Lukuvi amefanya mengi sana pale wizara ya ardhi na alikuwa na maono, mipango na mikakati sahihi.
Lukuvi ndiye aliyehamisha kazi ya kutoa hati milki za ardhi kutoka wizarani na kwenda kwenye ofisi za Kanda. Haikupita muda akashusha mpk ofisi za mikoa.
Kaingia Angelina Mabula akataka kuendeleza maono ya Lukuvi lkn viatu havikumtosha.
Sasa kaingia Jerry Slaa. Hyu tangu aingie anatoa ahadi na matamko tu na wakati mwingine kusimamisha maafisa ardhi lkn kero ziko pale pale.
Matamko ya Slaa yameanika udhaifu wake kiuongozi. Aliahidi na kutamka kuwa ndani ya siku 100 atakuwa kamaliza migogoro yote ya ardhi nchi hii. Wenye akili waliishia kumcheka tu, kwasabb wanajua wingi na mizizi ya migogoro ya ardhi na ugumu wa kuimaliza. Siku 100 zimeisha hata 1 ya 8 ya migogoro hajaitatua.
Sasa ametoa tamko jipya ambalo bila shaka wazoefu wa wizara hii akina Lukuvi huko waliko watakuwa wanakunywa juisi huku waking'ong'a tu. Eti kapiga marufuku wananchi kununua ardhi isiyopimwa. Na kwamba kuanzia Sasa ardhi itauzwa na maafisa ardhi tu.
Maskini Jerry Slaa!!! Natamani mtu amnong'oneze kwamba hiki alichokisema ni kituko cha karne.
*Hivi anafahamu kwamba nusu ya migogoro ya ardhi nchi hii imesababishwa na hao hao maafisa ardhi?
*Hivi anafahamu utofauti wa bei uliopo kati ya viwanja vilivyopimwa na visivyopimwa Vs uwezo wa wananchi kiuchumi?
Mwambieni Jerry Slaa kwamba ama atengue tamko lake ama asubiri kutenguliwa yeye.
Lukuvi ndiye aliyehamisha kazi ya kutoa hati milki za ardhi kutoka wizarani na kwenda kwenye ofisi za Kanda. Haikupita muda akashusha mpk ofisi za mikoa.
Kaingia Angelina Mabula akataka kuendeleza maono ya Lukuvi lkn viatu havikumtosha.
Sasa kaingia Jerry Slaa. Hyu tangu aingie anatoa ahadi na matamko tu na wakati mwingine kusimamisha maafisa ardhi lkn kero ziko pale pale.
Matamko ya Slaa yameanika udhaifu wake kiuongozi. Aliahidi na kutamka kuwa ndani ya siku 100 atakuwa kamaliza migogoro yote ya ardhi nchi hii. Wenye akili waliishia kumcheka tu, kwasabb wanajua wingi na mizizi ya migogoro ya ardhi na ugumu wa kuimaliza. Siku 100 zimeisha hata 1 ya 8 ya migogoro hajaitatua.
Sasa ametoa tamko jipya ambalo bila shaka wazoefu wa wizara hii akina Lukuvi huko waliko watakuwa wanakunywa juisi huku waking'ong'a tu. Eti kapiga marufuku wananchi kununua ardhi isiyopimwa. Na kwamba kuanzia Sasa ardhi itauzwa na maafisa ardhi tu.
Maskini Jerry Slaa!!! Natamani mtu amnong'oneze kwamba hiki alichokisema ni kituko cha karne.
*Hivi anafahamu kwamba nusu ya migogoro ya ardhi nchi hii imesababishwa na hao hao maafisa ardhi?
*Hivi anafahamu utofauti wa bei uliopo kati ya viwanja vilivyopimwa na visivyopimwa Vs uwezo wa wananchi kiuchumi?
Mwambieni Jerry Slaa kwamba ama atengue tamko lake ama asubiri kutenguliwa yeye.