Lowassa ni msomi, anapata nyomi

Lowassa ni msomi, anapata nyomi

Hakika Lowassa ni mwana sanaa na amedhihirisha hilo kama mnavyojionea wenyewe.
 
Mzee tupa tupa wa Ufipa, baba wa wanafiki, vipi Slaa ameshatangaza nia kugombea kupitia Ukawa? Lipumba kashajitosa kilingeni tunamsubiri babu slaa.

Du! sasa hapa Ukawa inaingia vp kwenye hayo mazingaumbwe ya Lowasa? Au ndo tuseme ni tatizo la kuolewa kabla hujapevuka?
 
Usomi si tu wingi wa shahada,stashahada au astashahada. Usomi hasa ni uwezo wa kutumia elimu,hasa fani yako,katika maisha halisi. Ndivyo alivyo Lowassa. Lowassa ni msomi wa shahada ya sanaa toka UDSM. Amejifunza na kufuzu maigizo,ngoma,utunzi wa mashairi na mazingaombwe.

Sasa Lowassa anatumia usomi wake. Fani yake. Alipotamka tu Rais Kikwete kuwa wanachama wawashawishi wagombea wazuri,Lowassa akapata pa kutokea. Kwakuwa msomi wa usanii hupaswa kuwa sharp,mbunifu na muangalifu,Lowassa akatumia haraka fursa.

Kinachoonekana na kusikika sasa,ni zao la usomi wa Lowassa. Hakuna mwanasiasa mkongwe chamani mwenye usomi wa usanii kama Lowassa. Wengine hutumia usanii wa kuzaliwa tu. Usomi una raha yake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Hakika nmependa uhodari wa EL,ametisha na amebobea kwenye sanaaa
 
mh . hv hao watu woote wanahongwa ....hapana mwenye macho haambiw tazama..
jamaa anakubalika kwa sasa....ukweli umeshajulikana
ndo maana mkwere hana amani
 
Kilicho waponza baadhi ya viongozi CCM ni ile dhambi ya kumzunguka Waziri wao Mkuu kipindi kile Edward Lowassa na kumtengenezea kashfa ili wamlize kisiasa lakini Mungu wa Watanzania akasimama baada ya miaka 7 na kumpa mtumishi wake nguvu tena, kama alivyofanya kwa Samsoni.

Kile kilichotendeka kipindi kile ulikuwa kama mtu anayetoboa boti analosafiria huku akiwa katikati ya bahari. NNdiyo makada wa CCM walivyofanya. Tatizo halikuwa ni uwaziri mkuu bali urais wa 2015. Hili ndilo lilokuwa tatizo kubwa kwako.

Wengine walienda na kuanzisha chama (CCJ) ndani ya chama(CCM) hii ulikuwa ni sawa na uhaini. Waliofanya hivyo hakuchukuliwa hatua za kinidhamu balii walipongezwa kwa vyeo. Hii ulikuwa sababu kubwa ya wanachama CCM kutopiga kura 2010.

Nawapongeza Sana CHADEMA kwa kuwashughulikia wasaliti. Huu ndiyo msingi wa uongozi. CCM tunataka kuwa na double measures hii haisadii kumjenga chama.

Nimalizie kwa kusema Watanzania wanamtaka Lowassa wao ndani au nje ya CCM ilikuwaletea ukombozi! Watanzania wamesema ndani ya mioyo yao tupewe Lowassa wetu. Wabunge walitangulia, wakafuata rafiki sake kutoka makundi mbalimbali mashehe, wanafunzi, Bodaboda na wachungaji.Sijui nani atafuata!
 
Kama CCM wanataka wajijengee heshima wanatakiwa wachukue maamuzi magumu kwa kuwabwaga wote waliotangaza nia ya kugombea urais kinyume na utaratibu wa chama chao vinginevyo watadharau mpaka na sisimizi.
Utaratibu usio kinyume ni upi?
 
Sasa Mbona umeshasaliti? Hata mwehu asiye na akili hata tone, akisoma mabandiko yako yaliyosheni kejeli juu ya CCM anafahamu wazi kabisa wewe ni mfuasi mtiifu wa Mzee Mtei. Inawezekana Hujawahi kuwa mwanachama wa CCM.


Wewe ndio hujielewi . warioba pia amesaliti?
 
Kama CCM wanataka wajijengee heshima wanatakiwa wachukue maamuzi magumu kwa kuwabwaga wote waliotangaza nia ya kugombea urais kinyume na utaratibu wa chama chao vinginevyo watadharau mpaka na sisimizi.

Thubutuuuuh, haitogokea kamwe
Lowasa hakamatiki kwani humuoni menyekiti wao yupo kimya na wala hawatomgusa
 
Usomi si tu wingi wa shahada,stashahada au astashahada. Usomi hasa ni uwezo wa kutumia elimu,hasa fani yako,katika maisha halisi. Ndivyo alivyo Lowassa. Lowassa ni msomi wa shahada ya sanaa toka UDSM. Amejifunza na kufuzu maigizo,ngoma,utunzi wa mashairi na mazingaombwe.

Sasa Lowassa anatumia usomi wake. Fani yake. Alipotamka tu Rais Kikwete kuwa wanachama wawashawishi wagombea wazuri,Lowassa akapata pa kutokea. Kwakuwa msomi wa usanii hupaswa kuwa sharp,mbunifu na muangalifu,Lowassa akatumia haraka fursa.

Kinachoonekana na kusikika sasa,ni zao la usomi wa Lowassa. Hakuna mwanasiasa mkongwe chamani mwenye usomi wa usanii kama Lowassa. Wengine hutumia usanii wa kuzaliwa tu. Usomi una raha yake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Si mchezo, ana degree ya Theatre Arts ya UDSM. Knowledge application!!
 
Usomi si tu wingi wa shahada,stashahada au astashahada. Usomi hasa ni uwezo wa kutumia elimu,hasa fani yako,katika maisha halisi. Ndivyo alivyo Lowassa. Lowassa ni msomi wa shahada ya sanaa toka UDSM. Amejifunza na kufuzu maigizo,ngoma,utunzi wa mashairi na mazingaombwe.

Sasa Lowassa anatumia usomi wake. Fani yake. Alipotamka tu Rais Kikwete kuwa wanachama wawashawishi wagombea wazuri,Lowassa akapata pa kutokea. Kwakuwa msomi wa usanii hupaswa kuwa sharp,mbunifu na muangalifu,Lowassa akatumia haraka fursa.

Kinachoonekana na kusikika sasa,ni zao la usomi wa Lowassa. Hakuna mwanasiasa mkongwe chamani mwenye usomi wa usanii kama Lowassa. Wengine hutumia usanii wa kuzaliwa tu. Usomi una raha yake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Si mchezo, ana degree ya Theatre Arts ya UDSM. Knowledge application!!
 
NAENDELEA KUNENA NA SWAHIBA
Swahiba nliposema mtaishi bora sikumaanisha, kupora na kutumia makombora. Nadhani mjue, nlisema ili mkue. Ajira na mijadara inatakiwa iwafunze na mjifunze. Swahiba, tumeishi zaidi ya utumwa ingawaje tu wazawa, mhh! Umetukuza saaaana naona umetufunza. Swahiba amani yetu ghalani na huku kitaa tunaitamani au huoni kila mtu akiamaki?
Swahiba wapo walao pasipo vikwazo nab ado maisha yetu mitaani ni gumzo, au ndo matokeo ya uleuozo?, hebu tuache mizozo tuombe mwongozo ili kukemea uozo. Swahiba unaonekana Mungu unamcha lakini uongozi umekuwa mchungu, au ndo upo jirani na wapenda majungu?, swahiba ile dini ya Machiavelli haimjui Mungu, ukiifuata lazima mambo yawe machungu zaidi ya miiba ile ya nungu nungu.
Nanyi wanazuoni hebu achene ukoloni, huyu swahiba nae anakuja kwa niaba pia, tusijidai kutojua alichonuia. Hakuaminika kwa vidogo ila kwa vigogo, tusijidai tusoshai. Kama nyie ni magogo basi majaribio ni ndiyo, mpeni mbwea mifugo ailinde ili tushangae, hee!, beeee!, ye halye. Wanazuoni wa kelele na vigeregere nawaona mwewe, hivi kweli hamna simile?, acheni mambo ya mwewe.
Swahiba sasa tumekuwa, hatuwataki wale wa mali zetu kibindoni. Tunataka atulindaye kama mboni, hatuwataki wale wasio nyoni. Hivi hamwoni swahiba usoni?, mbona macho huonyesha yalo mawazoni?, wanazuoni mmekosa kuingia mawazoni, hebu msijidai hamwoni. Wanazuoni mnanipa shida kisogoni kwani hata nifikiriapo kiongozi simwoni labda wadau nipeni maoni.
Swahiba anaonyesha kutokuwa na aiba, eti wanazuoni mbona sioni ule usomi?, oneni soni basi kidogo. Mnakuwa wa kitu kidogo ivo!, eti viongozi wa kiroho nao wamwendea swahiba hao wanataka mgao. Kumbe kila kitu ni mgao kimtindo etii?, hebu tusisahau mgao utatupa kichapo mwisho wa mlongo hebu achene longolongo.
Swahiba hivi na wale wa badobado pia walikuja?, hebu waambie wafuate sheria mbalimbali kuepusha ajali. Waachane na hiyo sanaa kwani haiwajali. Swahiba unaonyesha kuogopesha?, hivi umependwa kweli au ndio kejeri za kibepari?, me sioni heri labda niende kwakweli. Swhiba yule mwenye ndoto na maono alitoa onyo, hakukupa kibari so me naona we sio halali. Mbona ujasiri siku zote kwako ni asili ila sioni kama una kibali.
Nimenena kwa niaba.
 
Usomi si tu wingi wa shahada,stashahada au astashahada. Usomi hasa ni uwezo wa kutumia elimu,hasa fani yako,katika maisha halisi. Ndivyo alivyo Lowassa. Lowassa ni msomi wa shahada ya sanaa toka UDSM. Amejifunza na kufuzu maigizo,ngoma,utunzi wa mashairi na mazingaombwe.

Sasa Lowassa anatumia usomi wake. Fani yake. Alipotamka tu Rais Kikwete kuwa wanachama wawashawishi wagombea wazuri,Lowassa akapata pa kutokea. Kwakuwa msomi wa usanii hupaswa kuwa sharp,mbunifu na muangalifu,Lowassa akatumia haraka fursa.

Kinachoonekana na kusikika sasa,ni zao la usomi wa Lowassa. Hakuna mwanasiasa mkongwe chamani mwenye usomi wa usanii kama Lowassa. Wengine hutumia usanii wa kuzaliwa tu. Usomi una raha yake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Kwa hiyo Mzee Tupatupa,unataka kutuletea MSANII mwingine?Duh,kweli hutupendi Wadanganyika.........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom