Lowassa awapasha akina Nape na Mangula...

Lowassa awapasha akina Nape na Mangula...

Huyu Nape Nnauye asubiri huo moshi unaofukuta huko CCM
ImageUploadedByJamiiForums1389323202.651168.jpg
ImageUploadedByJamiiForums1389323219.780762.jpg
 
Last edited by a moderator:
Hivi hamjiulizi kwa nin wameshindwa kumuwajibisha? EL is clean richmond anaijua Kikwete.
 
Mimi simtetei Lowassa wala Nape au Mangula lakini nataka niwakumbushe watanzania.

Jamani ebu kumbukeni mwaka 1995, walijitokeza wagombea urais kutoka ndani ya CCM kama 9 hivi. kuna mgombea mmoja alihojiwa hivi na Nyerere " Mwenzetu umepataje utajiri huu kwenye nchi maskini ". alishindwa kujibu na hajajibu mpaka leo.
Sasa hivi ndani ya CCM kuna watu wameanza kujitangaza kupitia makanisani na misikitini wakitoa pesa kwa njia ya harambee. Mmoja ameulizwa mwenzetu hizi fedha nyingi unazochangisha umezitoa wapi? Nimesikia amejibu yeye hana fedha ila anachangiwa na marafiki zake. Lakini nimeambiwa huyu anayechangisha ni yule yule ambaye Nyerere alimhoji . Kama ni yeye basi awaambie watanzania alifirisika lini?. Lakini pia naambiwa ni yeye yule yule kwa namna fulani alihusika na ufisadi wa Richmond. Lakini naona watanzania kama wamesahau. Jambo moja niliseme: Mimi naona mtu akiingia madarakani kwa kutoa hela yake kuwashawishi watu ni afadhali kuliko yule anayechangiwa fedha na matajiri kwani akipewa madarka watamsakama wakidai riba kwa fedha walizo mchangishia hivyo ataliweka taifa rehani. huyu anayetoa fedha zake ni hatari lakini ni nafuu kwani yeye atataka arudishe hela yake tu. Huyu anayechangiwa hafai kabisa kwani baadae ataiuza nchi kwa marafiki waliomchangia. Kumbukeni awamu ya nne ilivyoingia madarakani na misukosuko ya Richmond, EPA, na meremeta. Halafu aliyetakiwa ajivue gamba ni nani eti?
Nawasihi watanzania tukumbuke historia tunapofanya maamuzi.
Halafu mimi sijui pesa zinazotolewa makanisani na miskitini na wanasiasa wanaotaka urais zinakubalika kama sadaka mbele ya Mungu. Nakumbuka kwenye maandiko matakatifu juu ya mama aliyetoa senti moja na mafarsayo matajiri yaliyotoa maelfu lakini imeelezwa sadaka iliyokubalika ni ile senti ya mama maskini siyo zile fedha nyingi zilizotolewa?!. Haya makuhani na mashehe angalieni changamoto hiyo.

Halafu naomba mtafakari falsafa ya moja inayosema:mtu anayetaka sana kuwa kiongozi hadi anunue watu hafai kabisa kuwa kiongozi. Kiongozi atkayefaa ni yule jamii inamtafuta siye anayetumia vishawishi kama rushwa. niishie hapa leo.
 
Tofauti ya Edward Lowassa na wanachama wengine wa CCM wanaofikiria kuwa marais wa nchi hii ni kuwa

1. Lowassa anatoa pesa nyingi na kushiriki harambee nyingi nadhani hii ni kutokana na uwezo wake kifedha.

2. Anapata ''air-time'' ya kutosha kwenye vyombo vya habari.

Kwahiyo CCM imeshindwa kusimamia sera zake yenyewe badala yake baadhi ya Viongozi wa juu kumuona Lowassa ameshashinda nafasi ya kugombea urais kupitia CCM.

Ni ajabu sana unapokuwa na Chama kinachokubali kuwa Lowassa hafai, lakini bado kina hofu na mipango ya Lowassa kama ni kweli ana mpango wa kugombea Urais kupitia CCM.

Ni mwendelezo tu wa siasa za kuungaunga kwa maana kama Lowassa anakosea kwa kuchangia kwenye harambee na mnajua kuwa kwa kufanya hivyo ameshaji-disqualify kuna haja gani ya hiyo kuwa sehemu za hotuba majukwaani?
Kwa nini msingoje vikao husika mkajadili hayo tena kipindi mtakapokuwa mnatafuta mgombea wa Urais kupitia CCM?!
Kama CCM ingekuwa makini basi huu ulikuwa ni wakati wa kukusanya ushahidi ili kama ikitokea Lowassa akaleta jina lake iwe rahisi kumuondoa kwa kuvunja kanuni zenu za Chama kama zipo?!

CCM na viongozi wake punguzeni hofu juu ya Lowassa, mara nyingine huwa nafikiri kwamba inawezekana Lowassa ana wafuasi wengi sana CCM kiasi cha kuipa hofu juu ya nafasi yake.

KUHUSU MISAADA YA LOWASSA

Tatizo si Lowassa bali ni Serikali hii ya CCM..

Wakati mwingine kusingekuwepo na haja ya Lowassa kuchangia vitu kama huduma ya maji kama Serikali hii ya CHama cha Mapinduzi wangetekeleza Sera za maendeleo kwa mwananchi.

Kama Lowassa anakuwa yupo tayari kuchangia ama kukamilisha kile Serikali ilichoshindwa kukifanya kwa wananchi lazima wananchi watamwona kuwa ni bora bila kujali motives za michango hiyo...

Serikali ya CCM itekeleze sera zenye maendeleo kwa nchi na kuacha kujadili masuala ya Urais 2015......
 
Jan 8th 2014

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Brother Edward Lowassa, ametembelea miradi ya maji katika kata ya Selela iliyopo Jimbo lake la Mondul na kuongea na wapiga kura wake na kuwapiga vijembe viongozi wa chama chake waliomwambia watamchukulia hatua kali kwa sababu ya kutangaza nia ya kugombea kiti cha urais mwanzoni mwa mwezi hata kwa chama JIWE atakuwa rais 2015.

Brother Lowasa aliwakumbusha akina Nape na Mangula kwamba yeye Uwezo a
nao, nia anayo, wananchi wananipenda wakanitangazia siyo mimi nimetangaza na kuhusu harambee nimechangia kama wenzangu wanavyochangia, au nikiitwa kwenye harambee nisishiriki mpaka uchaguzi wa rais 2015 upite? Hiyo ni adhabu. Tuwe wangalifu na kuchambua maneno, Tusiwe wepesi kulaumu na kuhukumu na pia kuwa kiongozi siyo kutisha na kuogopesha wanachama, wote tuna haki sawa katika chama chetu.

Ni hivi majuzi viongozi wa juu wa CCM walimuonya Lowasa na wananchama wengine wa chama hicho kuacha kujitangazia kuwania urais kupitia CCM kwa vile muda wake rasimi bado na pia kutoa michango ya harambee mbali mbali, na kwa kufanya hivyo ni kuvunja kanuni, sheria za mwongozo wa chama na adhabu yake ni ku-jiqualify automatically wenyewe kwenye kuwania urais. Hata kinana mmoja ndugu sebastiani Kiondo wa Sanawari Arusha alisema vyama siasa nchini vyote lao moja kupigania maslahi yao badala ya wananchi,...ebu niambe ndugu mwandishi Brother Lowasa anakosa gani kama siyo fitina za viongozi wakuu wa CCM?, ukiona hivyo wana mgomea wao tayari na tayari ameshajaza fomu ya kugombea kinachosubiliwa ni siku ya kumtangaza, alimaliza ndugu kiondo kwa masikitiko. —

in Magu Kahangara.









Rubbish ndio maana watanzania tunaambiwa wajinga huitaji kuwa mtu mwenye akili kuona Lowassa harambee zake sio za kutoka moyoni bali kuwania urais pamoja na kashifa za wizi na utajiri wa haraka alioupata. Hata anaoita marafiki zake wanakuja kutoa pesa kwa kutarajia kurudishiwa siku Lowassa akiukwaa urais. Nyerere aliwahi kusema Lowassa hafai Kikwete akatia jeuri kwa kumchagua kuwa waziri mkuu matokeo yake akachukua 10% Richmond na kufukuzwa uwaziri mkuu
 
Rubbish ndio maana watanzania tunaambiwa wajinga huitaji kuwa mtu mwenye akili kuona Lowassa harambee zake sio za kutoka moyoni bali kuwania urais pamoja na kashifa za wizi na utajiri wa haraka alioupata. Hata anaoita marafiki zake wanakuja kutoa pesa kwa kutarajia kurudishiwa siku Lowassa akiukwaa urais. Nyerere aliwahi kusema Lowassa hafai Kikwete akatia jeuri kwa kumchagua kuwa waziri mkuu matokeo yake akachukua 10% Richmond na kufukuzwa uwaziri mkuu

Unaita RUBBISH ? alivyokuwa anatumia hizo hizo pesa ili JAKAYA KIKWETE akubalike as a CANDIDATE haukuona chochote akifanyacho as RUBBISH...

Then... the same this is coming back with the same teeth to bite back NOW you called that RUBBISH ???
 
Kwa Ccm hii dhaifu wakimtimua Lowassa ndo mwisho wa chama, hawana uwezo huo
 
Back
Top Bottom