HIZI NDIZO HOJA ZINAZOMTAFUNA LOWASSA
Copy+Paste: HIZI NDIZO HOJA 10
ZINAZOMTAFUNA
LOWASSA,Soma hapa kujua
1 Gazeti la Raia Mwema la
Novemba 2010 ,
liliripoti na kuonyesha picha ya
nyumba
ambayo familia yako inamiliki
Uingereza .
Ukasema ni ya mwanao . Je,
kwa nchi
maskini kama ya kwetu , ni
sahihi kwa
kiongozi mkubwa kumiliki
nyumba kubwa na
ya kifahari nje ya nchi ?
2 . Mkapa alipounda Baraza la
Mawaziri
jipya mwaka 1995 alikuacha .
Wengi
wanasema kwamba Mwalimu
alimwambia
asikupe hata Uwaziri je
Kwanini mwalimu
Alikukataa???
3 . Tangu mwaka 1994 , yaani
miaka 20
sasa, Afrika ya Kusini imekuwa
inakodisha
nyumba yako Masaki kama
Ubalozi wake .
Kuna tetesi kwamba huko
nyumba walitaka
kuhama lakini wakaogopa
kuihama nyumba
inayomilikiwa na kiongozi
mkuu na kuna
tetesi kwamba sasa wanataka
kuhama
lakini wanatishiwa kwamba
hamuwezi
kuhama nyumba ya Rais
ajaye . Ni kiasi
gani cha fedha umepata kwa
miaka 20 ya
kukodisha nyumba hiyo ? Je
kiasi hicho
kimeripotiwa kwenye fomu ya
maadili?
4 . Kuna maelezo kwamba
nyumba hiyo ya
Masaki ambayo Mzee Mandela
alikuja
mwaka 1994 kuufungua
ubalozi mpya wa
Afrika ya Kusini ndicho chanzo
kikuu cha
Mwalimu kusema kwamba
inakuwaje kijana
wa miaka 41 , akiwa mtumishi
ya umma
maisha yake yote na mshahara
wake
unajulikana , anamiliki hekalu
kama lile na
tena kulikodisha kwa Serikali
ya kigeni . Je,
unasemaje kuhusu hili ?
5 . Pia unamiliki ranchi kubwa
sana kule
Mzeri Handeni . Ranchi hiyo
ilikuwa ranchi
ya taifa lakini ukajimegea na
sasa
umeipanua kwa kumega
maeneo zaidi .
Ranchi hiyo uliipata ukiwa
bado kiongozi wa
umma. Je, mtu aliyewahi kuwa
Waziri wa
Mifugo na Waziri Mkuu kujiuzia
ranchi
iliyokuwa ya Serikali inaendana
na dhana
ya uongozi safi na uliotukuka?
Tukikupa
madaraka makubwa zaidi
hautajiuzia kila
kitu? Vilevile, katika nchi
ambayo wananchi
wengi hawwamiliki ardhi , kwa
kiongozi
anayetaka kuwa Rais wetu ,
kuhodhi eneo
kubwa la ardhi , inatuma picha
gani kwa
wananchi hao ?
6. Katika miaka yako 40 ya
utumishi wa
umma, kuna jipi jipya ambalo
umelisahau
na sasa utalifanya kwenye
Urais???
7. Umekuwa Waziri wa Ardhi ,
mbona
matatizo ya ardhi bado tele
nchini ?
Umekuwa Waziri wa Maji ,
mbona matatizo
ya maji bado tele ? Umekuwa
Waziri wa
Mazingira, mbona kuna
matatizo ya
uchafuzi wa mazingira ?
Umekuwa Waziri
wa Mifugo, mbona wafugaji
bado maskini
na wanahangaika ?? huo urais
unautaka wa nini kama uwaziri
umekushinda???
8. Kwenye sikukuu hii , kila
MNEC kapata
milioni 1 , hizo ni milioni 370
na kila
mjumbe 500 , 000 hizo ni
bilioni 2 . Hizi pesa
zinatoka wapi na zitarudishwa
vipi? Je,
kuna zoezi la usafishaji wa
pesa chafu
linalofanywa kupitia kampeni
yako???
CHANZO; FULL HABARI