makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Wana JF,
Wachangiaji mmeongea sana kuhusu Kiingereza cha Magufuli na Lowassa. Uzi huu ulianza na Kiingereza kibovu kuliko maelezo cha Mgombea Uraisi wa CCM Bwana Magufuli. Lakini cha ajabu kibao kimegeukia kwa EL kwamba ndo hajui Kimombo. Magufuli ni PhD holder ilhali Lowassa ni Masters holder. Sasa nani anayetakiwa kuongea Kiingereza kizuri kuliko mwenzake?
Ikumbukwe kuwa kwa sasa tuna shule za English Medium ambazo zinafundisha Kiingereza kuanzia primary level mpaka A Level na ukikutana na hawa watoto pamoja na PhD yako kama Bwana Magufuli unaweza ukatolewa kamasi!
Je, kwa vile hawa watoto wa English Medium wanaongea English nzuri basi wapewe kugombea Urais??
Hili tatizo la Kiingereza cha kuongea na kuandika ni tatizo kwa Watz walio wengi sio la Magufuli, Lowasa, Kikwete na wasomi wengine. Wewe kama unataka kujua Watz wengi hasa viongozi sikiliza mijadala ya Bungeni uone kile kinachoitwa Kiswa-nglish! Unapoona mtu anachanganya Kiswahili na English ujue hapo kuna tatizo. Kwamba lugha ya Kiingereza haipandi lakini anajaribu kuchomekea anapowasilisha hoja au swali ili aonekana naye wamo ilhali hakuna kitu!
Kwa hiyo basi hapa hoja ya English ni upuuzi mtupu wala haitusaidii katika mjadala huu.Hata Rais Kiwete anayeondoka madarakani ndani ya siku 26 zijazo HAJUI KIINGEREZA lakini ameongoza taifa hili kwa hii miaka 10. Hakuna issue hapa.
Hata kama ni Magufuli au Lowassa ataenda UN, cHINA, USA, RUSSIA na kwingineko WAKALIMANI wapo ndiyo kazi yao. Nyie mnafikiri kwanini kuna wakalimani? Ni kwasababu huwezi kujua lugha zote kwa usahihi wake.
Mwisho, ili kukata mzizi wa FITINA kati ya Magufuli na Lowassa naomba taasisi ambazo zinaweza kuandaa midahalo ya Wagombea Urahisi(Uraisi) waandae kipindi cha TV/RADIO na kiendeshwe kwa lugha ya Kimombo halafu tuone nani ataonekana ni mzuri kwa kujieleza kwa English! Nachelea watu wanaweza kuingia mitini!
English is not our mother tongue! Wala Rais wetu hatutegemei kila siku atakuwa akihutubia Bunge, au mihadhara mbaimbali kwa Kiingereza. Kiswahili kipo kama lugha ya mama na ndicho tunachotaka Rais wetu awasiliane na sisi ili tumwelewe. Akienda huku majuu, Wakalimani watafanya hiyo kazi ndiyo maana wameajiriwa kwa kazi hiyo.
Zungumzieni issues ambazo hawa wagombea Urais tunataka wazikabili watakapoingia magogoni ili tuweze kupata mwelekeo na mstakabali sahihi wa Taifa letu. English is neither an issue nor an agenda here!
Wachangiaji mmeongea sana kuhusu Kiingereza cha Magufuli na Lowassa. Uzi huu ulianza na Kiingereza kibovu kuliko maelezo cha Mgombea Uraisi wa CCM Bwana Magufuli. Lakini cha ajabu kibao kimegeukia kwa EL kwamba ndo hajui Kimombo. Magufuli ni PhD holder ilhali Lowassa ni Masters holder. Sasa nani anayetakiwa kuongea Kiingereza kizuri kuliko mwenzake?
Ikumbukwe kuwa kwa sasa tuna shule za English Medium ambazo zinafundisha Kiingereza kuanzia primary level mpaka A Level na ukikutana na hawa watoto pamoja na PhD yako kama Bwana Magufuli unaweza ukatolewa kamasi!
Je, kwa vile hawa watoto wa English Medium wanaongea English nzuri basi wapewe kugombea Urais??
Hili tatizo la Kiingereza cha kuongea na kuandika ni tatizo kwa Watz walio wengi sio la Magufuli, Lowasa, Kikwete na wasomi wengine. Wewe kama unataka kujua Watz wengi hasa viongozi sikiliza mijadala ya Bungeni uone kile kinachoitwa Kiswa-nglish! Unapoona mtu anachanganya Kiswahili na English ujue hapo kuna tatizo. Kwamba lugha ya Kiingereza haipandi lakini anajaribu kuchomekea anapowasilisha hoja au swali ili aonekana naye wamo ilhali hakuna kitu!
Kwa hiyo basi hapa hoja ya English ni upuuzi mtupu wala haitusaidii katika mjadala huu.Hata Rais Kiwete anayeondoka madarakani ndani ya siku 26 zijazo HAJUI KIINGEREZA lakini ameongoza taifa hili kwa hii miaka 10. Hakuna issue hapa.
Hata kama ni Magufuli au Lowassa ataenda UN, cHINA, USA, RUSSIA na kwingineko WAKALIMANI wapo ndiyo kazi yao. Nyie mnafikiri kwanini kuna wakalimani? Ni kwasababu huwezi kujua lugha zote kwa usahihi wake.
Mwisho, ili kukata mzizi wa FITINA kati ya Magufuli na Lowassa naomba taasisi ambazo zinaweza kuandaa midahalo ya Wagombea Urahisi(Uraisi) waandae kipindi cha TV/RADIO na kiendeshwe kwa lugha ya Kimombo halafu tuone nani ataonekana ni mzuri kwa kujieleza kwa English! Nachelea watu wanaweza kuingia mitini!
English is not our mother tongue! Wala Rais wetu hatutegemei kila siku atakuwa akihutubia Bunge, au mihadhara mbaimbali kwa Kiingereza. Kiswahili kipo kama lugha ya mama na ndicho tunachotaka Rais wetu awasiliane na sisi ili tumwelewe. Akienda huku majuu, Wakalimani watafanya hiyo kazi ndiyo maana wameajiriwa kwa kazi hiyo.
Zungumzieni issues ambazo hawa wagombea Urais tunataka wazikabili watakapoingia magogoni ili tuweze kupata mwelekeo na mstakabali sahihi wa Taifa letu. English is neither an issue nor an agenda here!