Lowassa ndani ya Kigoma

Lowassa ndani ya Kigoma

Kuna wakati huko nyuma niliuliza lakini hata Mzee Mwanakijiji alishindwa kunisaidia, Lowasa alijiuuzulu uwaziri Mkuu kwa kashfa ya Richmond ili amnusuru rafiki yake BoyZ to Men Mheshimiwa Jakaya Kikwete.

Kwa upeo wangu mdogo mtu akijiuzulu anakosa sifa ya kuwa mstaafu kwa hiyo Kama CCM wanamwita mstaafu ni kosa kubwa na Waziri wa fedha pamoja na Rais hawakupaswa kuidhinisha Edward Lowasa(MB) kulipwa mafao ya Waziri Mkuu mstaafu ambayo ni asilimia 80% ya Mshahara wa Waziri Mkuu anayeko madarakani.

Once tukijua hicho kiasi ndipo tukokotoe hizo gharama anazochangia makanisa na kipato chake Halali of course aliiba sana na anazo pesa nyingi no doubt, hii inanipa wakati mgumu pia na usafi wa haya makanisa ambayo siku hizi yameanza biashara na kwa kuwa yana wafuasi wengi ni jambo la hatari kwa mwanasiasa kukaa nyuma ya dini.

All the time religious extremism is a cancer "whether Muslim or Christian " misingi yake mikuu ni ubaguzi : sisi na wao: mwisho wa siku ni vita. Tumwogope mwanasiasa staili ya Lowasa na lazima aangushwe at any cost!

Nitajibu moja tu hapo:
Sehemu kubwa ya pesa anazotoa "Mgeni/mwongoza harambee" hutoka kwa marafiki zake na watu wema wengine-si zake!

Kwa viongozi wa Serikali walioko madarakani na wenye mafungu ya kuchochea maendeleo kwenye ofisi zao huweza kutoa sehemu ya pesa za kuchochea maendeleo kama mchango kwenye harambee zenye faida kwa jamii.
 
EL viva sana kwa michango unayotoa kusaidia jamii na hakika Mungu yuko pamoja nawe. Kuhusu urais 2015 we are together with you, the hard working and creative man
ogopa sana mtu aliyeona loop za kukwapua kipindi cha nyerere. Sasa hivi kila sehemu anaona ni pa kuchukua tu, huyo huyo lowasa mzee wa artificial rain ndo facilitator wa richmond baadaye dowans(ambayo bado inatudai kama taifa) mchuma majanga hayo yote ndo mnaye mpepelea kuingia ikulu!! Lowasa ni mwizi mwandamizi, hakuna cha kutunziana heshima na jk hapa wote wezi. Jiulize, dili la richmond lisinge bumbuluka.............?
 
Nenda jukwaa la Utambulisho mkuu hapa c penyewe

Mkuu huyu jamaa hata kabla haja andika kesha kuwa janga la JF .Maana maandiko yake kama yuko facebook hapa si mahali pake ndiyo maana kavamia mada .
 
Nitajibu moja tu hapo:
Sehemu kubwa ya pesa anazotoa "Mgeni/mwongoza harambee" hutoka kwa marafiki zake na watu wema wengine-si zake!

Kwa viongozi wa Serikali walioko madarakani na wenye mafungu ya kuchochea maendeleo kwenye ofisi zao huweza kutoa sehemu ya pesa za kuchochea maendeleo kama mchango kwenye harambee zenye faida kwa jamii.
kwahiyo lowasa ndiyo mkondo pekee wa kupgtishia? La viongozi wa dini nalo ni donda ndugu kwa taifa, sijui ni Mungu gani huyo anaye waongoza mpaka watangazie umma kuwa flani ni chaguo lake (Mungu) afu baadaye wanamtolea matamko huyo mteule wa Mungu wao, tujiadhari nao pia.
 
Hivi nyie mnaodai EL ni fisadi mna EVIDENCE? na kama mnazo kwa nini msizipeleke mahakamani? Acheni uvivu wa kufikiri na chuki binafsi enyi wafuasi wa NEPI. Na kwa taarifa yenu EL ni chaguo la watu wote wanaotaka rais mchapa kazi, mwenye credibility katika leadership, creative na confidence. 2015 mtalia na kusaga meno enyi wafitini
 
Tatizo la viongozi wetu ni kutokubali kushindwa,hivi kweli Lowassa ni mstaafu? mimi ninavyo fahamu maana ya neno mstaafu ni mtu aliyefanya kazi ya utumishi na kuimaliza kulingana na umri na kwa nafasi za kuteuliwa ni mtu aliyemaliza muda wake bila kujiudhuru kwa kashfa yeyote.
Na je unajua maana ya kuwajibika kulingana na nafasi yako ya kiuongozi[ political responsibility]?
 
Sasa kule mbona chama chake huwa kinaangukiaga pua kila mwaka angalia ata majimbo ua uchaguzi utakuta mengi NCCR AU CDM
 
Atazunguka sana huyo Mmasai! Hadi mwaka 2015 wakati wa uchaguzi mkuu, nywele zake zote zitakuwa zimegeuka kuwa nyeusi.
 
hivi zitto si aliwahi kuwa kwenye payroll ya RA&EL?Kamfata swahiba..iam just thinking..
 
Jamani naomba msaada wenu wa jibu la swali hili.Hivi ni kweli kwamba Makanisa yote Tanzania yanamuona Edward Lowasa kwamba ndiyo National figure kiasi cha kumuhitaji katika hafla zao zote za fundraising?.
viongozi wa makanisa wana elimu na uelewa wa mambo mkubwa sana. To an educated and visionary one, EL is a right presidential material
 
swali kuu la kujiuliza je EL huwa anaomba awe mgeni rasmi au anaalikwa kuwa mgeni rasmi ?
kwa nini yeye mara nyingi anaalikwa kuliko viongozi wengine ?
kwa nini viongozi wa serikali hawaalikwi ?

Tuache wivu na majungu tumuache EL analo weza kufanya afanye maadamu ni jema Kuhusu kashifa ya Richmond alisema hakuwa peke yake yke ni system kubwa sana ndani ya chama kumhukumu pekee yake ni kumuonea
 
Mara nyingi Lowassa huwa anatoa maoni/michango mizuri sana kuhusu mambo changamoto zinazokabili taifa hili. Lakini kwa nia njema kabisa naomba niseme mfumo anaotumia Lowassa kuongelea hizi changamoto unanipa shida sana. Hii mialiko ya kuongoza harambee za dini moja (ukristo) is a self-defeating strategy. Huku ni kutugawa sisi kama taifa. Kwa nini aalikwe yeye tu? tena kwa madhehebu mbalimbali ya kikristo?

Nahisi siko mwenyewe kweli hili, watu wengi (kichinichini) watakuwa wanahoji ukaribu wake Lowassa na makanisa. Mara alipojiuzulu uwaziri mkuu tulishughudia jinsi kanisa hasa KKKT lilivyokuwa linamkwepa waziwazi, sasa nini kimetokea? wamefanya uchunguzi wao (kama kanisa) na wakagundua kile kilichokuwa kinawakimbiza mbali na huyu bwana ni uwongo?

Ningeshauri, kama kuna mkakati wa kutumia dini ili kufikia malengo ya kisiasa basi mkakati huo uguse dini zote (wakristo, waislam, hindu na dini za asili). Tukumbuke ukiwa kiongozi unaongoza watu wa dini zote, hivyo kuegemea upande mmoja ni sawa na kujiwekea akiba ya malalamiko toka pande zingine. Na watakaomia na wananchi wa kawaida.
 
Hivi nyie mnaodai EL ni fisadi mna EVIDENCE? na kama mnazo kwa nini msizipeleke mahakamani? Acheni uvivu wa kufikiri na chuki binafsi enyi wafuasi wa NEPI. Na kwa taarifa yenu EL ni chaguo la watu wote wanaotaka rais mchapa kazi, mwenye credibility katika leadership, creative na confidence. 2015 mtalia na kusaga meno enyi wafitini
hebu twambie kwanini selikali selikari ilijiuzuru?
 
Jamaa ni mtu wa watu, anayekubalika,hata kama haupendi. Matatizo yetu viongozi wengi hawayajui kwa kuwa hawapo karibu na wananchi, viongozi wengi wapo mijini, ila EL muda mwingi yupo na wananchi wa kada zote, wa kada ya chini na juu.

EL hana mipaka. Fanya utafiti maeneo mengi ya nchi utaupata ukweli.

Nyie mnawaza urais 2011 kwa kufanya fitna, ila jamaa anapambana na umasikini na kujenga chama chake.

Tafakari.
 
kama ccm watamteua EL kuwa mgombea wao ntam support, maana ni haki yangu kikatiba no matter what am for EL.
 
Back
Top Bottom