Lumumba hapakaliki, CCM kwafukuta

Lumumba hapakaliki, CCM kwafukuta

hahahaha kichaa kakabidhiwa rungu......siku moja nilimskia sumaye akisema ..msimchague magufuli mana huwa hashauliki..ila kwa kuwa anawatumbua wakulu awatumbue tu hakuna namna
 
Kweli magufuli hatari, ila nasubiri nione maana mengi yanasemwa sana
 
Ujinga Maradhi na Umasikini kwa saanaaa ..... Kama kuna mtu mwenye akili bado anamatumaini ya maisha bora chini ya ccm ajipime mwenyewe kabla ya kwenda kwa daktari ...
 
atakuwa bora akifuta mwenge unaoeneza Ukimwi, na kumaliza fedha za watanzania
 
Sisi Wakwere tuna methali isemayo : kidege che sikiumanyile ulimbo kigwilaga na mabawa gose. Yaani, ndege asiyeujua ulimbo, hunaswa na mabawa yote. Ndege kanaswa, dawa yake ni kuliwa tu!

Hii methali ya kikwere inaweza kutusaidia kumbua jibu la mkwere nambari one!? Msaada tafadhali, maana hilo ni jipu baya kabisa.
 
Teteteeee...pressure za UKAWA hizo ndani ya Lumumba kutaka mabadiriko yatoke ndani na si nje.....tutaona.
 
Ndoa ndoano?
Mbavu zangu? Yaani Magufuli asipokuwa makini atavunja ndoa ya Chama chake na Sirikali na mwisho wa siku sijui atakuwa mgeni wa Nani?
Ndoa wanajuana waliooana na thamani yake! Wale wakuja na kuingilia ndoa za watu ni kuhatarisha Ndoa za watu na watu watapigana kufa na kupona kulinda ndoa zao.

Bibi na bwana wakigombana nyumbani, waache wenyewe wataelewana, ikawa ukawaingilia, utanakinanieee....wimbo'
 
Nyerere aliposema mabadiliko ya kweli yatatoka ndani ya ccm ni pamoja na chama kuondoa kama sio kuwafichua wote waliokichafua chama kwa kashfa za kipuuuzi,rushwa na ufisadi,ni pamoja na kulipuwa wale wote wanafiki waliokuwa wanatumia mgongo wa kuwepo ndani ya chama kukihujumu chama,tuliotaka mabadiliko ya kweli ndani ya chama tupo nae sambamba wao waliofikiri wataendeleza unafiki wao ndani ya chama ndo hao wanaoanza kujikanyaga na watanyoooshwa tu.....tusubiri 2017 jembe tutakapomkabidhi rasmi rungu la chama.........
 
salute kwako mzee edward lowassa kwa kusababisha CCM wamteue magufuli kuwa mgombea urais.vinginevyo tusinge yashuhudia/sikia haya.mungu ibariki Tanzania,mungu mbariki Edward lowassa.

Kula tano baba umeona mbali sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom