Lowassa awapasha akina Nape na Mangula...

Lowassa awapasha akina Nape na Mangula...

1. Wafuasi wanaongeza siku hadi siku 2. Utajiri wake ni toka miaka hiyo ya nyerere/kabla ya richmond. Huyu jamaa anafaa sana kuwa president na wewe njoo umuunge mkono.
kwa scope yako sifa yakwanza na pengine ya pekee ya mtu kuwa rais ni ukwasi,hata kama ukwasi wake umepatikana kwa kukuibia?
 
Nimependa hiyo kuwa wana mgombea wao na ameshajaza form anasubiri siku ya kurudisha. ..

Mkuu,

hivi Visebengo vya Lumumba vipo CCM-EL,CCM-Sitta,CCM-Migigro ama CCM-Membe?
 
Kama Zitto alinunuliwa na CCM, basi Lowassa anaweza kununua mtu yeyote kuwa kwenye kambi yake. Na anaweza akaununua na Urais pia. Lowassa ni janga la kitaifa..mtu gani asiyejali na kuogopa mamlaka zilizo juu yake? Je yeye mwenyewe akiwa ndio mamlaka...kuna atakayemgusa kweli?
 
Lowassa ni Rais wa Tanzania 2015 - 2025...! Kama hutaki kajizike...!
 
mini kilimzuia kutokea kwenye kikao cha msasani ili akasafishwe kama alivyoomba,hadi akasababisha mzee wetu kuunganishwa naye,wote wakahitwa wapumbavu nakutakiwa kuacha upumbavu wao?

mama yako ndiye aliyemzuia
 
Hii ndio inaonyesha ni jinsi gani tulivyo wapumbavu!!
Mipesa anayotoa kwenye harambee anatoa wapi? kama ni marafiki zake...ni kina nani? na atazilipaje hizo pesa akifika Ikulu?

Lowassa Mwizi bwana, nenda TTCL yeye ndie kaifilisi na anaendelea kuinyonya!!! Hatuwezi kuongozwa na lijizi bwana!!

Kivp mkuu Lowassa na Ttcl kuna uhusiano gani?
 
Lowasa anafaa sana kua Rais wa Tanganyika,hata huku ndani ccm viongozi wakuu wengi wao wanapenda Edo ashika nchi,tatizo linalowafanya wanapata woga kidogo ni roho yake ya ULIPIZAJI KIISASI, sasa wanadhani akishika madaraka atawalipiza maba
ya wale wote walio kua wabaya wake.
 
Jan 8th 2014

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Brother Edward Lowassa, ametembelea miradi ya maji katika kata ya Selela iliyopo Jimbo lake la Mondul na kuongea na wapiga kura wake na kuwapiga vijembe viongozi wa chama chake waliomwambia watamchukulia hatua kali kwa sababu ya kutangaza nia ya kugombea kiti cha urais mwanzoni mwa mwezi hata kwa chama JIWE atakuwa rais 2015.

Brother Lowasa aliwakumbusha akina Nape na Mangula kwamba yeye Uwezo a
nao, nia anayo, wananchi wananipenda wakanitangazia siyo mimi nimetangaza na kuhusu harambee nimechangia kama wenzangu wanavyochangia, au nikiitwa kwenye harambee nisishiriki mpaka uchaguzi wa rais 2015 upite? Hiyo ni adhabu. Tuwe wangalifu na kuchambua maneno, Tusiwe wepesi kulaumu na kuhukumu na pia kuwa kiongozi siyo kutisha na kuogopesha wanachama, wote tuna haki sawa katika chama chetu.

Ni hivi majuzi viongozi wa juu wa CCM walimuonya Lowasa na wananchama wengine wa chama hicho kuacha kujitangazia kuwania urais kupitia CCM kwa vile muda wake rasimi bado na pia kutoa michango ya harambee mbali mbali, na kwa kufanya hivyo ni kuvunja kanuni, sheria za mwongozo wa chama na adhabu yake ni ku-jiqualify automatically wenyewe kwenye kuwania urais. Hata kinana mmoja ndugu sebastiani Kiondo wa Sanawari Arusha alisema vyama siasa nchini vyote lao moja kupigania maslahi yao badala ya wananchi,...ebu niambe ndugu mwandishi Brother Lowasa anakosa gani kama siyo fitina za viongozi wakuu wa CCM?, ukiona hivyo wana mgomea wao tayari na tayari ameshajaza fomu ya kugombea kinachosubiliwa ni siku ya kumtangaza, alimaliza ndugu kiondo kwa masikitiko. —

in Magu Kahangara.







Sijuhi huyu mzee akitemwa na kamati kuu ya CCM katika mchujo wa awali wa wagombea Urais atakuwaje? pressure na kisukali zitapanda sana!
 
kumbe ukiwa unamfukuza mwizi kwa kitendo chake kiovu cha kupora,alafu ukakutana na kiibaka mwingine anakwapua unaacha kuukemea wizi na unaushangilia?

Imagine, mko wawili mnamkimbiza mwizi, unakuja kujua kuwa huyu unayesaidiana naye kukimbiza mwizi amepata mgao kwenye wizi uliofanywa na yule mnayemkimbiza, unafanyaje?

1. Utaendelea kumkimbiza yule mwizi kwa kusaidiana na mtu ambaye tayari ana mgao?

2. Utamwambia huyu we baki kwa sababu ni mmoja wao, then umkimbize yule kwanza halafu baadae urudi kumkimbiza huyu uliyekuwa unasaidiana naye?

3. Utamkamata huyu wa karibu, then urudi kumkimbiza yule mwizi wa mwanzo?
 
Lowasa akishika nafasi katika serikali Nape itabidi aishi india
 
Utabiri wa mtoto wa marehemu Shekhe Yahaya unaonyesha kuna nguli wa siasa atatemwa na chama chake na kisha kufariki. Bila shaka mwanasiasa huyu ni E. Lowasa ama Zitto.
Kwahiyo acha Lowasa atapetape maana mfa maji haachi kufanya hivo.
 
Kinachoendelea kwa EL ni ushahidi tu kwamba watanzania tuna bongo kama za samaki.eti leo lowassa naye anajadriwa kwenye masuala ya uraisi,tena kibaya zaidi anao wapambe wanaozidi kuongezeka siku hadi siku.imefika mahala eti wapambe wa lowasa wanauliza kwani lowasa alifanya kosa gani?lile halikuwa kosa lake.hivi wamesahau au ni upofu utokanao na pesa anazogawa mithiri ya njugu?hivi ukiacha kashifa ya Richmond huyu bwana ana historia safi kweli?kama huyu jamaa ni msafi nikwanini mwaka 1995 alikwepa mwaliko wa kawawa pale msasani,appointment ambayo ilitakiwa kumkutanisha na nyerere,ili nyerere akamsafishe kama lowasa alivyokuwa ameomba kabla?kwanini maswali ya mwalimu juu ya huyu bwana alivyopata kumiliki mali nyingi kiasi kikubwa cha utajiri alionao,utajiri ambao mwalimu alidai unazidi wakwake yeye aliyekuwa rais wa nchi kwa miaka 23,hayakuwahi kujibiwa mpaka anaingia kaburini?kwanini matakwa ya mwl.nyerere ya ccm kuhitisha cc kwa gharama zake mwenyewe(mwalimu) ili akapate kumsafisha lowasa huko hayakutekelezwa?
Endelea kupaka rangi kwenye upepo...EL ni maarufu anakubalika zaidi ya CCM na WanaCCM kwa umoja wao x 1000... I'm afraid so far CCM haina option nyingine zaidi ya EL... Kubali kata ujinyonge ...
 
Utabiri wa mtoto wa marehemu Shekhe Yahaya unaonyesha kuna nguli wa siasa atatemwa na chama chake na kisha kufariki. Bila shaka mwanasiasa huyu ni E. Lowasa ama Zitto.
Kwahiyo acha Lowasa atapetape maana mfa maji haachi kufanya hivo.

mtaanza kufa ww na huyo mumeo mtabiri,na mshindwe mlegeee hadi ---- washirikina wakubwa nyie
 
Ndugu zangu, Mh Lowasa aachane na siasa mwambie asije akajikuta anakufa kwa presha. Serikali haitompa ruhusa luwa Rais huu ndio ukwel. Watamdhohofisha kwakweli niliwah sema nauona mwisho wa Lowasa

Kama kweli Edward Ngoyayi Lowassa atateuliwa na CCM kama mgombea wa Urahisi kwa mwaka 2015 basi itakuwa ni kudhihirisha tu kuwa nchi hii inaweza kuongozwa na Juha yeyote!!!

Hivi huyu Lowassa si ndiye aliyepatikana na kashfa au tuhuma za Ufisadi wa Richmond(Richard wa Monduli) na kwa hiari yake kabisa tena bila kulazimishwa akajiuzulu Uwaziri Mkuu???Kama Uwaziri Mkuu tu ulimshinda akamwaga manyanga iweje leo atushawishi kuwa anaweza kukalia kiti cha Ikulu the Highest Office in our Country???

Haya ni matusi kwa Watanzania wote. Hatutakubali FISADI aingie Ikulu asilani. Kama tu kwenye Uwaziri Mkuu alifanya ufisadi itakuwaje huyu bwana akipewa Ikulu?? Believe me huyu jamaa atauza nchi yote. Hivi watu wanafikiri hii pesa anazowahonga Maaskofu na Mapdre makanisani na hao Masheikh na Maustazi kwenye miskiti anazitoa wapi???Jueni kuna mahali anaziiba na akiingia Ikulu lazima arudishe kwa kupitia nyie Wananchi!!!

Mimi naomba CCM waharakishe kumteua kuwa mgombea wao wa Urahisi kwa 2015. CCM ndipo wataijua Tanzania ya sasa na siyo ile ya zidumu fikra sahihi na mbovu za Mwenyekiti. CHADEMA itakuwa imepata tiketi ya moja kwa moja kwenda Ikulu bila mpinzani kutoka CCM. Lowassa hawezi kuwa Rais wa nchi hii,hafai na hakubaliki kama Malaria!!!

Tafakari
 
Back
Top Bottom