Lowassa ni Powerful Kuliko ya JK?!

Umenena vyema great thinker!
 
el ana nguvu sana comparatively. na sio kwa wanoamwamini tu, hata wale wasio mwamini au kumsapoti. kama kiongozi kwa muda wote aliokuwa ndani ya serikali amejenga network yake ya allegaince na hiyo network probably ipo katika kila sekta, kuanzia kwenye chama hadi idara za gavument, kwa hiyo kwa mfano kama ana sapoti ya wakurugenzi wa halmashauri, wakuu wa wilaya na mikoa, wakuu wa polisi, wafanyabiashara, inteligensia, viongozi wa chama mikoani na wilayani, kata hadi shina,---hao viongozi wata-streamline umma ili kumsapoti. na wanasiasa wote hufanya hivyo.
 

hata ndani ya cdm anao watu wake wakutosha.
 

Kingereza kibovu kabisa !
 
Uwezo wa Lowassa kiuongozi is too far compared to kikwete anayeshindwa kufanya hata maamuzi madogomadogo!

mbona hii kauli ni kama mmekua trained kuikariri?maana kila mpiga debe wa jamaa ataandika kama ulivyoandika wewe mstari kwa mstari lakini bahati mbaya huwa hamuainishi maamuzi magumu aliyowahi kuyafanya Lowassa akiwa waziri mkuu ukuiacha lile maarufu la kulazimisha mkataba wa richmond ikiwa haina vigezo kwa ushahidi wa vimemo kwa waziri wa nishati muadilifu na lile la kuamua kununua mvua ya "kichina" Thailand ambalo jakaya ndio alifanya maamuzi magumu ya kumkatalia upu.uzi wake huo!
 
Angekuwa na nguvu asingejiuzulu.Mwenye nguvu ni JK aliyebaki madarakani.Ndiye rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, who is EL?

Hapa naona nitaambiwa sijui maana ya hiyo "power, command and capabilities"

Bora hata wewe umemstukia bwana P.LOWASA,naona aliweka akiba ya maneno(power,command & capabilities)ili kushut down hoja akiona anaelemewa,utawaweza makanjanja wetu hawa?Hivi ule mpango wake wa kukirejesha kiti moto chake kijanja kwa kutumia mgongo wa jf umeishia wapi?au ndio umekufa kifo cha kawaida baada ya kupata mapokezi yasiyostahili alipouleta hapa jamvini na kuishia kuzomewa?
 

Nchini hapa na hasa kwa ccm na serikali yake huwezi kuwa na power bila kuwa fisadi!! Wote Kiwete na Lowassa power waliokuwa nayo inatokana na wizi wa mali za umma!!!
 
hii ndo tanzania na hawa ndo waandishi wetu, mtihani kweli kweli.
Mungu wabariki waandishi wetu, Mungu laani wanaowahonga waandishi wetu kwa bahasha za khaki.
 
Pasco,
Nimekusoma mkuu wangu, sasa kama kweli Lowassa ni powerful na kaweza wateka watu woote waliotajwa humu hili kweli sii Taifa la Wajinga?. Penigne mimi ndio simfahamu vizuri lakini kwa yale alokwisha yafanya hakika kama alivyosema Mwanakijiji tunapo amini Uchawi na Uganga basi EL ni mchawi na mganga kuliko yule aloshuka na Ungo Dar, na mganga kuliko Babu wa Loliondo. Na maadam nasikia mkuu wetu naye mwoga wa wachawi, basi kazi imekwisha..
 
Watanzania wanapenda ushabiki wa kijingajinga na ndio maana watu kama Lowasa wanaendelea kupeta. Watu walikuwa wanamsifia Mobutu na akaondolewa na askari wenye kandambili.
 

Binafsi sioni alichofanya EL kiasi cha kusifiwa nini kujiuzuru! kwa vile hapajawahi kuwepo kiongozi alijiuzuru toka tuitwe watanzania? kama alijiuzuru kwa uchafu ni lini kasafishika mpaka astahili kusifiwa tena?
 
sijawahi kusikia kafanya maamuzi kama unajaribu kutushawishi ila hali ni mbaya maisha yanapanda kila siku na yeye yupo kwenye system miaka kibao
yawezekana anakumbumbukwa kwa maamuzi yake magumu ya kwenda Thailand kutafuta mvua ya mabomu ...
 
JK staili iliyompeleka madarakani ndiyo inamgharimu, tuliambia na Hatati Mwalimu JKN kabla huja wanunua watanzania lazima uwe umenunuliwa wewe kwanza.... sasa JK alinunuliwa awe kiongozi, nae akatununua watanzania.... ujasili wa lowasa unatokana na JK mwenyewe kuwa legelege
 
nani aliyemuambia au kumruhusu lowasa kujiuzulu?nauliza tu?


Ni power zake na command labda! Maana naona tunaanza kusahau nani anapigiwa mizinga kumi na mbili na nani anayewaamuru Gen Mwamunyange na IGP Mwema kutekeleza orders za serikali.
 

Sitachangia mada yako hii ya kuokota barabarani mpaka utakaporekebisha aibu yako ya kizungu kibovu ulichoandika humu. Ukijijua una matatizo ya ung'eng'e basi tumia kirangi ulichokizoea, siyo kurukia lugha za watu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…