Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,331
- Thread starter
- #141
Mkuu Mtoi
Nadhani mpaka sasa hivi unajiuliza kwa nini napingana na kauli za mh. Lowassa; yeye ndiye muasisi wa shule za kata; mpango mzima ulifeli kwasababu hakukuwa na uwiano kati ya majengo na vitendea hii ikijumuisha na idaidi walimu; mh. Lowassa ni mwanasiasa ambaye upepo wake kisiasa umezimika na anajitahidi kila siku kusema vitu ambavyo havina mpangilio; au inahitilafiana na sera makini za CCM; sisi tunasema kilimo kwanza yeye kadakia elimu kwanza; yote hii ni kuwa kaishiwa kisiasa. Mkuu Mtoi sera ya elimu ya CCM haijatukataza tusipeleke vijana wetu kwenye mashule ya binafsi; mwenyekiti MBOWE amepeleka watoto wake shule ya vichekechea nasikia analipa milioni 7 hivi unategemea Chadema ikiingia madarakani MBOWE atawapeleka wanawe kwenye shule za serikali? Sijafanikiwa kimaisha najihini ili niwapeleke shule wanangu; nimekuambia kuna siku nakula muhogo usio na towezi; mkuu usiwaamini sana hao watu wana ajenda binafsi.
Chama
Gongo la mboto DSM
Mkuu chama.
Hongera kwa kurudi kujadili hoja maana ulianza kunipa mashaka ulipoanza kutoka nje ya mada na nduguyo Ritz.
Naomba nijibu hoja zako lakini pia nakuomba upitie Makala ya kiuchambuzi ya Dr Kitila Mkumbo niliyoweka kwenye mchango wangu uliopita.
1. Umesema EL ndiye muasisi wa shule za kata. Kama hivyo ndiyo basi kuna udhaifu mkubwa sana unao uanika kwenye sera za ccm maana nilijua ilikuwa ni sera iliyo kuwa kwenye ilani ya chama. Hii maana yake ni kwamba kiongozi yoyote ndani ya ccm akishauriana na mkewe au kuota usiku anakuja na kutekeleza aliyoota au kushauriana na mkewe! Huo ni msiba na udhaifu wa hali ya juu!
Hata hivyo ukienda mbali zaidi unaweza kujiuliza nafasi ya makamu wa raisi, raisi, baraza la mawaziri na serikali kwa ujumla kuhakikisha kuwa kuna uwiano kati ya majengo, vitendea kazi na walimu bora wenye sifa, hiyo ilikuwaje ili kuboresha wazo la muasisi?! kama serikali nzima iliaacha wazo la muasisi bila kuriboresha maana yake ni kwamba udhaifu ni mkubwa sana kuliko tunavyofikiri kwenye hiyo serikali husika.
2. Umeongelea upepo wa El kuzimika.
Upepo wa El kuzimika au kuwaka sio hoja ya msingi! Swala hapa ni mashiko kwenye hoja zake bila kuangalia kuwa nyota yake ina waka au imezimika. Mfano anaposema kuwa haamini katika sera ya kilimo kwanza kwangu naweza kusema kuwa yuko sahihi maana elimu ndio mama wa taaluma zote na dira ya shughuli zote za uzalishaji, hata wakulima pia wanahitaji elimu bora ili wafanye kilimo bora na chenye ufanisi na tija. Kama hivyo ndivyo, basi elimu bora ni muhimu sana ili kukipa manufaa kilimo. Na kwa mujibu wa takwimu za kitafiti kwenye uchambuzi wa mwanazuoni Kitila Mkumbo elimu bora naya bure inawezekana na hii ndiyo ilikuwa sera ya chadema, basi jamii za wakulima na wafugaji wanatakiwa kufaidi hili kama jinsi watakavyo faidi jamii za watu wengine ili kuleta tija na kuongeza uzalendo kwa taifa.
3. Sera ya ccm haija kukataza kupeleka watoto wako shule za private. Sawa kabisa! Lakini je mnapeleka watoto wenu shule za private kufuata nini na huko shule za Kayumba (Kata) mmekimbia nini na kwa nini mkimbie?! Hili ndilo la msingi, kula kwako muhogo au ndondo ili watoto wasome ni hisani yako maana ungeweza hata kuamua kufunga swaum isiyo na kikomo kwa nuizi la wanao kusoma. Hahaha.
4. Umepoteza uhalali wa kumjadili Mbowe na mimi pia napoteza uhalali huo! Kwa nini?! Umesema "nasikia analipa milioni 7 hivi unategemea Chadema ikiingia madarakani MBOWE atawapeleka wanawe kwenye shule za serikali?" Msisitizo wangu wa mimi na wewe kukosa uhalali wa kumjadili Mbowe ni hapo kwenye "NASIKIA" tusijadili kusikia bila kuwa na uhakika! Weka data ili tuepuke kujadili maneno ya mtaani, wenye tabia ya kujadili maneno ya kusikia ni watu wasio kuwa makini na huwa wana maneno laini kama maini. (Wengine huwaita wambeya).
5. Umesema "usiwaamini sana hao" hao ni kina nani unao sema wana ajenda ya siri? Na siri hiyo ni ipi maana tayari bila shaka umeshaifahamu kwa kuwa ile sifa/dhana ya usiri haipo tena. Karibu tuendelee mkuu. Majibu yako yatanisadia sana kunijenga hasa kama utaendelea kugusa masuala (issues) na si vioja kama alivyo anza na kuendeleza kaka yangu Ritz.
Kila jema na lenye kheri lisikuponyoke chama.
Last edited by a moderator: