Naamu mambo huko dodoma yako mwishoni na taarifa zikiwa wazi kabisa kuwa,
1. Swala la kupingwa vikali kwa Membe na JK, kutoka ubande unaosadikiwa kuwa ni wa Lowasa kupitia kwa vijana wake na kundi lake linalojitapa kuwa na fedha. Lowasa na kambi yake wameshindwa kabisa kutimiza adhima yao, membe amechomoza na ushindi wa kutosha tu hata kama hayuko nafsi 3 za juu, lakini pia Jk amechomoza na ushindi wa kishindo wa kukataliwa na watu wawili tu kati ya wajumbe 2397. Mbali ya vipeperushi vyoote vile,press conferencde za bashe za kumponda wazi Membe, vitisho, kampeni chafu za mtu kwa mtu,kuhonga nakadhalika, hata bidii ya kuhonga watu hadi milioni moja moja ili kufanikisha lengo lao lakini wapi mambo yamekwenda alijojo kwa lowasa na timu yake. Hizi ni gori mbili ndani ya dakika moja langoni mwa Lowasa na Bashe mbali ya bidii zoote za kuteketeza zaidi ya milioni 200 kuhakikisha hilo jambo halitokei. Pia kunaushahidi wa mazingira unaoonyesha kuwa wakati woote wa kikao hiki dodoma mama salma na familia yake mara nyingi wameonekana wakiwa karibu sana kinafasi na kimazungumzo na membe, na hiyo ni kuashiria kwamba hiyo familia ya membe na Jk ni kitu kimoja. Polesana Lowasa
LOWASA UNAPASWA KUJUA KUWA HATA KAMA UKIWA NA WATU NDANI YA CC NA MAFEDHA YAKO, LAKINI BAADHI YAO WAPO KATIKA SAFU YA UONGOZI WA SERIKALI ILIYOPO CHINI YA JK, SO KWA MANENO YA MDOMO NI KWAMBA WATAKUPAKA MAFUTA KWA MGONGO WA CHUPA, LINAPOKUJA KWENYE SWALA LA KURA YA SIRI WANAMPENDA JK, NA MATOKEO HAYO HAPO JUU NI USHAHIDI TOSHA KUWA WANAKURA PESA ZAKO, LAKINI BADO WAMEKUTOSA VIBAYA. JIPANGE MZEE
2. Kupendekezwa kwa mzee mangula, kurudi kuwa makamu mwenyekiti wa ccm, ni pigo lingine takatifu kwa Lowasa, kwani licha ya kwamba mwanzoni mwa mwaka 2004 kuelekea 2005 jk na Lowasa walikuwahawaivi na mangula, lakini kwa sasa jk hana cha kupoteza, thats why kaamua kumrudisha now baada ya kuona rushwa ndio msingi wa nafasi za uongozi wa ccm. Hili linakuja sambamba na kuwepo kwa tetesi kuwa wasira au makamba(senior) kumrithi Mkama, hapo litakuwa ni pigo lingine goli mbili (2) kwa kambi ya Lowasa, kwani hata kwa waliofuatilia leo madongo toka kwa makamba (senior) leo wakati akimnadi jk... laivu alikuwa akimchana lowasa
baadi ya kauli hizo ni hizi
a. JK ni changuo la Mungu na leo wanachagua Kocha tu kwani kikosi cha ushindi (team) ndio hiyo cc, ambapo Lowasa hana turufu ya kutosha ya kuweza kuiteka kama ambavyo goli mbili za kwanza zilivyoingia ndani ya dakika moja rejea pointi no 1 hapo juu
b. Kauli ya kwamba mtu anayesema tupige kura za maruhani na tumpunguzie raisi majukumu, hana maana huyo, huyo mtu anakazi moja nayo imemshinda leo anasema tumpunguzie mteule wa Mungu (akimfananisha jk na Isaya) huyo mtu hatufai
kwafupi sana leo Makamba (senior) ameongea asa if yeye bado ni katibu wa chama kamaliza kila kitu, na bila shaka kauli zake zinaimpact katika ushindi wa jk leo. mapaka hapo ni goli mbili zingine
c. Makamba anatambua kuwa jk alifanya makosa kama binaadamu labda kukutosa (Lowasa) na kukuingiza mkenge ujiuzuru, lakini Makamba anasema hiyo si sababu ya yeye kuchukiwa na watu bali achukiwe kwa kushindwa kutimiza ilani ya ccm, so kilichotokea hakina impact kwa chama wala kwake. Pole Lowassa
3. Goli la tano limefungwa kutokanana, na ukweli kwamba cc hiyo hiyo ndiyo iliyoamua kuwe na mgombea mmoja katika nafasi za unyekiti na makamu mbali ya kwamba katika cc hiyo kuna wanamtandao wa Lowassa hiyo kudhihirisha kuwa bado watu wake Lowasa hawana nguvu, kuzidi group lililoko karibu na Jk na automatically karibu na membe kwani inasemekana jk na membe wanaundugu kiukoo.
4. Goli la kufutia machozi kwa kambi ya lowasa ni lile lililotokea kwa maeneo mbalimbali kama hanangi kwa kushinda watu wake, lakini ukirejea maneno ya Makamba kuwa jk ni kocha na timu tayari imeshaundwa yaani cc ambayo ndiyo hiyohiyo iliyoridhia kurudi kwa mangula, na jka kuwa mgombea pekee tayari hapo lowasa utakufa kwa pressure tu mzee wangu hata kabla ya siku zako, mbali ya kuhonga mijihela makanisani, msikitini na hata kuwahonga wajumbe
USHAURI WANGU
1. Lowasa baki na biashara zako tu, usubiri kufa siku Mungu aliyokupangia lakini kucheza na siasa za bongo za unafiki zimeshakushinda na zitakuua mapema, kama unaweza kufanya transaction mpaka za milioni 500 kwa siku, kama mwanao fred anavyoeleza unatatizo gani zaidi, baki tu kama wakina bakheresa na mohamedi interprise wanaokula kuku kwa mrija tu katika biashara zao... huku wakiwaiti 10% toka serikalini katika dilimbalimbali za serikali, kwani wakati wa kampeni ndio wafadhili wakubwa wa kampeni za chama (ccm)
2. Lowasa kama bado unania na uogozi wa nchi hii, basi jua kuwa muda si rafiki yako kabisa, na jk ameshakucheza shere mbaya, ni dakika ya 89 sasa gori 5 kwa moja, unachoweaza kufanya ni kuweka mambo yoote hadharani.. ili wananchi wachambue kipi ni pumba na mchele, Licha ya kwamba utakuwa na kazi kubwa sana ya kujisafisha kwani watakuuliza ulikuwa wapi siku zooote hzio usieleze kama jk ndiye mwizi, na hata ukakubali kujiuzuru.. Pole sana. Jk ni mnafiki na anakutoa katika mstari taratibuu.....hii njia ya kudhani kuwa jk atakuachia madaraka sahau.. jk hanaga rafiki wa kudumu.. Pole sana
Endelea kutoa sadaka msikitini na Kanisani, labda Mungu ATAKUSAMEHE MAKOSA YAKO, Lakini kuendelea kufikiria Uraisi ni ndoto za mchana, kwani jk bado ananguvu ya zaidi ya 70% kwa vyombo vyoote vya usalama, lakini pia hata kaulili zake za kuwa 2015 hawataki kisimamisha mtu ambaye atakuwa kazi sana kumnadi kwa wananchi hasa kwa kuwa atakigharamu chama na atakuwa amechafuka hilo ni kudhihirisha kuwa huyo si mwenzio.
nakala, kwa chama, ritz1, pasco, zomba, Cafu ngangari na kwa mafisadi woote....