Anarudia kosa lile lile la kampeni ya Kikwete 2005, kashaanza kuwadanganya Waislamu kwamba ataingiza Mahakama ya Kadhi serikalini wakati Rais hana uwezo wa kubadilisha suala la kikatiba kama hilo."Alisema pia akifanikiwa ataangalia jinsi ya kushirikisha dini katika muundo wa Serikali ili mambo ya Serikali na ya dini yaende vizuri bila mijadala nje ambayo inatishia amani na utulivu.
"Kuna nchi nyingine, mahali kama Pakistan mambo ya dini yana wizara yake ndani ya serikali. "
His calculus is simple if misguided. Kampeni ya Lowassa inajua Wakristo hawana voting bloc, hawapigi kura ya pamoja ya kidini, not least because hawana kadhia ya kidini wanayotaka msaada wa serikali, kwa hiyo kura ya Mkristo itagawanyika, utahitaji kura ya Muislam, hata kama Wakristo ndio majority constituent. Kura ya Muislam rahisi kuipata, maimam wa mrengo wa kulia ya mbali wanafundisha huwezi kutenganisha siasa na Uislam, kwa hiyo mwanasiasa mkora anajua kumuingia muislam muongeleshe siasa za dini, Mahakama ya Kadhi, na kuunda wizara ya dini.
Lakini hata kama Lowassa akiweza kuwarubuni Waislamu, bado ana safari ngumu kwa vile vita vyake viko ndani ya chama, ambako Waislamu wako more sophisticated than the pedestrian ilk, huwezi kumdanganya Muislam wa Executive Committee ya C.C.M. kwa Mahakama ya Kadhi, suala la Kikatiba, much less kwa mialiko ya kula ubwabwa.