHAMA kisipate mushkeli kwenye UCHAGUZI mkuu kwa kuambiwa kwamba CCM ilianza kampeni mapema.
2.Ningejiondoa kwenye uenyekiti nikamwachia Mangula kiti kwa kisingizio kwamba ....SITAKUWA huru kwenye kuamua wathungu wangesema 'INTEREST OF CONFLICTS'
3.Ningeacha waliobaki wajieleze kwenye kamati ya maadili na kila mmoja ajibu kulingana na INTERVIEW atakayokuwa amepewa na jopo la KAMATI ya maadili
4.Ningesubiri kwenye mkutano mkuu yale majina yakiwa yameshachambuliwa.
Kutoka hapo ningekuwa nimenawa mikono kama alivyofanya PONSIO PILATO,makundi yangekuwepo,lakini yangeweza kuelewa kwa uwazi kabisa bila kuleta CHUKI wala mvurugano kwenye chama, nina uhakiak ningetoka kifua mbele kwa uamuzi huu.
Simfagilii LOHASSA ila kilichofanyika ndiyo siyo sahihi.............
Naomaba ya tafakari haya kisha unijibu kama ningekuwa MSHINDI au?Na ndiyo maana nasema '
Tupewe nafasi Tu, Tusiwezeshwe kwani Tunaweza bila Kuwezeshwa'.