Magazetini
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 588
- 1,698
Akichangia hotuba ya waziri wa viwanda na biashara, mbunge Kisesa, Luhaga Mpina ameongelea mambo mbalimbali ikiwemo uhusiano kati ya sekta binafsi na umma, mikataba mibovu ukiwemo wa Tanesco na Symbion, bilioni 70 za mkataba wa maendeleo ya tehama Tanesco na Mahindra ya India, mkataba mpya unaokuja TPA, bei ya mafuta nchini na mfumuko wa bei.
=======
Luhaga Mpina: Suala la uwekezaji wa Serikali na sekta binafsi linahitaji kuangaliwa kwa makini sana, mikataba mingi tuliyoingia inanyonya mapato ya nchi, uchumi wa nchi, inahamisha rasilimali, inapora ajira za watanzania.
Sasa hivi TPA nae ameanza kutafuta mbia, mikataba ya namna hii lakini ipo mikataba inayotusumbua mpaka sasahivi ya TRA na sicpa. Ipo mikataba tumeingia majuzi ya India Mahindra na Tanesco zaidi ya bilioni 70 kwaajili ya kuendeleza mifumo ya Tehama wakati wataalamu wa tehama tunao hapa wa kila aina wanaoweza kudevelop mifumo ya Tehama. Vijana wetu wamedevelop mifumo kama GPG, POS na hata Maxmalipo, leo unaenda kutafuta mfumo India kwaajili ya kufanya nini?
Sasa hivi naskia symbion wanapigiwa chapuo tuilipe bilioni 356 lakini inapigiwa hili chapuo wakati huohuo hatuambiwi alieingia mkataba huo na kutusababisha tuwe na mkataba ambao hatuwezi ku-exit hata kama mkataba unatuingizia hasara, amechukuliwa hatua gani?
Wabunge tukataeni mikataba ya namna hii lakini tukataeni hata kulipa hizi fedha, uchunguzi ufanyike kilichojificha nyuma ya Symbion.
Mikataba yote ambayo tunaitambulisha kama mikataba mibovu iitishwe hapa bungeni tuweze kuifuta.
Mwisho Luhaga Mpina ameongelea mfumuko wa bei nchini na kusema pamoja na Covid na vita lakini mfumuko umechangiwa na kukosekana uadilifu na usimamizi makini.
Mpina amesema upangaji holela wa bei kinachoshangaza kwanini wahusika hawajachukuliwa hatua. Amedai waziri anawajua waagizaji wa mafuta nje ya nchi, ngano na anawajua wazalishaji wa ndani ya nchi.
=======
Luhaga Mpina: Suala la uwekezaji wa Serikali na sekta binafsi linahitaji kuangaliwa kwa makini sana, mikataba mingi tuliyoingia inanyonya mapato ya nchi, uchumi wa nchi, inahamisha rasilimali, inapora ajira za watanzania.
Sasa hivi TPA nae ameanza kutafuta mbia, mikataba ya namna hii lakini ipo mikataba inayotusumbua mpaka sasahivi ya TRA na sicpa. Ipo mikataba tumeingia majuzi ya India Mahindra na Tanesco zaidi ya bilioni 70 kwaajili ya kuendeleza mifumo ya Tehama wakati wataalamu wa tehama tunao hapa wa kila aina wanaoweza kudevelop mifumo ya Tehama. Vijana wetu wamedevelop mifumo kama GPG, POS na hata Maxmalipo, leo unaenda kutafuta mfumo India kwaajili ya kufanya nini?
Sasa hivi naskia symbion wanapigiwa chapuo tuilipe bilioni 356 lakini inapigiwa hili chapuo wakati huohuo hatuambiwi alieingia mkataba huo na kutusababisha tuwe na mkataba ambao hatuwezi ku-exit hata kama mkataba unatuingizia hasara, amechukuliwa hatua gani?
Wabunge tukataeni mikataba ya namna hii lakini tukataeni hata kulipa hizi fedha, uchunguzi ufanyike kilichojificha nyuma ya Symbion.
Mikataba yote ambayo tunaitambulisha kama mikataba mibovu iitishwe hapa bungeni tuweze kuifuta.
Mwisho Luhaga Mpina ameongelea mfumuko wa bei nchini na kusema pamoja na Covid na vita lakini mfumuko umechangiwa na kukosekana uadilifu na usimamizi makini.
Mpina amesema upangaji holela wa bei kinachoshangaza kwanini wahusika hawajachukuliwa hatua. Amedai waziri anawajua waagizaji wa mafuta nje ya nchi, ngano na anawajua wazalishaji wa ndani ya nchi.