Jana katika runinga Vuvuzela wetu CCM akijigamba kuwa "Sera ya Elimu" ni sera ya CCM na sio CHADEMA. Kitu ambacho hakusema ni kuwa sera ya elimu bure ilikuwa ni Sera na ilitekelezwa na "CCM ya Nyerere ya Wakulima na Wafanyakazi; na sio CCM hii ya walanguzi wa raslimali za taifa".
Ili tuweze kubaini kama "CCM hii ya walanguzi wa raslimali za taifa" inaweza kutekeleza sera ya "elimu bure au la" tutazame utekelezaji wa Sera ya elimu ya CCM na Serikali yetu ya hivi sasa ambapo Serikali inatakiwa kuzipelekea Shule za Msingi "Capitation Grant" ya Shs 10,000/= tu kwa kila mwanafunzi kwa ajli ya Vitabu,Vifaa vya kufundishia, ukarabati wa Majengo na Uchapaji wa Mitihani.
Katika Shule ya Msingi anayosoma mwanangu hapa jijini Dar yenye wanafunzi 750,mwaka 2010 ililetewa Shs 1,160,000/= tu badala ya Shs 7,500,000/= ikiwa ni aslimia 15% tu. Kushindwa kwa CCM na Serikali yetu kutekeleza kwa vitendo "Sera yetu ya Elimu ya Msingi, husababisha wazazi kurundikiwa michango isiyoisha kama vile kulipa mlinzi, kutengeneza madawati, ukarabati wa majengo, kuchapa mitihani n.k
Kama hivi sasa CCM na serikali yetu inatekeleza Sera yake ya Elimu ya Msingi kwa 15% kwa kumtumia kila mwanafunzi wa msingi Shs 1,546/= tu badala Shs 10,000/= tujipangia wenyewe na kupitishwa katika bajeti ya Wizara ya Elimu na Tawala za Mikoa. Je tutaweza vipi kutekeleza Sera ya Elimu Bure?
Kwakuwa katika bajeti kila mwaka hupitishwa Shs 10,000/= kwa kila mwanafunzi wa shule za msingi hapa nchini, CCM na Nape wanapaswa kwanza kutueleza Shs 8,454/= kwa kila mwanafunzi wa msingi zidisha kwa idadi ya wanafunzi wote wa msingi Tanzania nzima zinakwenda wapi kila mwaka? Hizi na haki za watoto wa Tanzania zitokanazo na kodi tunazolipa wananchi bial ya kujali vyama vyetu.
Kama CCM hii hii ya akina Nape, Mwingulu, Makamba wameshindwa kufuatilia haki hizi za watoto kwa takribani miaka miwili waliyokuwa madarakanii katika Sekreterieti ya CCM, wataweza vipi kutekeleza kuisimamia serikali hivi sasa kama anavyodai Nape jana katika runinga? nakubkuka miaka miwili iliyopita Nape pia alitoa kauli kama hii lakini hadi sasa hakuna kilichotokea hata ufisadi mkubwa ulipotokea na ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali kiuwatuhumu baadhi ya mawaziri Sekreterieti yao ilishindwa kabisa kuchukua hatua hadia waziri Mkuu kutishiwa kung'olewa.
CCM na viongozi wake wengi aina ya akina Nape hawajatambu kuwa watanzania wa sasa sio watanzania wa kale, bado wanapiga poyoyo na kufikiri kuwa wataweza kuwafunga kamba wananchi kama walivyofanya miaka ya nyuma. Tunawaomba muache kukichafua chama chetu kwa taarifa zisizofanyiwa utafiti na zisizo za kweli katika mazingira haya ya ushindani mkali wa kisiasa.