EPISODE 1: Uchambuzi wa kitabu cha Siri za Akili ya Mtu Tajiri

Aug 25, 2019
79
80
EPISODE ONE
________________________________

UCHAMBUZI MAKINI WA KITABU CHA:

"SIRI ZA AKILI YA MTU TAJIRI" (SECRETS OF THE MILLIONAIRE MIND).
NA:

LEONARD JULIUS SHIGANGA WA MWANAMATINGATINGA.

Kitabu hiki kimeandikwa na T. HARV EKER, ambaye ni milionea, mwandishi na mzungumzaji maarufu nchini marekani. Kupitia mafudisho yake, watu wengi wametajirika na kufanikiwa sana kutoka kwenye umasikini wa kutupwa hadi kuwa milionea.

Ikiwemo mwandishi yeye mwenyewe (Eker), ambaye hapo awali alikuwa maskini wa kutupwa lakini mara baada ya kuzijua na kuzifanyia kazi SIRI hizi aliinuka na kuwa milionea ndani ya muda mchache.

Karibu tujifunze kwa pamoja SIRI ZA AKILI YA MTU TAJIRI. Siri ambazo watu waliofanikiwa walizitumia na wanaendelea kuzitumia ili kujiletea utajiri zaidi na zaidi.

Eker, ambaye ni tajiri mkubwa anasema kwamba, watu waliofanikiwa huwa wanafikiri kwa namna fulani ambayo ni tofauti sana na jinsi watu maskini wanavyofikiri na kupitia tofauti hiyo ya fikira ndio inaamua matendo yao na kuleta matokea tofauti kati ya mtu tajiri na maskini.

EKER, anaendelea kusema kuwa, kama utafikiri kwa njia ambayo matajiri huwa wanafikiri na kufanya kile ambacho matajiri wanafanya, utakuwa miongoni mwao.

(Shika kichwa chako na useme kwa imani)
"NINAKICHWA CHA DHAHABU"

Eker, anatufundisha somo kuwa, ikiwa unataka kupiga hatua flani katika maisha kuelekea juu, lazima uwe tayari kuachilia baadhi ya fikira zako za zamani ambazo zimepitwa na wakati au fikira potovu na kuwa tayari kukopi na kujifunza fikira mpya zitakazokusaidia kupiga hatua na matokeo yake yatajizihilisha menyewe.

MWONGOZO JUU YA PESA NA MAFANIKIO.

Eker, katika kitabu chake ameonyesha kuwa SHERIA ZA PESA zimegawanyika katika makundi makuu mawili.

KUNDI LA KWANZA: sheria ya PESA ya ndani au mwongozo wa PESA uliyoko ndani kabisa ya mtu. Mwongozo huu unatokana na maswali yafuatayo:
i: wewe ni nani?
ii: unawaza nini?
iii: unaamini nini kuhusu pesa?
iv: tabia zako ni zipi?
v: unajiamini vipi?
Vi: ni kweli kuwa unahisi unasitahili kuwa tajiri?
Vii: uwezo wako wa kutenda dhidi ya hofu ni upi?

Ukweli hapa ni kwamba, Tabia yako, fikira zako na imani yako ni sehemu muhimu zinazotoa mwelekeo na kiwango cha mafanikio yako. Kumbuka kuwa, kitu pekee kinachozuia mafanikio yako SIO kitu ambacho hukijui, rahasha, kikwazo pekee cha mafanikio yako ni kile kitu ambacho unakijua kwa njia isiyo sahihi.

Eker, anasema kuwa, moja ya kanuni ya utajiri ni kwamba, KIPATO CHAKO KINAWEZA KUKUA NA KUONGEZEKA KUTOKANA NA JITIHADA UNAZOCHUKUA.
ulishawahi kuona watu ambao walikuwa na pesa nyingi sana lakini baadae zikawatoka? Hii ndio sababu ya kwamba, ukipata pesa nyingi na ukawa haujajitayarisha ndani yako (mwongozo wa ndani), pesa zitaishi kwako kwa muda mfupi na kutoweka kabisa.

Na hii ni kwasabu, watu wengi hawana uwezo wa ndani wa kutengeneza na kumiliki pesa nyingi ndio maana haziji kabisa au zinakuja na kuwakimbia. Mfano halisi, ni wale wanaoshinda michezo ya kubahatisha au wale wanaopata pesa nyingi kwa ghafla machimboni kwenye migodi ya madini.

Mara baada ya kuipata, pesa huwa inawakimbia na hatimaye kurudi kwenye kiwango chao cha pesa wanachoweza kumiliki kutokana na uwezo wao wa ndani. " Internal Comfort zone"

#Jambo pekee la kujifunza hapa ni kwamba, MIZIZI NDIO INATENGENEZA MATUNDA.

Chukulia kwa mfano, mti huu unasimama kwa niamba ya mti wa maisha na kwenye mti huu kuna matunda. Kwenye maisha matunda yetu ni matokeo yetu. Kwahiyo tukiangalia matunda (matokeo yetu), ikiwa hatuyapendi, hayajitoshelezi, mabaya, madogo sana na hayana radha.

Kwahiyo tufanyeje? Wengi wetu tutaangalia zaidi matunda (matokeo yetu). Lakini ukweli ni kwamba, tunahitaji kujiuliza zaidi juu ya kitu gani kimeyatengeneza hayo matunda (matokeo)? Jibu ni kwamba, ni mbegu na mizizi ndio inatengeza matunda (matokeo).

#Eker anasema, ni kile kitu ambacho kiko chini ndicho kinatengeneza kile kitu kinachoonekana juu ya ardhi, ni kitu ambacho hakionekani ndicho kinaunda kitu ambacho kinaonekana.

Somo pekee la kujifunza kwenye EPISODE#1. Ni kwamba, ikiwa unataka kubadilisha kipato chako lazima ubadilishe kazi au uboreshe mazingira ya kazi yako, karibisha fikira, elimu, ujuzi, maarifa, uzoefu, ufahamu, mawazo, mtazamo, hisia, imani na matendo mapya.

MWISHO wa EPISODE#1

"You cannot change the fruits that are already hanging on the tree. You can, however, change tomorrow's fruits. But to do so, you will have to dig below the ground and strengthen the roots"
______________________________________
#kama umependezwa zaidi na makala hii, niandikie "comments" hapo chini, PIA kumbuka " kulike" na "kushare" na wengine ili wajifunze zaidi na kufuatilia " EPISODES" zinazofuata.

Lakini pia, kumbuka "kunifollow" Facebook, Twitter na Instagram kwa majina ya: Leonard Julius. Ili tujifunze zaidi kwa pamoja.

#THINKANDTAKESTEPS
shiganga@gmail.com
 
________________________________________________
UCHAMBUZI MAKINI WA KITABU CHA:

"SIRI ZA AKILI YA MTU TAJIRI" (SECRETS OF THE MILLIONAIRE MIND)

NA:
LEONARD JULIUS SHIGANGA WA MWANAMATINGATINGA.

Kitabu hiki kimeandikwa na T. HARV EKER, na kimechapishwa mnamo mwaka 2005.

KUHUSU MWANDISHI

EKER, ni mwandishi wa vitabu, milionea na mzungumzaji maarufu nchini Marekani.

Ambaye kupitipia uandishi wake na Mafundisho yake, amefanikiwa kubadilisha maisha ya watu wengi sana, kutoka kwenye umaskini wa kutupwa hadi kuwa Mamilionea.

EKER, ameweza kubadili fikira za watu wengi sana kuhusu miongozo na kanuni za pesa na utajiri, hasa fikira za watu ambao hapo mwanzo, waliamini kuwa, wao hawajazaliwa kuwa matajiri.

Lakini mara baada ya kupatiwa mafunzo na kusoma kitabu chake, wameweza kubadilika na kuchukua hatua na leo hii ni Mabilionea.

Karibu sana katika EPISODE ya PILI ya uchambuzi wa kitabu hiki cha SIRI ZA AKILI YA MTU TAJIRI. Siri ambazo zimebadilisha maisha ya EKER kutoka kwenye umaskini wa kutupwa hadi kuwa Milionea.

Kama SIRI hizi zimeweza kusaidia watu wengi kiasi hicho kuwa matajiri. Wewe ni nani ushindwa kutajirika kupitia SIRI hizi? kama wewe ni mtu mwenye akili timamu, basi itoshe kusema karibu tujifunze kwa pamoja.

MWONGOZO JUU YA PESA NA UTAJIRI_SEHEMU YA PILI.

Eker, anaanza kwa kueleza kuwa, mwongozo wako juu ya pesa na utajiri unajumuisha mambo makuu manne yaani, fikira, hisia, hatua na matokeo.

Eker, anauliza maswali ya msingi kuwa, "Unadhani kuwa, mtoto huwa anazaliwa kutoka tumboni mwa mama yake akiwa na fikira juu ya pesa? Au Unaamini kuwa mtoto huwa anafundishwa jinsi ya kushughulika na pesa?

Eker, anajibu kuwa, "kila mtoto huwa anafundishwa jinsi ya kufikiri na kushughulika na masuala yote yanayohusu pesa"

Na huu ndio ukweli usiopingika, kwangu, kwako na kwa kila mmoja. Sote tulifundishwa na tunafundishwa jinsi ya kufikiri na kushughulika na masuala yote yanayohusu pesa, na Mafundisho haya ndio huwa TABIA yako ambayo huwa inakuwa mwitikio wako wa moja kwa moja kwenye maisha yako yoye.

Eker, anaendelea kueleza na kuuliza kuwa, "Fikira za mtu huwa zinatoka wapi? " Kwanini TAJIRI anafikiri tofauti na mtu MASKINI?

Eker, anaeleza kuwa, fikira zako huwa zinatoka kwenye Majalada (files) ya taarifa zilizotunzwa kwenye kumbukumbu za akili yako ambazo huwa zinatokana na historia ya maisha yako ya nyuma.

Historia ya maisha yako ya nyuma ndio huwa inaongoza FIKIRA zako, na fikira zako ndizo zinaongoza HISIA zako, na hisia zako ndizo zinaongoza MATENDO yako, na matendo yako ndio yanaleta MATOKEO ya kila kitu unachofanya.

Eker, anatufundisha somo kwamba, ukitaka kubadilisha matokeo yako lazima kwanza uanze kwa, kubadilisha historia na taarifa zako za nyuma.

HISTORIA YA MAISHA YAKO (MFUMO WA MAISHA YAKO)

Mfumo wa maisha yako juu ya pesa, umejengwa na vishawishi vikuu VITATU. Ambovyo ni:-
1: Programu ya Maneno (Verbal Programming).

2: Kuiga au kushuhudia (modeling).

3: Matukio maalum (specific incidents).

NB: Twende tujifunze kishawishi kimoja baada ya kingine.

1. KISHAWISHI CHA PROGRAMU YA MANENO (Verbal programming)

Kishawishi hiki kinatokana na chimbuko lako kuwa, uliambiwa na kusikia nini wakati ukiwa mdogo?

Uliambiwa nini kuhusu pesa na utajiri?
Uliambiwa nini kuhusu matajiri kipindi unakua?

Uliwahi kusikia au kuambiwa kuwa, pesa ndio chanzo cha maovu yote?
Uliwahi kuambiwa kuwa, matajiri ni wachoyo na bahili?

Uliwahi kuambiwa kuwa, matajiri ni waovu?
Uliwahi kuambiwa kuwa, huwezi kuwa tajiri na ukawa mtu mwema kiroho?

Kwa kifupi ni kwamba, mambo yote uliyosikia kuhusu pesa huwa yanatunzwa kwenye kumbukumbu za akili yako, na baadae yanakuwa ndio mwongozo wako wa maisha kuhusu pesa na utajiri.

Eker, anaeleza kuwa, chukulia kwa mfano, uliwahi kuambiwa "Matajiri ni wachoyo, bahili na wanajipatia pesa na utajiri wao kwa kuwanyonya watu maskini"

#Somo la kujifunza hapa ni kwamba, kama hili ndio Jalada (file), lililotunzwa kwenye kumbukumbu ya akili yako. Daima huwezi kuwa Tajiri kwasababu utaogopa kuwa MCHOYO, MUOVU, BAHILI na MNYONYAJI wa watu Maskini.

Eker, anasema kuwa, ili uwezo kuzitoa fikira potovu za namna hiyo kwenye akili yako, lazima utoe TAMKO kutoka moyoni mwako kuwa:

"Nilichoambiwa au kusikia kuhusu pesa na utajiri siyo lazima kiwe cha kweli, kwahiyo ninachagua na kukopi njia mpya na fikira ambazo zitanisaidia kuwa mtu Mwema, mwenye furaha na mafanikio"

(Shika kichwa chako na useme kwa imani)
"Ninakichwa cha Dhahabu"

2: KISHAWISHI CHA KUIGA AU KUSHUHUDIA (modeling)

Kishawishi hiki pia, kinatokana na chimbuko lako na historia ya maisha yako kuwa, "Uliwahi kuona kitu gani kipindi unakua?"

Eker, anatueleza kuwa, wazazi au walezi wako walikuwa na mtazamo gani kwenye eneo la PESA? Wote walikuwa wasimamizi na watunzaji wazuri wa PESA? Au mmoja wapo alikuwa hajui kusimamia na kutunza PESA?

Wazazi au walezi wako, walikuwa watunzaji "savers" au walabata "spenders" wa PESA?

Wazazi au walezi wako walikuwa ni wawekezaji wazuri?

Wazazi au walezi wako walikuwa na maarifa ya biashara? Mikakati ya uwekezaji?

Pesa ilikuwa inapatikana kwa urahisi kwenye familia yenu? Au ilikuwa inapatikana kwa kupambana sana?

PESA ilikuwa ndio chanzo cha amani na furaha nyumbani kwenu? Au ilikuwa chanzo cha migogoro na makabiliano makali ndani ya familia?

#Somo la kujifunza hapa ni kwamba, kwanini hizi taarifa ni muhimu kwako kuzijuwa? Bila shaka ulishawahi kusikia msemo kwamba, "Nyani huwa anaangalia jinsi nyani mwenzake anavyofanya". (Naomba samahani kwa kutumia mfano wa NYANI). Bila shaka na wewe ndio kusudi la kujuwa taarifa hizi za wazazi au walezi wako ili mwishoni uchague mwelekea mpya wa maisha yako.

Eker, anatueleza kwamba, kila kitu ulichojifunza kipindi unakua kitakuja kutumika kama mwongozo wa maisha yako juu ya PESA na UTAJIRI.

Eker, anaeleza kuwa, kama Shauku na Motisha yako ya kuwa TAJIRI Itatokana na sababu dhaifu kama vile, uoga, hasira, kulipiza kisasi, kinyongo au kujionyesha kwa watu kuwa wewe ndio mwamba. Pesa au Utajiri utakaoupata hauwezi kukuletea Amani na Furaha, kwasababu utajiri wako utakuwa umeambatana na mambo maovu.

#Njia pekee ya kujitoa kwenye mnyororo juu ya mambo uliyowahi kushuhudia ni kutoa TAMKO kutoka moyoni mwako kwamba, "Niliyoshuhudia kuhusu PESA na UTAJIRI ulikuwa ni mtazamo wao, lakini kwa sasa ninayo fursa ya kuchangua na kwenda na mtazomo wangu ambao utakuwa tofauti na wao"

3: KISHAWISHI CHA MATUKIO MAALUM (specific incidents)

Hii inatokana na ukweli kwamba, "uliwahi kupitia uzoefu gani kuhusu PESA na UTAJIRI?"

Eker, anasema kwamba, uzoefu huu ni muhimu kwasababu ndio unatoa taswira halisi ya imani yako kuhusu PESA na UTAJIRI.

#Mfano mzuri ni kwamba, Kuna mtu kipindi akiwa mtoto alikuwa kila akiomba pesa kwa Mama kwa ajili ya kununua PIPI, Mama yake alikuwa akimjibu kila mara kwamba:-

" Samahani mpendwa, sina pesa yoyote. Nenda kamuombe Baba yako ndiye mwenye pesa zote"

#Somo la kujifunza hapa ni kwamba, mtoto amekua maisha yake yote akijuwa kuwa, baba ndiye mwenye uwezo wa kutafta pesa na sio Mama. Kwahiyo mtoto atatembea na hili Jalada (File) kwenye akili yake hadi kwenye utu uzima.

MWISHO wa EPISODE#2

" Remember that, the first element of all change is awareness, watch yourself, become conscious, observe your thoughts, your fears, your habits, your actions. Put yourself under a microscope. Study yourself".
=============================
#kama umependezwa zaidi na makala hii, niandikie "comments" hapo chini, PIA kumbuka " kulike" na "kushare" na wengine ili wajifunze zaidi na kufuatilia " EPISODES" zinazofuata.

Lakini pia, kumbuka "kunifollow" Facebook, Twitter na Instagram kwa majina ya: Leonard Julius. Ili tujifunze zaidi kwa pamoja.

#THINKANDTAKESTEPS
shiganga@gmail.com
 
________________________________________________
UCHAMBUZI MAKINI WA KITABU CHA:

"SIRI ZA AKILI YA MTU TAJIRI" (SECRETS OF THE MILLIONAIRE MIND)

NA:
LEONARD JULIUS SHIGANGA WA MWANAMATINGATINGA.

Kitabu hiki kimeandikwa na T. HARV EKER, na kimechapishwa mnamo mwaka 2005.

KUHUSU MWANDISHI

EKER, ni mwandishi wa vitabu, milionea na mzungumzaji maarufu nchini Marekani.

Ambaye kupitipia uandishi wake na Mafundisho yake, amefanikiwa kubadilisha maisha ya watu wengi sana, kutoka kwenye umaskini wa kutupwa hadi kuwa Mamilionea.

EKER, ameweza kubadili fikira za watu wengi sana kuhusu miongozo na kanuni za pesa na utajiri, hasa fikira za watu ambao hapo mwanzo, waliamini kuwa, wao hawajazaliwa kuwa matajiri.

Lakini mara baada ya kupatiwa mafunzo na kusoma kitabu chake, wameweza kubadilika na kuchukua hatua na leo hii ni Mabilionea.

Karibu sana katika EPISODE ya PILI ya uchambuzi wa kitabu hiki cha SIRI ZA AKILI YA MTU TAJIRI. Siri ambazo zimebadilisha maisha ya EKER kutoka kwenye umaskini wa kutupwa hadi kuwa Milionea.

Kama SIRI hizi zimeweza kusaidia watu wengi kiasi hicho kuwa matajiri. Wewe ni nani ushindwa kutajirika kupitia SIRI hizi? kama wewe ni mtu mwenye akili timamu, basi itoshe kusema karibu tujifunze kwa pamoja.

MWONGOZO JUU YA PESA NA UTAJIRI_SEHEMU YA PILI.

Eker, anaanza kwa kueleza kuwa, mwongozo wako juu ya pesa na utajiri unajumuisha mambo makuu manne yaani, fikira, hisia, hatua na matokeo.

Eker, anauliza maswali ya msingi kuwa, "Unadhani kuwa, mtoto huwa anazaliwa kutoka tumboni mwa mama yake akiwa na fikira juu ya pesa? Au Unaamini kuwa mtoto huwa anafundishwa jinsi ya kushughulika na pesa?

Eker, anajibu kuwa, "kila mtoto huwa anafundishwa jinsi ya kufikiri na kushughulika na masuala yote yanayohusu pesa"

Na huu ndio ukweli usiopingika, kwangu, kwako na kwa kila mmoja. Sote tulifundishwa na tunafundishwa jinsi ya kufikiri na kushughulika na masuala yote yanayohusu pesa, na Mafundisho haya ndio huwa TABIA yako ambayo huwa inakuwa mwitikio wako wa moja kwa moja kwenye maisha yako yoye.

Eker, anaendelea kueleza na kuuliza kuwa, "Fikira za mtu huwa zinatoka wapi? " Kwanini TAJIRI anafikiri tofauti na mtu MASKINI?

Eker, anaeleza kuwa, fikira zako huwa zinatoka kwenye Majalada (files) ya taarifa zilizotunzwa kwenye kumbukumbu za akili yako ambazo huwa zinatokana na historia ya maisha yako ya nyuma.

Historia ya maisha yako ya nyuma ndio huwa inaongoza FIKIRA zako, na fikira zako ndizo zinaongoza HISIA zako, na hisia zako ndizo zinaongoza MATENDO yako, na matendo yako ndio yanaleta MATOKEO ya kila kitu unachofanya.

Eker, anatufundisha somo kwamba, ukitaka kubadilisha matokeo yako lazima kwanza uanze kwa, kubadilisha historia na taarifa zako za nyuma.

HISTORIA YA MAISHA YAKO (MFUMO WA MAISHA YAKO)

Mfumo wa maisha yako juu ya pesa, umejengwa na vishawishi vikuu VITATU. Ambovyo ni:-
1: Programu ya Maneno (Verbal Programming).

2: Kuiga au kushuhudia (modeling).

3: Matukio maalum (specific incidents).

NB: Twende tujifunze kishawishi kimoja baada ya kingine.

1. KISHAWISHI CHA PROGRAMU YA MANENO (Verbal programming)

Kishawishi hiki kinatokana na chimbuko lako kuwa, uliambiwa na kusikia nini wakati ukiwa mdogo?

Uliambiwa nini kuhusu pesa na utajiri?
Uliambiwa nini kuhusu matajiri kipindi unakua?

Uliwahi kusikia au kuambiwa kuwa, pesa ndio chanzo cha maovu yote?
Uliwahi kuambiwa kuwa, matajiri ni wachoyo na bahili?

Uliwahi kuambiwa kuwa, matajiri ni waovu?
Uliwahi kuambiwa kuwa, huwezi kuwa tajiri na ukawa mtu mwema kiroho?

Kwa kifupi ni kwamba, mambo yote uliyosikia kuhusu pesa huwa yanatunzwa kwenye kumbukumbu za akili yako, na baadae yanakuwa ndio mwongozo wako wa maisha kuhusu pesa na utajiri.

Eker, anaeleza kuwa, chukulia kwa mfano, uliwahi kuambiwa "Matajiri ni wachoyo, bahili na wanajipatia pesa na utajiri wao kwa kuwanyonya watu maskini"

#Somo la kujifunza hapa ni kwamba, kama hili ndio Jalada (file), lililotunzwa kwenye kumbukumbu ya akili yako. Daima huwezi kuwa Tajiri kwasababu utaogopa kuwa MCHOYO, MUOVU, BAHILI na MNYONYAJI wa watu Maskini.

Eker, anasema kuwa, ili uwezo kuzitoa fikira potovu za namna hiyo kwenye akili yako, lazima utoe TAMKO kutoka moyoni mwako kuwa:

"Nilichoambiwa au kusikia kuhusu pesa na utajiri siyo lazima kiwe cha kweli, kwahiyo ninachagua na kukopi njia mpya na fikira ambazo zitanisaidia kuwa mtu Mwema, mwenye furaha na mafanikio"

(Shika kichwa chako na useme kwa imani)
"Ninakichwa cha Dhahabu"

2: KISHAWISHI CHA KUIGA AU KUSHUHUDIA (modeling)

Kishawishi hiki pia, kinatokana na chimbuko lako na historia ya maisha yako kuwa, "Uliwahi kuona kitu gani kipindi unakua?"

Eker, anatueleza kuwa, wazazi au walezi wako walikuwa na mtazamo gani kwenye eneo la PESA? Wote walikuwa wasimamizi na watunzaji wazuri wa PESA? Au mmoja wapo alikuwa hajui kusimamia na kutunza PESA?

Wazazi au walezi wako, walikuwa watunzaji "savers" au walabata "spenders" wa PESA?

Wazazi au walezi wako walikuwa ni wawekezaji wazuri?

Wazazi au walezi wako walikuwa na maarifa ya biashara? Mikakati ya uwekezaji?

Pesa ilikuwa inapatikana kwa urahisi kwenye familia yenu? Au ilikuwa inapatikana kwa kupambana sana?

PESA ilikuwa ndio chanzo cha amani na furaha nyumbani kwenu? Au ilikuwa chanzo cha migogoro na makabiliano makali ndani ya familia?

#Somo la kujifunza hapa ni kwamba, kwanini hizi taarifa ni muhimu kwako kuzijuwa? Bila shaka ulishawahi kusikia msemo kwamba, "Nyani huwa anaangalia jinsi nyani mwenzake anavyofanya". (Naomba samahani kwa kutumia mfano wa NYANI). Bila shaka na wewe ndio kusudi la kujuwa taarifa hizi za wazazi au walezi wako ili mwishoni uchague mwelekea mpya wa maisha yako.

Eker, anatueleza kwamba, kila kitu ulichojifunza kipindi unakua kitakuja kutumika kama mwongozo wa maisha yako juu ya PESA na UTAJIRI.

Eker, anaeleza kuwa, kama Shauku na Motisha yako ya kuwa TAJIRI Itatokana na sababu dhaifu kama vile, uoga, hasira, kulipiza kisasi, kinyongo au kujionyesha kwa watu kuwa wewe ndio mwamba. Pesa au Utajiri utakaoupata hauwezi kukuletea Amani na Furaha, kwasababu utajiri wako utakuwa umeambatana na mambo maovu.

#Njia pekee ya kujitoa kwenye mnyororo juu ya mambo uliyowahi kushuhudia ni kutoa TAMKO kutoka moyoni mwako kwamba, "Niliyoshuhudia kuhusu PESA na UTAJIRI ulikuwa ni mtazamo wao, lakini kwa sasa ninayo fursa ya kuchangua na kwenda na mtazomo wangu ambao utakuwa tofauti na wao"

3: KISHAWISHI CHA MATUKIO MAALUM (specific incidents)

Hii inatokana na ukweli kwamba, "uliwahi kupitia uzoefu gani kuhusu PESA na UTAJIRI?"

Eker, anasema kwamba, uzoefu huu ni muhimu kwasababu ndio unatoa taswira halisi ya imani yako kuhusu PESA na UTAJIRI.

#Mfano mzuri ni kwamba, Kuna mtu kipindi akiwa mtoto alikuwa kila akiomba pesa kwa Mama kwa ajili ya kununua PIPI, Mama yake alikuwa akimjibu kila mara kwamba:-

" Samahani mpendwa, sina pesa yoyote. Nenda kamuombe Baba yako ndiye mwenye pesa zote"

#Somo la kujifunza hapa ni kwamba, mtoto amekua maisha yake yote akijuwa kuwa, baba ndiye mwenye uwezo wa kutafta pesa na sio Mama. Kwahiyo mtoto atatembea na hili Jalada (File) kwenye akili yake hadi kwenye utu uzima.

MWISHO wa EPISODE#2

" Remember that, the first element of all change is awareness, watch yourself, become conscious, observe your thoughts, your fears, your habits, your actions. Put yourself under a microscope. Study yourself".
=============================
#kama umependezwa zaidi na makala hii, niandikie "comments" hapo chini, PIA kumbuka " kulike" na "kushare" na wengine ili wajifunze zaidi na kufuatilia " EPISODES" zinazofuata.

Lakini pia, kumbuka "kunifollow" Facebook, Twitter na Instagram kwa majina ya: Leonard Julius. Ili tujifunze zaidi kwa pamoja.

#THINKANDTAKESTEPS
shiganga@gmail.com
Ngoja nikae kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom