Lowassa na Tatizo la Uongozi CCM

Mchambuzi

JF-Expert Member
Aug 24, 2007
4,850
9,405
Suala hili lilitokea muda mrefu kidogo lakini nalirudisha tena kwa sababu binafsi nadhani halikupewa uzito unaostahili na hivyo kufifia wakati ni suala ambalo leo hii ndilo linalo tuweka kama taifa katika hatari ya kutumbukia katika mgogoro mkubwa kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hivi karibuni, Waziri Mkuu wa Zamani Edward Lowassa alitoa kauli juu ya matatizo ya kiuongozi yanayokikabili chama cha CCM, kauli ambayo iliamshwa mjadala mkubwa nchini. Kwa mujibu wa vyombo vya habari, Lowassa alinukuliwa akisema yafuatayo kuhusu CCM na uongozi wake:

"Pamoja na uzuri wake, muundo wa chama chetu ni mzuri sana, imani ya chama chetu ni nzuri sana, misingi inayoongoza chama chetu ni mizuri sana, lakini tuna tatizo la utendaji na uongozi ndani ya chama chetu."
Lowassa pia aliongeza kusema:

"…Ama katika kufanya maamuzi, ama kufanya maamuzi yasiyo sahihi au kutochukua hatua kwa matatizo yanayowakabili wananchi kwa wakati muafaka..."

Pamoja na umuhimu wa hoja hii, hasa katika nyakazi hizi ambazo CCM inatakiwa kujisahihisha kama ina nia ya kuendelea kupewa dhamana ya kuongozo nchi, badala yake hoja ya Lowassa ilibezwa na viongozi wengi ndani ya CCM, lakini mbaya zaidi ni kwamba hata jamii haikupa uzito unaostahili na hivyo kuifanya hoja ififie mapema. Wengi tunakumbuka kwamba Baba wa taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kwamba CCM ikiyumba, nchi itayumba. Huu ndio uhaliasia wa mambo baada ya miaka zaidi ya kumi na tano tangia Nyerere atoe utabiri wake kwani leo hii nchi yetu inapita katika kipindi kigumu pengine kuliko vyote tangia uhuru na sababu kuu ya tatizo hili ni matatizo ya uongozi ndani ya chama. Imekuwa ni jadi kwa jamii kushuhudia jinsi gani mienendo na lugha za baadhi ya viongozi wa CCM na baadhi ya wabunge wa CCM inavyozidi kukigharimu chama. Kwa mfano, kwa wengi wa wanaofuatilia kikao cha sasa cha bunge watakubali kwamba udhaifu wa kiuongozi miongoni mwa wabunge wengi wa CCM unazidi kulipeleka taifa letu kwenye hali ya hatari kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Ni muhimu sana kwa vyama vya upinzani vikatumia muda na nafasi hii kujifunza juu ya matatizo na changamoto zinazokikabili CCM badala ya kutumia muda mwingi kucheka na kuikebehi CCM kwani matatizo yanayokikabili CCM yanaweza kukikumba chama kingine chochote kitachofanikiwa kushika madaraka ya nchi yetu siku za usoni.
Tukirudi kwenye hoja ya Lowassa juu ya CCM na matatizo ya uongozi, moja ya sababu kubwa ya tatizo hili ni CCM kujaa wanasiasa huku kikipungukiwa viongozi wa kisiasa. Ni muhimu tukatambua kwamba kuna tofauti kubwa sana kati ya Mwanasiasa na Kiongozi katika utawala wa nchi. CCM kama chama lakini pia kama taasisi ina hazina kubwa sana ya wanasiasa, huku kikiwa na uhaba mkubwa wa viongozi. Nitajaribu kufafanua huku nikitaja tofauti zilizopo baina ya neno Mwanasiasa na Kiongozi.

1. Kiongozi anajali watu/wananchi anaowatumikia; Mwanasiasa anajali chama chake, nafsi yake, familia yake, lakini muhimu zaidi viongozi wake wakuu, hasa waliomteua kushika wadhifa husika. Mara nyingi tumeona jinsi gani wanasiasa wa CCM wamekuwa na unconditional obedience kwa wakubwa waliowateua. Hili linachangia sana matatizo ambayo Lowassa anayazungumzia.

2. Kiongozi ni mtu ambae hufanya maamuzi yanayolenga maslahi ya taifa au jamii inayomzunguka; Mwanasiasa hufanya maamuzi yanayokilinda chama chake, lakini hasa kuwaimarisha wanasiasa au makundi yaliyomfadhili/yaliyompa nafasi yake ya uongozi.

3. Kiongozi uhimiza matumizi ya fedha za walipa kodi kwa ajili ya miradi ya muda mrefu na yenye manufaa kwa jamii/maslahi ya taifa; Mwanasiasa uangalia zaidi miradi ambayo aidha inamnufaisha yeye binafsi katika kipindi chake cha madaraka au pamoja na wote waliomfadhili wadhifa husika;

4. Kiongozi hufukuza kazi watumishi wa umma wasiofaa; Mwanasiasa huwajenga na huwakinga kila wanapofanya maovu;

5. Kiongozi hujifunza kutokana na makosa; Mwanasiasa hakubali makosa, badala yake hujiona yupo sahihi wakati wote;

6. Kiongozi hufanya kazi vyema na wenzake bila ya kujali itikadi za vyama ili mradi ni kwa manufaa ya umma/maslahi ya taifa; Mwanasiasa mara nyingi huwa ni mnafiki, mfitini na mwoga. Mara nyingi, mwanasiasa hutumikia waliomteua au mfadhili wadhifa wake na hivyo huwa anaishi na kufanya kazi katika mazingira yaliyojaa hofu ya kuvuliwa wadhifa alionao, aidha na chama chake au wakubwa zake.

7. Kiongozi wakati wote husema ukweli; kwa Mwanasiasa, ni desturi kuwa muongo na mara nyingi huwekeza zaidi katika kugeuza uongo kuwa ukweli;

8. Na mwisho, katika usimamizi wa fedha za walipa kodi na rasilimali za umma, Kiongozi hujali kubana matumizi yasio ya lazima, na uhimiza matumizi yenye kulenga kuendeleza taifa na watu wake; Mwanasiasa mara nyingi hujikitika zaidi kuhakikisha fedha za walipa kodi na rasilimali za umma zinamnufaisha yeye na familia yake pamoja na wale waliompa fadhili ya uongozi.

Ningependa kuendeleza hoja ya Lowassa katika mazingira ya kuchambua aina ya viongozi waliopo ndani ya CCM. Nimefanikiwa kubaini aina tatu ya viongozi ndani ya CCM kama ifuatavyo:


· Wanaitikadi (Ideologues);
· Wapambe (Jesters);
· Wachochezi (trouble makers);


1. Wanaitikadi (Ideologues) – Ingawa hawa wamebakia wachache na ni wa kauli na sio vitendo, bado ni muhimu tukajadili kundi hili. Katika nchi iliyokomaa kisiasa, kwa kawaida, leaders define themselves in terms of a set of beliefs and values ambazo wanaziamini na kuzi tekeleza, lakini muhimu zaidi ni kwamba they consistently base their political action in the context of ideologies that they believe in. Suala la itikadi limeshajadiliwa sana humu JF lakini

ni muhimu kuhimiza tu kwamba itikadi ni suala la kijamii huku siasa ikiwa ni chombo tu cha utekelezaji wa mtazamo na malengo ya jamii husika. Siasa haizai itikadi, ni jamii ndio huzaa itikadi na siasa hujaribu kutelekeza itikadi husika.

Nchi za wenzetu kuna wanaitikadi (ideologues) wa aina nyingi lakini common zaidi ni liberals, conservatives, moderates n.k. Kwa viongozi wa kisiasa katika jamii hizi ni common practice kujipambanua na kuji position mbele ya umma/jamii kwa vigezo vya itikadi wanazoziamini na kuzisimamia. Vile vile, viongozi wa aina hii hujitofautisha na washindani wao (upinzani) kwa vigezo vya itikadi. Ni jadi misimamo, kauli na matendo yao kushahibiana na itikadi zao na zoezi hili uendela katika maisha yao yote ya uongozi. Ndio maana kwa wenzetu, ideologues die in their ideological boots.

Wanaitikadi wa dhati wameisha CCM. Walipo leo ni wale wanaojaribu kujipambanua kama wana itikadi wa ujamaa, lengo ikiwa ni kuwaadaa wananchi kwani wanatambua kwamba CCM hakikuwaandaa watanzania kuhamia kwenye mfumo wa soko huria kutoka kwenye ule wa awali wa Ujamaa. Watanzania wengi leo hii wamebakia kuduwaa na wasijue jinsi gani ya kukabiliana na maumivu ya sera za soko huria huku viongozi wanaohimiza CCM ni chama cha kijamaa wakiishi maisha ya ubepari uliopitiliza.

2. Wapambe (Jesters) – kundi la pili la viongozi wa CCM lile la wapambe. Hawa wamejaa ndani ya CCM na kwa jadi yao, wakipewa nyadhifa, kazi yao kubwa ni to ‘amuse', ‘cheer' and ‘charm' their masters (waliowapa madaraka). Hivyo ndivyo jinsi wapambe wanavyofanikiwa kuhudumia matumbo yao na familia zao. Enzi za uchifu, hii ilikuwa ni ajira rasmi, lakini katika dunia ya sasa ya serikali ya jamhuri, upambe sio ajira rasmi ingawa wapo wanaoteuliwa kwa vigezo hivi na wapambe hawa ni nuksi kweli kweli. Na ni heri ufarakane au tofautiane na the master kuliko mpambe kwani career-wise, kibiashara na mara nyingine kimaisha unaweza angamizwa. Vinginevyo kila siku tunashuhudia jinsi gani wapambe ndani ya CCM wanatumia nyadhifa walizopewa kiupambe to amuse viongozi waliowapa madaraka lakini muhimu zaidi, kukisaidia CCM to divert attention ya umma/wananchi from major issues of the day. Wapambe wamejaa kwenye majukwaa ya siasa za CCM, lakini wengi zaidi wapo bungeni.

3. Wachochezi (Political trouble makers) – kundi la tatu na la mwisho la viongozi wa CCM ni lile la wachochezi. Kazi kubwa ya viongozi hawa ni kushawishi na bamboozle umma, na wanatumia vyema prejudices na stereotypes zilizopo kwenye jamii yetu kwa maslahi ya CCM. Lakini hasa wakubwa waliowapa madaraka. Tabia na matendo yao viongozi wa namna hii mara nyingi ni very irrational and inhuman. Viongozi wa namna hii hawaheshimu mantiki (logic), human decency, consistency na hawana muda kusoma alama za nyakati.

Wachochezi hustawi na kujiendeleza kisiasa kwa kutengeneza kauli mbiu na misamiati ya ovyo ambayo CCM inaichukua na kujengea hoja na propaganda kwamba huo ndio ukweli uliosadidika, usiopingika na unaotakiwa kuabudiwa. Mtu yoyote ambae anapingana na viongozi wa namna hii, basi watamuita kila aina ya majina – haramia, adui, mhuni, mkabila, n.k, na mara nyingine kujikuta hatarini kimaisha Viongozi wa namna hii kwa kawaida hawana muda wa kuheshimu dhana ya uhuru wa mawazo na huwa hawaoni any merit on a political opponent (mfano tazama tabia na kauli zao dhidi ya upinzani bungeni) na badala yake wanajaribu kuwatuhumu wale wote wanaowa ‘challenge' kwa mbinu za udini, ukabila, ukanda, n.k. Lakini zana muhimu inayotumiwa na wachochezi ni popular prejudices and stereotypes zilizopo katika jamii, na huwa ni mabingwa wa kupika madai na ahadi za uongo ili kujiimarisha kisiasa pamoja na CCM. Viongozi wa namna hii ni mabingwa wa ku-appeal on stereotypes, prejudices, emotions, fears, na expectations za umma kwa kujenga propaganda based on themes za kidini, kikabila, ukanda n.k.

Tumeshuhudia mara kwa mara viongozi wa aina kutwa wakishambulia wenzao na mara nyingi huchangia sana kuchafua hali ya hewa ya kisiasa nchini kwani wana inspire paranoia na kuchochea mgawanyiko. Mbaya zaidi, viongozi wa namna hii hawana muda wa kuja na nguvu ya hoja na badala yake wengi ni wavurugaji na wahujumu wakubwa wa demokrasia.

Kwa mtazamo wangu, iwapo tutaweza kupambanua na kuelewa aina ya viongozi wa CCM kwa njia hii au nyinginezo, hivyo ndivyo tutakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kupata ufumbuzi juu ya jinsi gani kama taifa tutaweza epusha nchi yetu isiingie katika machafuko kutokana na CCM kuyumba kama alivyotabiri baba wa taifa, Mwalimu Nyerere.

Nawasilisha na Nasimama kukosolewa.
 
Mchambuzi Artcle yako ni nzuri sana, inaeleweka. Na yote ulioongea ni kweli, ninapenda tu kutoa wazo langu kuhusu kwa nini hoja ya Lowasa ilififia kwa haraka. Mara nyingi binadamu ana hulka ya kwamba kama mtu akishaonekana hafai ndani ya jamii kama yalivyotokea kwa Lowasa, basi hata atakachokisema inaonekana hata kama ni kizuri basi anaonekana mnafiki tu, kwanini asingesema akiwa madarakani akakosoa akiwa na madaraka bali akishapoteza madaraka ndo anayaona matatizo, ni sawasawa ni Maige kauli zake ni sahini lakini ni wakati gani amezitoa...hapo ndo shida ilipo.

Jambo lingine ni kwamba hizo tofauti ulizozieleza, kwa wananchi wengi hawajui au hawawezi kuzipambanua na kuzielewa, wangezielewa wangeweza kuwa makini katika kuchagua viongozi sio wanasiasa, hivyo kutokana na ujinga wa kutokujua elimu ya uraia kama hii, matokeo yake wamekuwa wakichagua wanasiasa tena kwa ushabiki bila kujua kufanya hivyo inagharimu maisha yake na taifa kwa ujumla. Mimi nashauri kwakweli bila kuwapatia elimu wananchi wetu wakajua umuhimu wa kuchagua viongozi sio wanasiasa, nina hakika Tanzania inaangamia... kibaya zaidi hata haki za msingi wanachi hawazijui kwahiyo ni vigumu kuzidai na wachache wanaozijua wamekuwa waoga kwakuwa walio madarakani wanafahamu kuwa ujinga wa wananchi ndio mtaji wao kuendelea kutawala, na hao wachache kudhibitiwa kwa vitisho hata kugharimu maisha yao.

Kuna usemi zamani mzee Jomo kinyata aliwahi kumcheka Nyerere kwamba ' Jomo Kinyata yeye anaongoza watu waliosoma na wanajua haki zao na kuzidai, ndio maana challenge ni nyingi, wakati Nyerere anaongoza watu wasiosoma, hawajui haki zao, hivyo hana challenge na kulinganisha na maiti" ambayo leo tunafumbwa kuwa nchi ya amani na mshikamano wakati sio kweli kwakuwa hali sasa inajieleza angalia mauaji,uhalifu, njaa, hata zanzibar kudai Muungano hauwafai, kwa uchache nameyataja.
 
Last edited by a moderator:
Nimeipenda article yako na uchambuzi wako makini, hayo maneno ni kweli ila ningependa kuongeza kidogo kwa kulingana na wakati huu wa vyama vingi. Ni kweli kuna wanasiasa na viongozi wa siasa lakini ukumbuke kwenye demokrasia ya kweli vyama vyote nguli vya siasa huwa vina faction(makundi) ndani yake, kwa hiyo sio kitu cha ajabu kuona CCM nayo ikiwa hivyo ni kitu cha kawaida kwa chama ambacho ni kikongwe kuliko vyote hapa nchini, hata CDM na CUF wanaelekea hukohuko suala ni muda au siku wakishika madaraka tutayaona hayo kwao pia.

Tatizo jingine kwenye demokrasia ya vyama vingi ni rahisi ukiwa mpinzani i.e. CDM au CUF kuonyesha udhaifu wa utawala bila hata kueleza wewe utafanyaje tofauti, ni rahisi siku zote kukosoa ila ngumu kuongoza. Ila kwa hili tuliliona wazi kwenye bajeti mbadala pale CDM walipochemka na kutoa bajeti yao ambayo hata wanachama wao waliona ina mapungufu(i.e. haikuleza wapi watatoa mapato yao) mengi zaidi ya ile ya serikali.

Vilevile kwenye demokrasia ya vyama vingi wanasiasa wengi hujikita zaidi kwenye populist agenda sababu wanaangalia uchaguzi ujao na hili tatizo sio kwetu tu hata kwa nchi zilizoendelea i.e. US na UK ni hivyohivyo wanaangalia na watu wanataka matokeo now!! na ndio tofauti na China ambayo kwa vile ni chama kimoja wana uwezo wa kuangalia mbali na kupanga mambo yao bila kujali wananchi wao na kuleta maendeleo ya muda mrefu.
 
kwa hyo mleta mada unachotka kusema ni kwamba lowasa ni kiongozi na si mwanasiasa sio??!!...naona umempalilia kweli
 
kwa hyo mleta mada unachotka kusema ni kwamba lowasa ni kiongozi na si mwanasiasa sio??!!...naona umempalilia kweli

Nia yangu haikuwa kumzungumzia Lowassa bali hoja yake kuhusu CCM na matatizo ya uongozi. Suala la Lowassa kuwa kiongozi au mwanasiasa nadhani hilo ni debatable.
 
Nyerere alimaliza shule akawa mwalimu akafundisha kidogo akajikita kwenye siasa moja kwa moja.

Mwinyi sina hakika sana na background zake za kazi lakini nadhani na yeye hana zaidi ya mambo ya kisiasa kwenye CV yake.

Mkapa angalau kidogo alijitahidi kama mtumishi wa umma lakini alifanya kazi kwenye magazeti ya Chama , wakati ule hizo kazi ni kama za kisiasa maana magazeti yalikuwa kwa ajili ya propaganda zaidi. Baada yapo mkuu wa wilaya etc

Kikwete alipomaliza shule akaingia TANU then CCM akaenda Monduli akafundisha chuo cha jeshi lakini hata yeye hana zaidi ya siasa kutoka Zanzibar , Singida, Mtwara nk kote kama mtumishi wa Chama.

Ndoto yangu siku moja tupate rais ambaye ana background ya Private sector mtu ambaye Lawyer ame practice, Banker, Doctor , Engineer, CEO,CFO, Manager, Enterpreneur, etc alete ladha tofauti hapo Magogoni. Hawa watu wenye background za chama na serikali huwa mtazamo wao wakiserikali serikali. Speed yao inakuwa ndogo wanaamini kila kitu kina take time.

Lete CEO wa benki mpe urais uone kama hajaanza kuwafanyia Performance appraisal mawaziri na wao wataenda kwa watu wao chini kufanya the same. Halafu uone huduma za umma zitakavyobadilika. Tatizo tunapenda sana watu wanaoweza kucheza na maneno :happy:
 
Huyu Lowasa ameshakwisha, na ni sawa na kumlinganisha na Profesa mstaafu. Uongozi hauwezi tena, hata umri wake haumruhusu kwani siasa za Tanzania sasa hivi zahitaji vijana au kuwa muwazi zaidi ni miaka kuanzia 40 mpaka 60. Baada ya hapo staafu na piga longo longo nje ya ulingo kama akina Walioba na wenzake wanavyofanya. Ukibahatika uongoze tume na si vinginevyo.

Hebu piga hesabu za haraka haraka, huyu mtu alitemwa na Nyerere mpaka akatoa machozi katika kinyanganyiro cha urais. Kipindi hiki katemwa na Kikwete, sasa unahitaji mpaka atemwe na M Mungu ndio ujue kuwa hafai.

Hebu muacheni akapumzike au akimbilie CHADEMA.
 
Huyu Lowasa ameshakwisha, na ni sawa na kumlinganisha na Profesa mstaafu. Uongozi hauwezi tena, hata umri wake haumruhusu kwani siasa za Tanzania sasa hivi zahitaji vijana au kuwa muwazi zaidi ni miaka kuanzia 40 mpaka 60. Baada ya hapo staafu na piga longo longo nje ya ulingo kama akina Walioba na wenzake wanavyofanya. Ukibahatika uongoze tume na si vinginevyo.

Hebu piga hesabu za haraka haraka, huyu mtu alitemwa na Nyerere mpaka akatoa machozi katika kinyanganyiro cha urais. Kipindi hiki katemwa na Kikwete, sasa unahitaji mpaka atemwe na M Mungu ndio ujue kuwa hafai.

Hebu muacheni akapumzike au akimbilie CHADEMA.

Ingekuwa na manufaa zaidi kwetu sote kama ungejikita zaidi kujadili hoja na sio mtoa hoja.
 
Ingekuwa na manufaa zaidi kwetu sote kama ungejikita zaidi kujadili hoja na sio mtoa hoja.

Mkuu Unakaribisha Mashambuliz Kutoka kwa Anti Lowasa. Huko CCM kuna Lowasa Camp, Sitta Camp na Membe Camp ( Si Uliona Lowasa alipotoa Hoja yake ni akina nani walikurupuka kumjibu)
 
Ingekuwa na manufaa zaidi kwetu sote kama ungejikita zaidi kujadili hoja na sio mtoa hoja.

Tatizo ni wewe mleta mada ambaye badala ya kuweka title inayosema Tofauti kati ya Kiongozi na Mwanasiasa wewe umeandika Lowassa na Tatizo la Uongozi CCM; sasa walalama nini??? Umeyataka mwenyewe kwa makusudi au kwa kutojua!!!
 
Mkombozi,
Makala nzuri sana lakini sisi waislaam husema Hata Shetani hutoa ahadi kaa za Mungu na ukimfuata utapotea wewe.
Lowassa alikuwa KIONGOZI na katika Sifa za Viongozi ulizozitoa hapo juu Lowassa hana hata moja isipokuwa anazo sifa za Mwanasiasa.. Hivyo ni rahisi kwa mwanasiasa kuzungumzia Uongozi wakati akipewa Uongozi hauwezi kutokana na kwamba Uongozi una sifa tofauti kabisa na uanasiasa. Sii alipata mnwamnya huo mbona ndio ilikuwa madudu makubwa!.
He is the reason behind what CCM has become lakini kama shetani ap;endaye ushindani haoni ubaya..isipokuwa kuna mchawi mwingine naye ni kiongozi na sii mwanasiasa.

Lini umemsikia Lowassa akitetea Afya bora, Elimu bora Madaktari, walimu au akipinga posho na matumizi yasiyokuwa na maana, lini umemsikia Lowassa akisema hata sera moja ambayo yeye anatarajia kuisimamisha - Hakuna! Lakini watu wanasema EL kiongozi bora wakati hawajui atatuletea nini au ubora wake unatokana na kipi alichosimamia. Lowassa anasema serikali kutochukua hatua kwa matatizo yanayowakabiri wananchi.. Umeme na Maji ilikuwa wakati muafaka - Je, alichukua hatua gani yeye kama sii kutuweka ktk mgao hadi leo hii..
 
Tatizo ni wewe mleta mada ambaye badala ya kuweka title inayosema Tofauti kati ya Kiongozi na Mwanasiasa wewe umeandika Lowassa na Tatizo la Uongozi CCM; sasa walalama nini??? Umeyataka mwenyewe kwa makusudi au kwa kutojua!!!

Msingi wa hoja yangu ni kwamba, kwanza mimi ni mwana CCM, lakini muhimi zaidi ni kwamba miaka ya nyuma, mwalimu Nyerere alionya kwamba CCM ikiyumba, nchi itayumba na kiini cha kuyumba huko itakuwa matatizo ya uongozi ndani ya chama. Tangia mwalimu atoe kauli hii, hapakutokea kiongozi mwingine yeyote aliyethubutu kutamka kwamba CCM imekumbwa na tatizo la uongozi mpaka hivi majuzi Lowassa alijipotokeza, ambapo kimsingi hata yeye anaendeleza mjadala wa Mwalimu aidha kwa kujua au kutokujua. Nimeweka title ya Lowassa kwa sababu yeye ni mtu wa ndani ya chama na ameyatamka hayo kwa ufasaha kabisa. Kwahiyo ilikuwa aidha nisukumwe na hoja ya nyerere au ya Lowassa, nikachagua hoja ya Lowassa kwasababu ipo more contemporary. Hata nisingeweka title ya Lowassa, bado hoja yangu ingebebwa na nukuu za Lowassa na sio vinginevyo. Kwahiyo badala ya ku reinvent the wheel, mimi kama mwana CCM nikaonelea niendeleze mjadala ulioanzishwa na kada mwenzangu wa CCM yani Edward Lowassa lengo likiwa ni kujadili mada, sio mtoa mada.
 
Mkombozi, Makala nzuyri sana lakini sisi waislaam husema Hata Shteani hutoa ahadi kaa za Mungu na ukimfuata utapotea wewe.
Lowassa alikuwa KIONGOZI na katika Sifa za Viongozi ulizozitoa hapo juu Lowassa hana hata moja isipokuwa anazo sifa za Mwanasiasa.. Hivyo ni rahisi kwa mwanasiasa kuzungumzia Uongozi wakati akipewa Uongozi hauwezi kutokana na kwamba Uongozi una sifa tofauti kabisa na uanasiasa. Sii alipata mnwamnya huo mbona ndio ilikuwa madudu makubwa!.
He is the reason behind what CCM has become lakini kama shetani ap;endaye ushindani haoni ubaya..isipokuwa kuna mchawi mwingine naye ni kiongozi na sii mwanasiasa.

Lini umemsikia Lowassa akitetea Afya bora, Elimu bora Madaktari, walimu au akipinga posho na matumizi yasiyokuwa na maana, lini umemsikia Lowassa akisema hata sera moja ambayo yeye anatarajia kuisimamisha - Hakuna! Lakini watu wanasema EL kiongozi bora wakati hawajui atatuletea nini au ubora wake unatokana na kipi alichosimamia. Lowassa anasema serikali kutochukua hatua kwa matatizo yanayowakabiri wananchi.. Umeme na Maji ilikuwa wakati muafaka - Je, alichukua hatua gani yeye kama sii kutuweka ktk mgao hadi leo hii..

Mkuu Mkandara,
Naelewa hoja yako kimsingi. Lakini ili kutatua tatizo la uongozi ndani ya CCM na pengine pia vyama vya upinzani kujifunza kutokana na mapungufu haya, tufanye nini ili siku za usoni watoto na wajukuu wetu wawe katika mazingira ya nchi inayoongozwa kwa misingi bora ya uongozi? Kumjadili Lowassa haisaidii sana, lakini tutafaidika zaidi kujadili hoja yake ambayo ina uzito mkubwa sana kutokana na ukweli yeye ni mmoja wa wanasiasa wakubwa ndani ya CCM. Vinginevyo ni dhahiri kwamba Lowassa hatokuwepo kwenye uongozi wa CCM na nchi hii forever, tujadili na kujaribu kusaidiana kuweka misingi kwa viongozi wajao. Huo ndio mtazamo wangu mkuu.
 
Msingi wa hoja yangu ni kwamba, kwanza mimi ni mwana CCM, lakini muhimi zaidi ni kwamba miaka ya nyuma, mwalimu Nyerere alionya kwamba CCM ikiyumba, nchi itayumba na kiini cha kuyumba huko itakuwa matatizo ya uongozi ndani ya chama. Tangia mwalimu atoe kauli hii, hapakutokea kiongozi mwingine yeyote aliyethubutu kutamka kwamba CCM imekumbwa na tatizo la uongozi mpaka hivi majuzi Lowassa alijipotokeza, ambapo kimsingi hata yeye anaendeleza mjadala wa Mwalimu aidha kwa kujua au kutokujua. Nimeweka title ya Lowassa kwa sababu yeye ni mtu wa ndani ya chama na ameyatamka hayo kwa ufasaha kabisa. Kwahiyo ilikuwa aidha nisukumwe na hoja ya nyerere au ya Lowassa, nikachagua hoja ya Lowassa kwasababu ipo more contemporary. Hata nisingeweka title ya Lowassa, bado hoja yangu ingebebwa na nukuu za Lowassa na sio vinginevyo. Kwahiyo badala ya ku reinvent the wheel, mimi kama mwana CCM nikaonelea niendeleze mjadala ulioanzishwa na kada mwenzangu wa CCM yani Edward Lowassa lengo likiwa ni kujadili mada, sio mtoa mada.
Aaaaah Mchumbuzi weee! Lowassa mtu wa kwanza?
Pengine umesahau unakumbuka kina Butiku, Warioba, Salim na Mwinyi waliwahi kumzungumzia JK maneno haya haya kwamba achukue maamuzi magumu. Ikafika hadi wakajiita CCM Asilia?. Unakumbuka Gen. Ulimwengu makala zake za mwanzo wakati wa EL au jamani ya EL yanawagusa zaidi kuliko waliotangulia..Nimesema wazi kuwa yeye ndiye sababu sasa ukisema haisadii kitu basi tayari una majibu yako. Hutaki kuutazama ukweli maana Uongozi bora ni watu na sii chama. Yeye ndiye pia behind your failures 2010 Je, unalijua hilo?
 
Aaaaah Mchumbuzi weee! Lowassa mtu wa kwanza?
Pengine umesahau unakumbuka kina Butiku, Warioba, Salim na Mwinyi waliwahi kumzungumzia JK maneno haya haya kwamba achukue maamuzi magumu. Ikafika hadi wakajiita CCM Asilia?. Unakumbuka Gen. Ulimwengu makala zake za mwanzo wakati wa EL au jamani ya EL yanawagusa zaidi kuliko waliotangulia..Nimesema wazi kuwa yeye ndiye sababu sasa ukisema haisadii kitu basi tayari una majibu yako. Hutaki kuutazama ukweli maana Uongozi bora ni watu na sii chama. Yeye ndiye pia behind your failures 2010 Je, unalijua hilo?

Naomba mwongozo wako mkuu ili tujadili mada - je tuombe admin abadilishe title ili tuwe katika nafasi nzuri zaidi ya kujadili mada husika badala ya mtoa mada? Ni dhahiri kwamba tukiweka uzito kwenye mtoa mada, hatutafikia muafaka wa maana zaidi ya he says she says pamoja na lawama na shutuma zisizo na kikomo. Naomba unisaidie ili tufanikishe lengo mkuu.
 
Kwa mtazamo wangu, iwapo tutaweza kupambanua na kuelewa aina ya viongozi wa CCM kwa njia hii au nyinginezo, hivyo ndivyo tutakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kupata ufumbuzi juu ya jinsi gani kama taifa tutaweza epusha nchi yetu isiingie katika machafuko kutokana na CCM kuyumba kama alivyotabiri baba wa taifa, Mwalimu Nyerere.
...Ufumbuzi upo kwa wale wachache sana -ambao, at least wako sane na sober- waliobaki ku-take charge kusimamia na kupigia debe misingi bora ya utendaji kazi. Wakubali kuwa "wenye akili kwenye kundi la vichaa" bila kujali kama watapoteza favors au mapenzi ya wenzao, hatimae watafanikiwa kuwaonyesha waTanzania mwanga at the end of the tunnel.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom