Lowassa: Sitategemea wahisani kuendesha serikali

Lowassa: Sitategemea wahisani kuendesha serikali

Mapovu na msongo wa itikadi zilezile
chakavu, kwa watu walewale, kwisha habari fisiem.

Wewe wacha porojo, tulikotoka ilikuwa asilimia 60% na yeye Lowassa akiwemo kwenye serikali. Leo Kikwete kaishusha mpaka asilimia 8 tu, na ukitazama rikodi ya mwaka jana na juzi zaidi ya pesa nusu wahisani hawajatowa, ina maana hiyo nane inaweza kuwa 4% tu au NIL.

Isitoshe, mwakani kuna kila uwezekano 100% zikawa ni pesa zetu wenyewe, hilo limeshasemwa tena bungeni. Uko wapi wewe? Umelala?

Hapo mamvi kama kawa, kawadanganya wapumbavu na malofa.
 
Bingwa wa kutaja,bigwa wa jutokujua ilani,na ziro wa kufafanua




Angekua ziro asingekua na mafanikuo makubwa tangu wakati anasoma mpaka leo.
Amejiuzulu na kuwa nje ya serikali ya kifisadi ya CCM kwa miaka nane lakini hakutetereka kiuchumi zaidi ya kuwa taini la watanzania.
Kagame alisena anaweza kutumia bandari tu kuendesha nchi ya Ruanda na Tanzania .

Tatizo la Tanzania ni CCM na serikali yake inayosimamiwa na wabunge wenye kutukana tu na kupiga makofi ya ndio.
Mawaziri watakaotokana na serikali ya Magufuli ni ile ile iliyokuwepo tangu enzi za Mkapa na wabunge wale wale waliopatikana kwa kuhonga kanga ,viberiti na kanga na kununua shahada.

CCM ni chama kinachoingia madaarakani kwa hila na magufuli anapiganiwa kwa kila hila ili aingie ikulu na akishaingia watamwambia kua bila hila na kukusanya pesa za kuwarubuni wananchi hawezi kuingia awamu ya pili .

Lowasa ana maono makubwa sana na uwezo wa kutumia rasilinali za nchi.
Bila shaka serikali ya Lowasa itakua na mawaziri na wabunge bora na waadilifu kuliko ya Magufuli.
CCM haitakua na mawaziri wenye uwezo kutokana na kukosa wabunge na madiwani bora. CCM ni wale wale wenye maisha bora huku wakiwadanganya wananchi kuwa nchi ni maskini na hatuna namna ya kupata naendeleo zaidi ya kuuza nchi na kuomba misaada.

CCM wangekua wema kwa watanzania wote wasingetumia rushwa na uovu wa kila namna kupiga kampeni wangeonyesha tu mafanikio waliyoyafanya tangu walipokabidhiwa nchi yenye amani na utajiri mkubwa toka kwa serikali thabiti ya mwingereza.
 
Ishu sio kuwa warz mkuu ishu nine alipopewa amefanya,
Pili na kama unapinga kuwa magufuli sio mkali wewe ni mtanzania wa kwanza kukutana nae ambaye anasema magufuli sio mkali,

Mkali kwa mke wake na watoto wake.raisi mkali atumuhitaji .tunataka raisi mbunifu anaeonesha njia na kusimamia uwajibikaji na kusimamia utawala wa sheria juu ya tuliokubaliana.vinginevyo mbwa ndio anaitaji kuwa mkali
 
Bajeti hewa ungeyaona maendeleo?

kabla ya ujio wa Kikwete ilikuwa kwenda Mwanza tu kutokea Dar mpaka upite Kenya, leo yapo hayo na aliyesimamia utekelezaji ni huyo huyo Magufuli.

nenda kaitazame Muhimbili leo, kabla ya ujio wa Kikwete mlikuwa mkiumwa moyo kama huna fedha unakufilia mbali, leo unatibiwa Muhimbili, jengo jipya, vifaa vipya, wataalaam wapya na bado shughuli inaendelea, na magufuli anasema ataendeleza na kuhakikisha kila mkoa una hospitali ya rufaa, kila wilaya inaunganishwa kwa lami, kila mwanafunzi kusoma bure, kila kia kupatiwa ajira kwa kuongeza w=viwanda.

Lowassa kasema atafanya nini? Zaidi ya porojo za dakika mbili tatu anazoongea?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?

Kwa rasilimal tulizonazo na kwa mda ambao Tulpata uhuru mwaka huu haikutakiwa tuwe tunaongelea vitu ambavyo ni Basic kabisa kama barabara,umeme,maji,nk. Miaka hii taifa lilitakiwa liwe linalenga kwenye Technologial ya mawasiliano na Usafirishaj wa kiwango cha kmataifa kama Air tz kuwa na ndege znazosafr dunia. Kuna kpnd hl shirika llkua na ndege moja inayoruka na ilkua mbovu lakini shirika lilikua na wafanyakaz 201
 
Kwa rasilimal tulizonazo na kwa mda ambao Tulpata uhuru mwaka huu haikutakiwa tuwe tunaongelea vitu ambavyo ni Basic kabisa kama barabara,umeme,maji,nk. Miaka hii taifa lilitakiwa liwe linalenga kwenye Technologial ya mawasiliano na Usafirishaj wa kiwango cha kmataifa kama Air tz kuwa na ndege znazosafr dunia. Kuna kpnd hl shirika llkua na ndege moja inayoruka na ilkua mbovu lakini shirika lilikua na wafanyakaz 201

Asee maneno yako yanasikitisha sana watu waliokuelewa japokuwa mbumbumbu watadhihaki
 
Bajeti hewa ungeyaona maendeleo?

kabla ya ujio wa Kikwete ilikuwa kwenda Mwanza tu kutokea Dar mpaka upite Kenya, leo yapo hayo na aliyesimamia utekelezaji ni huyo huyo Magufuli.

nenda kaitazame Muhimbili leo, kabla ya ujio wa Kikwete mlikuwa mkiumwa moyo kama huna fedha unakufilia mbali, leo unatibiwa Muhimbili, jengo jipya, vifaa vipya, wataalaam wapya na bado shughuli inaendelea, na magufuli anasema ataendeleza na kuhakikisha kila mkoa una hospitali ya rufaa, kila wilaya inaunganishwa kwa lami, kila mwanafunzi kusoma bure, kila kia kupatiwa ajira kwa kuongeza w=viwanda.

Lowassa kasema atafanya nini? Zaidi ya porojo za dakika mbili tatu anazoongea?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?

Tenda wema uende zako. Binadamu hawana shukrani. Kwenye utawala wa Magufuli sidhani kama kutakuwa na upinzani kama tunavyoona leo. Kwa sababu atajitahidi atatue matatizo ya watanzania wote ili wapinzani wakose pa kuanzia. Lkn kuna baadhi ya watu hawana shukrani.
 
Kwa rasilimal tulizonazo na kwa mda ambao Tulpata uhuru mwaka huu haikutakiwa tuwe tunaongelea vitu ambavyo ni Basic kabisa kama barabara,umeme,maji,nk. Miaka hii taifa lilitakiwa liwe linalenga kwenye Technologial ya mawasiliano na Usafirishaj wa kiwango cha kmataifa kama Air tz kuwa na ndege znazosafr dunia. Kuna kpnd hl shirika llkua na ndege moja inayoruka na ilkua mbovu lakini shirika lilikua na wafanyakaz 201

Muda uliopata Uhuru Tanzania ilitengwa na dunia kwa siasa mbovu za Nyerere. Kumbuka hilo.

Mabadiliko ya kweli na Tanzania imeanza kufunguka na kuondokana na siasa ya ujamaa wazi wazi katika ujio wa Kikwete tu - Kumbuka na hilo pia.
 
Mapovu na msongo wa itikadi zilezile
chakavu, kwa watu walewale, kwisha habari fisiem.

Nnawasubiri niwaone mtavyolalamika kuibiwa baada ya umagufuli kuapishwa.

Maana kuna wengine wameshaanza kulalamika hivi sasa.

Jee, unajuwa kuwa CCM tayari ina majimbo zaidi ya 15 bila kupingwa?
 
Muda uliopata Uhuru Tanzania ilitengwa na dunia kwa siasa mbovu za Nyerere. Kumbuka hilo.

Mabadiliko ya kweli na Tanzania imeanza kufunguka na kuondokana na siasa ya ujamaa wazi wazi katika ujio wa Kikwete tu - Kumbuka na hilo pia.

Aisee ni kweli, utawala wa Kikwete Ulikuwa mzuri sana. Uchumi umeimarika. Maisha ni bora kwa kila Mtanzania, Tsh imekuwa more stable, na pia anamaliza mda wake huku wananchi wengi wakitamani km angeendelea kutawala...

Chama cheke cha CCM pia anakiach kikiwa na uhakika wa ushindi kwa 80%:sly:
 
mimi namshukuru Mungu nilisoma shule bora enzi za Mwalimu. Sasa ni kuulize wewe ulisoma zipi? Izi za kupanua goli au?

Ikumbukwe kwamba maendeleo tunayo yazungumza sio ya vitu. Bali maendeleo ya watu.

Na ndio maana nyerere alitengeneza mfumo mzuri sana wa elimu ya kujitegemea.

Kulikuwa na viwanda. Kilimo ilikuwa ni uti wa mgongo. Nchi ilikua na morali ya kimaendeleo tofauti na sasa.

Sawa maospitali ya mejengwa mabarabara ya mejengwa lakini jiulize swali.

Ni wangapi wa kiugua wanauwezo wa kujitibu?

Ni wangapi wanayatumia mabarabara ya magufuli kusafiri?

Ikiwa uchumi wa watanzania upo Icu? Reli ime uwawa viwanda vime uwawa. Kilimo imekua laana kwa wakulima.

Ivi unajua kwanini nyerere alipigania maendeleo ya watu na sio vitu?

Alikuwa na maana taifa litajengwa na watanzania wenyewe ikiwa watawezeshwa na serikali kwa kujengewa uwezo.


Ndio maana tulikua tunafanya kazi masaa 24 ili kujenga uchumi wa taifa na watu.

Ni malizie kwa kusema. Watanzania wanataka maendeleo ya watu na sio vitu, ikiwa serikali itawajengea uwezo watu wake.

Maendeleo watayaleta wenyewe bila kutegemea wa isani kwa kutembeza bakuli kwa wazungu. Africa itajengwa na waafrica wenyewe. Jambo ambalo chama cha mapinduzi kimeshindwa.

Hizo ulizoziona bora wakati huo alizirithi tu na akaziua kabla hajafa. Kumbuka hilo.

Pia uliziona shule bora lakini hukupata elimu.

Ni Kikwete aliyeanza kuifufua elimu kwa kasi ya ajabu, Wakati wake tu shule za sekondari zaidi ya 4,000, vyuo vikuu zaidi ya 50.

Changanya wote wa kabla yake, hata robo ya hiyo rikodi hawafikishi - kumbuka hilo.

#HapaKaziTu
 
Aisee ni kweli, utawala wa Kikwete Ulikuwa mzuri sana. Uchumi umeimarika. Maisha ni bora kwa kila Mtanzania, Tsh imekuwa more stable, na pia anamaliza mda wake huku wananchi wengi wakitamani km angeendelea kutawala...

Chama cheke cha CCM pia anakiach kikiwa na uhakika wa ushindi kwa 80%:sly:

Naam wala haujakosea.

Nani mwengine aliyefanya zaidi yake?
 
Huyu ndio Lowassa ninayemfahamu,ndani ya muda mfupi Tanzania itakuwa na shirika lake la ndege lenye ndege kama Ruanda Air wanaotegemea kumiliki airbus 300 mbili hivi karibuni.
 
Naam wala haujakosea.

Nani mwengine aliyefanya zaidi yake?

Hahahaa dada FaizaFoxy nchi yetu kwa hii miaka 10 ni km vile haikuwa na Rais, kosa tulilofanya 2005/2010 litaigharimu nchi kwa kipindi kirefu sana, naamini kizazi kijacho kitakuja kutandika fimbo makaburi yetu kwa upumbavu wetu wa kumchagua mtu km Kikwete aongoze nchi!

Ni aibu hata kwa nchi za jirani!
 
Last edited by a moderator:
Hahahaa dada FaizaFoxy nchi yetu kwa hii miaka 10 ni km vile haikuwa na Rais, kosa tulilofanya 2005/2010 litaigharimu nchi kwa kipindi kirefu sana, naamini kizazi kijacho kitakuja kutandika fimbo makaburi yetu kwa upumbavu wetu wa kumchagua mtu km Kikwete aongoze nchi!

Ni aibu hata kwa nchi za jirani!

Wewe ni hasidi.

Kikwete pekee vyuo vikuu zaidi ya 50.

Tulikuwa tukienda Mwanza tu kutokea Dar, lazima tuzungukie Kenya.

Leo unaenda na chai unakunywa ndani ya gari na unafika huna hata vumbi. Zamani mkisafiri mkishuka kuchuma dawa lazima mchekane, sura zimejaa vumbi watu mnaonana meno na macho tu.

Nnajuwa u mdogo sana na haujaishi ukiwa mtu mzima zaidi ya wakati huu wa Kikwete kwa hiyo huwezi kuyaelewa ya waliokuwa kabla yake. Sikushangai
 
Wewe ni hasidi.

Kikwete pekee vyuo vikuu zaidi ya 50.

Tulikuwa tukiend Mwanza tu kutokea Dar, lazima tuzungukie Kenya.

Leo unaenda na chai unakunywa ndani ya gari na unafika huna hata vumbi. Zamani mkisafiri mkishuka kuchuma dawa lazima mchekane, sura zimejaa vumbi watu mnaonana meno na macho tu.

Nnajuwa u mdogo sana na haujaishi ukiwa mtu mzima zaidi ya wakati huu wa Kikwete kwa hiyo huwezi kuyaelewa ya waliokuwa kabla yake. Sikushangai

Vyuo vikuu zaidi ya 50 vimeanzishwa wakati wa awamu ya Kikwete?😕 OMG

Hebu niorodheshee vyuo vitano tu vilivyojengwa kwa juhudi za awamu hii! Unless utakuwa ni muongo uliepindukia!
 
Hizo ulizoziona bora wakati huo alizirithi tu na akaziua kabla hajafa. Kumbuka hilo.

Pia uliziona shule bora lakini hukupata elimu.

Ni Kikwete aliyeanza kuifufua elimu kwa kasi ya ajabu, Wakati wake tu shule za sekondari zaidi ya 4,000, vyuo vikuu zaidi ya 50.

Changanya wote wa kabla yake, hata robo ya hiyo rikodi hawafikishi - kumbuka hilo.

#HapaKaziTu

tatizo lako ni mfia chama. Na ili tatizo limekufanya uwe kipofu wa ufaam. Kwa taarifa yako mimi nilianza kuwa mwanachama wa ccm tangu ikiwa tanu.

Kwaiyo naifahamu ccm kuliko wewe unavyoifahamu. Na nilihama baada ya mambo kwenda ndivyo sivyo.

Uwezi kulinganisha Elimu ya leo na kipindi cha mwalimu nyerere. Leo mtoto anamaliza darasa la saba hajui kusoma na kuandika? Maajabu ya Mussa!

Ikiwa sisi tulisoma bure. Kwa kutegemea, katani. Pamba na tumbaku. Na elimu ilikua bora na sio bora elimu. Ni nani afadhali kati ya nyerere na uongozi uliopo sasa?

Hivi unajua taifa lolote lililochezea mfumo wa Elimu ilo taifa lipo hatarini kwa kuzalisha viongozi hovyo kabisa?

Hao hao tunao tembeza mabakuli usiku na mchana ndio wanarudi kwa mlango wa ujinga wa viongozi watarajiwa wa baadae ambao watakua mazao ya bora elimu!

Ndio maana serikali ya awamu ya kwanza ilikua na vipaumbele vitatu.

1 - ujinga
2 - maradhi
3 - umaskini


Mwisho:
ni mbumbutu atamdharau nyerere. Ni niwale ambao wamezaliwa juzi. Hawakuishi katika utawala wa nyerere.
 
Aisee ni kweli, utawala wa Kikwete Ulikuwa mzuri sana. Uchumi umeimarika. Maisha ni bora kwa kila Mtanzania, Tsh imekuwa more stable, na pia anamaliza mda wake huku wananchi wengi wakitamani km angeendelea kutawala...

Chama cheke cha CCM pia anakiach kikiwa na uhakika wa ushindi kwa 80%:sly:

Unavyoflow na bi. Kidude vizuri nae anaona mko pamoja.
Yaani kama unamdanganya Mtoto mdogo nae anakubali tu
 
Unavyoflow na bi. Kidude vizuri nae anaona mko pamoja.
Yaani kama unamdanganya Mtoto mdogo nae anakubali tu

Hahaha zuzu yule dada aisee, yy kazi yake ni kumuosha JK hata km haosheki, cjui amempa nn aisee!
 
Back
Top Bottom