Lowassa, Nchi ilipokuwa njiapanda kwanini ulikaa kimya?

Lowassa, Nchi ilipokuwa njiapanda kwanini ulikaa kimya?

Chademakwanza

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2014
Posts
6,346
Reaction score
1,872
Edward Kwanini nchi Ilipokuwa Njiapanda Ulikaa Kimya? Ni Kiongozi waaina Gani Wewe?Kuna wakati nchi ilipita kipindi kigumu sana cha sintofahamu.

Kwanza ilikuwa wakati wa Bunge Maalumu la katiba ambapo nchi iliyumba na kutokea kutokuelewana kwa hali ya juu. Na kama sio wapinzani kuamua kutoka nje hakika bunge lile lingeishia waheshimiwa kupigana na kuvuana nguo kabisa.

Edo kama mjumbe ndani ya BMK hakuwahi kusikika akichangia kitu wala kutoa ushauri wakati ule mgumu kwa taifa katika kupata maamuzi yenye tija. Ni kiongozi wa aina gani asiyejihusisha au kuonyesha busara zake pale jambo zito linapo wakanganya watu?

Kukaa kimya ni kuonyesha huna upande au hujui utatuzi wa jambo hilo? Kama ulishindwa utatuzi wa utata wa Katiba jee changamoto za nchi itakuwaje?

Kulijitokeza suala lingine la Tegeta Escrow ambalo kidogo liiangushe serikali ya chama chako Bungeni, mapesa mengi yalichotwa na serikali na chama chako kilivuliwa nguo hadharani ila wewe hakuna aliyekusikia ukisema au kuchangia chochote katika jambo kubwa kama lile jee ulikuwa hujui ufumbuzi wake?

Au wewe ulikuwa huna uchungu na kilichotokea kwa vile wewe hupati maumivu ya hasara ile?

Ukiwa kama Mbunge lile lilikuwa jukwaa lako la kusemea hisia zako, sasa mbona watu leo hawajui kuhusu hisia zako katika lile? Huoni kuwa uwepo wako Bungeni ulikuwa sawa na kile kiti tuu, maana kiti Bungeni huwa kipo mwanzo mwisho wa kikao lakini hakina mchango wowote wa maana kwa kile kizungumzwacho.

Ndio maana watu wanaamini habari kuwa kuna watu matajiri wanamwaga mapesa yao kuhakikisha kuwa unashika nafasi ya juu kabisa kwa vile mambo mabaya kwa nchi hutasema, utakuwa BUBU kama ulivyokuwa Bungeni.
 
alishasema yeye siyo mtu wa kusema sema sana ni vitendo tu! ulitaka afanye nn wakat hayupo kwenye mamlaka ya uamuz maswal hayo waulize akina pinda , makamba, mwigulu na membe walioko kwenye kabinet hapo lowasa unamuonea bure! waulize hao washaur wa rais!
 
Hana jipya si ndio mafisadi hao wao ndio wameiweka nchi njia panda kwa wizi wao Leo anajidai anauchungu Na wananchi wakati anaiba hela za Richmond Na Tanesco mbona hakuwaonea huruma watanzania? Chonde chonde watanzania mwogopeni huyo msaka uraisi kwa kuonga mpaka makanisa Na misikiti ni hayati sana
 
Mtoa post nafikiri bado uelewi bado utaratibu wa bungeni.Nadhani unasahau CCM as a party kilichukua a collective cohesive decision ya kuunga mkono katiba pendekezi na Mh hasingeweza kwenda kinyume na msimamo wa chama chake. Mtendaji mkuu wa shughuli za kibunge ni Prime minister, sasa ulitaka aingilie mamlaka ambayo sio yake?
 
Lowasa huyu jambazi na ni muunda mitandao ya ukwapuaji.Chenge mshauri mkuu wa mtandao ,rostam mtoa pesa

Ni vuzuri watanzania tukajijengea utaratibu wa kufanya research kwanza and we can speak out our mind. Waingereza walisema 'no research no right to speak'
Sasa mh naomba utoe ushaidi wa hayo uliyosema hapo juu.
 
Uwe unaongea kwa facts sio unaongea tu ili kumchafua mtu kisa hana mpinzani nafikiri unapomtuhum mtu lazima achukuliwe hatua sa sijawahi sikia mh kama kweli alichukuliwa hatua za kisheria hii inanifanya niamini kuwa lowasa hana kosa coz angelikuwa ameshiriki hao waliomtaja wangemchukulia hatua,,,,tuacheni siasa na chuki za vijiweni hebu tuwe na utaratibu wa kufuatilia mambo na sio kudanganywa na wanasiasa
 
Hana busara huyu mzee wa monduli.kwahiyo hasingeweza kuongelea kuhusu hayo matatizo yetu
 
That's the most irresponsible comment a mature person can give.

And what is wrong with my comment? All what I mean is that he can do whatever he pleases to do BUT becoming the next President of Tanzania is out of question. You can take that to the nearest bank!

Only in Tanzania can a consummate well known corrupt politician dare to put his name to be considered for a such a post.

He has blinded so many people (including you) with his corruptly acquired wealth that he thinks he can do whatever he dreams. Be reminded that there are still some sane people in Tanzania.

I am glad that you have realized I am a mature person.
 
Labda kachaguliwa na Mungu akachunge ng'ombe kule Mondurichmond.
Urais wa Tanzania asahau!

Wewe ndiyo hujui lolote kuhusu haya maswala, yaani wewe ndiye utakaeenda kuchunga ng'ombe mwezi wa kumi wakati Lowassa aneyoyoma kwenda Ikuyu, utaelewa tuuuuu
 
kwani yeye angefanyaje wakati wenye dhamana zao wamekaa kimya?.kanuni ya ccm hutakiwi kuwahurumia wananchi.
 
Tangia atangaze nia mimi nimekuwa nikufunga usiku na mchana hili huyu bwana FISADI wala hasipitishwe na Cc mana tutakufa kwa njaa na taifa litauzwa,jamani watanzania wenye moyo safi wanao wajali watanzania wenzao tuungane kwa pamoja na hasa waislamu wenzetu tufunge kwa ajili ya taifa letu,Lowassa hafai ni Zimwi,Koboko,chunusi na kirusi mkubwa tutageuka mafukara.Kwa pamoja tunaweza dhidi ya FISADI HILI,Amen/Inshalah.
 
Back
Top Bottom