Lowassa: Nimeshawishika, Nitagombea urais...!

Lowassa: Nimeshawishika, Nitagombea urais...!

Waziri mkuu aliejiuzulu,bwana Edward Lowassa amekanusha kutangaza ni ya kugombea uraisi na badala yake amesisitiza kuwa ameshawishika lakini hajatangaza nia.

Hapa namnukuu,"Nimeshawishika lakini sijatangaza nia".

Mh.Lowassa pia ameongeza kuwa anasubiri wakati wa kufanya hivyo ufike(chama kitangaze).

Chanzo:Channel 10.

watuibie zaidi maana hawana jipya lolote lile
 
Lowasa ndio tunamtaka. Mbona Zito anasema wazi anautaka Uwenyekiti wa Chama na Anataka Kuwa Rais wa Tanzania , Mbona hammkemei badala take mnamshangilia?. Acheni Unafiki.
 
Waziri mkuu aliejiuzulu,bwana Edward Lowassa amekanusha kutangaza ni ya kugombea uraisi na badala yake amesisitiza kuwa ameshawishika lakini hajatangaza nia.

Hapa namnukuu,"Nimeshawishika lakini sijatangaza nia".

Mh. Lowassa pia ameongeza kuwa anasubiri wakati wa kufanya hivyo ufike(chama kitangaze).

Chanzo: Channel 10.
Hii ni kauli standard ya watia nia ndani ya ccm - Pinda na wengine wanaotumia pia.
 
kiukweli anafaa sana ila lazima atueleze kinagaubaga mchawi aliye sababisha ang'atuke maana alifanya vile kutunza heshima ya serikali yeye avyodai.
 
Taarifa zilizopo ni kwamba hata hizo shilingi 700,000 amezitoa yeye mwenyewe
He hao masheikh 50 wametumwa na nani?na kakubali kugombea sababu ya hao masheikh kutoka Bagamoyo,amekubali ombi la hao masheikh wa Bagamoyo ili tuamini kuwa ni chaguo la Kikwete,kwa kuwa hao masheikh ndio anao swali nao Mh raisi kwa hiyo wana sikio la raisi,huo ni ujanja wa kitoto sijui washauri wake huyu Mheshimiwa IQ zao zikoje kwani kama hawa ndio washauri wake mbona akikukwaa uraisi tutakuwa na shida,walianza wamachinga,wamekuja masheikh na sasa wanavyuo,imekuwaje wote hao wafanye jambo moja katika kipindi kimoja utadhani maandamano ya kuunga mkono ''Azimio la Arusha'' na wote eti hutoa fedha za kumsaidia,nani kawaambia Edo hana fedha ya kumwezesha,ni fedha ngapi katoa makanisani,misikitini na kwingineko?kwa wasiojua hizo ni mbinu za tisha nyau kwa CCM ili kuonekana Mh anapendwa na CCM isipomteua itakuwa imefanya makosa,ni kama kui ''blackmail''CCM.Wagombea kama hawa ndio mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Dr Kamata anawaita ''Vifurushi'' ni kama zile bundle za kwenye simu za mkononi unaambiwa hiki kifurushi ni cha GB 1 na ni unlimited,ukilala na kuamuka baada ya kutumia 200 MB tu unaambiwa kifurushi kimeisha.Huu sasa ushakuwa wenda wazimu!!
 
Hata hao masekhe kawatafuta yeye kawapa nauli na hela kuacha nyumbani kwa mda wa mwezi mmoja.

Ningependa kuona wachungaji na mapadri kama nao wana jeuri ya kufanya maandamano hadi Dodoma na kuchanga 700,000 kama hao masheikh wa Bagamoyo.
 
Kama kawaida mnawafanya Watanzania ni wajinga, mbumbumbu au mapoyoyo. Kama Lowasa anashawishiwa sasa hivi kugombea urais; kwa nini alisimamishwa na ccm kwa kuanza kampeni mapema?
 
Hebu nijuzeni.....kama Lowassa akishinda uraisi halafu wabunge zaidi ya 85%wakatoka upinzani..serikali itakuwa ya nani????Naomba usinitukane.
 
Kupitia gazeti la Mwananchi, nimekutana na habari kuwa 'Masheikh 50 wamemchangia Lowassa 700,000/- Tsh. kwa ajili ya kuchukulia fomu za kugombea Uraisi! swali langu moja tu: Hivi huko watokako (BAGAMOYO) hakuna tatizo la kijamii ambalo linahitaji kiasi hicho cha pesa ili kulitatua?
Nawasilisha.
 
waliagizwa na alowapa hizo fedha kufanya walichokifanya,
 
11037586_1177050072309409_872469977191814068_o.jpg


10517412_1177050075642742_5274303387275892654_o.jpg


LOWASSA ACHANGIWA SHILINGI LAKI 7 NA MASHEIKH KUGOMBEA URAIS

Masheikh zaidi ya 50 kutoka Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, leo wamemkabidhi kiasi cha shilingi 700,000/- za kuongezea kuchukua fomu ya kuwania urais 2015.


Mashekhe hao wakiongozwa na Yusuf Surulu na Alli Mtumwa wamemkabidhi fedha hizo nyumbani kwake mjini Dodoma na kushuhudiwa na Mbunge wa Urambo Magharibi, Prof Juma Kapuya.


wamesema kuwa wameona mtu pekee anayefaa kushika wadhifa huo ni yeye hivyo wanamsihi atangaze nia na achukue fomu ya kugombea na wapo nyuma yake katika dua.


Lowassa amewaambia viongozi hao wa dini kuwa makundi mbalimbali ya jamii yamekuwa yakimuomba kugombea Urais lakini wao wamemfanya ashawishike sasa kufanya hivyo wakati ukifika.

chanzo.
http://www.2jiachie.com/2015/03/lowassa-achangiwa-shilingi-laki-7-na.html
 
Na hii je?
 

Attachments

  • 1427062284085.jpg
    1427062284085.jpg
    100.2 KB · Views: 108
Kapuya nae ni shehe wa Bagamoyo?
 

Attachments

  • 1427062366681.jpg
    1427062366681.jpg
    117.5 KB · Views: 114
He hao masheikh 50 wametumwa na nani?na kakubali kugombea sababu ya hao masheikh kutoka Bagamoyo,amekubali ombi la hao masheikh wa Bagamoyo ili tuamini kuwa ni chaguo la Kikwete,kwa kuwa hao masheikh ndio anao swali nao Mh raisi kwa hiyo wana sikio la raisi,huo ni ujanja wa kitoto sijui washauri wake huyu Mheshimiwa IQ zao zikoje kwani kama hawa ndio washauri wake mbona akikukwaa uraisi tutakuwa na shida,walianza wamachinga,wamekuja masheikh na sasa wanavyuo,imekuwaje wote hao wafanye jambo moja katika kipindi kimoja utadhani maandamano ya kuunga mkono ''Azimio la Arusha'' na wote eti hutoa fedha za kumsaidia,nani kawaambia Edo hana fedha ya kumwezesha,ni fedha ngapi katoa makanisani,misikitini na kwingineko?kwa wasiojua hizo ni mbinu za tisha nyau kwa CCM ili kuonekana Mh anapendwa na CCM isipomteua itakuwa imefanya makosa,ni kama kui ''blackmail''CCM.Wagombea kama hawa ndio mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Dr Kamata anawaita ''Vifurushi'' ni kama zile bundle za kwenye simu za mkononi unaambiwa hiki kifurushi ni cha GB 1 na ni unlimited,ukilala na kuamuka baada ya kutumia 200 MB tu unaambiwa kifurushi kimeisha.Huu sasa ushakuwa wenda wazimu!!

Ni kweli Kikwete anatimiza ahadi yake ya kumwachia nchi. Mafisadi at work.
 
Wanaomsupport Lowasa ni wajinga kama lowasa.

Hata hivyo ccm hawana mgombea wa uraisi zaidi ya mashindano ya nani zaidi kwenye ulaghai, matumizi makubwa ya rushwa na ufisadi.

Ninachokiona ccm imerasimisha ufisadi, wizi na matumizi ya rushwa. Ni dhahiri kwamb maneno uadilifu, uzalendo na usafi wa viongozi, hayapo tena kwenye kamusi ya ccm.

Wakati ccm mnatafuta mtakayemsafisha kwa urahisi ili aingie ikulu, wakati mwenyekiti wenu akiona hana namna zaidi ya kumpata laghai nyangumi mwenye kipaji cha kuwalaghai watanzania wajinga na maskini ili aibu ya anguko la chama isiwe mikononi mwake, WATANZANIA TUNASEMA, CCM HAMTARUDI IKULU.

TANZANIA SI MALI YENU MUICHEZEE NA KUPOKEZANA ILI KUENDELEZA UHARAMIA WENU KWA NAMNA MNAVYOTAKA. TANZANIA INAWENYEWE NA WENYEWE NI SISI WATANZANIA.

UKAWA JIPANGENI VIZURI NA MTUONYESHE NAMNA GANI MTAUNGANISHA TAIFA LILILOGAWANYWA VIPANDE VIPANDE NA CCM. TUONYESHENI NAMNA GANI THAMANI YA MAISHA YA MTANZANIA ITARUDI. TUONYESHENI JINSI GANI MTANZANIA WA KAWAIDA (SIYO WALE MATAJIRI) ATASHIRIKI KATIKA KUTELEKEZA NA KUMILIKI UCHUMI WA NCHI ILI AJISIKIE YUKO NYUMBANI NA SI UKIMBIZINI.

TUONYESHENI NAMNA MTAKAVYOREJESHESHA HADHI NA UKUU WA TAASISI YA URAISI.

TUNAHITAJI KUWA NA SERIKALI YENYE MIFUMO NA IDARA ZOTE ZINAZOJITAMBUA NA KUTAMBULIKANA KWAMBA ZIKO KWA AJILI YA WATANZANIA.

TUONYESHENI NI KWA JINSI GANI ELIMU YA MTANZANIA ITAREJEA MAHALA PAKE ILI KUONGEZA COMPETITIVENESS YA WATANZANIA KATIKA NDANI NA NJE YA NCHI.

UKAWA SASA PIGENI MBIO KWA KASI KUFIKA KILA KONA YA NCHI.
 
Back
Top Bottom