Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 21,854
- 26,094
CCM INAHITAJI REFORMATION IKIBIDI IZALIWE UPYA!
PRES.MAGUFURI REFORM THIS PARTY ONCE AGAIN!
ii
PRES.MAGUFURI REFORM THIS PARTY ONCE AGAIN!
ii
Watu wametishwa. Watu wametishika. Makada watakosa za watoto ada. Kujenga kutasimama. Miradi itapigwa radi na kuishia kuwa ahadi. Chama kina utawala wake. Chama kina Mwenyekiti wake. Si huyo Rais wa Tanzania. Kwanini majipu ya chamani nayo yapaniwe kutumbuliwa?
Tumepata taarifa, isiyo na ya kuvutia sifa,kuwa jamaa anataka kupewa nafasi ajinafasi kuyatumbua majipu ya chamani. Lakini, ameombwa asubiri wakati wake ufike. Makada wanakipenda chama kwa 'maslahi yanayoleta uhai'. Yakikaushwa ghafla,hapatatosha. Lakini, Ofisi Ndogo za CCM Lumumba hapakaliki. Hakuna raha ila karaha kusubiri pigo la ghafla.
Makada nchi nzima wanamuunga mkono Rais kutumbua majipu pengine lakini si chamani. Chamani kunafukuta kwa hofu ya 'bifu' kuporwa mnofu. Makada wanatumikia chama na wao wenyewe. Wanatamani wale waminywe na wao wasiguswe ili wasisuse. Hawataki sera ile ifike humu chamani.
Serikalini sawa, chamani si sawa. Double standards!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
unaleta utani. jengo linamilikiwa ki halaliTetesi zinadokeza kwamba jengo la ofisi ndogo lumumba kurejeshwa kwa wananchi ili lifanywe machinga complex ( maana liko sehemu nzuri ya biashara ) kazi ipo .
Natamani sana ile katiba ya Wananchi iliyokuwa na kipengele cha uwepo wa mgombea binafsi ingepita ili Maghufuli agombee pasipo na chama next election. Nadhani Mh.Maghufuli angekuwa hana chama chochote angefanya kazi kwa nguvu zaidi. Kwa namna moja ama nyingine Mheshimiwa atapunguzwa kasi na chama chake tu.
Sisi tupo mtaani tunajionea jinsi wakubwa wa chama wanavyovunja sheria na kuibia serikali ila hakuna anayedhubutu kuwagusa.
Kwa kweli nimetokea kumkubali zaidi Maghufuli kwa mda mfupi japo sikumpigia kura. Na sikumpigia kura maana naichukia sana ccm"
"EWE MWENYEZI MUNGU TUNAKUOMBA UMLINDE RAIS WETU JOHN P MAGUFULI NA HILA ZOTE ZA ADUI SHETANI. UMLINDE NA WABAYA WOTE WANAOTAKA KUMKWAMISHA KATIKA SAFARI YAKE ALIYOIANZA YA KUIJENGA UPYA TANZANIA".
Hivyo ndivyo vitakavyotumiwa kisiasa,yale majipu mama na sugu hakuna mwenye ubavu wa kuyatumbua.
Huu ndio ukweli na hata DuppyConqueror na wenzie wanayajua yote haya
Mi nataka watumbue lile jipu linalomaliza tembo wetu lile ni likatibu mkuu pale Lumumba,,, hapo nitajua JPM anamaanisha anachosema
Wakiona anawazingua sana waropoke tu kwamba "kushinda kwenyewe hukushinda tulikubeba halafu unaleta za kuletwa?"
Wakiona anawazingua sana waropoke tu kwamba "kushinda kwenyewe hukushinda tulikubeba halafu unaleta za kuletwa?"
Kwi kwi kwi kwi!! Mkuu hebu tupe tofauti ya shuka na pazia
CCM ndo wanaisoma namba!
Mimi nataka jipu lililomaliza muda wake
Tutegemee kuona magofu ya majumba mengi sana maana watu walipata fedha za kideal deal tu, sasa mzee kaziba deal mtajiharish......., heri yetu sisi tulisha yazoea!