Lumumba hapakaliki, CCM kwafukuta

Lumumba hapakaliki, CCM kwafukuta

CCM ndo wanaisoma namba!

ImageUploadedByJamiiForums1448349901.966297.jpg
Hakika mchimba kaburi kaingia mwenyewe. Nikikumbuka zile nyimbo za bashasha za kuisoma namba na hofu iliyotanda ndani ya vigogo wa chama na serikali kwa sasa naishia kucheka tuu.
Yupo jamaa yangu aliposikia lile katazo la safari za nje aliishia kusema "mama yangu, tumekwisha!" Nilipomuuliza kwa nini aliishia kunikata jicho kali kweli. Ila nilielewa kuwa nami vile vijizawadi kila akirudi ndio vimefikia ukomo.
 
Sio kwamba namba inasomwa tu!!! La hasha bali namba inasomwa na kuandikwa na wavivu, walarushwa wazee wa short cut na wazee wa chajuu (10%)
 
salute kwako mzee edward lowassa kwa kusababisha CCM wamteue magufuli kuwa mgombea urais.vinginevyo tusinge yashuhudia/sikia haya.mungu ibariki Tanzania,mungu mbariki Edward lowassa.
 
Natamani sana ile katiba ya Wananchi iliyokuwa na kipengele cha uwepo wa mgombea binafsi ingepita ili Maghufuli agombee pasipo na chama next election. Nadhani Mh.Maghufuli angekuwa hana chama chochote angefanya kazi kwa nguvu zaidi. Kwa namna moja ama nyingine Mheshimiwa atapunguzwa kasi na chama chake tu.
Sisi tupo mtaani tunajionea jinsi wakubwa wa chama wanavyovunja sheria na kuibia serikali ila hakuna anayedhubutu kuwagusa.
Kwa kweli nimetokea kumkubali zaidi Maghufuli kwa mda mfupi japo sikumpigia kura. Na sikumpigia kura maana naichukia sana ccm"
"EWE MWENYEZI MUNGU TUNAKUOMBA UMLINDE RAIS WETU JOHN P MAGUFULI NA HILA ZOTE ZA ADUI SHETANI. UMLINDE NA WABAYA WOTE WANAOTAKA KUMKWAMISHA KATIKA SAFARI YAKE ALIYOIANZA YA KUIJENGA UPYA TANZANIA".
 
Wee nawe hata hujielewi Moshi imeingiaje hapa wivu mwingine bana aliyepewa kapewa tu wee endelea kushikilia vibuyu na ulozi ukiusubiri utajiri na mendeleo Moshi falsafa ya hapa kazi tu ilianzia toka enzi za mababu zetu angalia kihoro kisikuuwe karibu.

mambo meku
 
Watu wametishwa. Watu wametishika. Makada watakosa za watoto ada. Kujenga kutasimama. Miradi itapigwa radi na kuishia kuwa ahadi. Chama kina utawala wake. Chama kina Mwenyekiti wake. Si huyo Rais wa Tanzania. Kwanini majipu ya chamani nayo yapaniwe kutumbuliwa?

Tumepata taarifa, isiyo na ya kuvutia sifa,kuwa jamaa anataka kupewa nafasi ajinafasi kuyatumbua majipu ya chamani. Lakini, ameombwa asubiri wakati wake ufike. Makada wanakipenda chama kwa 'maslahi yanayoleta uhai'. Yakikaushwa ghafla,hapatatosha. Lakini, Ofisi Ndogo za CCM Lumumba hapakaliki. Hakuna raha ila karaha kusubiri pigo la ghafla.

Makada nchi nzima wanamuunga mkono Rais kutumbua majipu pengine lakini si chamani. Chamani kunafukuta kwa hofu ya 'bifu' kuporwa mnofu. Makada wanatumikia chama na wao wenyewe. Wanatamani wale waminywe na wao wasiguswe ili wasisuse. Hawataki sera ile ifike humu chamani.

Serikalini sawa, chamani si sawa. Double standards!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

aha ha mzee tupa, kuna vibwengo humu kutoka lumumba , jingalao, ritz faiza fox, tatamadiba, mwandiwani, lizaboni gentamycine, hawa kazi yao wakiamka tu ni kutukana UKAWA tu kwa ujira wa buku saba

Magufuli ameahidi kukifuta hiki kitengo cha matusi dhidi ya UKAWA kilichokuwa kinaratibiwa na Nape,
kwani amegundua kwa sasa hakina tija kwa chama chake,

amini amin zile buku saba walizokuwa wanalipwa kutwa hao niliowatja hapo juu zimefutwa rasimi,

sasa tutarajie kurudisha hadhi ya jf kama zamani, JF for great thinkers na watu wasomi wenye weledi kama ilivyokuwa zamani kabla ya mradi huu ovu wa nape,

buku saba lumumba wameidhoofisha jf mpaka kufika hatua watu makini kujitoa JF hii hakika itakuwa ni habari njema kwa GT
 
CCM na wale wavivu ndani ya nchi hii, wanaotegemea udhaifu wa uongozi kujinufaisha wataisoma namba.

Magufuli anaweza kuirudishia siasa heshima yake stahiki, wanaokimbilia siasa kujinufaisha huenda wakajitoa mapema.

Ifike mahali wananchi wanawatafuta watu wa kuwaongoza, baada ya wao kuhongwa kuongozwa.

Rais Magufuli kaza zaidi wanakaribia kukimbia siasa warudi kwenye professional zao, mtu ni Injinia, Daktari, Nahodha unahangaika kuwa mwanasiasa wapi na wapi, rudieni kazi zenu mlizosomea.
 
waliompenda wanamchukia, waliomchukia wanampenda
 
Hamieni kule walikoenda wale wengine.
Awamu hii tutajua tu kutofautisha kati ya shuka na pazia.

Raha sana naomba kuuliza nani alikuwa mmiliki wa Uchumi supermarkets na mbona walikuja kwa kasi ya ajabu na wakaondoka kwa kasi ya ajabu vip kuhusu home shopping centre
 
Pelekeni ufataani wenu Ufipa, Lumumba yupo kiboko yenu Kinana.

Mtapaota sana.

Habari za asubuhi mama, umeona tofauti ya rais wa dini hii na ile? Zamani watu walikuwa wakizungumzia udhaifu wa rais ulikuwa unamkingia kifua kwa ajili ya dini yake. Nadhani sasa umeona tofauti ya utendaje na sio kuingiza mambo ya imani kuficha udhaifu. Sikumpa kura Magufuli na wala sidhani kama nitampa kura mwanaccm yoyote ila kwa hili analofanya Magufuli imekaa sawa. Na hakuna mtu anamsifia Magufuli kwa ajili ya dini yake bali ubora wake na ukiona mtu anasifiwa kwa ajili ya dini yake ujue huyo ni dhaifu.
 
CCM ndo wanaisoma namba!

Kwa kufafanua ni kwamba wanaoisoma namba ni team Lowassa ndani ya CCM ambao walitegemea awe rais kwa tiketi ya CCM akakatwa. Walitegemea apate kwa UKAWA akakatwa tena. Laiti angepata tungeona wakihama toka CCM kwa wingi wao kumfuata bosi wa mtandao, EL. Waliasisi MFUMO uliokichafua chama cha ccm. Hao ndo walikuwa wakiimba pale Dodoma- tuna imani na Lowassa. Hao ndo JPM aliwasema mchana ccm, usiku UKAWA. Hao ndo wanaisoma namba T2015JPM. Wengine sisi roho kwatuuu. CCM mbele kwa mbele.
 
Hahaaaaaa hii umehack kwa mafunzo ya Mkorea aliyekuja kugushi matokeo uchaguzi Mkuu? Ccm haipokei order toka Moshi,kila mteuzi ana madaraka yake ya kuongoza. Kama yapo majibu huko Ccm jitayarisheni kuyapokea yaje yatumbuke huko. Wameshaambiwa wanafiki waondoke. Kwa kasi hii ya Magufuli hata haitaji nguvu ya chama sisi wananchi tuko nyuma yake

Sumu ya ukabila na ukanda haitakuacha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom