Lowassa: Elimu ya bure inawezekana!

Lowassa: Elimu ya bure inawezekana!

HApo kitu cha kufanya ingia katika kampen ya mabadiliko ya kweli inayoongozwa na CHADEMA. Kumbuka tumetoka kwenye zama za uwaz na ukweli tupo kwenye zama za kuin'goa CCM madarakani.
TheOne,
Mwaka 1990 ndipo nilipoingia kwenye harakati za mageuzi, natumaini ulikuwa umeshazaliwa wakati huo. CHADEMA ninayoijua mimi kwa nje wanaonekana wanajitahidi lakini ukweli ni kuwa wana-uwalakini mwingi na utapeli mwingi ambao wenyewe wanaufahamu lakini hawataki kuutibu. Wewe uliyeamua kuwa mpiga makofi wao endelea lakini ningekushauri usiwe wa kuitikia hewalaa tu, jaribu kuwa mdadisi na mpimaji wa yanayosemwa na kutendwa. Huku nje tupo wengi tunaotaka mabadiliko ya kweli na hatutaki kuwa wapigia makofi matapeli. Karibu na wewe.
 
Lowassa anajaribu ku-copy & ku-paste sera ya Chadema.

Ni kama anaendelea kujipanga kuwagaragaza Membe (decoy) na Migiro (Chaguo la Kikwete kwa staili ileile ya Makinda/jinsia) kwa kutumia sera za kutoa Elimu bure ambazo chama chake kinazipinga kabisa.
________

Wakati wa kampeni za 2010 Dr Slaa na Chadema walisema kuwa serikali yao itatoa huduma za Elimu na Afya bure kwa wananchi.

Hii inawezekana kwani kuna jinsi ya kupata pesa. Kwa sasa serikali inatumia zaidi ya sh bilioni 800 kwa kulipana posho, na 'wawekezaji' wanasamehewa zaidi ya sh trilioni moja ambazo wangepaswa kulipa kodi.
 
Lowassa anajaribu ku-copy & ku-paste sera ya Chadema.

Ni kama anaendelea kujipanga kuwagaragaza Membe (decoy) na Migiro (Chaguo la Kikwete kwa staili ileile ya Makinda/jinsia) kwa kutumia sera za kutoa Elimu bure ambazo chama chake kinazipinga kabisa.
________

Wakati wa kampeni za 2010 Dr Slaa na Chadema walisema kuwa serikali yao itatoa huduma za Elimu na Afya bure kwa wananchi.

Hii inawezekana kwani kuna jinsi ya kupata pesa. Kwa sasa serikali inatumia zaidi ya sh bilioni 800 kwa kulipana posho, na 'wawekezaji' wanasamehewa zaidi ya sh trilioni moja ambazo wangepaswa kulipa kodi.

Mkuu Che Guevara.
Kwa kuijazia minofu hoja yako naomba nitoe na mfano mwingine halisi kwenye hili.

Kampuni ya kufua umeme ya Richmond ilikuwa inalipwa milioni 152 kwa siku, kwa mwezi yaani siku 30 ni sawa 4260 bilioni, ukiipiga hesabu hiyo kwa mwaka unaweza kuchanganyikiwa. Tukirudi kwenye hoja, kama tumeweza kugharamia umeme wa magumashi kwa karibu mwaka mzima, tunakosa vipi udhati wa kugharamia elimu ya vijana wetu?! Hapa kina ndugu yangu chama lazima watueleze tuwaelewe vizuri.
 
Last edited by a moderator:
Elimu ya bure inawezekana na ni muhimu itolewe kwa wote wenye uwezo mkubwa wa kiakili kwa faida ya wote bila kuangalia uwezo wa kifedha au daraja lake katika jamii.
Serikali ina wajibu wa kuhakikisha inatoa elimu bure kwenye shule na vyuo vyake kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Muhimu zaidi ni kuhakikisha wanaochaguliwa wanapatikana kwa ushindani wa haki katika mitihani.
Hata hivyo wale wenye uwezo mdogo kiakili wapewe nafasi za kujilipia wenyewe kama wanaweza.
Kwa hali ilivyo sasa watoto wa walalahoi ambao ndio wengi wataendelea kupungua katika shule na vyuo hadi hapo watakapokuwa na ujasiri wa kufanya mapinduzi ya nguvu!
 
Mkuu Mtoi
Rasimu ya CCM ni kuhakikisha elimu kwa kila mtanzania; bure sio suluhisho la matatizo ya elimu tuliyonayo; serikali ya CCM inaendelea na jitahada zake; hivi kuna ongezeko la vyuo na shule za sekondari hizo ni moja ya jitahada; wakati serikali inaanzisha shule kata za waziri mkuu alikuwa ni mh.Lowasa hivi huoni ajabu ya mtu aliyekuwa PM leo hii aje kwenye majukwaa kutoa miongozo alikuwa wapi alikuwa na nafasi nzuri tu kutekeleza azimio hilo wakati akiwa PM; matatizo ya shule za kata Lowasa ni mhusika mkubwa hakukuwa na uwiano wa idadi ya shule na walimu nadhani matokeo yake unayajua, mkuu hili neno bure tunalitumia vibaya unakumbuka jamii ya wasandawe? Mwl. Nyerere alifanya jitihada kubwa wasome nakumbuka miaka ya 84 waliletwa wasandawe kama 30 pale Galanos secondary walipokwenda likizo walirudi wanafunzi wa 4 tu kama suala ni kusoma bure haimfanyi mtu asome; nakubaliana na wewe kwenye matumizi ya rasilimali zetu kwa kuanzia tu peleka hoja mtaa wa Togo wagomee ruzuku uone kauli itakavyopokelewa. Hizi ruzuku zitalipwa hadi lini wkati vyama hivi vimeshakomaa; mh. Lowassa anakuja na hoja za kutafuta kuongelewa kwenye maredio; tungependa aje kutufanunulia kitendawili cha Richmond yeye ni mhusika mkubwa watanzania tunapenda atujuze haya ya elimu serikali inafanyia kazi kwa kadri ya uwezo wake.

Chama
 
Lowasa namkubali aje mbele ya umma tu atuambie ukweli tutamwamini na atuahidi serikali ya mseto ili abanane na kina Lisu ndani ya serikali.
Tunaweza kumuamini Lowasa ila ili tumuamini aeleze umma wa Watanzania ni nini anachokifahamu kuhusu RICHMOND Na ni nani mmiliki wake,akieleza haya tumfikirie huo urais anaoutaka
 
TheOne,
Mwaka 1990 ndipo nilipoingia kwenye harakati za mageuzi, natumaini ulikuwa umeshazaliwa wakati huo. CHADEMA ninayoijua mimi kwa nje wanaonekana wanajitahidi lakini ukweli ni kuwa wana-uwalakini mwingi na utapeli mwingi ambao wenyewe wanaufahamu lakini hawataki kuutibu. Wewe uliyeamua kuwa mpiga makofi wao endelea lakini ningekushauri usiwe wa kuitikia hewalaa tu, jaribu kuwa mdadisi na mpimaji wa yanayosemwa na kutendwa. Huku nje tupo wengi tunaotaka mabadiliko ya kweli na hatutaki kuwa wapigia makofi matapeli. Karibu na wewe.
Kubwajinga zama za kutishana na kudanganyana zimepitwa na wakati sasa hivi hadanganyiki mtu mabadiliko ni lazima kuwaita wenzio matapeli huwatendei haki hao wanaowadanganya watanzania kwa miaka 50 sasa lakini hali ya maisha bado ngumu wananchi wategemee lini watapata nafuu ya maisha? Sasa ndio viongozi wa CCM wanahamisha pembe za ndovu wakati Mtanzania bado hana uhakika wa milo mitatu kwa siku hata huo mmoja anbahatisha madidi wamegawana yote,gesi wameanza kuhujumu,mtanzania maskini ategemee nini kutoka kwenye uongozi huu? Nafikiri na wewe ni mmoja wao ndio maana unawakatisha tamaa wenzako kwa tamaa zako za kufikiria neema ambayo hutaipata, Watanzania wameamka sio kama wenye mawazo hasi kama yako
 
Last edited by a moderator:
TheOne,
Mwaka 1990 ndipo nilipoingia kwenye harakati za mageuzi, natumaini ulikuwa umeshazaliwa wakati huo. CHADEMA ninayoijua mimi kwa nje wanaonekana wanajitahidi lakini ukweli ni kuwa wana-uwalakini mwingi na utapeli mwingi ambao wenyewe wanaufahamu lakini hawataki kuutibu. Wewe uliyeamua kuwa mpiga makofi wao endelea lakini ningekushauri usiwe wa kuitikia hewalaa tu, jaribu kuwa mdadisi na mpimaji wa yanayosemwa na kutendwa. Huku nje tupo wengi tunaotaka mabadiliko ya kweli na hatutaki kuwa wapigia makofi matapeli. Karibu na wewe.
Kubwajinga zama za kutishana na kudanganyana zimepitwa na wakati sasa hivi hadanganyiki mtu mabadiliko ni lazima kuwaita wenzio matapeli huwatendei haki hao wanaowadanganya watanzania kwa miaka 50 sasa lakini hali ya maisha bado ngumu wananchi wategemee lini watapata nafuu ya maisha? Sasa ndio viongozi wa CCM wanahamisha pembe za ndovu wakati Mtanzania bado hana uhakika wa milo mitatu kwa siku hata huo mmoja anbahatisha madidi wamegawana yote,gesi wameanza kuhujumu,mtanzania maskini ategemee nini kutoka kwenye uongozi huu? Nafikiri na wewe ni mmoja wao ndio maana unawakatisha tamaa wenzako kwa tamaa zako za kufikiria neema ambayo hutaipata, Watanzania wameamka sio kama wenye mawazo hasi kama yako
 
Last edited by a moderator:
Ccm walisema 2010 kwenye kampeni kwamba haiwezekani kutoa elimu bure tanzania,leo makada wake wanasema elimu bure inawezekana. Kuanzia leo siwezi kuiamini tena ccm labda wapinzani!
 
Kimsingi kinachofanywa na ccm saiv ni POLITICAL TRIANGULATION. Wanachukua hoja za vyama pinzani na kuzifanya kuwa za kwao lakini siamini kama kweli hawa wamafia wa rasirimali zetu wana nia ya dhati ya kuweza kulitekeleza hilo. kinachowaogofya ccm ni watanzania kuelewa kwamba ilani ya chadema ya 2010 ingeweza kutekelezeka kikamilifu.
 
Elimu ya bure inawezekana na ni muhimu itolewe kwa wote wenye uwezo mkubwa wa kiakili kwa faida ya wote bila kuangalia uwezo wa kifedha au daraja lake katika jamii.
Serikali ina wajibu wa kuhakikisha inatoa elimu bure kwenye shule na vyuo vyake kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Muhimu zaidi ni kuhakikisha wanaochaguliwa wanapatikana kwa ushindani wa haki katika mitihani.
Hata hivyo wale wenye uwezo mdogo kiakili wapewe nafasi za kujilipia wenyewe kama wanaweza.
Kwa hali ilivyo sasa watoto wa walalahoi ambao ndio wengi wataendelea kupungua katika shule na vyuo hadi hapo watakapokuwa na ujasiri wa kufanya mapinduzi ya nguvu!

Haswaaaaa. Tukimaliza elimu ya msingi na sekondari tutageukia elimu ya juu kwa serikali kutoa mikopo kwa wahitaji wote bila mashariti.
 
Naona kama anasupport chadema maana hiyo ni sera ya chadema...elimu bure...ila kwakweli watanzania wengine wanaudhi...mtu kashaambiwa elimu bure...anachagua ambapo atalipa hela...zero brain kabisa
 
Matukio yaliyojiri hivi karibuni katika medani ya siasa nchini yameonyesha kua mustakabali wa kisiasa wa Mwanasiasa mkongwe Mh Edward Ngoyai Lowasa una utata mkubwa!

Lowasa ni kada wa siku nyingi wa chama chetu cha Mapinduzi. Ni kada ambae amefanya mambo mengi katika chama toka alipokua UDSM miaka ya mwanzoni mwa 1970 enzi za TANU na amewahi kushika nyadhifa mbali mbali za Uongozi katika CCM. Mh Lowasa, kama wote tujuavyo, kwa kutumia ushawishi mkubwa wa fedha ambazo yeye pamoja na familia yake wanazano, aliweza kupata ushindi mnono jimboni kwake Monduli katika chaguzi za NEC pamoja na watu wake wengi kushinda katika NEC wilaya mbalimbali nchini. Kama hiyo haitoshi, kwa kutumia ngawira aliweza pia kuingiza watu wengi katika jumuia zote tatu za chama(Wazazi, Wanawake na Vijana).

Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM katika hotuba zake kwenye jumuia zote tatu alitoa hotuba nzito za kulaani matumizi makubwa ya rushwa kwenye chaguzi. Haiitaji kua "Rocket Scientist" kutambua kua makombora hayoya mwenyekiti wetu mpendwa yalimlenga LAIGHWANAN. Kana kwamba hiyo haitoshi, Mwenyekiti ameunda Secretariat kabambe ya maadili ikiongozwa na Watanzania wazalendo ambao jamii yote (Isipokua wale wabishi wa kuzaliwa ) wanatambua kua wanaichukia SANA rushwa (Mangula na Kinana). Lengo la Mwenyekiti ni kikirudisha chama kwa wananchi na kukiondoa kwa wala rushwa.

Aidha kauli ya mwenyekiti kua "Kuna watu wenye Ndimi mbili, yaani mara wanakisema vizuri chama cha Mapinduzi lakini wakati mwingine wanakiponda" ni dhahili mlengwa ni Laighwanan. Hii ni kutokana na ukweli kwamba Laighwanan amekua akitoa kauli zenye utata mkubwa ambazo si tu zinapingana na sera za chama chake mwenyewe bali pia zinakidhalilisha chama. Mfano akichangia ujenzi wa shule ya Mkinde tar 2.5. 2012 Laighwanan alisema "Vijana wengi waliokua ccm wamehamia chadema kwani ccm haiwajali na haina nia ya kuwaendeleza". Kauli hiyo ilijibiwa na Waziri Mkuu Mh Pinda tar 6.5. 2012 ambae alisema kua "CCM bado inapendwa na vijana na ccm ina mikakati mingi ya kuwaendeleza, tuache kusikiliza porojo". Aidha, wakati wa chaguzi za ccm huko Dodoma, Mwenyekiti alimpiga kijembe Laighwanan kwa kusema "Wapo wanaosema Vijana wote wamehamia upinzani, ccm tumechagua viongozi wengi vijana na wasomi wazuri na tunaamini watatupa mawazo mapya ya kisasa".

Aidha majuzi Lowasa, bila kupepesa wala kungata maneno nae akawapiga vijembe ccm kwa kusema "Elimu ya sekondarilazma itolewe bure". Hii ni Sera ya wazi ya Chama Dume-Chadema ambayo Mh Dr. W. Slaa aliilezea kwa ufasaha mkubwa kama agenda ya Chadema 2010 lakini ilipingwa vikali na ccm ambayo iliwabeza Chadema kwamba wasiwadanganye na kuwahadaa wananchi hilo haliwezekani kabisa!

Lowasa ameishawatanguliza vijana wake kadhaa kuhamia Chadema mfano Steven Mlontei na James Millya. Kwa hakika, kiroho, LAIGHWANAN yupo CHADEMA!Vile vile , kwakua Lowasa inajulikana wazi kua alitumia rushwa ambayo ilikua ikigawiwa vyooni, kwa mama ntilie na kwenye vibanda vya vocha na kuandikwa sanana magazetini hivyo kitendo cha watu wake kuingia kwa wingi katika NEC inaonyesha wazi rushwa hiyo ililipa. Kutokana na hali hii, kauli kali iliyotolewa na Mh P. Mangula pale mnazi Mmoja ambapo alisema "Wale wote ambao waliingia kwa rushwa watafukuzwa ndani ya Miezi sita" inaonyesha kwamba lowasa huenda nae akatimuliwa CCM kwani haitaeleweka kwa Mangula na wenzake kuwatimua Dagaa na kumwacha KAMBARE.

Je WANACHADEMA, Kwakua Mh S. Sita alisema Chadema ni chama kizuri ambacho kilisifiwa hata na Baba wa Taifa lakini hakina viongozi wa kutosha, ikitokea LAIGHWANAN ametimuliwa CCM apokelewe CHADEMA na kuibeba bendera yake mwaka 2015? Hii pia inazingatia maoni ya baadhi ya watu humu JF ambao wamekua wakisema LAIGHWANAN ni JEMBE na kama Dr Slaa asiposhinda 2015 bora Lowasa awe Rais.

Wadau, je LAIGHWANAN apokelewe CHADEMA??
 
Mkuu unampamba Lowassa as is ni mtu makini.
Si hivyo, kiburi ya Lowassa inatokana n pesa yake, na anataka kuwekeza katika siasa.

Aende CDM au abaki CCM, pesa haina sera nzuri kisiasa.
Sasa mnaompamba Lowassa mpeni ukweli tu kuwa aendelee kutengeneza noti kabla haujaingia utawala utakaoamua kula naye sahani moja.

Mfanyabiashara yoyote anajua kuwa siasa na pesa haviendi pamoja.
 
EL ashindwe na kulegea. Kama CDM watafanya kosa la kumkaribisha wataishia kulia na kusaga meno. Maana fisadi ni fisadi atauleta ugonjwa wake huko.
 
Nashindwa kukuelewa unaposema ccm imechagua viongozi wazalendo wanaoichukia sana sana RUSHWA yaani Kinana na Mangula unaweza kututajia matendo yao ya kizalendo waliowhi kuyafanya nchini zaidi ya kusaidia wezi?
 
Mkuu naona umeamua kutumia fikra zako na kutunga simulizi...Lowassa ni CCM hawezi kwenda popote.

Mkuu Ritz
Makamanda hawana mgombea wanahaha kila kona usije kushangaa kusikia Mzee Mtei ndio mgombea wao 2015

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ritz
Makamanda hawana mgombea wanahaha kila kona usije kushangaa kusikia Mzee Mtei ndio mgombea wao 2015

Chama
Gongo la mboto DSM
Teh teh teh, si afadhali mtei, wanaweza hata kumteua LEMA au LISSU
 
Back
Top Bottom