Siandiki kuhusu falsafa na wenyewe kuwarejea, tena siandiki kuhusu mzaha ili wale kuwatania, bali naandika kuhusu amana kwa watu wake kuirejesha,tena nasisitiza naandika kuhusu neema ya akili popote kuizungumzia.
Akili kwa ufupi sana na kwa lugha nyepesi ni kizuizi kinachomfanya mtu asitumbukie katika makosa, na kujua lipi baya na lipi zuri, lipi linafaa na lipi halifai, kuiongelea akili kuna hitaji muda mwingi na marejeo tele. Lakini leo nawakumbusha jamaa, watoto na wavyele juu ya utukufu wa akili, kwa kumili katika maswali mawili ya msingi sana, na kwa kutumia akili ipasavyo utaona hazina iliyofichika.
Fikiri kwa makini na utafakari, juu ya maswali haya mawili hapa chini, kisha utuonyeshe ulichokiona.
1. Kwanini watu wanaomba uongozi, yaani wanaomba kupewa uongozi na wawe viongozi ? Je hili lina faa na ni jambo la busara au kinyume chake?
2. Je, kwanini watu wanachagua viongozi ? Ni nani mwenye sifa madhubuti na stahiki ya kuchagua kiongozi ?
Akili kwa ufupi sana na kwa lugha nyepesi ni kizuizi kinachomfanya mtu asitumbukie katika makosa, na kujua lipi baya na lipi zuri, lipi linafaa na lipi halifai, kuiongelea akili kuna hitaji muda mwingi na marejeo tele. Lakini leo nawakumbusha jamaa, watoto na wavyele juu ya utukufu wa akili, kwa kumili katika maswali mawili ya msingi sana, na kwa kutumia akili ipasavyo utaona hazina iliyofichika.
Fikiri kwa makini na utafakari, juu ya maswali haya mawili hapa chini, kisha utuonyeshe ulichokiona.
1. Kwanini watu wanaomba uongozi, yaani wanaomba kupewa uongozi na wawe viongozi ? Je hili lina faa na ni jambo la busara au kinyume chake?
2. Je, kwanini watu wanachagua viongozi ? Ni nani mwenye sifa madhubuti na stahiki ya kuchagua kiongozi ?