Lowassa, wananchi wanakuhitaji zaidi ya unavyowahitaji wewe

Lowassa, wananchi wanakuhitaji zaidi ya unavyowahitaji wewe

Familia za mafisadi ndo zinamhitaji Lowassa mwizi mkubwa
 
Matokeo ya utafiti yaliyotolewa juzi na taasisi ya TWAWEZA juu ya kama uchaguzi mkuu ungefanyika leo nani angekua mshindi, yamempa alama za kuongoza waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa aliyepata 13% akifuatiwa kwa karibu na waziri mkuu wa sasa mh.Mizengo Kayanza Peter Pinda ambaye amepata alama 12%.
Wakati haya yakijiri,wachambuzi wa mambo ya siasa wanachambua kuwa kwa matokeo haya ni dhahiri kuwa pamoja na mh Lowassa kuongoza, ujio wa waziri mkuu Pinda na alama alizopata unaonesha shaka katika nguvu za Lowassa.

Mosi, Edward Lowassa ameanza harakati za kutafuta urais akiwa miongoni mwa waliochukua fomu ya kuomba ridhaa ya kusimamishwa na CCM mwaka 1995 akiwa na Jakaya Mrisho Kikwete. Bahati mbaya jina lake lilienguliwa.
Mwaka 2005 Lowassa aliamua amuunge mkono mwana mtandao mwenzie aliyekuwa waziri wa mambo ya nje mh. Jakaya Kikwete kutokana na kuwa Jakaya nyota yake ilikua juu kisiasa hasa baada ya kuongoza duru ya kwanza ya kura mwaka 1995. Hivyo Lowassa aliona aahirishe ndoto yake hadi baada ya JK kumaliza muda wake.

Pili, uteuzi wa nafasi ya waziri mkuu mwaka 2005 ulimpa Edward Lowassa nafasi nyingine ya kujipanga kuingia Ikulu. Alihakikisha kuwa nafasi karibu zote zenye kuweza kumsaidia kufikia malengo yake anaweka watu watiifu kwake. Hii ni kuanzia wakuu wa mikoa,wilaya, wakurugenzi na maafisa mbalimbali waandamizi ambao ama alikua na mamlaka ya kuwateua ama nafasi ya kushawishi na kumshauri Rais awateue. Lowassa alitumia vema ukaribu wake na Mh. Rais kupanga mtandao wake wa urais.

Tatu, baada ya kujiuzulu ama kupata ajali ya kisiasa kama anavyoiita mwenyewe, Lowassa alipata fursa nyingine ya kujiimarisha zaidi katika jamii kama mbinu ya kufikia malengo yake ya kisiasa. Alitumia harambee za makanisa, misikiti, bodaboda,walimu na makundi mengine kama mbinu ya kujijenga kisiasa kuelekea 2015. Alitumia ushawishi wake na uwezo wake kifedha kuyatekeleza haya. Kwa ufupi Lowassa ameanza kampeni kubwa nchi nzima kwa miaka 8 tangu ateuliwe kuwa waziri mkuu, kuliko mtanzania yeyote akiwemo Dr Slaa. Nguvu zake zilielekezwa pia katika kudhibiti wapinzani wake kisiasa, kuweka watu wake kupitia chaguzi za ndani za chama chake na jumuiya zake.
Mapambano haya ndiyo yaliyomuangusha waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye, mama Anne Kilango Malecela na hata mtoto wa muasisi wa taifa Makongoro Nyerere. Aidha nguvu za Lowassa zinasemekana kumpa ushindi Sadifa Juma (mkt UVCCM taifa ),mama Sofia Simba (mkt UWT taifa ) na Abdallah Majura Bulembo (mkt Wazazi taifa ).

Waziri mkuu Mizengo Pinda ameanza kutajwa kuwa anawania nafasi ya Urais miezi mitatu iliyopita. Katika kipindi hiki kifupi amefanikiwa kupasua kambi za vigogo wenzie kama Lowassa na Bernard Membe Kwa kiasi kikubwa. Pinda ameendelea kupata uungwaji mkono mkubwa ndani ya CCM na jumuiya zake. Wafuasi wakubwa wa Lowassa akiwemo Abdallah Bulembo sasa wako na mzee wa asali. Kualikwa kwa Pinda kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa baraza kuu la UVCCM taifa chini ya mwenyekiti wake Sadifa ni ushahidi wa nguvu ya Pinda kwa sasa.
Hivyo, kwa miaka 8 ya kujipanga kwa Lowassa na miezi mitatu ya Pinda, huwezi kusema kuwa Lowassa ni mshindi kwa kupata 13% ya maoni katika utafiti, huku Pinda akiwa nyuma yake kwa kupata 12%, tofauti ikiwa asilimia 1 pekee.
Ndio maana nashawishika kusema Lowassa anaongoza lakini Pinda ndiye mshindi. Pengine Pinda angeanza mapema zaidi tusingemjadili Lowassa leo kama anaongoza. Ama pengine baada ya miezi kadhaa kama kambi ya Pinda itaendelea na kasi hii, huenda jina la Lowassa likapukutika kama majivu kwenye upepo.
Kwa matokeo haya kambi ya Lowassa haina sababu za kushangilia. Bali watafakari kwa kina nguvu zao kwa uwiano na juhudi zao.
Lowassa anaporomoka, Pinda anapanda.
 
Wala sio kitu cha kuongea kwa kigugumizi,ndio kiongozi pekee ambaye anaweza kusafisha hii nchi,am sure ndo kiongozi pekee anayeweza ku rescue hii elimu ya tanzania,naamini ndo kiongozi pekee anayeweza vunja mtandao wote wa ufisadi,naamini ndio kiongozi pekee tunayeweza sema NI CHAGUO LA MUNGU
Go baba Go baba Tuko nyuma yako makamanda wako and we pray GOD will give you strength tuweze fika huko

Fisadi amalize ufisadi! Wewe ni mtanzania wa kwanza kuwa na IQ ndogo.
 
Uchambuzi mzuri mura....

Matokeo ya utafiti mwingine yatatupa mwangaza zaidi
 
Lowasa -atupe Jina la Mgombea Mwenza

Sote tunakubali kwamba mhe. Edward Lowasa amefanya juhudi kubwa kujisafisha na kushawishi watanzania wamuunge mkono katika harakati zake za kuwania urais mwaka 2015. Kwa kiasi fulani amefanikiwa kwani amepata wafuasi wengi wanaompigia -chapuo na kumtetea kuwa anafaa kuwa rais. Amepewa sifa za kila aina kama vile mchapa kazi, mfanya maamuzi magumu nk.

Jambo ambalo -wapambe wa karibu wa mhe. Lowasa wanalifahamu kwa dhati ni kuwa pamoja na kumwagia sifa kemkem Boss wao, ipo sifa moja ambayo hawawezi kumpa- -Lowasa hana siha njema. Ugonjwa alionao wa PARKINSON unashambulia na kuharibu sehemu ya ubongo wake. Ugonjwa huo ambao HAUNA -TIBA ni endelevu kadri miaka inavyokwenda na uharibifu wake hauna kikomo. Dalili kubwa za ugonjwa wa parkinson ni kutetema kwa viungo vya mwili (tremor) kama vile mikono; mwendo pole (bradykinesia); na kukaza misuli (rigidity).Athari zake zinamfanya mgonjwa apoteze kumbukumbu na kushindwa kumudu shughuli za kawaida za kila siku. Ndio kusema, kadri umri unavyokwenda mgonjwa wa parkinson anakuwa -hajiwezi (disabled) kimwili na kiakili.

Kwa maana hiyo, ugonjwa wa -Mhe. Lowasa utamfanya, miaka michache baada ya kuingia madarakani (kama akifanikiwa), ashindwe kumudu majukumu mazito ya Urais. -Bahati nzuri Rasimu ya Katiba -inaeleza vizuri kwenye Ibara ya 84 sehemu 1-3 endapo Rais atashindwa kumudu madaraka kutokana na maradhi ya mwili na akili nini kitatokea. Ibara hiyo inasema wazi kuwa Makamu wa Rais ndiye ataapishwa kuwa Rais. Sasa swali la WATANZANIA ni hili: Je, nani atakuwa makamu wa rais wa Lowasa?. maana huyo ndiye rais wetu -mhe Lowasa itakaposhindwa kumudu madaraka ya rais.

Kutokana na ukweli huo, tunamwomba Lowasa ahakikishe mgombea mwenza wake ni solid, maana huyo ndiye atayemrithi. Yeye akishakamilisha ndoto yake, ampishe makamu wa rais atuongoze. Tutakuwa tayari kumsaidia akamilishe ndoto ya kwenda Ikulu endapo Lowasa atatuchagulia mgombea mwenza makini, mchapa kazi na anayechukia ufisadi. Tunataka Lowasa amtaje mgombea mwenza wake, ama sivyo atakuwa sio mzalendo wa kweli.
 
Kwakweli hata mimi nashawishika kuamini kuwa Lowassa hana nguvu ambazo anadaiwa kuwa nazo. Watanzania wanamfahamu sana uchafu wake. Pinda atampiku kwa mbali ndani ya kipindi kifupi
 
Hivi mbona kila kukicha vijana mnazidi kutumika? hivi huyo lowasa hamuijui historia yake? daaa! kweli kizazi bongo fleva
 
Lowasa -atupe Jina la Mgombea Mwenza

Sote tunakubali kwamba mhe. Edward Lowasa amefanya juhudi kubwa kujisafisha na kushawishi watanzania wamuunge mkono katika harakati zake za kuwania urais mwaka 2015. Kwa kiasi fulani amefanikiwa kwani amepata wafuasi wengi wanaompigia -chapuo na kumtetea kuwa anafaa kuwa rais. Amepewa sifa za kila aina kama vile mchapa kazi, mfanya maamuzi magumu nk.

Jambo ambalo -wapambe wa karibu wa mhe. Lowasa wanalifahamu kwa dhati ni kuwa pamoja na kumwagia sifa kemkem Boss wao, ipo sifa moja ambayo hawawezi kumpa- -Lowasa hana siha njema. Ugonjwa alionao wa PARKINSON unashambulia na kuharibu sehemu ya ubongo wake. Ugonjwa huo ambao HAUNA -TIBA ni endelevu kadri miaka inavyokwenda na uharibifu wake hauna kikomo. Dalili kubwa za ugonjwa wa parkinson ni kutetema kwa viungo vya mwili (tremor) kama vile mikono; mwendo pole (bradykinesia); na kukaza misuli (rigidity).Athari zake zinamfanya mgonjwa apoteze kumbukumbu na kushindwa kumudu shughuli za kawaida za kila siku. Ndio kusema, kadri umri unavyokwenda mgonjwa wa parkinson anakuwa -hajiwezi (disabled) kimwili na kiakili.

Kwa maana hiyo, ugonjwa wa -Mhe. Lowasa utamfanya, miaka michache baada ya kuingia madarakani (kama akifanikiwa), ashindwe kumudu majukumu mazito ya Urais. -Bahati nzuri Rasimu ya Katiba -inaeleza vizuri kwenye Ibara ya 84 sehemu 1-3 endapo Rais atashindwa kumudu madaraka kutokana na maradhi ya mwili na akili nini kitatokea. Ibara hiyo inasema wazi kuwa Makamu wa Rais ndiye ataapishwa kuwa Rais. Sasa swali la WATANZANIA ni hili: Je, nani atakuwa makamu wa rais wa Lowasa?. maana huyo ndiye rais wetu -mhe Lowasa itakaposhindwa kumudu madaraka ya rais.

Kutokana na ukweli huo, tunamwomba Lowasa ahakikishe mgombea mwenza wake ni solid, maana huyo ndiye atayemrithi. Yeye akishakamilisha ndoto yake, ampishe makamu wa rais atuongoze. Tutakuwa tayari kumsaidia akamilishe ndoto ya kwenda Ikulu endapo Lowasa atatuchagulia mgombea mwenza makini, mchapa kazi na anayechukia ufisadi. Tunataka Lowasa amtaje mgombea mwenza wake, ama sivyo atakuwa sio mzalendo wa kweli.

jiandae
 
attachment.php
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hakuna anayemuhitaji mwizi na jambazi, tumewachoka na tumechoshwa Ikulu kunajisiwa kwa miak 30 sasa, TUPA KULEEE
 
Lowassa ni tumaini la mafisadi, wezi, wahuni, majangili na magaidi na wauza unga nchini. Haiwezekani kiongozi mzuri mwenye sifa za kuiongoza nchi aanze kampeni zake kwa kutoa rushwa ya mamilioni katika nyumba za ibada halafu akadaiwa eti ni "tumaini la Watanzania"

LOWASA ni tumaini la Watanzania!
 
Ukweli halisi ni huu hapa wakuu wala msihangaike bure:

Hata kama wapinzani watashinda kwa kupata kura zote hawawezi kuingia magogoni! Magogoni ni kwa ajili ya ccm baasi. Wapinzani baadae sana, sio sasa wakati bado nchi inatawalika. Wapinzani wataingia ikulu pale ambapo nchi haitawaliki lakini si kama ilivyo sasa hv! Niwakumbushe kulalamika lalamika haina maana kuwa nchi haiendi, inaenda sana tu! Si mnakumbuka ishu ya mzee wa vijisenti?Au mmeshamsahau mara hii? Mlilalamaika weeeee lakini juzi kai mzee wa vijisenti ndo anawaandikia katiba! Mpo hapo?

Hii nchi ni ngumu kwa wapinzani!! Kuna mengi hamjui, ila wanajitahidi sana lakini bado kabisa.

Dawa hazipatikani hospitali, wananchi wapo busy na foleni za kuwahi kibaruani kwa wahindi naye rais wao yupo maryland kapumzika kidogo! Mola amjalie afya njema!

Hela za escrow 200bln zinapigwa, wananchi wapo busy na yanga na simba nani mtani jembe!

Nchi bado inatawalika sanaaaaaaaa!! Na kwa hali hii wafuasi wa upinzani endeleeni kuota ndoto zenu za alinacha!
Mkitaka kunielewa jinsi ilivyo ngumu kupenya kwenda kuishi karibu na posta (magogoni) angalieni kwa yanayotokea Syria. Assad kakomaa hatoki ikulu; na ndio maana yake hatoki ikulu ndo habari ya ikulu hio baba/mama!

Sasa nyie ndo muende ikulu kama mnaendeka mlimani city vile kucheki show za akina sitti mtemvu??!! Thubutuuuu!! Acheni utani jamani nyie wapinzani! Sometimes muwe serious walau kidogo! Au mnafikiri ikulu ya Tanzania ni kama ya Burkina Fasso eeeehhhh!!!!! Imekula kwenu wakuu!!

2015 Kidume Edward Lowassa anatinga magogoni rasmi......Asieamini aendelee kuamini hivyo hivyo, Oct 2015 ataelewa ninachokisema hapa!!!!


Jembe Lowassa likiingia ikulu, Tanzania mpya itazaliwa! Unadhani watanzania wanaitaka Tanganyika???? Aaah wapi! System ya nchi ndo imekaa kushoto.....kwa hio wananchi wanatafuta namna ya kukabiliana nayo; yaani ayo ni utanganyika ni mahangaiko tu ya wananchi kukabiliana na mateso ya kiuchumi, kielimu na kiafya na si vinginevyo!

Lowassa akiingia ikulu tu baasi Tanganyika inasahaulika kabisa! Subirini muone!

Mungu iendelee kubariki uwepo wa Lowassa!

Ahsanteni sana wakuu!

Tuondolee upumbavu wako Lowassa akamuongoze nani labda hiyo team yenu ya waganga njaa.

Tumaini la watanzania ni mtoto wa Mkulima a.k.a Mrina Asali Kayanza Mizengo Peter Pinda
 
Unahangaika sana ndugu yangu wagonjwa ni kama wakina Marehemu rais Sata,lowassa yuko gado kuliko unavyomfikiria,hayo maneno yenu ni yawaliokata tamaa,but the fact is ufe,ulie,ujinyonge LOWASA Is the NEXT Amiri jeshi Mkuu wa majeshi,usijali tutakualika kwenye inaguration worry not

Kawadanganye watoto wenzio, let me tell the truth Afya ya Lowassa ni tete kuliko unavyofikiri, nani ampe Urais?
 
Fisadi amalize ufisadi! Wewe ni mtanzania wa kwanza kuwa na IQ ndogo.

Nguchiro wewe una uashahidi na ufisadi alioufanya lowassa kama unao peleka kwenye vyombo husika ukafanyiwe kazi siyo unabwabwaja maneno tu wakati huna ushahidi
 
Yaa inawezekana sababu mijitu mirafi ndio imezungika sahani ya biliani,mpaka matumbo yatakapo pasuka ndipo sahani itakuwa free Lowasa hafai ila kwa ushabiki dhaifu wa wtz sijui sio chaguo langu kabisaaaaaaa afadhari nchi iongozwe na kipofu kuliko mrafi huyo
 
Back
Top Bottom