Lowassa kuwa rais sawa, lakini kwanini anahonga?

Lowassa kuwa rais sawa, lakini kwanini anahonga?

mimi siamin kama amehonga chadema wanasubiri ccm watamfanyaje huyu bwana, je watamtosa au atabeba bendera ya ccm na wakimtosa mbadala ni nani? ili wapange shambulizi

Hilo la Chadema kuhongwa liko wazi mno. Na kwa taarifa Lowassa ameshakubaliwa kugombea kupitia Chadema endapo jina lake litaondolewa CCM. Karata ya Lowassa sasa ni kutishia kuondoa CCM na kuitaadhalisha CCM kwamba anauwezo wa kukiua chama. Chadema nao wanasindikiza team Lowassa katika wimbo huu wa vitisho. Maana wao pesa wamekula na hapo hapo wanasubiri ccm ifanye kosa kumweka Lowassa ili wachukue nchi au kumfukuza ili ajiunge Chadema na kudhohofisha ccm.

CCM kujiokoa na kifo itachagua kumbwaga Lowassa kwenye urais maana kumpitisha yeye ni kutia sahihi kwamba ufisadi rushwa na matumizi mabaya ya madaraka ndio sera za ccm. Lile gamba ambalo lilishindikana kuvuliwa sasa akina Kinana na Mangula wanaweza kulivua. Report ya Mwinyi juu ya kuwafukuza wanachama wasio waadilifu, report ambayo Lowassa na Makamba senior waliikalia, sasa nayo inaweza ikaleta matumaini kwa wanachama wa ccm. Akishafukuzwa Muhongo wa Escrow Lowassa wa Richmond na EPA naye atatakiwa apigwe chini urais ili wanaccm warejeshe imani kwenye chama. Naamini ccm haitafanya kosa na wala haipo kwenye wakati mgumu kufanya uamuzi huu sahihi. Mrema hadi sasa anajuta kuhama chama na sasa Lowassa anatayarisha meza ya majuto na sidhani kama atakuwa na ubavu wa kuhama kama anavyojaribu kutishia.

Ifahamike kwamba wanaowapa ukawa ushindi ni CCM na sio wanachama wa ukawa. Hivyo basi CCM ikionyesha dhati ya kukomesha Rushwa, utovu wa maadili, kuwawajibisha wahusika wa ubadhilifu kwa kutowarudisha madarakani, na kukemea matumizi mabaya ya madaraka pamoja na kupiga vita kujilimbikizia mali kwa viongozi wa umma, ccm itakuwa imejihahakikishia ushindi. Ajabu malalamiko haya yote ya msingi kwa wanaccm sio ajenda za Lowassa na wala hutamsikia akiongelea.
 
Kutoa rushwa ili kuteukiwa au kuchaguliwa ni jadi ya CCM. Hakuna kiongozi hata mmoja CCM asiye mtoa rushwa. Nashangaa kwa nini Lowasa anahambuliwa kwa kutoa rushwa!

Kwa ujumla Hakuna mwana CCM asiye mtoaji Au mpokea rushwa. CCM=RUSHWA
 
Hilo la Chadema kuhongwa liko wazi mno. Na kwa taarifa Lowassa ameshakubaliwa kugombea kupitia Chadema endapo jina lake litaondolewa. hoja zako zingine nimeikubali ila lowasa kuhama chadema bado sikubali kwa sabab ufisadi wa lowasa uliibuliwa na chadema na wakati wa richmond chadema walishupalia sana kumkubali lowasa ni kula matapishi yao na pia kuwaambia watanzania wao chadema hawachukii ufisadi ila tunadanganya tu ndio mana nashindwa kuamin lowasa kuhamia chadema
 
Kutoa rushwa ili kuteukiwa au kuchaguliwa ni jadi ya CCM. Hakuna kiongozi hata mmoja CCM asiye mtoa rushwa. Nashangaa kwa nini Lowasa anahambuliwa kwa kutoa rushwa!

Kwa ujumla Hakuna mwana CCM asiye mtoaji Au mpokea rushwa. CCM=RUSHWA

kwa sabab anasifiwa kuwa ni kiongoz bora
 
wanajanvi nimekuja na hoja hii kwamba lowasa kuwa rais sina shida lakin kwa nin ana tumia hela nyingi kuhonga honga makanisan na misikitin? "nyerere alisema anayetaka urais kwa kuhonga watu huyo mwogopeni kama ukoma" akijenga hoja kwamba ikulu kuna biashara gani? hela anayotumia kuhonga watu amepewa na nani? na atarudishaje akiwa rais wetu? haya ni maswali ya msingi sana tunatakiwa kuweka ushabiki pembeni namtaka yeye mwenye lowasa aje atujibu kwa ufasaha kama anataka kuwa kiongoz wetu kwa sabab ikulu ni mahali pa takatifu haiwez kuwa pango la walanguz lowasa anachofanya ni ulanguz mkubwa ili aingie ikulu. nawasilisha.

lowasa anaombwa kusaidia na wenye hizo taasisi hatoi rushwa walio chapa hadi ma T-shirt hamuwaoni ila lowasa tu. acheni chuki? wapi lowasa katoa rushwa? kuna watu wanajinadi wazi wazi hamuwaoni ila lowasa tu. acheni hofu mnaogopa nini. na ni kweli jamaa akipita wapiga dili wote watakuwa hatarini.mwacheni akakataliwe kwa kura halmashauri kuu.
 
wanajanvi nimekuja na hoja hii kwamba lowasa kuwa rais sina shida lakin kwa nin ana tumia hela nyingi kuhonga honga makanisan na misikitin? "nyerere alisema anayetaka urais kwa kuhonga watu huyo mwogopeni kama ukoma" akijenga hoja kwamba ikulu kuna biashara gani? hela anayotumia kuhonga watu amepewa na nani? na atarudishaje akiwa rais wetu? haya ni maswali ya msingi sana tunatakiwa kuweka ushabiki pembeni namtaka yeye mwenye lowasa aje atujibu kwa ufasaha kama anataka kuwa kiongoz wetu kwa sabab ikulu ni mahali pa takatifu haiwez kuwa pango la walanguz lowasa anachofanya ni ulanguz mkubwa ili aingie ikulu. nawasilisha.

lete ushahidi wa mtu hata mmoja aliehongwa na Lowasa
 
kinachogomba ni matumiz ya fedha kuendea safar yake ya kuwa rais sadaka sio shida anachofanya lowasa na mambo aliyofanya ni zaidi ya sadaka ametoa hela nyingi kwa vikundi vya kwaya kwaya na hela izi anatoa wap? hii ndio hoja kama unajua kisima anachotumia lowasa kuchota hiz hela utuambie

pesa anazotoa anapewa na marafiki zake Lowasa ni masikini tu hana pesa yoyote
 
Acha kuogopa a.k.a unafiki. EL hafai kuwa rais wa nchi hii kwa sababu baadhi ni hizo ulizozitoa kwenye main thread. Tulisha mtupa jalalani kwa kuwa alithibitika kuwa ni takataka. Leo afae kugombea urais kwa usafi upi? Tusishawishiane kurudi vyooni kufuata vyakula tulivyovitupa kutoka matumboni mwetu baada ya kuvitupa kwa namna ambayo tumeumbwa. Think out of the Box! Tumeng'ang'ania Lowasa! Lowasa! kama vile wengine hawawezi!

Basi tutamchagua shangazi yako awe rais
 
lowasa anaombwa kusaidia na wenye hizo taasisi hatoi rushwa walio chapa hadi ma T-shirt hamuwaoni ila lowasa tu. acheni chuki? wapi lowasa katoa rushwa? kuna watu wanajinadi wazi wazi hamuwaoni ila lowasa tu. acheni hofu mnaogopa nini. na ni kweli jamaa akipita wapiga dili wote watakuwa hatarini.mwacheni akakataliwe kwa kura halmashauri kuu.
umehongwa kiasi kumtetea huyu mchafu mwenzako .
 
Back
Top Bottom