Lowassa kachezeshewa "chekundu cheusi"?

Lowassa kachezeshewa "chekundu cheusi"?

Angalau sasa watanzania tumeona kuwa jk amefahamu MUNGU yupo na ameanza kurudi kwa wengi kwani ndo aliko na kuachana na shetani na kazi za mikono yake.
 
kwahio Ritz unakubaliana na huyo jamaa kuwa hadi tuwe na elimu ya majini kama masheikh uoni huko ni kuudhalilisha uislamu itakuwa sheikh awe na elimu ya majini?

Uislam umeingiaje tena hapa?
 
Last edited by a moderator:
Mwanakijiji wewe ni mchambuzi mzuri mfano wa chekundu - cheusi unafurahisha lakini katika muktadha huu ni mfano mfu. Nani alikwambia kuwa Mh. Lowassa na Rais Kikwete ni maadui? Watu wanawekewa maneno nao wanayabeba kama majuha.
Lowassa na Rais Kikwete ni Marafiki wa siku nyingi na hakuna wa kuwatenganisha wala wao hawana sababu za kuwa maadui, wawe maadui kwa lipi???

Anayesema kuwa hawa ni maadui ama atakuwa ana matatizo kwenye ubongo na mfumo wote wa ufahamu wake au atakuwa ni wakala wa kuendelea kupumbaza watu kwa makusudi yao na hapo ndipo wanaokubali na kufikiri kuwa ni maadui ndio wanachezeshwa chekundu- cheusi!!

Hii ni JF watu tuna vichwa vizuri!!
Mkuu wewe kweli uko sawasawa! Siku zote nimekuwa nikijiuliza ugomvi tunaoaminishwa kati ya lowasa na kikwete chanzo ni nini? Nimefuatilia sijaona hata mtu mmoja mwenye ushahidi kwamba hawa watu hawapatani! Tanzania ni nchi ya MAZUZU, siku zote ni watu wakuchezewa propaganda na wenyewe wana dance without questioning. Hii ni cinema walipanga siku nyingi hawa mabwana kutuhadaa, but at the end of the day watanzania wataingia kingi! Tangu EL alipopigwa chini u prime minister kutokana na maskendo, walikaa chini na kupanga watoke vipi! Kaka akamwambia bwana eeh mimi nikikuunga mkono directly watu hawatatuelewa! Tujifanye haziivi but nitakuwa nakusapoti kuandaa watu watakaokupitisha ili uni replace kwa ofisi! Kama tunaipenda TZ ni lazima tuhakikishe WANAMTANDAO WOTE WASITUCHEZEE AKILI, KWANI NDIO WALIOTUWEKEA KAKA, NA HIVI SASA WANATULAGHAI KWA KUTAKA KUTUWEKEA MWANAMTANDAO MWINGINE! KINACHOFANYIKA NI KUHAKIKISHA WATANZANIA HAWAFIKIRI WATU WENGINE ILA WAO TU ! HII INARATIBIWA NA MAKANJANJA WA VYOMBO VYA HABARI, AMBAO KWA HAKIKA NDIO WALIOTUFIKISHA HAPA TULIPO. HII MEDIA YA BONGO IS TOO SUBSTANDARD KUTUELEKEZA NANI ANAFAA KUWA RAIS! NI WAKATI MUAFAKA SASA WATANZANIA KUWAHOJI WANAOTAKA KUTUONGOZA NINI WANAWEZA KUTUFANYIA AND HOW B4 KUWAPA MADARAKA NA SI KUSIKILIZA VIGAZETI UCHWARA! All in all BIG UP SANA MKUU, TUPO PAMOJA!
 
Kama kawaida Pro-Chadema JF wanamjadili rais atakayekuja ambaye hatatoka CCM wamemsahau kabisa Dr Slaa na Chadema yao.

Watu wanajadili kilichopo na kinachoendelea kusikika kwenye masikio ya watu.Dr.Slaa muache atulie zake hakuna cha kumjadili kwa sasa tusubiri wakati wake na chadema tutawajadili
 
Ni wazi mwisho wa kundi la Lowassa utaanzia leo; hasa tukisubiri uundwaji wa sekretariati mpya ya CCM ambayo itakipeleka chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Mtu kaliwa. Lakini atarudi tena na fedha nyingine kujaribu kucheza mchezo ambao uko dhidi yake?

Kama EL alikuwa na nia ya dhati ya kutaka kupewa nafasi ya kuongoza CCM ili awee kujiandalia mazingira mazuri kwa 2015 basi alipaswa kuiga mbinu za Jacob Zuma wa South Africa. Hali ya ANC ilikuwa kama ilivyo sasa hali ya CCM, Jacob Zuma ambaye alikuwa amechafuka sana mbele ya jamii kwa kashfa za ufisadi alijipanga na kuweka wazi uadhaifu wa kiutendaji wa Rais Thabo Mbeki. Na alichofanya Jacob Zuma hakujificha nyuma ya migongo ya wanachama wa ANC, alijitokeza wazi wazi na kupata support ya vijana wakiongozwa na aliyekuwa mwenyekiti wa Youth League Julius Malema. Jacob Zuma aliamua kuweka nia yake ya kutaka uongozi wa juu wa NC, na Alijaza form, na walipoingia kwenye uchaguzi alimgalagaza Thabo Mbeko vibaya mno. Baada ya Miezi michache Jacob Zuma aliitisha NEC ya ANC iliyojadili utedaji kazi wa Serikali na kuamua kuiunda upya serikali iliyokuwa imeyumba kiuongozi na kiutendaji na kuomba Thabo Mbeki ajiuzuru. Kwa vile NEC ya ANC ilikuwa imeundwa na washabiki na wafuasi wa karibu wa Jacob ZUma kama ambavyo NEC ya CCM imejaza Pro Lowassa, haikuwa kazi kumuengua Thabo Mbeki na kusadia Jacob Zuma Kushinda uraisi wa Afrika kusini kamatika uchaguzi mkuu uliofuata hapo Baadaye. Nilitegemea Lowasa angejitokeza blodly kama Jacob Zuma kumpinga JK wazi wazi katika uchaguzi, na kama Lowassa angedhamiria na kujipanga mapema bila shaka angemuondoa JK katika kinyangányiro hiki.
 
Wale wa Kichekesho Membe wanajiliwaza.All in all tua enjoy sana ze CCM comedy ndani ya kipindi cha miaka miwili.Watakaorogana sana.sasa hivi kuna watu kusubiri tena ni kama adhabu ya kutogombea maisha.

Kuna watu waliopoenda fia ikulu ila hawana nafasi kwani tokeni yao imekaa vibaya, au ipo mbalia, kuna ambao zamu yao ikifika CDM watakuwa ndio watwala.
 
Nadharia feki. EL alimwambia JK pale Wakati anazindua barabara yeye akiwa ujerumani kwa matibabu, nanukuu 'baada ya wiki mbili tutaelekea Dodoma kuidhihirishia dunia imani tuliokuwa nayo kwa mwenyekiti wetu kwa kumpa kura za ndio' sasa MM, unatufanya mazuzu kirahisi hivyo? suala la vipeperushi si kila mtu anajua ni Membe? Bashe alipomuattack source si ni vipeperushi? aah ficha hisia zako mkuu. Mission ya JK ni kuweka mfuasi wake he can be Membe, EL au mwingine yeyote mashaka yake ni je? atauzika nje ya chama? naamini JK n EL have never bn real foes bt occasitions of misunderstdndings? may be yes!
 
Naomba niwasaidie msiojua. Neno ni "MAADUI" kwa Jk & El ni fahari kwao na ndo nguzo ya kutimiza matakwa yao kisiasa. Tujikumbushe tu kwamba suala la El Kumfikisha Jk Magogoni halihitaji miwani, na kazi hihi Eli kama Mkristo hakuifanya kwa maana ya kutenda wema na kuundoka zake!

Bali ulikuwa ni mpango wake kuhakikisha awamu ijayo nae anaingia Magogoni. Kwa maana hiyo El maana yake halisi kumfikisha Jk hapo alipo ni kwamba alimwaga sehemu ambayo ni rahisi kuzoa.
 
This was well said mwanakijiji, thank you. I think Lowasa's camp will retreat and rethink, plan anew on throwing the last card. The question is; will they make it? will they be able to out-compete with JK's machinery?
 
Tatizo la Lowassa ni kudhani kuwa anapendwa na fedha zake zinaweza kufanya kila kitu. Jamaa zake wa karibu hawamwambii ukweli, wanamficha huku wakitafuna fedha zake. He will see all colours at the end of the tunel!!
 
jamani labda mie mtaniita mshamba wa siasa lakini panapokua na mgombea mmoja kwenye nafasi ya uongozi sasa uchaguzi hapo wa nini? nilifikiri uchaguzi maana yake unachagua kati ya A au B...sasa leo hii ukiambiwa uchague kati ya A au A huo ni uchaguzi kweli...O.I.T(ONLY IN TANZANIA)
 
Tatizo la Lowassa lilianzia baada ya kujiuzuru. Kusema ukweli angefuata njia sahihi ambazo watu walimshauri wala asingefikishwa hapa. Alikuwa na nafasi moja tu ya kujikita ndani ya CCM - kupitia Mkutano Mkuu wa CCM. Kushindwa huku kwa Lowassa ni dalili ya kushindwa kufikiri kimkakati na kushindwa kuangalia mbali. Alichagua njia mbaya ya kushughulika na wabaya wake wa kisias.
 
Huyu kijana anaejiita Mzee Mwanakijiji, anaonesha kwa dhati kabisa kuwa ni fataani kwelikweli na anataka kuwaaminisha watu yasiyokuwepo.

Humjui Kikwete humjui Lowassa, unawasikia tu.

Mtakufa navyo vijiba vya roho!
Gaidi siku hizi umehamia kwenye Taarabu nini? Naona unakuja ni misemo ya Hadja Kopa
 
Back
Top Bottom