Lowassa kakosea? Hapana, tujikumbushe ushauri huu

Lowassa kakosea? Hapana, tujikumbushe ushauri huu

Kama ungepingana na Lowasa mwana hisa mkuu wa chama baada ya kuuziwa na Mbowe ningeomba ban ya miezi sita!

Hivi ninacho jiuliza kwanini haukujitokeza kuwazuia Bavicha kwenda dodoma kabla ya mwenye chama Lowasa kuwakemea kuacha maandamano?

Hivi Mbowe alikuwa wapi kutoyasema hayo na amewazuia vijana baada ya mwenye chama kukemea maandamano?

Hivi ni nani ataamini mnakubaliana na Lowasa na hamuogopi ikiwa mlishindwa kuwazuia vijana kabla ya Lowasa kuwakemea?

Hakika hakuna wa kupingana na Lowasa ndani ya chadema!
 
Kwa hiyo sisi ndio tulikuwa tunakosea??
Kwa hiyo aliposema "tumegraduate na kuwa chama cha siasa" yupo sahihi?? Kabla hajaja tulikuwa chama cha kufa na kuzikana??
Yani Lowassa sasa ni wa kuabudiwa na kusifiwa tu hata akiongea upuuzi wa namna gani.
Halafu ina maana Lowasa asinge sema hiyo juzi wange waacha hao vijana wakavunjwe miguu?

Hakika Mbowe kwa Lowasa hana ujanja...Bavicha wote chaliii...

Hivi Malisa yuko wapi?
 
Tuwe na akiba ya maneno. Ona sasa jinsi Yeriko unavyoaibika kwenye mada hii
 
Ama kweli ukistaajabu ya Mussa utayaona ya firauni
 
Maelezo yako yalikua mazuri sana, ila tatizo Lowasa ulimshafua sana... Mtasingizia hakuna adui wa kudumu au rafiki wa kudumu.. Ila sio kwa Lowasa, yaani mwizi asiwe rafiki wa kudumu... Angekua mwanachama safi sawa
 
Bwana upo sawa wapuuzi ndio wanakuwa wazito kukuelewa. Maana hata mtu akitenda makosa, mungu humuandika kwenye kitabu cha hukumu ya milele. Lakini tu anapotubu na kumrejea mungu wa kweli, mungu huyuhuyu humsamehe na kumfuta katika kitabu cha hukumu, na kumuandika katika kitabu cha watakatifu. Sasa hawa wanaponang'ania kuwa alikuwa mwizi, napata kuwashangaa sana. Na kwanza alikwisha kuwaambia kuwa kwenye ushahidi, aende mahakamani na sio kukaa huku pembeni na kupiga kelele kama mbwa muoga. Mh. Lowasa ndiye rahisi chaguo la watanzania mkubali mkatae.
 
Nilizani wewe ni kijana imara,mwana BAVICHA alieiva, jitokeze hadharani kama alivokua mh. Zitto enzi zake kupinga kila ovu lilipokua linajitokeza hata kama limefanywa na kiongozi mzito wa chama.

Je na wewe pia unaunga mkono CHADEMA kuacha harakati? Umesahau usiku ule pale Loyola? Mnyika acha woga, kuwa na ujasiri kama Zitto.

Sema kweli hata kama utaudhi wengi.
 
muungwana akivuliwa nguo uchutama..katika jambo lolote linalomhusu lowassa ni heri ubaki kimya..huna cha kuwaeleza watu wenye kumbukumbu wakakuelewa,labda wendawazimu.katika watu waliochangia kwa kiasi kikubwa kumporomosha yule mzee wewe ni mmojawapo..ulivuka hadi mipaka..chochote utakachoongea sasa juu yake ni unafiki mkubwa..
 
Bwana upo sawa wapuuzi ndio wanakuwa wazito kukuelewa. Maana hata mtu akitenda makosa, mungu humuandika kwenye kitabu cha hukumu ya milele. Lakini tu anapotubu na kumrejea mungu wa kweli, mungu huyuhuyu humsamehe na kumfuta katika kitabu cha hukumu, na kumuandika katika kitabu cha watakatifu. Sasa hawa wanaponang'ania kuwa alikuwa mwizi, napata kuwashangaa sana. Na kwanza alikwisha kuwaambia kuwa kwenye ushahidi, aende mahakamani na sio kukaa huku pembeni na kupiga kelele kama mbwa muoga. Mh. Lowasa ndiye rahisi chaguo la watanzania mkubali mkatae.

Sasa umesema nini? alikuwa mwizi na sasa ametubu au si mwizi kwa vile ushahidi haupo?
 
Kwa hiyo sisi ndio tulikuwa tunakosea??
Kwa hiyo aliposema "tumegraduate na kuwa chama cha siasa" yupo sahihi?? Kabla hajaja tulikuwa chama cha kufa na kuzikana??
Yani Lowassa sasa ni wa kuabudiwa na kusifiwa tu hata akiongea upuuzi wa namna gani.
Kama hujaelewa jambo katika andiko hili na video hii omba ufahamishwe
 
Back
Top Bottom