Lowassa: Elimu ya bure inawezekana!

Lowassa: Elimu ya bure inawezekana!

hii ni sera mpya lowasa kuelekea 2015,na hili linawezekana kwa 100%.lowasa kwa sasa ana pesa haijalishi ni za kifisadi au la! Ni bora azirudishe kwa watoto wetu kwa njia ya elimu..
 
Mtoi,
I hate to say this, kwenye watu wanaoongelewa kuuwania uraisi, huyu bwana EL, licha ya wizi wake na ulevi wake wa madaraka akiwa nayo, ndio pekee ameonyesha kuwa na mawazo yenye meno ambayo nchi yetu inahitaji. Tatizo ni vigumu kumuamini kutokana na historia yake mbovu anapopewa madaraka. Tufanyeje sasa Watanzania?

HApo kitu cha kufanya ingia katika kampen ya mabadiliko ya kweli inayoongozwa na CHADEMA. Kumbuka tumetoka kwenye zama za uwaz na ukweli tupo kwenye zama za kuin'goa CCM madarakani.
 
Channel ten ilipaswa kumhoji EL ilikuwaje 2010 magamba walidhamini matangazo yakupotosha wakati wa campaign za Dr. Slaa kuwa elimu bure haiwezekani? Tena kupitia channel ten hiyo iyo?

siwezi kufanya mahojiano na waandishi wa habari wa tz wanapotosha! By Ben Mkapa.
 
Ni wazo zuri kwani vijana weng watapata fursa ya kuwa na elimu ya sekondary,juzi pia tulimsikia kinana akisapoti sera ya cdm kwenye ujenzi nafuu,sera zote hizo za cdm 2010 zilizoenezwa na dr.wa ukweli.
 
Mkuu chama.
Mchango wako una mashiko sana lakini kwa heshima na taadhima naomba nikuambie kuwa tukiwa na dhamira ya dhati na kuwa na viongozi wenye kutembea juu ya kauli zao huku wakihakikisha kuwa kila senti kwenye raslimali zetu inatumika ipasavyo bila upotevu au kudondokea kwenye matundu ya wajanja wachache, tunaweza kabisa kuwa na mashule bora yenye vifaa bora na walimu bora na elimu bora ya bure inayogharimiwa na serikali husika.

Kwa sasa hata mfumo wenyewe wa kukusanya kodi una mapungufu mengi na mapato mengi yanapotea bure. Ni Tanzania pekee ambayo mfanyakazi wa serikali wakati mwingine analipa kodi kubwa kuliko mfanya biashara anayeingiza mamilioni ya shilingi kwa siku au kwa mwezi.

Mkuu chama kwa swala la kusomesha serikali haija jitwisha mzigo! Hilo ni swala la kikatiba na ni jukumu lake la kimsingi kusomesha maana ina wakamua wananchi wake kodi kwenye huduma na biadhaa mbalimbali. Sikutegemea uionee huruma serikali kwenye hili maana ni jukumu lake la msingi tena bila visingizio.

Kaka chama! Leo umekuwa objective kutofautiana na wana ccm wenzako lakini pia na sera za ccm maana sikujua kuwa kwa mapenzi na mahaba yako unaweza kusomesha wanao private huku ukiacha shule zilizopigiwa chepuo la kufa mtu na chama chako.

Nimegundua kuwa huamini katika baadhi ya mambo ndani ya ccm! Sitaki kusema unaamini kwenye sera za chama gani lakini wewe ndio una majibu ya kina.

Kila jema na lenye kheri lisikuponyoke wangu.

Mkuu Mtoi
Suala la elimu bado ni mzigo kwa serikali; umefika wakati watanzania inabidi ujiulize umeifanyia nini serikali na sio serikali imekufanyia nini; lengo sio serikali kuutua mzigo huo mojamoja la hasha na sisi wananchi wenye uwezo tuchangie angalau wale wasio na uwezo kabisa wapelekwe shule; Serikali ingejizatiti kwenye elimu ya msingi na sekondari hizo na zitolewe bure au uchangiaji kidogo kama tunavyofanya; elimu za vyuo bodi ya mikopo iboreshwe ili kuhahakisha kila anayechukua mkopo anarejesha; hivi sasa wapo watu wengi wamechukua mikopo wanauwezo wa kurejesha lakini hawalipi hilo ndilo linaloiongezea serikali mzigo; tunapoongelea rasimali za nchi hata hii mikopo ni sehemu ya rasilimali zetu; ruzuku kwa vyama vya siasa ni moja ya matumizi mabaya ya rasimali zetu; mkuu unapoongelea yapo mambo mengi unayafumbia macho kwasababu za kisiasa; matatizo ya ukusanyaji ni matokeo ya kuwa na wafanyakazi ambao sio waaminifu, wapo wanasiasa utawakuta kwenye majukwaa wakikemea ukusanyaji mbovu wa kodi; kumbe wao ndio vinara wa kwenda TRA kupiga deal za kukwepa kulipa kodi; nina uhakika katika hili wapo wanachadema wengi wanajihusisha na hujuma hizi
Mkuu Mtoi kupeleka watoto private najima siku nyingine nakula muhogo usio na kitoweo yote nawatafutia watoto urithi;
Inshallah kwa dua zako nawe Mola akupe kila lilo na heri na wewe.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
wameamua kutumia ilani ya Chadema sasa, watachukua kimoja kimoja mwisho watajikuta wamemtoa JK wenyeewe
 
Akiongea kupitia kituo cha channel 10 kwenye taarifa ya habari ya saa 1 leo 18 Nov,2012 Mheshimiwa Lowassa amesema serikali inaweza kugharamia elimu ya msingi na sekondari kwa wananchi wake kuwa bure, na elimu ya sekondari ikafanywa kuwa ya lazima na ya kiwango (quality). Ili kuwafanya vijana kushindana kikamilifu kwenye soko la ajira.

Kauli hii ni muendelezo wa wana CCM kuendelea kukubali sera kadhaa kwenye ilani ya CHADEMA ya mwaka 2010, juzi Kinana alisema serikali iondoe kodi kwenye vifaa vya ujenzi ili wananchi wawezi kujenge nyumba bora kwa ajili ya makazi.

Na hawa waandishi wanaomuhoji mara kwa mara, je, huwa anawachagulia maswali ya kuulizwa??? kwa nini huwa hawamuulizi mauaji yanayofanywa na Polisi (serekali) dhidi ya raia anayazungumziaje akiwa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi?
 
kweli hadema ni vichwa yaani CCM,CUF WANACOPY ONE TO ONE ONTO,
NADHANI CDM WANAONGOZA NCHI WAKIWA NJE YA IKULU
1. KATIBA MPYA-ILANI CDM
2.ELIMU BURE-ILANI CDM
3.KUONDOA KODI VIFAA VYA UJENZI-ILANI CDM
4. CHUO KIKUU DODDOMA (UDOM)-ILANI CDM
5.KUPANGUA BARAZA LA MAWAZIRI KUFUATIA SAHIHI ZA WABUNGE KUMKATAA WAZIRI MKUU KWA SHINIKIZO LA WABUNGE WA CHADEMA-ZITO
6.HOJA BINAFSI YA HELA ZA USWIS -CDM -ZITTO
7.HOJA BINAFSI YA UMILIKISHAJI ARIDHI -CDM.MDEE
8.RAISI YUKO MBIONI KUWAFUTA MAJAJI FEKI KWA SHINIKIZO -CDM-TUNDU LISU
9.VUVUVUGU LA M4C vs KUJIVUA GAMBAVs V4C MWANZILISHI NI- CDM
10. MSUKOSUKO ULIOTOKEA BAADA YA DR SLAA KUWAANIKA MAFISADI PALE MWEMBEYANGA MPAKA LEO CCM HAKUJATULI-CDM
11.FAO LA KUJITOA HOJA NZITO ZA WABUNGE WA CHADEMA-MYIKA
 
Mkuu Mtoi
Suala la elimu bado ni mzigo kwa serikali; umefika wakati watanzania inabidi ujiulize umeifanyia nini serikali na sio serikali imekufanyia nini; lengo sio serikali kuutua mzigo huo mojamoja la hasha na sisi wananchi wenye uwezo tuchangie angalau wale wasio na uwezo kabisa wapelekwe shule; Serikali ingejizatiti kwenye elimu ya msingi na sekondari hizo na zitolewe bure au uchangiaji kidogo kama tunavyofanya; elimu za vyuo bodi ya mikopo iboreshwe ili kuhahakisha kila anayechukua mkopo anarejesha; hivi sasa wapo watu wengi wamechukua mikopo wanauwezo wa kurejesha lakini hawalipi hilo ndilo linaloiongezea serikali mzigo; tunapoongelea rasimali za nchi hata hii mikopo ni sehemu ya rasilimali zetu; ruzuku kwa vyama vya siasa ni moja ya matumizi mabaya ya rasimali zetu; mkuu unapoongelea yapo mambo mengi unayafumbia macho kwasababu za kisiasa; matatizo ya ukusanyaji ni matokeo ya kuwa na wafanyakazi ambao sio waaminifu, wapo wanasiasa utawakuta kwenye majukwaa wakikemea ukusanyaji mbovu wa kodi; kumbe wao ndio vinara wa kwenda TRA kupiga deal za kukwepa kulipa kodi; nina uhakika katika hili wapo wanachadema wengi wanajihusisha na hujuma hizi
Mkuu Mtoi kupeleka watoto private najima siku nyingine nakula muhogo usio na kitoweo yote nawatafutia watoto urithi;
Inshallah kwa dua zako nawe Mola akupe kila lilo na heri na wewe.

Chama
Gongo la mboto DSM

Mkuu chama.
Naomba niendelee kutofautina na wewe kwenye hii hoja ya msingi inayo ongelea mustakabali wa taifa letu.

1.Naomba utambue kuwa kwa taifa lolote makini lenye viongozi wenye dhamira ya dhati na utashi wa uongozi, elimu haiwezi kuwa mzigo! Chama elimu sio mzigo labda tuamue kukubali ujinga kama sasa hivi vijana wetu kufaulu huku wakiwa hawajui kusoma wala kuandika. Elimu ndio mama wa taaluma zote na ndio moyo na dira ya nchi kuamua wapi taifa hilo linaelekea.

Elimu kwenye nchi haiwezi kuwa mzigo na si mzigo kwa serikali yetu, elimu inakuwa mzigo kwa sababu hakuna dhamira ya dhati kuisimamia kwa maana ya kusimamia kwa viwango na ubora. Tunaweza kutumia raslimali zetu lukuki kuwekeza kwenye elimu na kutoa elimu bora naya bure. Tungeweza kuamua mapato yote ya utalii na madini yaingizwe moja kwa moja kwenye fuko la elimu huku na vyanzo vingine vikichangia hata 1% ya mapato yao kwenye fuko husika. Naamini tungekuwa mbali maana tuna mapato mengi yanapotea kutoka kwenye uvuvi, kilimo, usafirishaji, uwindaji nk.
Wenzetu Rwanda wametoka vitani miaka 4 iliyopita lakini wana mipango mizuri ya elimu yao kuliko sisi tunaojigamba na amani ya miaka nenda miaka rudi huku watoto wakifaulu bila kujua kusoma na kuandika! Hii ni Tanzania pekee.

2. Bodi ya mikopo haija serious kurejesha fedha zilizo kopwa, na huu ni moja ya udhaifu wa kiutendaji ulio pitiliza. Inawezekana vipi uwakopeshe watu kwa document za kisheria halafu baadae ushindwe kuwadai pale muda unapofika? Tena kibaya zaidi eti kuna kipindi fulani bodi ya mikopo ililalamika kuwa haijui wakopaji waliko!? Imefanya jitihada gani kuwapata?, majibu "Tuko kwenye mchakato wa kukamilisha upembuzi yakinifu". Huu nao ni msiba maana wadaiwa wengi miongoni mwao ni watoto wa vigogo walio pata mkopi 100%.

3. Kuhusu kufuta ruzuku hapa naungana na wewe! (Tuko pamoja kama samaki na maji hapa). Tatizo ni moja kwenye hili,kuna vyama wakala wa ccm vikifutiwa ruzuku ccm itashindwa kufaidika navyo kuwagawa watanzania. Mfano chama kama cha Dovutwa anapiga kampeni za uraisi mwisho wa siku ana muunga mkono mgombea wa ccm halafu bado anataka aonekane ni mpinzani. Au mzee Mrema aliye amua kumpigia Jk kampeni huku chama chake kikiwa kimesimamisha mgombea. Full sarakasi.

4. Mkuu chama hukutakiwa kuwapeleka wadogo zangu private wakati sera za chama chako ni shule za kata! Nyie mna nadi shule za kata machoni kumbe moyoni mnapinga mnayo hubiri?! Kama mna amini elimu ya shule za kata kwa nini mnapeleka watoto wenu St Wenyenazo?! Mnatupiga machanga ya macho watoto wetu wafaulu wakiwa hawajui kusoma wala kuandika huku wa kwenu wakifundishwa kwenye shule bora halafu baadae mnaitisha usaili wale wa shule zetu sisi (kayumba) washindane na wakwenu (St wenyehela)? Huu ni ulawiti wa maono uliopitiliza! Mungu atawauliza kwenye hili.

Kaka endelea kushindia mihogo watoto wasome shule bora hizi za ccm yenu ni changa la macho.

Ubarikiwe mpaka upigwe na butwaa.
 
Last edited by a moderator:
Sometimes nikisomaga comments za wabongo wengi kny JF inaonesha upeo wao mdogo wa kufikiri na ushabiki wa siasa uliombatana na malalamiko. Watanzania wanachotaka siyo CHADEMA au CCM kushika madaraka. wanachotaka ni maisha bora hata kama UDP wataongoza nchi. Kama Lowassa anahoja ya kuwezekanisha elimu ya bure na bora, tunachopaswa ni kuchangia maoni yetu kutizama uhalisia wa namna hoja yake inavyowezekana. Ni upuuzi mtu akitaka kutoa hoja yake tukang'ang'ania kusema ameiba hoja ama sera hiyo kutoka chama kingine. Dunia tunayoishi haiko kwenye upuuzi wa fikra hizo. Tujifunze kwa wamarekani, mtu hachaguliwi kwa kuwa ni wa chama fulani, anachaguliwa kama anayo hoja sahihi ya kumtoa mwanachi katika changamoto fulani. Tutaendelea kushabikia vyama badala ya kutathmini sera kama zinajenga. TUBADILIKE. wenzetu wanapopata nafasi ya kutoa maoni wanaenda beyond ushabiki wa vyama, wanajadili hoja, huu upuuzi wa kumjadili mtu, kutoa, kukejeli hoja ya msingi kama elimu ya bure ni tatizo la upeo wa kufikiri. Linganisha comments za wamarekani wakati wa uchaguzi inapotokea hoja, na comments zilizopo hapa.

Akiongea kupitia kituo cha channel 10 kwenye taarifa ya habari ya saa 1 leo 18 Nov,2012 Mheshimiwa Lowassa amesema serikali inaweza kugharamia elimu ya msingi na sekondari kwa wananchi wake kuwa bure, na elimu ya sekondari ikafanywa kuwa ya lazima na ya kiwango (quality). Ili kuwafanya vijana kushindana kikamilifu kwenye soko la ajira.

Kauli hii ni muendelezo wa wana CCM kuendelea kukubali sera kadhaa kwenye ilani ya CHADEMA ya mwaka 2010, juzi Kinana alisema serikali iondoe kodi kwenye vifaa vya ujenzi ili wananchi wawezi kujenge nyumba bora kwa ajili ya makazi.
 
Mkuu dazbaba umseomeka sema unaonekana umeandika ukiwa na jazba! Tulia! Ona ulivyo anza "Sometimes nikisomaga comments za wabongo wengi kny JF..." Kwa jinsi ulivyo andika kiswahili kizuri najua na wewe ni mbongo tu bali uliamua kujibagua.

Swala hapa sio ushabiki wa vyama wala itikadi ya kivyama. Swala hapa ni kukataa kuwa hayawezekani halafu miaka 3 baadae walewale walio kataa wanakuja kusema kuwa yanawezekana.

Ukiuweka mbali u-marekani na kuuvaa ubongo ulitakiwa uji hoji kwa nini hawa waliosema haiwezekani leo wanasema inawezekana?! Halafu upime kama wanafaa kuongoza.

Samahani kama nimetumia lugha ya kukukwaza.
 
Last edited by a moderator:
Na ili kulifanikisha hili lazma turudi kwenye nationalization of schools, kusiwepo na private schools ili usawa uwepo...baada ya hapo wahamie kwenye afya, nayo iwe bure!!

I bet you ain't serious, you are just :violin:
 
JK nae amekubali mfuko wa cement na vifaa vya ujenzi viteremke bei watu wajenge... safi sana CDM, sera walizikataa sasa wameanza kuziona zinafaa..
 
Hivi elimu bure kuanzia chekechea hadi sekondari inawezekana? Nauliza hivyo kwani kunajamii nyingi zinakosa kuipata elimu ikiwa eti sababu ni uchumi mbovu wa kifamilia. Kama inawezekana nadhani Serikakali ingewekeza ruzuku katika elimu ili kuhakikisha kuwa kila raia wake anaipata ili imwezeshe kumudu maisha yake yabaadaye. Na je! serikali hailioni hili? wangapi waliandikishwa darasa la saba miaka 7 iliyopita? wangapi wamefaulu baada ya kuchaguliwa? wote wamejiunga na kidato cha kwanza baada ya kufaulu? kwanini si wote?
 
SIASA

Ni kuhusu elimu bure hadi sekondari, asema iwe moja ya ajenda za ccm 2015

Na Na Mwandishi Wetu (email the author)

Posted Jumatatu,Novemba19 2012 saa 7:26 AM


KWA UFUPI

Lowassa akizungumza jana mjini Babati alisema, mjadala kuhusu elimu kutolewa bure hadi sekondari haukwepeki, hivyo kuwataka wadau wa elimu kuanza sasa kujadili suala hilo na kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapaswa kulifanya hilo kuwa moja ya ajenda zake katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema wakati umefika kwa sasa hapa nchini elimu ya Sekondari iwe elimu bure na kumwondolea mwananchi wa kawaida mzigo wa kubeba gharama za elimu hiyo.

Lowassa akizungumza jana mjini Babati alisema, mjadala kuhusu elimu kutolewa bure hadi sekondari haukwepeki, hivyo kuwataka wadau wa elimu kuanza sasa kujadili suala hilo na kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapaswa kulifanya hilo kuwa moja ya ajenda zake katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Alisema elimu ya sekondari ikifanywa bure, itakuwa ni fursa kwa kila mtoto wa Kitanzania kuipata. Hatua ambayo itaongeza weledi na uelewa wa mambo mengi katika jamii.

"Ninasema sasa wakati umefika elimu ya sekondari kuwa kama elimu ya msingi kwa watoto kusoma bure kuanzia kidato cha kwanza hadi kidato cha nne," alisisitiza Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM).

Kwa kauli hiyo, Lowassa ni kama ameunga mkono Sera ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao waliingia katika mgogoro na CCM kuhusu elimu kutolewa bure wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2010.

Chadema wamekuwa wakisisitiza kwamba elimu bure inawezekana hadi ngazi ya sekondari, lakini wakati wote CCM wamekuwa wakisema kuwa suala hilo haliwezekani na kwamba kauli za aina hiyo ni kuwahadaa wananchi.

Katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, aliyekuwa mgombea wa urais kupitia Chadema, Dk Willibrod Slaa alitumia sera ya elimu bure kuanzia chekechea hadi sekondari kama kete ya kusaka ushindi, huku akisema chama chake kingetenga asilimia 35 ya bajeti kwa ajili ya kuboresha elimu na kutoa elimu bure.

Hata hivyo, aliyekuwa mgombea wa CCM na baadaye kupata ushindi, Rais Rais Jakaya Kikwete alikuwa akiwatahadharisha wapigakura kuwa kwamba ahadi ya Chadema ni hewa na kwamba hilo lisingewezekana.

Mvutano huo uliwaingiza makada wengine ambao ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ambaye wakati huo alikuwa Meneja Kampeni wa CCM na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta na kwa upande wa Chadema, Dk Kitila Mkumbo naye alijitokeza kutetea sera ya chama chake.

Katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Novemba 10, 2010 katika Kata ya Mchangimbore katika Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma, Rais Kikwete alisema "Serikali haiwezi kutoa huduma za jamii bure" na kwamba lazima wananchi wachangie.

"Nimebahatika kukaa serikalini muda mrefu hiyo sera ya bure tulijaribu na ikatushinda na wakati huo Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, tulikaa naye tukaona hilo haliwezekani tukaamua tubadilishe sasa nawashangaa wenzetu wanawadanganya eti watatoa bure."

Kwa upande wake Dk Slaa akiwa mjini Arusha katika moja ya mikutano yake alisema kwamba CCM walikuwa wakipinga sera ya elimu bure hadi sekondari kutokana na kulea ubadhirifu na kuthamini anasa kuliko maendeleo kwa wananchi.

Kauli ya Lowassa

Jana akizungumza muda mfupi kabla ya kuanza kuendesha harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Babati, Lowassa alisema wakati umefika kwa kila Mtanzania kuzungumzia suala hilo bila ya woga.

"'Ni lazima tukubali na tujadili suala hilo kwa manufaa ya nchi kwa kila Mtanzania kukubali ushauri huo wa elimu ya sekondari kuwa ya bure," alisema Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli (CCM) na kuongeza:

"Tukishakuwa na mjadala wa elimu yetu kuwa bure hadi ngazi ya sekondari, tena basi iwe ni elimu bora, jambo hili linapaswa kuwa moja ya ajenda kuu za CCM katika Uchaguzi Mkuu wa 2015."

Alisema Serikali inapaswa kugharimia elimu ya sekondari bila ya woga na kwamba anaunga mkono wito uliotolewa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete akiwaagiza watendaji serikalini kusimamia ujenzi wa maabara katika shule za sekondari za kata.

Alisema mafanikio katika ujenzi wa shule za kata nchini yanatokana na mpango ambao yeye ni mwasisi wake alipokuwa Waziri Mkuu na kwamba ali aliusimamia kikamilifu kuhakikisha unafanikiwa.

Azungumzia tuhuma

Katika hatua nyingine, Lowassa alizungumzia tuhuma zinazoelekezwa kwake kwamba ana utajiri wa kupindukia kwamba siyo za kweli na zinalenga kumpaka matope.


Alisema wale wanaomtuhumu kutokana na yeye kushiriki katika uchangiaji wa shughuli za kijamii hawamtendei haki kwani kuchangia siyo kosa.

Lowassa alisema anachokifanya yeye katika shughuli anayoalikwa huwataarifu marafiki zake kote nchini na kwenda katika eneo husika na kuchangia na yeye hana utajiri huo kama inavyodaiwa.

Alisema, ataendelea kuchangia bila ya wasiwasi yeye na marafiki zake na hatishwi na tuhuma hizo kwani siyo za kweli na aliziita kuwa ni ‘uongo wa kupindukia'.

Naye Askofu wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dk Thomas Laizer aliwataka waumini wa kanisa hilo kote nchini na waumini wa makanisa mengine kuwapuuza baadhi ya watu wenye kutaka kuleta vurugu nchini.

Askofu Laizer alisema vurugu za kuchoma makanisa zilizofanyika Mbagala na maeneo mengi zinapaswa zikomeshwe, lakini akatoa wito kwa waumini Waksrito walioguswa kutokuwa na mawazo ya ulipizaji wa kisasi.

Alisema, nchini kuna Waislamu wengi wasiounga mkono vitendo vinavyodaiwa kufanywa na baadhi ya waumini wa dini hiyo, hivyo makanisa yaombee amani ya nchi, ili Watanzania waendelee kuishi kwa utulivu.

"Kila mtu mwenye dini afanye maombi kuiombea nchi amani, yapo makanisa mengi yamechomwa moto na siyo kama waumini wa dini ya Kikristo ni waoga la hasha, bali mafundisho yetu yanakataza ulipizaji wa kisasi, kisasi ni kwa ajili ya Mungu," alisema Askofu Laizer.

Katika harambee hiyo kiasi cha Sh133. 89 milioni kilichangwa, na kati ya hizo Sh87. 54 ni fedha taslimu na Sh45.85 ni ahadi. Fedha hizo ni zaidi ya malengo yaliyokuwa yamekusudiwa ya kuchangisha Sh120 milioni.

Hadi sasa ujenzi wa kanisa hilo umeshagharimu Sh186 milioni na hadi litakapokamilika linatarijiwa kuwa limegharimu kiasi cha Sh600 milioni.



 

Haya Wananchi wa TANGANYIKA... Kumbe HOJA za Dr. Slaa zilikuwa bora zaidi ya RAIS Mtawala aliyekuwa anataka kuwa RAIS tena 2010?

Captain KINANA alianza kwa kuchukua HOJA ya DR. SLAA na CHADEMA kwa kusema watapunguza BEI za VYOMBO vya UJENZI...

Captain LOWASSA sasa na yeye ameichukua HOJA nyingine ya DR. SLAA na CHADEMA...

Kwahiyo VYOTE DR. SLAA alivyokuwa anavizema VILIKUWA INAWEZEKANA; Zaidi ya RAIS na Kuifanya BANDARI ya KIGOMA kuwa kama DUBAI??

Sasa tusubiri wengine - kuiba HOJA za DR. SLAA na CHADEMA...
 
Akiongea kupitia kituo cha channel 10 kwenye taarifa ya habari ya saa 1 leo 18 Nov,2012 Mheshimiwa Lowassa amesema serikali inaweza kugharamia elimu ya msingi na sekondari kwa wananchi wake kuwa bure, na elimu ya sekondari ikafanywa kuwa ya lazima na ya kiwango (quality). Ili kuwafanya vijana kushindana kikamilifu kwenye soko la ajira. Kauli hii ni muendelezo wa wana CCM kuendelea kukubali sera kadhaa kwenye ilani ya CHADEMA ya mwaka 2010, juzi Kinana alisema serikali iondoe kodi kwenye vifaa vya ujenzi ili wananchi wawezi kujenge nyumba bora kwa ajili ya makazi.

Mkuu Mtoi, sera hii ya kutoa elimu bure haifai. Iwe kwa Chadema au CCM. Basic education ambayo haina quality nzuri inawezekana.

Lakini elimu yenye quality nzuri, hata Chadema hawawezi kuitoa. Ukisikia kiongozi anatoa kauli kama hiyo basi ujue ana maana kuwa waau watatozwa kodi zaidi, na watalipishwa michango mingi ili elimu hiyo iwe na kiwango.

Tatizo la ajira hapa Tanzania halitokani na watu kukosa elimu peke yake, sababu kubwa inatokana na kuwa job seekers ni wengi kuliko wanaotoa nafasi za ajira.

Kauli anayotoa Lowassa inabidi awe anaitolea maelezo, kama ajira zinatokana na watu kuelimika sana au kutokana na uchumi unaweza kuabsorb wanaotaka ajira. What about ajira ambazo hazihitaji elimu, zipo? Upagazi, ukuli, ujenzi,

Inawezekana Mh Lowassa is out of touch.
 
Maelezo hayo hapa chini nimeyachota kwenye tovuti ya Chadema bila kuongeza au kupunguza neno.

Serikali ya CHADEMA itafanyaje ili kuboresha Elimu ya Tanzania?

Itabadili mitaala ya elimu – Italenga mahitaji na maslahi ya Taifa, mitaala itakayochochea fikra, udadisi, ugunduzi na kuendeleza vipaji.

Itatenga kwa sekta ya Elimu na Elimu ya Uraia asilimia 35% ya bajeti yote ya Serikali – italenga kuboresha mazingira ya elimu, ya ufundishaji na uboreshaji wa maslahi ya Waalimu na kuweka mazingira mazuri kwa wanafunzi wenye ulemavu kupata elimu bila vikwazo

Kamwe elimu haitategemea misaada ya wafadhili na hatutakopa ili kusomesha Watanzania. Elimu italipiwa na fedha za ndani kutokana na makusanyo ya mapato ya kodi na pia mkakati utawekwa ili mapato yote yanayotokana na uchimbaji wa madini yalipie elimu ya watoto wa Tanzania.

Tutajali walimu kwa kuboresha kipato, makazi na mafunzo yao.

Mfumo wa elimu utarekebishwa kwa kiasi kikubwa na utakuwa na mtazamo wa kijinsia ili tuoe fursa sawa kwa wananfunzi wa kike na wenye ulemavu katika kujifunza.

Elimu itatolewa bure kutoka CHEKECHEA mpaka SEKONDARI.

Tutashirikisha wadau wote muhimu kuweka mfumo wa elimu unaowahisha kuhitimu – kuwahi kuanza (miaka 5) na kuwahi kumaliza (2,6,4,3+)

Elimu ya msingi itakuwa mpaka darasa na tisa (Kidato cha Pili) na itakuwa ni lazima kwa kila mtoto anaeishi Tanzania.

Ushirikishwaji wa jamii na wanafunzi katika uendeshaji wa shule utaimarika ili kuboresha ufundishaji na uwazi katika matumizi ya pato la shule.

Elimu sahihi ya Uraia inayochochea kujitambua na uzalendo itafundishwa katika ngazi zote.

Kila mwanafunzi wa sekondari atafundishwa somo la sayansi ya kompyuta na utumiaji wa kompyuta.

Tutageuza majengo yote ya Serikali Dodoma kuwa vyuo vikuu na vyuo vya ufundi kwa kuendelea na azma yetu ya kuachilia mbali mpango wa kuhamishia makao makuu kwenda Dodoma. Dodoma itakuwa ni jiji la vyuo na kitovu cha elimu cha nchi.

Uendeshaji wa shule za msingi na sekondari itakuwa ni jukumu la Serikali za Mitaa na Serikali kuu itatunga sera, kusimamia utekelezajiwa sera na kugawa rasilimali kama fedha.

Tutaelekeza kila halmashauri kwa kutumia rasilimali zao kuanzisha vyuo vya ufundi katika kila wilaya.

Tutatoa kipaumbele katika elimu ya ujasiriamali ili Watanzania waweze kujiajiri baada ya masomo.

Tutarejesha masomo ya biashara katika shule za sekondari ili kuwajenga vijana wa Kitanzania waweze kujiajiri.

Tutao ruzuku kwa shule za sekondari na vyuo vya elimu ya juu. Tutabadili shule za serikali kuwa ni vituo vya ubora wa elimu ili kuondoa matabaka.
 
Back
Top Bottom